Tuesday

Utajuaje ni "Good in bed"

Hili ni swali nimelipokea kutoka kwa msomaji wangu na linakwenda kama ifuatavyo;

"Dada Dinah nimekuwa nikisikia watu wakisifia wapenzi wao kuwa they are good in bed lakini nashindwa kuelewa ni kitu gani hasa kinapaswa kufanywa ili na mimi niwe good in bed? Amisha."

Amisha asante kwa mail, kuwa mzuri kitandani inategemeana na mpenzi wako ni kama vile uzuri wa sura, upo machoni mwa mtazamaji au mwenye macho sio wote watakao kuona mzuri.

Hali kadhalika ktk ufanyaji wa mapenzi ni hivyo, kuna baadhi ya wapenzi ukuwa unaweza kumfikisha kileleni kila mnapofanya basi wewe ni bingwa, wengine ukiwa unabadili mikao na mitindo kila dakika tano basi wewe ni championi (u dont actually enjoy) lakini ndio hivyo tena kwake ni hakuna kama wewe duniani vilevile kuna wale ambao wanahesabu mara ngapi mmefanyana kwa siku na kwao wewe ni bonge la mpenzi.

Pia wapo wale ukipiga kelele wakati unafika (hajawahi kupigiwa kelele) basi atakuona wewe ni bab-kubwa kunako kitanda, bila kusahau wale kuna baadhi pia ukiwapa ngono ya mdomo, kunywa na kumeza shahawa wanatangaza ndoa hapo hapo........nakadhalika.

Hivyo inategemea zaidi na mpenzi wako japo kuwa sio mbaya ukiwa mbunifu na kuboresha namna ya ufanyaji wako mara kwa mara.

Hebu tuambiane leo (wake kwa waume) unafikiri ni kitu gani mpenzi wako akikifanya wakati mnafanya mapenzi utampa sifa kuwa ni mzuri kitandani?

Mimi nitalianzisha hapa na wewe endelea sio? Poa,
Mimi binafsi nitakuona mzuri kitandani ikiwa utakubali Condom itumike kama kinga ya mimba (japo tumefunga ndoa), unajua tofauti kati ya kungonoka na kufanya mpenzi, vilevile kutumia muda wako na kufurahia kile tunachokifanya, bila kusahau kutowekeana "limit" yaani niachwe niwe huru kushika na kuramba popote.....

Na wewe je?.....karibu.


Monday

Mpenzi anaporudi "the old fashion"

Unakumbuka nilikupa maelezo ya mwanamke wa zamani alikuwa akifanya nini pale mpenzi/mume wanapokwenda safari? Nia na madhumuni ilikuwa ni kukupa nafasi wewe kuelewa nini kilikuwa kikitokea wakati ule alafu chukua moja au mbili (jifunze) kisha changanya na yale uyajuayo sasa (ya kisasa). Sasa leo hapa namalizia sehemu ya pili ambayo ni kitu gali kilikuwa kikifanyika mpenzi anaporejea kutoka safari ya mbali.



Kitu cha kwanza kilichokuwa kikifanyika ama kufanywa na mwanamke anapomuona mume wake kwa mara ya kwazna tangu walivyotengana (kwenda safari) ni kumsoma kwa macho yuko katika hali gani.....afauraha, ucchovu, hasira, mgonjwa, kukata tamaa n.k. alafu ndio anamlaki mumewe huyo kwa kutegemeana na hali aliyonayo mpenzi wake.



Kumbuka kuwa wakatihuo hakukuwa na mawasiliano kama sasa kwamba unajua kama sio kusikia kitu gani kinaendelea kabla hata hujamuona mtu hivyo unakuwa umejiandaa na jinsi ya kumpoke si ndio?



Sasa kwa mfano mume hana furaha au mchovu au amekata tamaa mwanamke alikuwa akimlaki kwa furaha lakini sio ile kumkimbilia na kutaka abebwe (jitu lina hasira/huzuni linaweza kukumwaga kwenye majani/chini)....baada ya hapo mume alikuwa akichukuliwa moja kwa moja bafuni/kwenye jiwe/kigoda/stuli kusafishwa kisha anafunikwa na blanketi, shuka au khanga (kaniki) alafu anakandwa sehemu ya pembeni ya kichwa chake kwa kutumia kitambaa kilicholowanishwa kwa maji joto ili kumpunguzia msongamano wa mambo/usumbufu alionao kichwani yaani kumfanya a-relax.



Baada ya hapo kilikuwa kikichukuliwa chungu kikubwa au karai leye maji ya joto yaliyochanganywa na mafuta ya karanga alafu unatumbukiza miguu yake humo na kuanza kuikanda nakuikausha mara tu unapomaliza shughuli ya ukandaji.

