Thursday

Mwaka kama wapenzi(online) ila hataki tuonane.

Am sorry dada dinah nina mpenzi kwa mwaka na nusu tangu tuwe kwenye mahusiano lakini hatujawahi kuonana.







Mpenzi huyu nilimpata kwenye Mtandao flani. Shida inakuja kwenye kuonana, hivi kwanini hataki niende kwake kwa suprise.





Hebu nisaidie je ni mtu mwema kweli?







Dinah anasema: no bother Mrembo, ahsante kwa Ushirikiano.





Sasa mdogo wangu humjui huyo mtu, hujawahi kumuona zaidi ya maandishi, simu na labda Picha....Kitu gani kinakufanya utake kum surprise nyumbani kwake? Akikubaka au kukuchinja je??!!







Mtu wa mtandaoni anaweza kuwa anybody kuanzia mtu genuine mwema tu Muuaji sugu.









Logically unapokutana na mtu Mtandaoni na kuanzisha uhusiano au kudhani mnauhusiano na kuitana majina matamu (ya kimapenzi) unashauriwa kuonana nae ana kwa ana mahali ambapo kuna kadamnasi ya Watu.











Hupaswi kukubali kwenda nae hotelini, guest au kwako/kwake ukiwa peke yako. Hakikisha unapokwenda kukutana nae watu wako wanajua na kama inawezekana wajue ni wapi hasa unaenda ili kuepusha Mauaji au Ubakaji.









Watu wa Mtandaoni wengi wao (Wake kwa Waume) huwa ama waongo au kuna walakini kwenye Utambulisho wao, kwamba maisha yao ya "online" ni tofauti na maisha yao halisia.







Siwezi kusema huyo bwana ni Muuaji au Mbakaji, ila nadhani atakuwa ama kwenye uhusiano au hataki kuwa na wewe kama mpenzi ila anafurahia ku-flirt tu na wewe.







Mapenzi ya Mtandaoni ku- pass time hasa kama ana issue na Mpenzi wake.







Kuna wengine hu-pretend kuwa wanaume/wanawake ili kuendesha maisha yao ya Mtandaoni.....ni tatizo la akili na linajina lake (nimelisahau).







Sasa mtu kama huyo hatokubali uonane nae, achilia mbali kum-surprise nyumbani kwake!!!









Nikijibu swali lako: Siwezi sema kama ni mwema au sio Mwema, ila nadhani hana mpango na wewe in real life, anafurahi na wewe kimtandaoni tu.









Natumai maelezo yangu ambayo hujayaomba(nimehisi kuwa responsible kukueleza) yatakusaidia kupanua upeo wako kuhusu Maisha ya Mtandaoni.



Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Haonyeshi kuumia baada ya kumuacha...

Habari dada dinah, pole na kazi pia hongera kwa kuelimisha
jamii.


Nimekua nikifatilia sana blog hii na kujifunza mengi, ila leo na
mie yamenikuta
(kabla ya yote kwanza naomba ulihifadhi jina langu).

Mimi ni Kijana wa Kiume mwenye miaka 22 nilivyoanza
chuo mwaka jana nilikutana na Msichana ambaye sijawahi ona!! inshort
nikampenda na nilichukua muda kumchunguza kama anatabia nzuri na
nikagundua kua anatabia nzuri na anafaa.


Tukaanza mahusiano ya kimapenzi na huu ni mwezi wa Sita ila
hatujawahi kufanya Ngono kwa sababu huwa anaogopa sana kwasababu hajawahi kuguswa.

Nimevumilia yote lakini sasa akaanza kuonyesha kutokunijali kama
mwanzo na hanitreat kama mpenzi ila kama rafiki nimemwambia
abadilike mara nyingi lakini hanielewi.


Mara ya mwisho wiki iliyopta
nikamuuliza mbona unanipa mapenzi nusu nusu akanambia kwasababu
haniamini! Nilishangaa coz najua anauhakika asilimia mia kua yupo peke
yake akaongea na mengine mengi yakuniudhi.

Some time anaenda kwa marafiki
zangu anakaa mpaka masaa mawili huko...pia fb na whatsapp
anachat muda mwingi na hufanya hivyo wakati nikiwa nae.

Kiukweli heshima yangu hanipi kama
mwanzo tena, sasa nimeamua kumuacha ili nipunguze hizi stress na maumivu coz nampenda mpaka nimepitiliza.

Tangu nimemuacha haonyeshi dalili za
kuumia wala kujali wakati mimi nazidi kuumia. Hii ni mara ya pili kumbuka niliamua kumwacha baada ya kuchoshwa na stress zake ila nampenda na natamani
hata arudi tena tuendelee na mapenzi. Nifanyaje???


Dinah anasema: Salama kabisan ahsante na shukurani kwa ushirikiano.

Dogo una asili ya u control freak eti! Kabla hujaanza uhusiano ukamchunguza kwanza, uliporidhika ndio ukaanzisha uhusiano nae.....ndani ya Miezi sita una demand msichana afanye mambo ka' Mkeo na umemuacha mara Mbili in 6months kwasababu hafanyi utakayo.

Unataka akuheshimu vipi? Ikiwa hakutukani mbele za watu au kukukebehi mbele ya ndugu, jamaa na marafiki as Gf atakuwa anakuheshimu....au unataka asikae na rafiki zako au asi-chat na rafiki zake kwenye Mitandao?


Ikiwa wewe unamiaka 22 ni wazi yeye ataluwa hivyo au mdogo zaidi, katika hali halisi Wasichana wadogo ndivyo walivyo....bado anajitambua, anajifunza mambo kama Binti anaeelekea kuwa Mwanamke, anapenda kuzungumza na marafiki na kujenga uzoefu na watu mbali mbali.


Nadhani ama umeaninishwa mambo kuhusu mahusiano ya kimapenzi ambayo ni tofauti na hali halisi ya Maisha au umejiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi bila kujua uhusiano wa kimapenzi ni nini hasa!


Huwezi kumtawala Binti wa watu kwa jinsi ulivyoelezea na yeye kuendelea kutaka kuwa na wewe kama Mpenzi wake.....inawezekana hapendezwi na tabia yako ndio maana ameamua akufanye uwe rafiki tu.

Nadhani timing ya wewe kumuacha ilikuwa mbaya, umemuacha wakati yeye tayari alikuwa kakuweka kwenye "friends zone" hivyo hakupata au hapati maumivu ya kuachwa kama mpenzi(hana habari).


