Saturday

Ushuhuda!

"Dinah mambo vipi? pole na kazi sijui utakuwa unanikumbuka mimi......(Dinah kaifadhi jina kulinda utu wako) nilishawahi kuomba ushauri kwako na nimefanikiwa nashukuru sana. .DINAH nashukuru sana yani ilikuwa kama kumsukuma mlevi juu ya daraja nitakualika kwenye wedding yangu.kila la kheri kazi njema"


Nimefurahi sana kwa kuwa umefanikiwa kupitia D'hicious na ukachukua wasaa kuja kunipa "ze auti kam", lakini nasikitika sitoweza kufanya vile ulivyo omba (nime-edit kulinda utu wako) kwasababau watu wengine wenye tatizo kama hilo wanaweza kujifunza mbinu-mbili tatu ili kufanikisha mambo yao fulani sio, sasa nitakachofanya ni kurekebisha kidogo tu, lakini sio kuiondoa topic nzima.

Nakuhakikishia kuwa wanawake "tukishafika bei" hasa baada ya urafiki ku-turn romance huwa inakuwa ngumu san akushawishika, hivyo hata wakijaribu vipi hakuna atakae weza kumuondoa Sisy duu wako ubavuni mwako.

Focus on your love relationship and have fun......wengine achana nao, wala wasikupunguzie kujiamini kwenu kwenye uhusiano wenu.

Unajua, unapo-share tatizo unapaswa kutambua kuwa sio wewe tu unaekabiliana nalo, wapo wengi ila wewe ndio umekuwa na moyo wa kuwa wazi na kujiamini nakuja kuliweka hapa. nakuhakikishia kuna wengi ambao walifaidika na maelezo yako na pia watakuwa wamefaidika namajibu yaliyotolewa hapa.

Monday

Mama Rahma, toka nimejifungua mmmh!-Ushauri.

"Hongera dada dinah.mimi ni mama mwenye mtoto 1nimeolewa miaka 2 iliyopita. Namshukuru mungu namrizisha mume wangu tatizo linakuja baada kujifungua nilikata ku-bleed kwa miezi 5 baada ya hapo nilianza kutumia dawa za uzazi November 2007, lakini nilishindwa kuzimudu kiasi kwamba mume wangu ilikuwa akinikumbusha kila siku.


December 3, nikaamua kuweka iud/kitanzi Doctor wangu aliniambia nita-bleed bila mpangilio after 2 month itaacha. lkn ninavyokwambia mpaka sasa na-bleed bila mpango nikitombana mimaji kila saa nafuta hata mboo yenyewe siisikii na nyege zimeisha wasiwasi wangu nitamchosha mume wangu na kutoka nje saa nyingine mboo iko kumani damu inatoka naomba ushauri je nikawaida au ninamatatizo wamama wenzangu naombeni mnisaidie, Mama Rahma wa Mikocheni"

Jawabu: Rahma kwanza kabisa napenda nikupe pole kwa tatizo unalokabiliana nalo, pili nakupa hongera kwa kuwa wazi. Tatizo la maji maji mengi huwatokea wanawake wengi wanaotumia madawa ya kuzuia mimba.

Sote tunafahamu kuwa kuna baadhi hupatana/endana nayo na wengine huhangaika kubadili-badili ili kupata ile moja ambayo haitowasumbua au kuwasababishai mabadiliko japokuwa karibu madawa yote yanasababisha matatizo makubwa kwenye mwili wa mwanamke.

Lakini tatizo la kuhisi maji-maji wakati unafanya mapenzi linawezekana linasababishwa na Saikolojia yako kuwa unajua kuwa uke wako umepanuka kutokana na kujifungua hivyo unaponyevuka (kuwa/kupandwa na nyege) na tendo kuendelea unaanza kuhofia zaidi hali unayoihisi kule chini (unyevy kupita kiasi).

Sasa kwa vile wewe umekuwa ukitumia madawa ya kuzuia mimba kuna uwezekano mkubwa kuwa unamchanganyiko wa vitu vitatu.......(1) Kisaikolojia (2) Madawa uliyowahi kutumia na (3) kutofungwa vema/kujeruhiwa baada ya kuwekewa kitanzi.


Nasikitika kusema kuwa tatizo lako ni la kitibabu zaidi hivyo nitakushauri ukamuone Daktari wa maswala ya uzazi wa mpango ambao wanapatika kwenye kila Hospitali Tanzania kwa ushauri zaidi na hatimae kuzuia swala zima la utokwaji wa damu.