Mume anaongozwa chumbani kisha alawa kitandani ili apumzike wakati mwanamke unaenda kuandaa chakula (zamani chakula kilikuwa kikipikwa ukiwa nyumbani na sio kabla kwani hakukuwa na vitunza joto/moto) na wakati unaandaa chakula hicho basi unaweza ukawa unaimba nyimbo mbali mbali zinazoelezea unavyojisikia au kilivyokuwa ukijisikia kutokana na upweke au kuonyesha jinsi gani unampenda mumeo.

Pole kwa kukusolemba, tuendelee kama ifuatavyo!

Chakula kikiwa tayari mwanamke humfuata mumewe na kumkaribisha, kwa kuanzia anaweza mlisha tonge mbili-tatu kabla hajakaa na kuanza kula nae. Wakati wanakula ndio wakati wa kuanza kuongea na kuuliza maswali ya huko alikotoka, safari ilivyokuwa na jinsi ulivyotaabika na upweke bila kusaha furaha yako iliyoje kuwa nae tena.

Ulikuwa ukidhaniwa kuwa huu ni muda muafaka kwa vile tayari ameonyesha anamjali, umempunguzia stress na kumfanya awe-relaxed zaidi hivyo atasikiliza na kuelewa kile unachomwambia tofauti na kama angeanza kuwakilisha hoja na malalamiko (ya mama mkwe mfano hahahaha) mara tuu baada ya kumuona.

Pia ulikuwa ni wakati mzuri kuliko kusubiri mpaka mko kitandani, kwani ni wazi kuwa ktk ile nyanja kusikiliza na kumuelewa mwenzio huwa sio rahisi kutokana na wingi wa nyege as you can imagine mtu ndio kajitokea safari lazima mambo fulani yawe mambo.

Sasa baada ya mlo kumalizika ndio unafuata ule wakati wa kujimwaga ktk kufanya mapenzi na kuonyesha ufundi na manjonjo yako uliouongeza wakati yeye hayupo.

Ikiwa narejea akiwa mwenye furaha kabisa yaani yuko kawaida mwanamke alikuwa hajitumi sana kama ambavyo nimeeleza hapo juu.

Friday

Maambukizo ya HPV

Human Papilloma Virus (HPV) ni maambukizo yanayotokea sana wanawake na huambukizwa kwa kufanya ngono, unapata maambukizo haya hata ukitumia kinga (Condom). Baadhi ya maambukizo haya huweza kusababisha Saratani iitwayo "Cervical" au Saratani ya Kizazi ambayo inaweza kusababisha usiweze kushika mimba/zaa ktk maisha yako yote au maambukizo mengine huko ukeni ambayo sio yale ya Ngono tunayoyajua nakutajia kila siku.

Hakuna dalili zozote za Saratani hii ya kizazi lakini ukiwahi kujua kuwa unayo kwa kufanya kipimo kiitwacho "Smear" basi unakuwa umeokoa maisha yako kwani Saratani hii inaua wanawake sambamba na ile ya Matiti.

Mwanamke anaeanza ngono mapema (chini ya miaka 21) anakuwa kwenye hatari kubwa ya kupata Saratani hii na wale wanaoanza Ngono ndani ya miaka 20 huwa x2 kwenye hatari ya kupata Saratani hii.

Huu ndio ukweli wa Ijumaa ya leo kwa maelezo zaidi Muone Dk bingwa wa magonjwa ya kike, Madaktari hawa wanapatikana kila Hospitali kuwa Nchini.

Mwisho mzuri wa wiki.

Thursday

Unapotengana na mpenzi

Siku hizi watu tunaachana na wapenzi wetu sio kwa kwenda kufanya kazi mjini au kijiji cha pili bali nchi ya mbali bonge la hatua eeh?

Kutokana na maendeleo ya Tekinolojia na ukaribu wetu na familia tumekuwa "relaxed" pale wapenzi wetu wanapokwenda mbali nasi kwa muda mrefu tofauti na miaka hiyo, kwa mujibu wa marehemu bibi yangu (Mungu amrehemu). Zamani mwanamke ukiolewa inakuwa wewe na mumeo tu sasa anapoaga kuwa nakwenda kijiji cha pili kikazi mke anakuwa ktk hali ya huzuni na kutafuta mbinu za kumshawishi mpenzi ama waende wote au asiende kabisa huko alikoagizwa.

Na hiyo huwa nafasi pakee kwa mwanamke kuonyesha kwa mpenzi wake huyo ni jinsi gani hawezi kuishi bila yeye, jinsi nakiasi gani anamhitaji mumewe na kwamba hatoweza kabisa ku-cope na upweke.