Kama kweli unampenda na unapenda akurudie basi ni vema kubadilika kwanza halafu ndio ujaribu kumshawishi tena kwa kuomba msamaha na kumhakikishia kuwa hutokuwa ukimtawala.

Akikubali kurudiana na wewe unatakiwa ku-relax na kumuacha awe huru kuzungumza na wenzake iwe mitandaoni au vinginevyo ailimradi tu havuki mipaka.

Akikataa basi nadhani ni vema umuache aendelee kuwa yeye na kujifunza who she is kama msichana na wewe zingatia Masomo na huko Mbele utakutana na mwingine na kuanzisha uhusiano mwingine.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Wednesday

Mpenzi haniamini, nifanyeje....

Habari Dada Dinah,

Naomba ushauri wako nifanye nini katika hili! Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 27 na nina mpenzi ambae tumetokea kupendana sana kwa muda wa mwaka mmoja sasa.


Niseme tu ananipenda nami nampenda sana katika swala la tabia sio muhuni kabisa! Niko free na simu yake muda wote ni msikivu na tumepanga kufanya mambo mengi sana.


Tatizo kubwa lililopo hajiamini hata kidogo kutokana na historia ya
mahusiano aliyokuwa nayo huko nyuma kwani alitendwa sana.

Nimejaribu kumuweka chini na kumuelewesha na kujaribu njia mbali mbali za kumfanya awe na amani na mimi lakini naona bado tatizo liko pale pale, kiasi kwamba nakosa raha kabisa.

Mfano naweza chukua simu yangu labda nikamjibu Dada angu msg yeye anakasirika kiasi cha kupoteza maelewano kwa muda wa dakika kadhaa! Hili linanifanya mpaka nikiwa nae niweke simu mbali kwa kuhofia kutoelewana.

Dada Dinah tafadhali nisaidie katika hili sitamani kumpoteza na mimi
wala sio muhuni kabisa, akitaka simu yangu anapata muda wote tatizo bado
haniamini.


Anasema hawezi muamini mwanamke katika maisha yake! kauli hii huwa inanisononesha sana mpaka kuna muda nafikiria kuachana nae.


**********

Dinah anasema: Habari ni nzuri sana, ahsante na shukurani kwa ushirikiano.


Bila shaka kutendwa huwa kunampotezea mtu hali ya kuamini tena na humchukua mhusika muda mrefu sana (inategemea na mtu).

Wengi huwa hawajiingizi kwenye Mahusiano ya kimapenzi mpaka watakaporudisha hali ya kuamini mwanamke/mwanaume tena.

Baadhi hujiingiza kwenye mahusiano tena wakitegemea wapenzi wao kuwarudishia hali ya kuamini kwavile wanahisi wao peke yao hawawezi. Huyu mpenzi wako inawezekana kabisa ni mmoja wao.


Ni vema amekuwa wazi kwako kwa kusema kuwa hatomuamini tena mwanamke hivyo kama unampenda kweli na hutaki kumpoteza basi ajira ndio hiyo, fanya yote ambayo unadhani yatamrudishia hali ya kuamini tena, na zaidi kukuamini wewe.

Unajua unapokuwa na Mpenzi mpya mara zote unakuwa hujui Uzoefu wake hivyo unajaribu "kumfanya" asahau alikotoka incase aliepita alikuwa "Mkali" kwa kuwa mbunifu au kufanya mambo ambayo unadhani hajawahi kufanyiwa au kama aliwahi kufanyiwa basi sio kama unavyofanya wewe....yaani unaweka "Ustadi" wa hali ya juu ili apagawe!

Unabadilisha ufanyaji mpaka siku aseme "sijawahi kupata uzoefu huu" au "ktk maisha yangu hakuna aliewahi kunifanyia hivi" au "duh wee ni kiboko".....ukipata hiyo ndio unaanza kupunguza speed na kumpa mambo makali once a week au mwezi(inategemea na ujisikiavyo)....


Sasa basi hata kwenye kumrudishia mwanaume hali ya kuamini na kukuamini wewe unapaswa kutumia mbinu kama hivyo.....badala ya matendo kingono, fanya kitabia, onyesha kumjali, mshirikishe, onyesha kuwa unajivunia yeye unapokuwa na watu wengine, toka nae na uonyeshe affection kwake....sio lambanana ndimi na sura bali unaweza tu kumshika mkono, bega au kumpa nusu kumbato huku mnatembea, kaa nae 0-destance mnapokuwa nje n.k.


Punguza au acha mazoea yasiyo ya lazima na Wanaume(rafiki zake wakiwemo) via Simu au Mitandao ya Kijamii.


Pia tambua kuwa baadhi ya wanaume ni sensitive na wanaweza kuwa emotional at times(sio Ushoga) ndivyo walivyo tu. Wanaume kama hawa wakitendwa huwa wanahitaji kuhakikishiwa kuwa unawapenda, hutowatenda kamwe, uaminifu wako kwao n.k.

Yaani mara kwa mara wanahitaji kuwa reassured japo hawasemi, sasa tangu unajua tatizo liko wapi Mrembo jaribu niliyosema alafu uone kama kutakuwa na mabadiliko.


Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Tuesday

Penzi kwa Simu, Nikimuona Penzi Nywiii...

Habari dada dinah, natumai umzima na pole na kazi. Kwanza napenda kukupongeza kwa hii blog yako kwa kweli tunafaidika sana na tunajifunza mengi kutoka kwako nakupenda sana.


Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 24 naishi Dubai. Nimepata Mchumba ana umri wa miaka 37 na kakubalika nyumbani na tuko kwenye harakati za kufunga Ndoa.


Kwakweli huyu bwana ananipenda sana kupita kiasi . Ananijali na kunithamini na kuniongoza katika kila jambo na kunishauri mambo yake yote kuhusu maisha yake na kwa kila kitu kiasi ambacho kanisubiri muda wa Miaka mitano ili nimalize masomo ili anioe.

Kwakweli miaka yote hatuna tabia ya kutoka pamoja wala kuonana ila nimazungumzo kwenye simu tu kwa muda wa miaka miwili.

Anakuja kwetu kawaida na mie kwakweli namempenda huyu kwa jinsi anavyonipenda na kunijali na navutiwa naye sana nikiwa naongea kwa simu kiasi ambacho siwezi kukaa siku bila kuongea nae na siwezi kufanya jambo bila kumshauri yeye tu.