Ukiondokana na tatizo hilo la kutokwa na damu mara kwa mara na ukaendelea kujihisi kuwa unamaji-maji kila ufanyapo tendo la ndoa basi nakushauri uwe ukifanya mzoezi ya kubana misuli ya uke kisha tumia "Vinegar" kwenye maji yako ya kuoga, weka kidogo tu kisha kaa kwenye maji hayo ambayo yatakuwa kwenye "bath tab" lakini kama huna basi tumia Karai au beseni kubwa litakalokurahisishia kukalia maji hayo yaliyochanganywa na "Vinegar".

Loweka uke wako kwa muda wa dakika kama kumi na tano hivi na fanya hivyo mara moja kwa wiki. Hii itasaidia kupunguza umaji-maji ndani ya uke wako.

Tafadhali fanya hii mara tu baada ya tatizo la damu kuisha.


Kila la kheri.

***Tafadhali kama unauzoefu na hili nitashukuru sana kama utachangia ili sote tujifunze kitu ambacho ndio lengo kuu la mahali hapa. Asante.

"Abnormalitie" ktk uhusino wa kimapenzi....Ushauri!

"Asante sana dada Dinah kwa kutoa Elimu kwa watanzania wenzako. Samahani mimi naomba nitoke nje ya maada kidogo. Naomba niongelee suala la abnomaralities katika miili yetu na madhara yake katika mapenzi.

Abnormalities zenyewe ni mfano mwanamke kuwa na ndevu, wasichana au wavulana kuwa na mvi katika umri mdogo au wanakuwa wamezaliwa nayo. Kidogo mvi watu hutumia dawa( dye) kuzuia mvi, ila ndefu kwa wanawake imekuwa vigumu.

Nataka kujua je wasichana wenye ndefu na ambao hawajaolewa, wanapata wachumba? Swala la pili ni mimi mwenyewe: Mimi ni mvulana wa miaka 27. Nina mvi kiasi kichwani.

Nimekuwa na tabia ya kuzipata rangi ili zisionekane. Lakini girlfriend wangu wa kwanza siku moja aninikuta nikipaka rangi nywele zangu, then nikamwambie sababu, tangu siku hiyo akasema niache kupata rangi kuwa yeye haoni tatizo na hizi mvi zangu, akasema tena zinanipendeza sana.

Nilikaa naye miaka 4 tukaachana. Sasa ninaye girlfriend mwingine. Nimekaa naye miaka 2 sasa lakini hajui kama nina mvi kichwani kwani huwa nazipaka rangi. Tunapendana sana na mwezi ujao nina mpango wa kumvisha pete ya ndoa. Je niache kuzipata rangi mvi zangu ili azione au nifanyeje? Naogopa labda huenda akapunguza upendo wake kwangu.

Kwa ujumla mimi sijui wasichana wanamchukuliaje mvulana au mwanaume mwenye mvi katika umri mdogo. Dada Dinah na wadau wengine naombeni ushauri."

Friday

Mpenzi apendae Familia/Rafiki zake!

Natumai unakumbuka tulipoanzia sio? Hujambo lakini mpendwa?

Nilitoa malezo ya jinsi ya kumshawishi mpenzi ampenade mpira ili atangaze ndoa mara baada ya kuwa ktk uhusino kwa zaidi ya mwaka na haonyeshi dalili yeyote ya kufanya hivyo.

Kwa kawaida sote tunapenda familia zetu kuliko kitu kingine katk maisha yetu na baadhi hupenda nakujali pia marafiki zao kama watu wao wakaribu. Ukiwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mtu wa aina hii unatakiwa kuwa mwanaglifu sana vinginevyo utapoteza mwenza na penzi kufa kabisa.

Kwanza unachotakiwa kukumbuka ni kuwa wewe ni mtu amabe amekupenda ukubwani lakini familia na rafiki zake aliwapenda tangu anakua na upendo kati ya wewe na familia/rafiki unatofautiana japo kuwa unaweza kuhisi kuwa wanapendwa nakujaaliwa zaidi au pengine unaweza kudhani kuwa wewe ndio unapendwa/penda zaidi ya ndugu/rafiki zake kwa vile tu unachangia mambo mengi yaukubwani na yeye yalakini ktk hali halisi si hivyo.

Usisahau kuwa wewe ni mtu baki na utabaki kuwa mtu baki kwamba wakati wowote unaweza ukamtenda mwenzio au kuamua kuachana nae kwa sababu zozote zile lakini familia yako wakati wote itabaki kuwa familia yake hata wakimtenda vipi kwa vile wamechangia damu.