Wakati huo mwanamke alikuwa akionyesha "affection" kwa mume wake zaidi ya siku zote pale inapojuliakana lini hasa anapaswa kuondoka na siku chache kabla mpenzi hajaondoka mwanamke akipaswa kumshawishi mume/mpenzi kutokubali kusafiri au waende wote kwa kutishia kujiua (kupanda juu ya mti....sio mrefu sana na kujiachia uanguke), kulia kila siku, kususa kula nakadhalika, lakini yote hayo yakishindikana basi mwanaume anaahidi kufupisha safari yake ili awahi kurudi kuwa na mkewe/mpenzi wake.

Mume anapokuwa mbali (kasafiri) mwanamke anajitenga kwa kutokuoga mara kwa mara, kutojipamba/remba, kutokuvaa vizuri na vilevile kutotembea/toka nje bila sababu ya msingi, yote hayo ilikuwa ni mapenzi juu ya mume wake nakujaribu kuepuka kuvutia wanaume wengine na yeye mwenyewe kushawishika na ku-cheat.

Wakati huo wote mwanamke anakuwa anajifunza mbinu mbali-mbali za kumfurahisha mume/mpenzi wake au mazoezi ya jinsi ya kumpa raha mume atakaporudi, mazoezi hayo sio kukata kiuno ktk mtindo tofauti tu bali, kucheza mbele ya mume wake (strip dance sio Umagharibi ulianza miaka ya zamani Tz),mapishi, kuimba na wakati huohuo mwanamke hutumia muda wake kuomba Dua ili mume wake arudi salama.

Wanawake wa sasa hatujishughulishi sana kwasababu tofauti kama sio wengiw etu hatujui au hatujaambiwa, vilevile ukaribu wetu na familia na maendeleo ya Tekinolojia vinachangia kutufanya tujisahau na kutokuwa wapweke as much as bibi zetu were!

Nitaendelea......

Wednesday

Hivi Limbwata kweli Ipo?

"Mimi dada Dinah, leo nataka kuja na mpya, huenda ikawa ni kero au nikuomba msaada. Si mpya kwamba ni jambo ambalo halipo, ni mpya katika uwanja huu wetu. Na huenda si mpya, umeshaligusia, ila hatukulipa kipaumbele kwasababu ni jambo lakukosa `elimu’. Na huenda sio kukosa elimu tu kwani wapo wenye elimu zao wanaliendekeza.


Tuliite ni Imani za watu fulafulani.Yupo jirani yetu ambaye tunaweza kumuita `womenizer’ au mhuni au mume mwenye pepo wa ngono. Jamaa huyu hakikatizi kitu, kila amuonaye kwake ni mzuri, na alivyo na kisimite, huwa akiomba hakosi.


Alikuwa akitamba kuwa wake kwake ni kama shati, hataki wamtawale milele ingawaje kaoa. Na cha ajabu alienda kupima ngoma hana! Mke wake ni mpole, mke toka kijijini, katulia home, kimya (kaziba masikio kwa pamba). Sasa mke wake akawa analalamika, baada ya mambo kumzidi na bahati alikuja hadi kwa my wife kuomba ushauri.


Kabla hajapewa ushauri alishakuwa na nia moja ya kwenda kutafuta `dawa ya mapenzi’-limbwata au love potion, alimwambia mke wangu ana nia hiyo.Hutaamini, kumbe licha ya mke wangu kumshauri vinginevyo, kuwa `ndoa’ ni kuvumiliana na hakuna dawa ya mapenzi inayoweza kusaidia, na huenda ikaharibu kuliko kusaidia.


Alipewa mifano ya watu mbalimbali ambao inasemekana waliwafanyia waume zao na matokeo yake yakawa kinyume chake. Lakini hakuelewa, alienda kwao mikoani na aliporudi, ndipo tulipoona mabadailiko. Hutaamini lakini ndivyo ilivyotokea.

Yule bwana akawa habanduki nyumbani, yule jamaa akawa hazungumzi na watu hasa wanawake. Hata marafiki zake ambao walikuwa wakikesha naye kwenye bar wakaanza kutilia mashaka. Kulikoni mwenzetu huyu vipi! Jamaa hutaamini hata kazi yake ya udereva wa masafa marefu akaamua kuiacha na alinzisha biashara ndogondogo karibu na nyumba yake.


Wengine waliofika kwake wanasema kawa mume-bwege. Jaribu kufikiria mtu alivyokuwa awali na sasa utafikiri ni watu wawili tofauti.Sasa dada Dinah, sio vizuri kuchimba sana undani wa huyu jamaa na mkewe, ila ndio nimekuja na hili swali jipya, huenda kuna watu wana uzoefu nalo. Huenda kuna watu ya mewakuta au jamaa zao.