Lakini cha kunishangaza akija kwetu kuonana na mie Moyo wangu unabadilika nahisi kuwa kama sijampendaa huyu mtu!

Naomba usinielewe vibaya dada dinah kusema kweli dada dinah nikikaa nikifikiria kiakili nahisi  sijaimpenda sura yake kwakweli na kwajinsi nilivyo huwa inanijia kama tukitoka wote itakuwa vipi?


Ila moyoni nampenda sana na siwezi kumkosa kabisa. Kwakweli dada dinah nahisi nachanganyikiwa sijui nijiamulie vipi niufate moyo wangu au akili yangu?

Naogopa sana ikaja ikawa tatizo kwenye ndoa yangu na kutompa furaha anayoitarajia au je hili halitokuwa tatizo nikioana nae kwa vile Moyoni nampenda ntakuja kumpenda na kutojali sura yake.


Naombaa unisaidie dadaa dinah, nakupenda sana. Asante sana.


*********


Dinah anasema: Habari ni njema tu Mrembo, ahsante. Aah! Nakupenda pia kwa kunipenda sana.....shukurani kwa ushirikiano.

Hapo ni Je, kufuata Moyo wako au Macho yako?....Akili haihusiki.


Binaadamu tupo tofauti na tunapendezwa na mambo tofauti na wakati mwingine pia umuhimu wa vitu/mambo maishani ni tofauti.

Kuna ambao hawajali sura ya mtu bali tabia, wapo wanajali Mali/Pesa tu....wengine hujali Umbo zuri sio sura wala tabia, wachache hujali Umaarufu/mtindo wa Maisha....alafu kuna wengine ka' Dinah hapa ambapo vyote ni muhimu isipokuwa Umaarufu/Pesa/Mali!


Kama unahisi Sura yake inabadilisha upendo ulionao kutoka Mpenzi kuwa jamaa tu wa kushauriana nae basi ni vema kutafuta namna ya Kuizoea sura yake.

Kwa maana kwamba tumia muda wako mwingi kuongea nae ana kwa ana, tokeni pamoja na mfanye mambo pamoja mara kadhaa kwa Wiki halafu uone kama utaendelea kumuona "mbaya".

Kama baada ya mwezi, miezi 3 bado unajisikia kutokumpenda kila unapomuona basi ujue kuwa humpendi kweli bali unapenda Msimamo wake kimaisha, unapenda anavyozungumza na wewe, unapenda anavyoshauriana na wewe, unavutiwa na sauti yake n.k.


Yeye kukusubiri wewe kwa Miaka Mitano ili umalize Masomo ilikuwa Choice yake wala usihisi Hatia kabisa na wala isikusukume kwenda kufunga Ndoa nae ambapo unajua wazi hautokuwa na furaha kila ukimuona (yeye na sura yake).


Ndoa sio "kitu" cha kuingia na kutoka kama unavyotaka.....kama haupo tayari ni vema kusubiri kuliko kuingia kwa ajili ya sababu nyingine na sio Mapenzi.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Thursday

Sina raha na Ndoa Yangu!

Hi, dada Dinah,
Hongera kwa kazi nzuri ya kuelimisha watu mbalimbali hususani juu ya suala la mahusiano au love affairs.


Mimi ni mmoja kati ya wadau wa blogu yako. Nimekuwa nikisoma na kujielimisha mengi yahusuyo love na relations kupitia ushauri unaotoa kwa wengine.


Unfortunately, leo nami nimejikuta naingia katika orodha ya watu uliowashauri kutokana na ishu ambayo imekuwa ikiniumiza kichwa katika ndoa yangu. Ishu yenyewe iko hivi:


Umri wangu ni 26 years, niimeoa mwaka mmoja na miezi nane iliyopita, Mwaka wa kwanza wa masomo yangu ya Chuo. Mke wangu ana miaka 24 sasa.


Kabla ya kuoana, tulikuwa tukifanya mawasiliano nae tangu niko form 5 na tukakubaliana ya kwamba tusubiri mpaka nimalize masomo yangu. Kutokana na utaratibu wa Dini, hatukuweza kuingiliana kimwili ingawa na admit kwamba mara kadhaa tumewahi kufanya romance ambayo ni kutokana na msimamo wake tuliweza kutoingiliana.

Nilikubali matokeo na kuvumilia. Sometimes she used to call me na kuniambia anahitaji tukutane kimwili but when tukiwa wawili tu akawa anataka tufanye tu romance kwani anaogopa kupoteza Usichana wake kabla ya ndoa. I agreed with her and let things go.

Hali yangu ya kiuchumi haiko sawa coz i had no Kipato cha maana sana kama Mwanafunzi wa Chuo, ishu ya Ndoa ilileta hali ya kutoelewana katika familia yao lakini akashikiria msimamo wake kwa kuwa alinipenda mno. Upande wa familia yangu was ready to support me mpaka namaliza Chuo.

Siku ya kwanza tukiwa katika honeymoon. Akaanza kulia na kunambia hayupo tayari kukutana nami kimwili. Niliumia mno. Mara akadai anaogopa kuitoa Bikra yake. Mara akadai kuwa dada yake hajaridhika na Ndoa yake.


Nikajitahidi kumliwaza na kumbembeleza sana asiwaze kuhusu ndugu zake coz maisha yashakuwa ni yetu wawili sasa hivyo ajali maisha yetu tu. Hakunielewa. Nilihisi ni njozi tu. Nikajipa moyo na kujaribu kumsahaulisha.


Nilipoona kaanza kuwa normal tukaendelea, mara baada ya tendo lile nikawa na kibarua cha kumliwaza tena.

Kwa ajabu akaanza kunambia kuwa haitaji tena kuwa nami na akawa anadai Talaka yake. Nilidhani ni masihara tu, kumbe she was seriuos. Akawa anajibu ovyo na kwa mkato. I was geting hungry. I slaped her once.

Toka siku hiyo Ndoa yangu ikaanza kupoteza mvuto na thamani. Hakutaka tukutane kimwili akidai anajiskia maumivu. Nikakubali kuvumilia but life yangu ilianza kuyumba slowly chuoni.


I decided to pospone my studies without informing my guardians. She did not want to hear kila ninachomuelekeza. Ujeuri ukawa ndio silaha yake kubwa. Niliumia mno.

