Thursday

U've made it! Heri ya mwaka Mpya!!

Hongera kwa kumaliza Mwongo (Decade) na Kila la kheri unapokwenda kuanza mwingine. Nakutakia afya njema, maisha ya Ndoa/Kimapenzi mazuri, marefu na yenye mafanikio zaidi ya 2000-2009.
Akupendae na kukujali,
Dinah.Xxx

Monday

Kaniacha, lakini bado ananijali...je Kukeketwa inaweza kuwa kikwazo?-Ushauri

"Kwanza napenda kukupa pole na kazi ambayo unatuelimisha, nilikuwa sifahamu mambo mengi lakini kupitia kwenye blog yako nimejifunza vitu vingi sana.

Naitwa Jack ninaishi Tanga, nina umri wa miaka 25. Tatizo langu ni kwamba nimekeketwa tangu nikiwa mdogo sana hata kujitambua ilikuwa bado kwani nimekuja kutambua nikiwa mkubwa kuwa nimefanyiwa kitu hicho.

Nilipomuuliza Mama kwa nini umenifanyia hivi? akasema nilikuwa nasumbuliwa na ugonjwa wa lawalwa nikawa sina jinsi bali kukubali jibu la mama. Baada ya kukua ndio naona umuhimu wa kuwa kama wenzangu ambao hawajakeketwa.

Nilikuwa na boyfriend nikamueleza suala hili akakubaliana nami nikawa naenjoy pale napo fanya mapenzi aliweza kunifikisha kileleni kama kawaida tulidumu na Mchumba kwa miaka 3 na nusu lakini baada ya kwenda Dar es Salaam kwa masomo Mpenzi wangu huyo akanichiti na msichana mwingine na hivyo aliniacha mwaka huu mwanzoni.


Mimi bado nampenda sana ila yeye hakutaka kurudiana nami tena, japokuwa alikuwa amekwisha achana na yule dada aliyenichiti nae muda mrefu lakini hakutaka kuwa na mimi. Sijui kama ana msichana mwingine ama la. Mpenzi huyo ni mwanaume pekee ambaye nilimwambia kuwa nimekeketwa!

Hivi sasa nimepata boyfriend mwingine lakini bado hatujafanya mapenzi na ninaogopa kumwambia kama mie nimekeketwa sasa nitafanyaje ili ajue?

Mtu ambaye aliyekuwa ananifikisha kileleni ni mwanaume wangu huyo niliyekuwa nae miaka 3 iliyopita na ndie alikuwa ananipa raha kuliko niliyekuwa nae mwanzo kabla ya yeye. Sisikii kabisa hamu ya kufanya mapenzi kwa sasa nilikuwa nampenda sana mpenzi wangu wa zamani.

Nimejaribu kumuomba turudiane hataki, ila kama nina tatizo hunisaidia pia kama ninashida labda ya fedha huwa ananitumia, na nilipokuja kusoma alikuwa ananisomesha yeye mwenyewe, Da Dinah kila nikijaribu kuwa na boyfriend mwingine nashindwa nisaidie Dada yangu?
samahani kwa email ndefu utanisahihisha pale nilipo kosea?"

Dinah anasema:Asante sana kwa ushirikiano, ningependa akina dada wote waliokeketwa wasijisikie au kuchukulia kuwa wao ni waathirika(Victims) kwani inaweza kuchangia (Kisaikolojia) kwa kiasi kikubwa kutofurahia ngono.

Natambua tendo lenyewe ni la kikatili hasa ukizingatia kuwa binti unafanyiwa hivyo ukiwa ktk umri mdogo, lakini kwa vile limekwisha tokea hauna budi kukubali maumbile yako na kusonga mbele na maisha yako.

Mimi binafsi sidhani kama kukeketwa ni tatizo kwani mwanamke kuwa au kukosa kisimi hamfanyi mwanaume ashindwe kukupenda na hata kufurahia ngono, Kisimi ni kwa ajili yako wewe mwanamke na si mwanaume. Hata kama ni suala la kushukiwa chini bado kuna maeneo mengine anaweza kufanyia kazi na wewe ukafurahia kama ifuatavyo......

Kwa bahati nzuri wanawake tumeumbwa na maeneo mengi ya kusikilizia nakupata utamu, hii inategemea na utundu wako lakini mimi binafsi nimegundua maeneo sita tangu nimeanza kushiriki uhusiano wa kingono.