Sasa mpenzi mwenye kupenda watu wake (familia na marafiki zaidi) anashawishika kirahisi sana japokuwa itakuwa ngumu sana kwako kwani wakati mwingine unaweza kujihisi mpweke ndani ya uhusiano.

Unachotakiwa kufanya ni kujiandaa kupendwa na kuchukiwa (kumpendwa na yeye haina maana na ndugu zake watakupenda au wewe kuwapenda), kila mtu anahitilafu nakasoro zake hali inayotufanya tuwe tofauti hapa Duniani. Hivyo unachopaswa kufanya ni kujenga heshima kwa watu ambao ni muhimu wa mpenzi wako hilo moja.

Pili, epuka kujipendekeza na kuachia ule ushemeji-shemeji, wifi-wifi uvuke mipaka, wazazi wake waite mama na baba badala ya mama/baba'ko au jaribu kutumia mzee na Bi'mkubwa......wakatimwingine huwa wanamajina yao kama vile mama Haruna (jina la mumewe ambae ni future ba'mkwe)

Tatu, mpenzi anapokuja na malalamiko kuhusu watu wake hao (vijimambo vya kifamilia) ambao wewe unajua wazi kuwa anawazimia kinamna, msikilize kwa makini na wakati huohuo tafakari kabla hujatoa maoni yako kutokana na tukio. Hapa unatakiwa kuwa na uwezo wa kuelewa na kuchambua mambo haraka au angalau jaribu kuwa msikivu na muelewa mzuri.


Epuka kuungana, kumcheka, shangaa au kupingana nae ikiwa ataonyesha kutofurahishwa na mama au baba'ke au ndugu zake wengine na badala yake jaribu kumpa mawazo ya nini cha kufanya kwa mapenzi na upole.

Ikiwa haelewi kutokana na hasira zake basi tumia "tekiniki" za kumpunguzia "stress" au hasira(natumai unazijua) ili a-calm down, hiyo itawasaidia nyote wawili kuzungumza na kuelewana.

Siku ikipita na mpenzi hajazungumzia tukio la jana lilikomkasirisha usianzishe tena kwani huo utakuwa umbea sasa....wewe tulizana akianzisha kwa kukupa matokeo ikiwa alifanyia kazi ushauri wako hiyo bonus vinginevyo "uchubue" tu usizungumzie yaliyopita kwani hayakuhusu wewe bali yeye na wazazi wake, umetoa ushaui basi jua kazi yako imekwisha.

Haya niliyokuambia hapa ukichanganya na mengine niliyokuambia huko nyuma na bado ndoa haitangazwi? Huyo hana mpango wa kuwa na wewe kama mke......anza mbele.

Kila la kheri.

Tuesday

Wakati mwingine simpendi!...ushauri!

"Mambo dada yangu naomba nitoke nje ya maada kidogo mimi mdogo wako nahis nina matatizo maana nina boyfriend wangu ambaye tunapendana sana ananipenda na mimi ninampenda ila sometimes inantokea mimi ule upendo unaisha kabisa.

Anakuwa hajanifanyia kitu ila nakuwaa simpendi kabisa yaan hata kuongea naye nakuwa sipendi, hata kumuona nakuwa sipendi sasa nimeanza kuogopa sana je hilo ndio chaguo langu au sio maana naogopa inaweza ikaniletea problems huko baadaye.naomba ushauri wenu jaman.asante".

Jawabu: Usiogope kuhusiana na chaguo kwani ktk maisha ya kimapenzi mnayoendesha sasa swala la chaguo halipo kwani tayariumechagua nandio maana uko nae.....swala hapa ni mapenzi yako juu yake na mapenzi yake juu yako.

Hilo ni tatizo ambao wanawake wengi wanalo huwa tunaambiwa ni "moody" (sina hakika kama ndio kisirani) na kwa baadhi huwa ni "extream moody" hali inayonifanya wakati mwingine niwaonee huruma wapenzi/waume wao.

Sidhani kama humpendi ila kutokana na uchache wa maneno ktk lugha yetu ya kiswahil inabidi utumie neno hilo "simpendi" lakini katika hali halisi kinachokutokea ni kutokufurahishwa nae au niseme kuna wakati unahisi "you dont like him" kwamba hutaki kuongea, akikuangalia basi ni kosa, akikusemesha basi kwako itakuwa kama anakuchokoza au anatafuta visa lakini "you love him" kwamba moyoni mwako unampenda kwa dhati kabisa.