Sometimes nilijaribu kuwaeleza ndugu zake ambao pamoja na kumkanya lakini niliona dalili za kumsapoti kwa kile anachokifanya. Nilizidi kuumia.


Mpaka hivi sasa, maelewano yetu si mazuri ingawa tukiwa nje watu wanaweza kusema tunapendana. Imefikia wakati hatuongei siku nzima. Dah!


Sawa na kipato changu cha Uanafunzi bado nimekuwa nikiacha pesa ya kawaida kwa ajili ya matumizi ya ziada coz mahitaji muhimu yote yapo, but wakati mwingine nakuta pesa imetumika kwa jambo lisilo na maana. Nikiuliza naamiwa 'mwanaume nina gubu unaulizia hadi chenji?' Sipaswi kuuliza pesa imetumikaje.


Maisha yamekuwa ni ya kununiana, kujibiana mkato mpaka inafikia muda sioni mapenzi kabisa. Sioni faida ya Ndoa tena.


Nikimuelekeza asifanye jambo fulani baya leo, kesho anarudia. Anaomba samahani then anaendelea kulifanya. Hana heshima kwangu kama mumewe no matter what i am trying to be.


Hivi sasa nimepanga nihamie hosteli za Chuo mara baada ya Masomo kuanza then nimrudishe kwao akapumzike au nimpeleke kijijini kwetu akakae mpaka nimalize masomo kwanza.


Nahisi ataniharibia future yangu na ya familia yangu ingawa bado hatujafanikiwa kupata mtoto.Nahitaji kuwa free ili nipange life yangu upya.


Nahitaji ushauri wako juu ya nini cha kufanya kabla sijachukua maamuzi mengine ambayo yanaweza kumkwaza yeye na famila yao.

Nimechoka kuishi maisha yasiyo na muelekeo mzuri. Please, dada ushauri wako ni muhimu mno kwangu.

************


Dinah anasema: Hello! Ahsante sana na shukurani kwa ushirikiano.


Muhimu: Kutokana na tabia za kitoto na kibinafsi za Mkeo usifikirie kabisa kuahirisha (tena) au kuacha Masomo kwa ajili yake. Unaweza kuacha mengine kwa ajili yake lakini sio hilo.

Hapo ulipompiga kibao Mkeo pameniudhi kweli, najua kuna maudhi yanakufanya utake kumdunda mtu(mke/mume).....sipendi watu wanaopiga wenzao bila kujali Kosa ni kubwa kiasi gani! Ni vema kujifunza kuzuia hasira zako Kichwani, usiziache zishuke "mikononi" na kufanya uharibifu!!

Kutokana na maelezo yako inaonyesha ama Mkeo hakuwa tayari kuolewa na wewe ukiwa Mwanafunzi, labda alitegemea mkifunga Ndoa utaacha Masomo na ufanye kazi (uwe na Kipato Kizuri)....possibility ni kubwa anafanya Visa na Vituko akitaka kufikisha ujumbe. Hilo moja.

Pili, inaonyesha ama huko kwao wanapenda kuolewa na watu wa "aina na kipato fulani" na Dada mtu ndio kinara (tumuite Control freak) anatumiwa "kuharibu".


Pia huyo Dada mtu(shemeji yako)inawezekana ama ana wivu (kama hajaolewa/kaachika).....maana wakati mwingine Adui mkuu anaweza kabisa akawa Ndugu yako wa Damu.....sema ile "sisi damu moja hatuwezi gombana" huwa inaficha ukweli wa mambo kuonekana.

Hapo kwenye "uaduia wa ndugu" hata wewe Mume hutokuwa na namna ya kumfanya mkeo aone Uadui wa ndugu yake kwake kwasababu utaonekana wewe "mtu wa nje" unataka kuwaharibia Undugu wao, wanajuana na wameishi wote kwa miaka!, wewe umeishi na Mkeo kwa Mwaka na Nusu tu(vichwani mwao)....MUHIMU ni kumuacha yeye mwenyewe aje kugundua with time.(Usiwaingilie).


Nini cha kufanya:

1-Acha tabia ya kumuambia au kumueleza, kumbuka huyo sio Mtoto, sio Mdogo wako na sio Mwanao!


Jaribu kuwasiliana nae kwa kuzungumza nae. Mpe nafasi ya kujieleza na wewe usikilize....hoji kwa upendo nini hasa tatizo linalipolekea yeye kununa na kususa?


Mjipe nafasi ya kila mmoja wenu kumueleza mwenzio jinsi anavyojisikia....kwa mabaya na mazuri. Kitu gani kifanyike ili wote kwa pamoja muishi maisha ya amani na furaha bila mikwaruzano ya mara kwa mara kama Wanandoa?

Zungumzeni kama ninyi na sio "wewe", "mimi"......kumbuka kutokurudia issue ya Fungate na yeye kuomba Talaka (nadhani alilopoka tu kutokana na maumivu).

Zingatia issues za kununiana, kutowasiliana, kujibizana kwa ujeuri, kuitana majina mabaya...(wacha kuulizia pesa zimetumikaje....unless ulikuwa na shida nazo).


Vyovyote utakavyoongea na mkeo kumbuka kusisitiza Mapenzi yako kwake, umuhimu wake kwako na kwenye Ndoa yenu kama Familia.


2-Usihamie Hostel kwani kutakuongezea gharama, huyo ni Mkeo na kama huna mpango wa kumtaliki basi mpeleke kwenu (umemuoa ni wa kwenu sio kwao....."Mke ataacha kwao aende kwa Mumewe").

Lakini kama umefanya yote na hakuna mabadiliko na unadhani mapumziko a.k.a "trial" Talaka au "separation" itamfanya abadilike au ku-rethink basi mrudishe kwako kwa muda maalum.

Nadhani kabla ya yote niliyoyasema kuna taratibu Kidini na Kisheria(mmefunga Bomani), inategemea Mmefunga Ndoa wapi au chini ya Imani gani?.....sio lazima kuyafuata kwa mtiririko lakini ni vema kuzingatia kulingana na Maagizo ya Ndoa yenu chini ya Imani zenu.


Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

"Hanitamani" sababu ya ku-Flirt Mitandaoni...

Habari dada, mimi ni kijana wa kiume na nina umri wa miaka 30 nina mke wa miaka 28 na mtoto wa miaka 3.


Kwenye ndoa yetu na Mke wangu kuna vitu vya hapa na pale ambavyo vinaniumiza kichwa kutoka kwa mwenzangu ambavyo ni; mara nyingi sana mimi ndiye naomba kufanya nae mapenzi sikumbuki mara ya mwisho ni lini yeye amenianza.