Maeneo 5 tayari nimekwisha changia hapa na Radioni ili wanawake wengine waweze kufurahia na wanaume kuyafahamu ili waweze kuyafanyia kazi vemana hilo eneo la sita nimegundua miezi michache iliyopita (nitachangia siku zijazo ili na wengine mkafurahie).

Uhusiano ule na wasasa: Kwavile uliamini tangu mwanzo kuwa kukeketwa ni jambo la ajabu (huenda ni kutokana na linavyolaaniwa kupitia vyombo vya Habari ) basi ilijengeka akilini mwako kuwa mwanaume atakae kuwa na wewe ukamwambia kuwa umekeketwa na akakukubali basi ndio atakuwa THE ONE.

Ulimuamini na kumpenda mpenzi wa zamani ambae inawezekana kabisa kuwa ndio alikuwa mwanaume wa kwanza kumpenda, kumuamini, kutoa "siri" yako na kufanya nae ngono, kutokana na kuhisi kukubalika kwa Jamaa huyo Kisaikolojia ukaamini kuwa hakutokuwa na mtu mwingine atakaekuparaha au hata kukupenda na kukubali japokuwa huna "Vikorombwezo" huko nyetini.

Sote tumepitia huko kwa mpenzi wa kwanza maishani, ni kweli kwa wanawake wengu huwa sio rahisi kumsahau yeye kama mtu, kusahau uhusiano ulivyokuwa na kutompenda mtu mwingine kama ulivyompenda yeye. Hakika unaweza penda mtu zaidi yake lakini mapenzi hayatokuwa enjoyable kama yale ya mtu wa kwanza), hii haina maana kuwa umg'ang'anie tu kwa vile ni 1st love hata kama yeye hataki.

Suala la yeye kukujali na kukusaidia haina maana kuwa anakutaka au anakupenda kimapenzi kama unavyompenda wewe, bali anakujali kama ex na angependa uendelee kuwa rafiki na njia peke ya kuendelez aurafiki huo ni kukusaidia na kuwa karibu kila unapomuhitaji labda kwa vile ni binti mwema, mzuri, unajiheshimu n.k.

Linapokuja suala la mpenzi uliyenae hivi sasa, huna haja ya kumwambia kuwa huna "vikorombwezo" kunako K na badala yake acha agundue mwenyewe na kama akiuliza mbona uko hivi hapo ndio utamwambia kuwa kwenu (kabila lako) huwa/walikuwa wanatahiri wanawake n.k

Huenda pia unahofia kuwa jamaa naweza asikufurahishe kingono ikiwa hutomwambia, unadhani kuwa ulipokuwa na yule wa kwanza alikuwa akikufikisha kwa vile alikuwa akijua....si ndivyo unavyodhania? Ukweli ni kuwa ulikuwa unasikia raha na utamu wa ngono kwa vile ulijiamini, ulikuwa unampenda na ulikuwa comfortable wakati wa tendo.

Mwanaume yeyote anaeujua mchezo (namna ya kufanya ngono ipasavyo) atakufikisha na kukupa raha isiyo kifani. Kitu muhimu ni wewe na yeye kujua kona nyingine za ume ambazo zinamsababishia mwanamke utamu (tafuta topic isemayo maeneo 5 ya kusikilizia utamu kwa mwanamke).

Kushindwa kupenda Bf mwingine: Ni kawaida kwa mtu yeyote anaetoka kwenye uhusiano wa kimapenzi wa muda mrefu kama wewe. Huwa ni ngumu sana kuanzisha uhusiano mwingine au niseme kupenda mtu mwingine. Baadhi hutumia muda huo kukusanya hisia zao na kuzi-review ili asirudie makosa pale atakapokuwa tayari kupenda tena.

Kwa kesi yako hakika itakuchukua muda mrefu kidogo mpaka utakapokubali kuwa umeachana na jamaa, hii ni kutokana na ukweli kuwa hujui kwanini hasa kakuacha na hivyo kila siku unapata matumaini ya Njemba hiyo kurudiana na wewe.

Kama unataka (sio lazima) kujisaidia ili kuondokana na hayo matumaini ambayo ni wazi yanakupotezea muda wa kuendelea mbele na maisha yako ya kimapenzi, ni vema kumuuliza mpenzi wako kwanini hasa ameamua kukuacha? Je ni kutokana na umbali kati yenu? Je ni aibu yake kuwa aliku-cheat? Je ameambukizwa HIV ndio maana hataki kuwa na wewe kwa vile anahofia kukuambukiza? n.k......kutakuwa na sababu moja inayomfanya ashindwe kurudiana na wewe.

