Thursday

Baada ya miaka 2 nimegundua kuwa mimi ni The Other Woman~Nifanyaje?

"Hi Dada Dinah na wachangiaji wengine, asante na pole kwa kazi ya kutushauri maana wadada kilakukicha hatujambo kwa maswali. Mimi ni mwanaama wa miaka 27 mwenye mtoto wa mwaka mmoja. Nimekuwa na uhusiano na Kijana mmoja wa miaka 25 kwa muda wa miaka miwili, sikufichi ananipenda sana na kunijali.Kijana huyu anashughuli zake binafsi kwani amejiajiri.

Sasa kipindi chote hicho tumekuwa pamoja ni hivi karibuni tu ndio nimegundua kuwa kumbe mwenzangu alikuwa na msichana mwingine na wamejuana kwa muda wa miaka 5. Baada ya kugundua tulikorofishana na alikuja kuniomba msamaha na mimi bilakujijua nikakubali na kumsamehe na hii imetoeka mara chache mpaka nahisi kama vile Jamaa ana dawa ya kunifanya nisamehe haraka.

Mpenzi huyu amekwisha enda nyumbani kujitambulisha kwa mama, kiukweli jamaa ananifikisha na kunijali pamoja na mwanangu ingawa hatuishi pamoja. Lakini ninapofikiria kuwa nina mwenzagu huwa nakosa raha na wakati huohuo sielewi huyu jamaa ana nia gani na mimi.

Swali la Kwanza: Unadhani huyu jamaa anampango gani na mimi?

Swali la Pili: Je niendelee kuwa nae au niachane nae?

Kama ni kumuacha nimejaribu mara nyingi lakini kila akirudi nakuniomba msamaha najikuta nasamehe tu, pia anatabia ya kunitumia pesa nyingi kama hana akili nzuri ikiwa nitamchunia.

Naomba mnishauri wana Dinahicious,
Asante."

Sunday

Ushuhuda: Asanteni kwa Ushauri!

"Hi da Dinah na wanablog wanzangu, nimewahi kuja na swali “"Ex ananirudisha nyuma kihisia, nami nataka ndoa-Ushauri" Nashukuru kwa ushauri wenu kwa ujumla umenisaidia na namshukuru Mungu kwa kuwa mvumilivu na kuyafanyia kazi mawazo yenu.

Nimejitahidi sana hadi nimefikia hap, kwa ufupi nimefanya kama mlivyo nishauri kwani niliona anazidi kunifatilia nilichofanya nilinunua line mpya nikamtumia x-boyfriend wangu na kumwambia kwa upole kabisa kua hii line ndio yangu ya sasa. Ile ya zamani usiitumie nimempa Mother atumie hivo ukitaka kunipata tumia hii ya sasa.

Hivyo ametumia kuwasiliana kupitia hii ya sasa na kunitaka tuonane lakini kila siku nikawa namdanganya kuwa kuna kazi kidogo imenibana anisubiri baada ya wiki kama nne hivi nitakua free then tutaenjoy nae akakubali.

Baada ya kuona amekubali nikarudi kwenye line ile ya zamani na kuanza kuitumia hii mpya nikaitupa hivo akawa anashindwa kunitafuta kupitia ile ya zamani kwani nilishamwambia kua ipo na Mother.

Nafikiri amesubiri hadi mwisho amekata tamaa akaacha kunitafuta na kitu cha kushangaza zaidi njiani hatukutani kama zamani, kwa sasa naishi maisha safi raha mstarehe na mpenzi wangu hakuna anaenisumbua wala nini.
Nawashukuru sana".

Dinah anasema:Nafurahi kuwa umefanikiwa kufanya uamuzi na sasa unaendelea vema na mpenzi wako ambae unataka kufunga nae ndoa. Lakini mbinu uliyotumia sio nzuri na nitakuambia kwanini?

Umekosea sana kumpa matumaini ya kukutana na ku-enjoy nae wakati huna mpango huo. Mwanaume sio mtu wa kukata tamaa kirahisi hivyo hasa kama anakupenda, ikiwa atakukosa kwenye Line uliyotumia anaweza akajaribu kupiga au hata kutuma ujumbe kwenye namba yako ya zamani ambayo ndio unayotumia sasa.

Siku moja mpenzi wako ulie nae sasa anaweza kukutana na ujumbe kutoka kwa Ex wako huyo na hivyo kutaka kujua ukweli wa nini kinaendelea kati yako na huyo Ex. Sidhani kama ungependa hilo likutokee.

Pamoja na kuwa kwa sasa hamkutani mtaani haina maana jamaa amehama Mji au eneo hilo, ipo siku atarudi na mtakutana, je utamueleza nini kuhusianana ahadi uliompa?!!

Unachotakiwa kufanya ni kumwambia jamaa ukweli ulio wazi kuwa humtaki na sasa uko kwenye uhusiano mwingine na usingependa uhusiano wako huo uharibuke kwa sababu yake. Kama mtu mzima atakuelewa na kukubali kuwa hawezi kuwa na wewe kwa vile tayari una mtu mwingine.

Kila la kheri!

Pages