Mara nyingine tunakaa mpaka mwezi mzima kila nikimwomba anasema hajisikii, pia mara nyingi sana tukifanya mapenzi Uke unakuwa mkavu matayarisho tunayafanya ya kutosha tu.

Mke wangu anapenda sana kuchat kwenye mitandao ya kijamii kiasi kwamba nishawahi kufumania mpaka chat za kimapenzi akaniomba msamaha!!

Nina mpenda Mke wangu naomba msaada kutatua hayo mambo.


***********


Dinah anasema: Habari ni njema kabisa, ahsante! Shukurani kwa ushirikiano.


Hivi mpaka karne hii mtu na mkewe wanaombana kufanya mapenzi? Kumuomba mpenzi wako kufanya mapenzi huoni inaweza kukata "stimu" eti? (Labda ni mimi tu).

Si wanawake wote wanapenda kuombwa tendo, wengi hupenda iwe spontaneously....kwamba yupo jikoni, unamnyemelea kwa nyuma kisha unaaza kunshika maeneo apendayo ambayo yatamfanya ajisikie kupendwa na nyege at the same time...kwa mfano:

Au mpo chumbani kisha unamnyanyua na kumuweka kitandani kisha unaufanyia mwili wake "shughuli" ili ajihisi kupendwa, kuvutia na wakati huohuo Nyege na mengineyo....sio "mama Kadala nipe haki yangu"....au "mke wangu naomba basi leo" n.k.

Pia ni vema utambue kuwa sio wote wenye kupenda "kulianzisha", hii ni kutokana na kuaminishwa kuwa mwanamke kumuanza mwanaume kitandani ni Umalaya* lazma Mwanaume akuanze kisha mwanamke kutoa ushirikiano (inategemea na Mazingira aliyokulia).

Ikiwa unapenda Mkeo "alianzishe" basi ni vema kuzungumza nae na kumwambia "najisikia kupendwa ikiwa mke wangu unaonyesha kunitaka kingono, unanipa dalili kuwa unanihitaji kimwili"....kwa mfano!

Nadhani kuna uwezekano Mkeo alikuwa ana-cheat kihisia (hashiriki kimwili) na hao anaochat nao lakini kitendo cha kuchat maswala ya kimapenzi/ngono (flirtation) kunaweza kumfanya Mtu akose hamu na Mume/Mke wake kwani yule au wale anaochat nao wanaonyesha kujua kumridhisha mwanamke/mwanaume kuliko Mume/Mke wake.

Hali hiyo hupelekea mhusika kutaka kufanyiwa yale anayoambiwa au chat about na watu hao lakini anashindwa kumuambia mwenza wake na hivyo anaishia kukukwepa.


Hali hiyo ikiendelea basi Mume/Mke hupoteza kabisa hamu/matamanio na mwenza wake na hivyo kutegemea kuridhika na chat za hao anao-flirt nao kwenye mitandao.

Baada ya kugundua kuwa ana-cheat (flirting online/via texts IS CHEATING) na yeye kuomba radhi, wewe kama Mumewe ulipaswa kuweka "rules" kwenye Uhusiano wenu au kumpiga marufuku kabisa kujihusisha na Mitandoa na aweke muda wake na attention yake kwenye maisha yake halisia ambayo ni familia yake(wewe na Mtoto).


Badilisha au boresha namna ya kumtaka mkeo kingono, badala ya kuomba....tumia vitendo kama nilivyogusia hapo awali.


Pia ni vema wewe na mkeo mkawa wazi kingono ili kila mmoja wenu aweze kumridhisha mwenzio bila kujali nani "kalianzisha"


Kufanya ampenzi sio Mshindano, sio Kazi, hivyo sio lazima yeye afanye jambo kwa vile wewe unafanya kila siku.....ukianza kulinganisha ni wazi utakuwa unachukulia suala zima la kufanya mapenzi kama Kazi au Mashindano.


Kwenye Ndoa/Uhusiano wenu kuna ukosefu wa Uaminifu, Ushirikiano na Mawasiliano.....ili msipoteze Ndoa yeni ni Muhimu mkaboresha hayo mapema.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Friday

Mimba ya Mume wa Mtu, Mama hanielewi.

Shikamoo Dada, pole na majukumu. Mimi in msichana mwenye umri wa miaka 22, naishi marekani na familia yangu nikimaanisha mama na ndugu Dada yangu. Nafanya kazi kama server kwenye restaurant maarufu hapa nchini.

Tatizo langu nilijishirikisha kwenye mapenzi na Boss wangu ambae pia ni mume wa MTU ni baba mwenye umri sawa na baba yangu japo muonekano wake na umri ni tofauti anaonekana mdogo.

Tokea tumeanza mapenzi ni muda usiopungua  miezi minane.  Familia hawakumkubali lakini kutokana na kuona ni furaha yangu ikabidi wajilazimishe hivyo hivyo. 

Wiki iliyopita nilikuwa naumwa hali iliyofika hadi kuhisi kizungu zungu na kutaka kuanguka kazini ndipo boyfriend wangu aliponipeleka Hospital, baada ya siku tatu nikaambiawa nina matatizo ya upungufu wa damu  nisipokuwa makini Anaemia inaninyemelea na kingine ni kwamba nina Ujauzito.

Hapo ndio nilipochanganyikiwa zaidi. Maana Mimba ni ya mume wa mtu japo mwenye yupo willing kuilea ila anahofia mkewe akijua sitakuwa na amani. Pili kuitoa huku inaruhusiwa kisheria ila anahofia nitaharibikiwa Kisaikolojia.


Ukija kwetu mama hajafurahia hata kidogo kwani miezi mitatu iliyopita Dada yangu alipata mimba hali iliofikia kutibuana na mama na kuamua kuhama nyumbani kwenda kwa bwana wake kwa maana alikataa kuitoa.

Sababu ikiwa ameshatoa mimba mbili kabla hivyo kuitoa ya sasa hataki kabisa. Hivyo kahama in kufanya mama kuchanganyikiwa na kunionya Mimi nisije nikafanya kama Dada yangu.


Hapa sasa hivi niko na mawazo mpaka nawaza mabaya. Kuitoa naogopa nitakufa ama kitu kibaya kitatokea. Pia nawaza kama nikiitoa Dada yangu akizaa nitazidi kuumia maana mtoto wake atakuwa ukumbusho wa kwangu.