Mimi kama Dinah nakushauri ujitahidi kumsahau kama mpenzi na jaribu kuji-keep busy na rafiki, ndugu na jamaa. Furahia maisha yako na kama huyo kijana uliyenae sasa unampenda basi focus kwenye penzi lenu na achana na ile njema ya zamani, kwani wakati wake umepita.

Ukiamua kupata ukweli:
Mara tu baada ya kujua ukweli kwanini alikutema, iwe ni Hasi au Chanya itakusaidia kusonga mbele na maisha yako. Kumbuka penzi ni hisia na hazilazimishwi bali hujitokeza zenyewe. Vilevile sio lazima hisia hizo zilingane bali kuzidiana na wakati mwingine kutokuwepo kabisa kutoka upande wa pili.

Kila la kheri!

Binti kaniacha...je nichukue gari langu n.k?-Ushauri

"Habrai yako Dinah,
Hebu tusaidiane hapa, nilikuwa na mpenzi wangu kwa miaka 4 hivi, na nia yetu ilikuwa tufunge ndoa mwaka huu. Baadaye binti alihama mji na kuishi mji mwingine kikazi, hivyo nikawa namtembelea mara mbili kwa mwezi, na nikafanya hivyo kwa takriban miaka miwili.

Kidogokidogo nikaanza kuona tofauti za mawasiliano na sikusita kumwambia, japo sikuona mabadiliko tofauti na hali kuzidi kuwa mbaya, nami nikaendelea kumueleza na kujaribu kuongeza mapenzi kwake ili nisimpoteze.

Baada ya kuona haitoshi nikaamua kumshawishi tufunge ndoa ili awe wangu kabisa na ikiwezekana nimrudishe mji ninaoishi mimi. Kwa kuwa dini zetu ni tofauti tukakubaliana kila mmoja akaongee na familia yake ili tuoane kila mtu na dini yake.

Mimi nikafanikiwa ila yeye akasema kwao hawataki kusikia eti mototo wao anaolewa na Muislam. Basi nikamshauri tuendelee tu kuwa wapenzi kwa muda zaidi kama hawataki tuoane kwa sasa.

Yeye akasema hana jibu maana anahisi anachanganyikiwa tu. Kuanzia hapo hali ikazidi kuwa mbaya mawasiliano ni tabu, sms nikituma asubuhi atajibu jioni, simu mpaka nipige mara 10 ndio ipokelewe nk. Hata nikisafiri kumfuata huko aliko ngono sipewi kwa kisingizio kuwa matatizo tuliyonayo yanamkosesha hamu ya ngono.

Hivyo nikakaa zaidi ya miezi 8 bila ngono japo tunaonana na kulala pamoja mara mbili kwa kila mwezi.Ghafla siku moja baada ya kutopokea simu zangu nyingi sana ndio akanambia alikuwa ananifanyia hivyo visa makusudi ili nimchukie alafu nimuache, maana anaona uhusiano wetu hauto work out as wazazi wake hawanitaki.

Katika kipindi chote hiki cha mapenzi kulikuwa na kusaidiana kwa hapa na pale na niliwahi kumuachia gari atumie. Jee ni haki niendelee kumuachia gari yangu atumie hata baada ya kuniacha?

Jee jamii itaniona nina roho mbaya, na nitajisikiaje siku nikikuta mwanaume mwingine anaye mtomba anatumia jasho langu? Nisaidieni mawazo yenu, kumbukeni kuna vingi nilivyomfanyia kama furnitures, Ada ya Pango etc.

Kindiki"

Dinah anasema:Kindiki asante sana kwa ushirikiano, Hakika kuna wanaume wenye mapenzi ya kweli na wavumilivu sana hapa Duniani. Nimesoma comments na nikagundua kina kaka wamekupa ushauri mzuri ambao natumanini umesaidia wewe kufanya uamuzi mzuri.

Hili liwe fundisho kwa kaka zangu, acheni tabia ya kuwafanyia kila kitu wanawake. Kwani nyie ni baba zao? Kama ni mapenzi mnapendana wote wawili, kama ni ngono mnaifanya wote wawili na kama ni utamu wote mnaupata, sasa inakuaje wewe umfanyie kila kitu yeye na yeye hakufanyii lolote zaidi ya kukuchanganya na Midume mingine?