Hii inaweza kusababishwa na mambo mengi kama vile usumbufu wa kiakili unaosababishwa na msongomano wa mambo yakikazi, kiuchum, kimaisha kwa ujumla lakini kuu kabisa ni mabadiliko ya homono zako kama mwanamke.


Ukijichunguza vema utagundua hali hiyo inakutokea mara nyingi unapokaribia siku zako za hedhi, ukiwa uko ndani ya hedhi au baada ya kumaliza hedhi, hakuna dawa bali ni yeye mpenzi wako kulitambua hilo ili aweze kuepuka vijimambo ambavyo vitakufanya uhisi humpendi I mean "dont like him" sio "dont love him".

Lakini kumbuka tu kuwa wewe ndio mwenye tatizo hilo hivyo ni wewe ndio unapaswa kujitahidi kukabiliana na hili na kuzuia kum-push away mpenzi wako tangu useme mnapendana kuwa mwangalifu kwani kupata mwenza unampenda na yeye anakupenda sio lelemama, trust me hutohitaji kupoteza hilo.

Anatosa wengi, Je atanikubali mimi?....ushauri!

"DINAH MIMI NAKUKUBALI KULIKO HATA MAELEZO NA NIME... DINAH MIMI NAKUKUBALI KULIKO HATA MAELEZO NA NIMEKUWA nikifuatilia blog yakO 4 long time lakini nimeona niombe msaada wako na naamini Utanisaidia, sasa dada yangu mimi nasoma chuo kikuu ughaibuni.lakini kuna mtoto nampenda sana, tuna miaka miwili tangu tujiunge na chuo ,lakini sasa huyu mtoto mimi sijawahi kunwambia kwamba nampenda ila mara nyingi nimekuwa namtembelea na kuongea naye mambo ya kawaida ila yeye ashajua kuwa namtaka .sasa dada yangu naogopa kumwambia manake ameshawa tosa watu kama watatu lakini hawa wote ni wa mwaka wa kwanza ambao walimkuta sasa DINNAH naomba ushauri wako manake watu wa nchi nyingine wanaweza kumbeba.NITASHUKURU KAMA UTANISAIDIA,KAZI NJEMA!!"

Jawabu:Acha uoga, hao aliowatosa huenda hawamvutii au yeye hawapendi, sote tuko hivyo kwamba ukitokewa na mtu hakuvutii,hana viwango (hehehehehe) au huna hisia hata za kirafiki unamtosa tu mpaka utakapotokewa na yule roho inapenda au kemikali zake zinakubaliana na zako.

Pia inawezekana huyu binti ana-focus kwenye masomo zaidi na urafiki wa kawaida tu sio wa "kimalavidavi" na inawezekana kabisa unapomsemesha kimapenzi anapoteza ile hali ya kukuthamini kama rafiki. Hata hivyo hayo ni mawazo yangu tu, swala muhimu hapa ni wewe kuchukua "risk" kisha mtokee kama ifuatavyo.

M-alike kwa ajili ya kinywaji au mlo wa mchana, pia unaweza ukam-alika/alika kwa ajili ya kwenda kuangalia sinema (mtokee kiughaibuni-ughaibuni) ukimtokea kibongo-bongo mambo utakosa mtoto na maji ya moto......ila kama kweli unadhani binti anakupenda (anahisia na wewe) basi toka nae kwaajili ya "movie" mwisho wa wiki hii alafu jaribu kumbusu kikawaida tu (sio denda unless ajilegeze) bila kumtongoza.

Baada ya hapo usionyeshe kuwa uko-too needy na badala yake tumia muda mwingi na marafiki zako wa kiume au kupiga kitabu, kwa vile huwa unakuwa nae time 2 time ataku-miss na kushangaa kwanini huonyeshi ule ukaribu wako kwake japokuwa ulimbusu siku ile.....(utakuwa umeshinda hapo),ukimuona msifie alivyopendeza (hata kama hajatoka hehehehe it works) baada ya hapo toka nae kwa matembezi, mfano park hivi na mkae huko mpaka kiza kitakapoingia kisha mpe busu la madaha ila usipitilize tu.

Baada ya hapo njoo uniambie......kila la kheri!

Msomaji mpenzi unaweza kuongeza ushauri wako ambao hakika utamsaidia muulizaji kufanikisha penzi lake jipya, karibuni sana.

Pages