Pia naanza Chuo Fall (September ) so kusoma na Ujauzito sijui kama nitaweza. Kiufupi Dada yangu nipo kwenye dimbwi la mawazo.

Dada yangu kaniambia nitulie kwanza na kufikiri nini nataka. Lakini still naona wazimu unataka kunijia. Silali vizuri, mama yangu haongei na Mimi. Ndipo nimeona  nikwandikie wewe labda msaada wako wa mawazo  unaweza kunikwamua katika hili dimbwi la mawazo.

nitafurahi kusikia majibu yako either kwa email au blog yako.

Ahsante.


************


Dinah anasema: Marhaba mrembo, pole kwa yote ila ungekuwa karibu ningekusema mpaka Mimba itoke....(Natania)! Ila kwanini? Jamani kwanini at 22 unachanyanga maisha yako kizembe hivyo?!!!

As if mume wa mtu haikutosha ku-mess up maisha yako, ukaamua kujiachia kabisa na kushika Mimba!! Mama hakukufundisha namna ya kujikinga dhidi ya Mimba?

Haijalishi muonekano wake wala umri wake, Mume wa mtu ni Mume wa mtu tu hukupaswa kumpanulia Miguu...end OFF!....well limetokea, let's deal with it.

Wewe sio Dada yako so option ya kutoa Mimba achana nayo na mimi sikushauri uitoe kwasababu siamini katika kutoa Mimba bali naamini katika kuzuia kushika Mimba.

Kutokana na maelezo yako ni wazi kuwa ulikuwa unataka kuzaa na mume wa mtu alikuwa easy target, hivyo hakuna cha "tulia uangalie unachokitaka".....unamtaka mtoto then keep him/her....utamtunzaje? Ulipaswa kujiuliza kabla hujafanya Ngono bila Kinga.

Kuna uwezekano mkubwa huyo Boss Mume wa Mtu boyfriend wako ama akakuachisha kazi ili kulinda Ndoa yake, kama alivyokuonya kuwa Mkewe akijua utakiona cha MTEMA KUNI. Hilo moja.

Pili, akasema yupo willing kumtunza mtoto, hiyo sio guarantee ya yeye kufanya hivyo bila mkewe kujua hivyo anaweza kuamua kukuchunia tu ili aendelee kulea familia yake.

Muhimu ni wewe mwenyewe ku-sort things out na Mama yako ili angalau uwe na mahali pa kuishi kwa Muda na ujiandae kuwa a single mother (kwa UK is a bonus maana single mother wanamisaada kibao kifedha hihihihihi sorry).

Kama nia ipo na umekamia unaweza kabisa kusoma ukiwa Mjamzito(kama mimba haitosumbua), lakini kama hujiamini kuweza kufanya hivo basi badilisha mipango na uanze shule Next Sept utakapo kuwa umejifungua (Mungu akijaalia).


Sasa mrembo fanya hivi; Umekwisha haribu na matokeo unayo, hakuna haja ya kuwaza na kuwazua ufanye nini (too late), Simama kama mwanamke na angalia mipango ya Chuoni ili ubadilishe mwaka/tarehe ya kuanza.

Angalia Mkataba wako wa kazi unakulinda vipi au unalinda vipi Wajawazito na Wazazi (waliojifungua)....soma Sheria za Kazi za hapo ulipo ili ukifukuzwa kazi uweze ku-sue Boss wako(sio bf) kuwa kakufukuza kazi kwa sababu ya Ujauzito....sijui US sheria zilivyo ila nadhani hazitofautiani sana na za hapa (UK).


Usimwambie mtu yeyote kuhusu mipango yako ya ku-sue ikitokea umefukuzwa kazi(iwe between mimi Dinah na wewe).

Nimejaribu kuwa mpole ili nisikufanye ujione mpweke, lakini nina hasira sana na wewe, zaidi ya Mama yako.


Kua mwanamke Imara, Soma, piga kazi, lea mwanao.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Thursday

Nahisi Mume wangu ni Shoga...

Habari dada Dinah, hongera sana kwa kazi yako nzuri mno! nimekuwa nikisoma Blog yako siku zote na kuifurahia sana.


Leo nami naomba ushauri dada yangu.Mimi ni mama wa watoto watatu, nimefunga ndoa ya Kikatoliki mwaka wa 11 sasa.


Siku zote tumeishi vizuri na Mume wangu, makwaruzano ndani ya Ndoa hayakosekani ila siku hizi Mume wangu amebadilika sana kiasi cha kunifanya nipate mawazo mabaya juu yake.

Hakuwa na kawaida ya kujipulizia pafume ila ghafla ameanza kijipulizia hadi sehemu za siri!!Inaniogopesha sana.

Anatumia muda mwingi kwenye kioo! anavaa Macheni na Mapete makubwa makubwa! Nimejaribu kumuuliza sababu ya kufanya hivyo kawa mkali kama pilipili.


Dada yangu inawezekana akawa amejitumbukiza kwenye masuala ya Ushoga?


Na mwanaume akiwa Shoga anaweza ngonoka na Mkewe kama kawaida? nifanyeje kukomesha tabia hii ambayo inaninyima raha katika Ndoa yangu?


Pole kwa maswali marefu naomba unisaidie dada-Asante(tafadhali hifadhi jina langu).

**********

Dinah anasema: Habari ni njema, ahsante sana kwa ushirikiano.


Ulivyo-panic umenifanya nicheke ghafla!....Miaka 11 ni mingi kiasi. Je mnampeana attention ya kutosha kama wapenzi au mnamchukuliana kama Wazazi tu?

Mumeo ana umri gani kwani? Maana kuna baadhi ya wanaume wakifikia umri fulani 49+ huwa wanabadilika ghafla.

Kuna Makala moja ya Uchunguzi nilisoma mwaka jana wakazungumzia hilo na hitimisho lao lilikuwa sio Ushoga bali Mwanaume kuelekea kwenye "kikomo cha Hedhi" usishituke, sina neno lingine la kiswahili la "Menopause".

Mie nikabisha(as usual) kwa kusema kuwa mbona wanaume hawana Hedhi sasa "kikomo" kinaibukia wapi? Mpaka leo sijui na sikufuatilia tena.