Sisemi kuwa usimsaide au kumnunulia zawadi mpenzi wako au usimjali kiuchumi kama anahitaji msaada huo, la hasha! Linapokuja suala la kufanyiana mambo makubwa kama kununua Kiwanja, nyumba, gari n.k mnatakiwa kufanya hayo mkiwa na uhakika na uhusiano wenu, kwamba ni wa kudumu/wachumba mnaelekea kufunga ndoa hivyo sio tu unamsaidia yeye bali wewe pia kwani mtakuwa mnaishi pamoja au kwenda kuishi pamoja.

Mf. kwa kulipa pango la nyumba na kununua vitu muhimu kama fenicha, gari n.k itakuwa kwa ajili yenu wote wawili na sio yeye peke yake....sijui mnanielewa? Kuna wanawake ukiwa nao basi utasomesha wadogo zake wote na kujengea wazazi wake nyumba na ukikamilisha yote hayo anakutema vilevile. Wapo wanawake siku hizi wanachukulia wanaume kama ajira, yaani akiwa kwenye uhusiano ndio kapata ajira.

Mimi binafsi nakushauri uchukue Gari lako na uliuze ili kuondoa mikosi na kumbukumbu za huyo mdada. Vingine ambavyo havishikiki achana navyo. Next time unajiingiza kwenye uhusiano hakuna kununulia mtu gari, mtafutie Dereva.

Mungu atajaalia mwaka huu mpya utaanza maishamapya na mpenzi mpya atakae kupenda kwa dhati, kukuthamini na kukuheshimu. Hakikisha hurudii makosa.

Kila la kheri!

Wednesday

Siko Comfortable kuwa karibu na Ma'mkwe-Ushauri

"Hongera sana dada Dinah kwa jinsi unavyotusaidia kwenye mambo mbalimbali, nimeshapost maswali yangu mawili lakini umeyatia kapuni dada yangu kulikoni?? chonde chonde usilitie na hili kapuni.

Dinah anasema: Mama M, sijapokea swali lolote kutoka kwako, hili ni la kwanza. Kwa kawaida kila swali linanolifikia ni muhimu na huwa nali-publish kwa kufuata lini nimepokea.

****************************************************************************

Mimi ni mwanamke niliyeolewa na nina watoto wawili, mume wangu alishawahi kunicheat hapo awali na nikagundua lakini bado aliendelea. Mpaka sasa bado sijatulia kutokana na kutendwa na mume wangu.


Mimi na mama mke hatupatani kutokana na yeye mama kumtetea mume wangu alivyonicheat. Mama huyu alinifokea sana na kuniambia nimuache mume wangu, Yaani alinijia juu mpaka wake wa mashemeji zangu wakawa wanamsema kwa kumwambia anavyofanya sio vizuri.


Nimejifungua hivi karibuni na mtoto sasa anamiezi saba, sijawahi kuwasiliana na mama mkwe wangu tangu mwezi wa kumi na mbili mwaka jana alipokuja kwangu hapa Dar ambapo aliondoka vibaya na hata kusema kuwa kamwe hata kanyaga kwangu.


Mama mkwe yeye anaishi Mkoani, na kiukweli mimi nilikuwa nikimuonyesha heshima zote wala sijawahi kumchukia wala kujibishana nae sembuse kubadilishana maneno makali. Nakumbuka kuna wakati nilimpelekea nguo za Christmass, lakini aliziponda sana akasema atazitupa "nguo gani mbaya hivyo"? japokuwa ilikuwa ni suti nzuri tu jamani! mpaka wifi yangu (mtoto wake) akajisikia vibaya akaja kuniambia mbele ya mama yake ambaye aliona aibu na kuanza kukana.


Tatizo kubwa naona kama huyu mama mkwe anachuki binafsi na mimi japokuwa ndio mchezo
wake kwani keshawakorofisha sana hata hao wake wengine wa mashemeji zangu ila naona kwangu kazidi.

Sasa hivi niko kwenye uhusiano mzuri kiasi na mume wangu japo bado machungu hayajaisha ila anajitahidi, aliniita akaniomba nimsamehe mama yake akidai kuwa "nyie wanawake mnajuana wenyewe sijui kwa nini anakuchukia hivyo" akaniomba nimsamehe na niwe nampigia simu na niwe karibu nae. Siku mjibu kitu mume wangu na wala sikumpigia huyo mama mkwe kwani mimi nimejifungua hata yeye angeweza kuja au kunipigia simu naa kuulizia mtoto lakini anaongea na mwanae tu.