Huenda hata wewe mwenyewe umeshawahi kuona, kukuta, hatuwezi kupata maoni ya jambo hili ili kuboreshana kimahusiano, kuonya au kupeana ushauri?What is `love potion’ Limbwata au neneo gani jingine sijui. Hiki ni kitu gani hasa, je kipo,? Je kinasaidia, je nini madhara yake kwa wanandoa au wapenzi? Je kinafanywaje kwa wale wanaojua, na wengi wanaoendekeza hili ni akina mama, twaomba msaada jamani." Mimi Emu-three

Jawabu: Well, mimi sina uzoefu na hili ila nimesikia na hata kuulizwa dawa ya mapenzi na nini na siku zote jibu langu ni kuwa mapenzi hayana dawa ni hisia za mtu juu yako, hazilazimishwi.

Limbwata kwa ufahamu wangu ni ushirikina na inafanyakazai kama ambavyo nguvu za giza/ushirikina unavyofanya kazi inategemea zaidi umenuia vipi (nia yako ni nini hasa when doing it).


Sasa unapomwendea mpenzi wako kwa mtoa Limbwata ni wazi kuwa humpendi na unataka kumbadilisha utakavyo wewe kwani atakapofanyiwa Limbwata atakuwa na "characture" nyingine kabisa na hatoonyesha mapenzi kwako bali atakuwa mjinga kwa kutofanya vitu ambavyo "real man does" hachezi mbali na wewe/nyumbani, haishi kukuzungumzia na kukusiafia mbele ya watu wengine, kulia nakuomba msamaha kila manapozozana, kufanya kila unachoamuru afanye n.k.


Hayo sio mapenzi kwa vile sio hisia zake juu yako na anafanya vitu sio kutoka moyoni kutokana na hisia zake ju yako bali kichwani kutoakana na ulivyo/alivochezewa/changanywa/blackmailed.
Mara nyingi hali hii inapomuishia mtu aliye-Limbwatika huwa hana mapenzi kabisa na mpenzi wake, yaani hali inakuwa mbaya kuliko ilivyokuwa awali.


Wanawake wengi wanaofanya hivi ni ama waliolewa kwa vile wanatabia njema kama wake lakini waume zao hawakuwapenda, wanawake ambao hawajiamini kiuchumi au kuendesha maisha bila mume/mwanaume, wanawake wanao Imini kuachika au kuomba Talaka ni aibu kwa jamii hivyo anaamua ku-stick kwenye ndoa yake n.k.


Hili lipo, linafanya kazi kama nguvu nyingine za giza na hufikia muda nguvu hizo zinaisha.Ushauri wangu kwa wanawake wenzangu ni kujiamini na kutolazimisha penzi, kwani hata ukim-limbwata mwenzio atafanya utakavyo lakini wewe unajua moyoni kuwa hakupendi.


Vilevile ni vema kuzingatia msemao wa kale usemao "mpende akupendae na asie kupenda achana nae".Hata kama uko kwenye ndoa na unaona wazi kuwa ndoa yako doesnt work pamoja na kujaribu kwako kote, usilazimishe omba Talaka endelea na maisha yako ukiwa huru.....mambo ya kung'ang'ania penzi wakati unajua hupendwi ni uzamani. Kunafaida gani ya kuwa mpweke ndani ya uhusiano/ndoa?

Wengine wataendelea.....Asante M3

Ushuhuda kutoka

Poleni kwa kuwaacha solemba kwa takiribani masaa 36 hivi kapajatop kangu kaliumia kidogo sasa nikakapeleka sipitali, kamerudi few min ago. Ktk kupitia comment nimekutana na ushuhuda huu, wengi huniandikia mail lakini naona huyu kaja kushuhudia hapa kwa faida ya wote...anasema,

"dinah mpenziilike 6-7 months ago nilikuandikia msg naomba ushauri nifanyaje niweze kuingia kwenye relation tena maaana i was betryaed by my ex niliyezaa nae!!ushauri wako ume work i met a nice guy we trully love eachother,anampenda mtoto wangu pia na inshallah mungu akisaidia tunampango wa kuhalalalisha relation yetu.he adores me n adore him we re in love dinah ,im in love at last hehhehe.endelea kushauri wengi kama mimi ..i took my time n he came along .thanksmamiii"
ni anony @ 5:07:00 PM ipo kwenye topic hiyo hapo chini.

Hongera sana nakila la kheri ktk maisha yako na familia yako.

Pages