Kuna umri fulani hufikia na watu kutamani au kutaka kujiamini tena kama walivyokuwa enzi zile kabla ya Ndoa na watoto, kwasababu walikuwa busy sana na majukumu ya "uzazi" sasa watoto wamekua na wao wanaamua kufurahia maisha yao.

Sasa mume wako kaamua kubadili Mtindo wa mavazi.....wengine huamua kufunga ndoa na mabinti wadogo, wengine kupunguza mwili, kurudi shule n.k ili kujiongozea hali ya kujiamini.

Mumeo ama hataki kuzeeka, kachoka kuonekana vilevile kwa miaka yote 11 au ame-miss attention aliyokuwa akiipata alipokuwa Kijana hivyo akivaa anavyovaa anazipata au alitegemea kupata....mf: wewe mwenyewe unampa attention japo sio nzuri (aliyotegemea ndio maana akawa mkali).


Nadhani ni vema kubadilisha uulizaji wako....badala ya kumkalipia, kumuita Shoga au kumkataza asivae anavyovaa kwavile anaonekana Fala. Pia ni vema kujipanga kwenye suala la Mavazi ambayo unadhani yatampa akitakacho lakini atapendeza na kutavutia kuliko sasa.

...mwambie kwa upole na kujali, "Mume wangu najua unapenda kuvaa unavyovaa, lakini uvaaji huo wala hauendani na wewe,.....jaribu kuvaa hivi".....onyesha mavazi ambayo unadhani yatamfanya Mumeo aonekane kijana na kuvutia na sio "Pimp"....Mvishe Mumeo.

Ushoga sio kitu/tabia za kujiingiza bali ni "ujinsia" ambao mtu anakuwa nao....kwamba anavutiwa na watu wa jinsia yake kingono/mapenzi.

Inategemea na jamii inayomzunguuka au "utayari" wake kuishi kama Shoga....wengi huishia kuoa na kuzaa ili kuficha "Ujinsia"....nikijibu swali lako ni kuwa sio lazima Shoga ashindwe kufanya Ngono/Mapenzi na Mkewe.


Mashoga huwa hawavai kama ulivyoelezea, Pimps ndio huvaa hivyo. Suala la kujipulizia Manukato sio tatizo, katika kujipenda na kujijali kunukia nayo imo!


Ila kujipulizia Manukato sirini mwambie aache kwani Manukato yana "alcohol" ambayo hukausha ngozi na hata kusabbaisha muwasho na maamukizi mengine ya Ngozi kutokana na joto la mahali huko(sirini).


Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Tuesday

Sitaki kufika 30yrs nikiwa Bikira

Habari dada, Natumaini hujambo. Naomba ushauri wako kwa hili. Mimi ni msichana soon will turn 26. Nilikua na bf lakini tuliachana miaka 2 iliyopita na tulikaa kwa miezi ka 6 tu kabla hajaniacha.


Alikuja niambia baada ya muda bila mimi kumuuliza sababu ya kuachana na mimi ni alirudiana na Ex wake.

Kipindi tulichokua pamoja kama couple hatukufanya sex wala hakuniforce kufanya coz alikua anajua sijawahi kufanya sex before.


Baadaa breakup tukawa friends tu though deep down ile breakup iliniuma sana na ilichukua muda kumove on, karibu mwaka.

Mwaka huu tumekutana kwenye course fulani tunafanya wote, dada naona bado yupo moyoni.

Tatizo niliambiwa ni player lakini nampenda bado, naona awe tu my first guy kwenye sex coz sioni mwanaume mwingine wa kufanya nae na umri ndio hivyo unakwenda na sina boyfriend.


Sijatokea kumpenda mtu tena baada yake nisije nikafika 30's na bikira yangu. Naweza sema he is my first love coz sijawahi kumpenda mwanaume yeyote na mapungufu yake kama yeye!


*******

Dinah anasema: Mie sijambo, ahsante kwa ushirikiano.

Sasa Mrembo, kama umeamua na unataka (unaona) awe tu wa kwanza kwako, mimi nishauri nini hapo wajameni? Ila kama unataka niseme on that here we go;


Yack! Katoka kwa mtu kaja kwako, karudi kule tena yamemshinda (au bado anae) bila kinyaa wala second thought upo radhi kujiachia kwake for the name of first love? what is the 1st/childhood love do to people's lives? NOTHING so it is NOT that important/special. Mwanamke labda hupendi kuwa Bkira basi angalau jithamini.


Sio kwamba hakuna mtu uliempenda kama yeye bali hukujipa muda wa kumsahau huyo Ex au hukutoa nafasi ili kupendwa/kupenda kwa sababu ya kushikilia hisia zako kwa mtu ambae alikuwa bado na hisia kwa Ex wake.


Kitendo cha yeye kutotaka Ngono na wewe kwa miezi Sita haina maana kuwa alikupenda, was more to do with his feelings to his Ex.....alimheshimu Ex wake na sio wewe, nadhani alikutumia kupitisha muda au kumtia Wive Ex aliemrudia.


Usikate tamaa na kujishusha kiasi hicho! Hata kama hutaki kuwa Bikira by the age of 30 na hakuna mwanaume "msafi" umpendae basi bora u-pretend not to be Virgin (in your Head) uendelee na maisha mpaka utakapopenda na kupendwa ila sio huyo.


Usikimbilie kujitoa kingono kwa kuhofia kufika miaka 30 na Bikira, fanya ngono kwa sababu unataka na upo tayari, Likitokea la kutokea ni your responsibility.


Mwanamke usikate tamaa na kujitoa utu wako kwa huyo Ex, toka nje ya mzunguuko wako eeh! Tanzania kubwa sana na inawanaume wengi tu ambao hawana Mizigo ya madeni ya hisia Exes (wasafi).


Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Sikati Ngono, lakini nampenda.

Shikamoo da dinah, pole na kazi. Nashukuru kwa msaada wako katika masuala haya.

Kwa kuanza mimi ni binti wa miaka 21 sijawahi fanya mapenzi kabisa hadi hivi sasa nipo Chuo Kikuu mwaka wa kwanza.

Nina mpenzi wangu ambaye anamiaka 27 na anampango wa kuoa miaka miwili ijayo kuanzia sasa! Anakazi nzuri na kimaisha kajiweka vizuri.


Tokea kuingia katika Uhusiano wetu ni miezi minne(4) sasa tunachat ila kuonana ni mara chache siku za weekends kutokana na kubanwa na shughuli zake.
 