Swali: Mume wangu anataka tukambatize mtoto wetu mkoani (kwa mama mkwe) Xmass hii na mimi sijisikii huru kwani sitamani hata kumuona yule mama kwa alivyonipa stress kwenye maisha yangu, yani hapa sijaandika yote, hata watu baki na ndugu zangu wanajua matatizo niliyoyapata kutokana na chuki ya mama mkwe.

Naomba ushauri kwanza, nikubali nikambatizie mtoto huko kwa mama mkwe au la, na kama nikikubali kwenda huko je nimnunulie huyu mama zawadi kama nguo?? kwani mume wangu huwa hana utaratibu wa kununua nguo za mama yake kabisa!! tafadhali nisaidieni nideal vip na huyu mama??
Wenu mama M"

Dinah anasema: Pole sana kwa kukabiliana na chuki ya mama mkwe wako, hili ni tatizo kubwa linalowakabili wanawake wengi sana hapa Duniani. Hata mimi sijui ni kwanini hasa mtu umchukie mkweo kiasi hicho. Tena mbaya zaidi ni pale Mumeo akiwa ndio mtoto wa Kiume kwa kwanza/mwisho/mtoto wa kiume pekee kwenye familia yao.....hapa mama wakwe/wifiz huwa hawataki mchezo!

Tatizo letu wanadamu huwa tunategemea kupendwa mara tu baada ya kuungana na familia nyingine (kufunga ndoa), Jamani! Mtu mmoja kukupenda haina maana Ukoo mzima ukupende. Kama ikitokea kwa bahati nzuri mkapendana poa, ikitokea hawakupendi safii tu au kama wewe huwapendi ni kawaida vilevile (kwani mlizaliwa pamoja bwanaaa!).....kitu muhimu ni kuheshimiana na kila mmoja wenu kujua mipaka yake kati ya yule aliye waunganisha in ur case mumeo.


Unachotakiwa kuzingatia ni Kumpa heshima lakini kamwe usijipendekeze kwa mama mkwe huyo, usijilazimishe kumpenda (huwezi kulazimisha hisia kama hazipo kubali kuwa hazipo), kutokumchukia (mchukulie kama alivyo na dharau uchokozi na chuki zake kwako), hata siku moja usimzungumzie vibaya kwa watu wengine (kwa kufanya hivyo itakufanya ujenge chuki dhidi yake) kumbuka kuwa huyo ni bibi wa watoto wako hivyo kubali kuwa hakupendi na muache kama alivyo aili mradi tu hamkai nyumba moja.

Ni kama kuwa Kazini/Shuleni, kutakuwa na watu wanakupenda na wengine hawakupendi(ni nature ya mwanadamu)....... lakini huwezi kuacha kazi au masomo kwa vile tu watu fulani wanakuchukia. Unawadharau na kufanya kazi/masomo yako kwa bidii.

Ukiangalia kwa undani asilimia kubwa ya wanawake huwa na tabia ya kuchukiana kweli kweli bila sababu, inawezekana kabisa mtu humjui lakini unajenga chuki. Sasa mimi nadhani hii asili ya baadhi ya wanawake kuwa na chuki za ovyo-ovyo ndio husababisha baadhi ya wakwe zetu kuwa hiyo kwani uanamke hauwatoki hata kama ni watu wazima sana.


Wataalam wa Saikolojia wanadai kuwa mama na mtoto wa kiume huwa na bond maalum, ukaribu huo kati ya mama na kijana wake kuendelea kwa muda mrefu sana. Mama huyu huendelea kudhani kuwa Kijana anahitaji kumsikiliza na kufanya maamuzi ambayo yeye mama anakubaliana nayo kama akipinga basi Kijana hapaswi kuendelea na maamuzi hayo na kiendelea basi atakumbwa na mabaya (si umewhai kusikia kuwa Radhi ya mama ni Kali kwa mtoto wa kiume kuliko wa kike? Jiulize kwanini iwe kwa mtoto wa kiume tu?).


Sasa Kijana anapokuwa na kuanza kujitegemea mama hupata hisia za kupoteza sehemu kubwa maisha yake na hivyo ataendelea kujiweka karibu na kutaka kujua kila kitu ambacho Kijana wake anakifanya. Ikitokea Kijana kaamua kuchumbia Binti ampendae mama huyu anaweza kukubali au kupinga (huwezi kuambiwa hili ni suala la familia yao).


Mama akikubali basi ataanza kujiweka sana kwenye uhusiano wenu na kuhoji vitu kama vile mtafunga ndoa lini? nani asimamie, aina ya nguo zitakazo valiwa, sherehe iwe wapi na iwe vipi? n.k. Baada ya kufanikiwa kufunga ndoa mama huyu ataanza "nataka mjukuu" wakati tayari wapo wengine waliozaliwa na dada/kaka wa mumeo....

Hii yote ni katika kutafuta ushindi na kukuonyesha wewe Mkwe (anakuona kama mwanamke mwingine unaechukua nafasi yake kwa mwanae) kuwa yeye ndio mwenye sauti na mamlaka kwani huyo Mumeo ni mtoto wake hivyo anatakiwa kufanya akisemacho yeye na sio wewe.

Kutokana na maelezo yako inaonyesha kuwa Mama mkwe wako hakupewa nafasi sana kwenye uhusiano wenu na ndio maana anakuwa bitter kila kukicha, na kilichonifanya nigundue hilo ni kutokana na maelezo yako kuwa alimtetea mwanae alipotoka nje ya ndoa.....alimtetea mwanae ili aweze kum-win back Kijana wake na wewe ubaki mwenyewe na maumivu yako moyoni.....alitaka Ushindi kwani wewe ndio unaemjali kwa kumnunulia zawadi na si mwanae......kwa mama mkwe huyu hili ni pigo kubwa kwani anadhani kuwa wewe as "mwanamke tu" ndio una-control kila kitu kwenye maisha ya mwanae.


Nini cha kufanya: Mimi binafsi sioni sababu yakwenda kumbatiza mtoto huko Mkoani unless otherwise kuna sababu za msingi kama vile Kabila la Wachaga (Xmas kuliwa Nyumbani Moshi kind muhimu), mnamtegemea yeye Mama mkwe kiuchumi, labda ndugu wengi wako huko Mkoani na wanataka kushuhudia Ubatizo na ili ku-save ni bora ninyi muende huko kuliko wao kuja Dar, Mama mkwe huyo mgonjwa na hawezi kusafiri lakini anataka kumuona mtoto n.k.

Ili kuondoa vurugu, wewe kubali kwenda kubatiza mtoto huko aliko mama mkwe lakini hakikisha unaelewana na mumeo kuwa hamkai sana ili kuepuka "chokochoko" za huyo mwanamama. Utakapo kwenda huna haja ya kumnunulia chochote huyo mwanamama asie na shukrani.....ili apate ujumbe kuwa kuponda zawadi =hakuna zawadi.

Baada ya shughuli ya Ubatizo kuisha ni vema wewe na mumeo kuwasiliana kwa mara nyingine tena kuhusiana na unavyojisikia kwa mama mkwe wako. Usipozungumza na mumeo na kuliweka hili wazi na kumfanya akuelewe ili asaidie kumaliza chuki za mama yake kwako.

Mumeo mpenzi ataendelea kudhani (mwanaume akisema "sijui kwanini mnachukiana, ni mambo yenu wanawake...naomba umsamehe mama") yaya tachukulia kuwa yameisha, kuwa umemsamehe mama yake na hivyo kuendelea kufanya mambo ya kumhusisha mama yake na wewe mara kwa mara hali itakayosababisha maumivu makali ya hisia kwa vile utadhani kuw amumeo hakujali pia hautokuwa comfortable na mkweo.


Liweke wazi suala la wewe kujisikia huna thamani kwa mama mkwe huyo kutokana na dharau zake, kutetea usaliti wa ndoa...tena sisitiza hapa kuwa ukimuona mama mkwe huyo unakumbuka uchafu aliokufanyia mumeo (umesema kuwa bado unamachungu/hujasahau japokuwa unajitahidi kusamehe....itachukua muda mpaka kurudia hali yako ya kawaida). Mwambie yote yalioujaza moyo wako bila hasira wala chuki.

Muombe mumeo amwambie na ikiwezekana amsaidie mama yake abadilishe tabia yake mbaya, na mara baada ya kubadilisha tabia yake basi anza kumnunulia/tumia zawadi lakini sio ktk kujipendekeza bali kumjali.

**Nani alisema maisha ya ndoa ni rahisi eei? Ni magumu ila ukijua namna ya kukabiliana na wanawake (mama mkwe/wifi) kila kitu kina kinaenda vema na kila mmoja wenu anafurahia maisha yake kivyake na familia yake.

Natumaini kuwa maelezo ya wachangiaji na haya yangu yatakuwa yamekusaidia kufanya uamuzi wa busara.

Kila la kheri!

Pages