Sasa imefikia wakati anaomba tufanye Mapenzi, ameshaniomba mara nyingi na kunihimiza nikamuambia sipo tayari kuanza mapenzi ningependa tusubiri.


Da dinah kijana huyu tumesha kiss mara kadhaa na kiukweli nimempenda ila naogopa kuanza ngono, halafu isitoshe sijui kwao, ndugu ,wala rafiki zake yaani tunajuana sisi wawili tu (mimi na yeye).
   

Kwa kuwa tu muazi kwako da dinah ni kwamba naogopa kuanza mapenzi nikiwa bado Mwanafunzi na familia inanisomesha, Pili naogopa kupoteza Bikra au Usichana wangu kwake.


Tatu naogopa maambukizi na Mimba zisizotarajiwa. Sijawahi kuumizwa katika mapenzi na ninavyohisi anavyo nga'ngania kufanya hivyo na mimi je tukifanya na akiniacha na kuingia mitini?


Da dinah naomba ushauri wako maanake kijana huyu hasikii wala haelewi. Na je ni sahihi kweli kufanya hayo mapenzi mkiwa bado bf na gf na je ni wakati gani bora wa kuanza hivo???

Ntashukuru kwa Your help.


Dinah anasema: Marhaba Mrembo, shukurani kwa Ushirikiano.


Kabla ya yote, Kazi yake nzuri na kujijenga kwake kimaisha hakukuhusu wewe (kunamhusu yeye na aliyemsomesha labda na ndugu zake)....usifanye uamuzi kwa ku-base kwenye material thingizi*


Nae kama ni mwizi vile eti! Atafunga Ndoa in Two years time....kukuoa wewe (ambaye huijui familia yake na wala haijui yako) au tayari anamchumba Kibindoni?


Maana kujipangia kufunga ndoa ndani ya miaka Miwili wakati sasa ni Mwezi wa Saba ni ama anakupa matumaini in a "ushawishi" way ili ukubali kumpa Ngono ukitarajia kuolewa au tayari anamchumba/mtu anaetarajia kumuoa.

Halafu mrembo unanichanganya, unasababu nyingi na za Msingi na Msimamo mzuri wa kutotaka Ngono sasa (unahitaji muda) ila sielewi kwanini unasema unampenda lakini hutaki usichana wako upotezwe na yeye?!!

Uhusiano wenu hauna miezi Minne kwasababu mnakutana mwisho wa Wiki(Weekends) tu....ikiwa kwa mwezi mnakutana mara Nane kwa mfano! Hiyo inafanya uhusiano wenu kuwa na Siku 32 which ni less than miezi 2!

Ikiwa umemuambia kuwa haupo tayari kwa Ngono lakini anashindwa kukuelewa na kuendelea kulazimisha ni wazi kuwa hakufai au "hamfaani"....yeye anataka uhusiano wenye kuhusisha Ngono na wewe hutaki kupoteza Usichana wako kwake.

Au labda ni vema kumwambia ukweli kuwa hutaki yeye awe mpenzi wako wa kwanza Kingono, hii itawapa nafasi nyote wawili kufanya mtakayo kwa uhuru.

Wakati mwingine Mapenzi ni bahati nasibu, ukiamua kujiingiza kwenye haya mambo hutakiwi kutegemea sana utakaeanza nae ndio atakae kuwa Mumeo.


Kama umeamua kujihusisha na Mapenzi ni wazi Ngono itahusika at some point lakini ili usiwe disappointed ni vema kuchukulia kila siku kama inavyokuja na kufurahia Maisha yako kama mwanamke.

Mimi siwezi kujua kama akipata Ngono ataingia mtini au Mtafunga Ndoa. Maumivu ya Mapenzi hayaepukiki, inawezekana Mwanaume asikuache lakini wewe ukagundua kuwa hakufai na hivyo ukaamua kuachana nae....bado utaumia, haijalishi unaacha au kuachwa, mapenzi yanauma sawa.

Kutokana na Maisha yalivyo hivi sasa, kwamba wengi tunabaki shule kwa Muda mrefu na tuna "uhuru" wa kuchagua tuwapendao wengi tunaanza Ngono tukiwa kama Bf na Gf....ila sio lazima, inategemea na Msimamo na Uamuzi wako binafsi.


Suala la Mimba, Maambukizi na hofu nyingine zote ulizonieleza ambazo hazihusu "uhusiano" nadhani ni vema ukizungumza na Mama yako kwa uwazi, yeye yupo kwa ajili hiyo.


Kamwe usifanye jambo kwa ajili ya kusukumwa au kulazimishwa, wewe ndio mwenye Mamlaka na Mwili wako na si mtu mwingine yeyote hivyo kama hutaki huo ndio Uamuzi wa mwisho!


Kama anakupenda kweli basi ataheshimu Uamuzi na Msimamo wako na kusubiri mpaka utakapokuwa tayari.....mmh lakini umesema hutaki upoteze Bikira kwake....Mwache aende zake basi!

Muda mzuri wa kuanza Ngono:

Miaka 21 nadhani ni umri mzuri kwavile mwili wako kama mwanamke unakuwa ume-settle lakini kama unaweza kusubiri mpaka 28 pia sio mbaya...ni uamuzi na msimamo wako. Usijitunze kwa ajili ya mwanaume bali kwa ajili yako wewe mwenyewe.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Sunday

Moyo umekubali, Akili imegoma!

Shikamoo dada, pole na majukumu na ufanisi mkubwa wa kazi unayofanya. Dada dinah problem yangu naileta kwako nafikiri itakuwa solved.











Ni muda sasa tangu niachane na ex wangu na bado sijapata mahusiano mengine, shida ni kuwa muda mwingine nikiwa nimetulia nashangaa namkumbuka tu yeye.









Kuna wakati hadi jina lake nalitaja hali ambayo sipendi na ninataka nisiwe nayo kwani nishakubali matokeo kwamba hanifaii  ila naona akili yangu kama imestuck kwake.









Sitaki memory yoyote ije kichwani kwangu kuhusu yeye, nifanyeje? Thanks inadvance dada.





***********





Dinah anasema: Marhaba mrembo, nashukuru kwa ushirikiano.







Inategemea ulimpenda kiasi gani? Uhusiano wenu ulikuwa wa Muda gani? na mliachana katika Mazingira gani?









Ni hali ya kawaida kwani ni mtu uliekuwa nae karibu na pengine ulitumia muda wako mwingi kuwa nae. Itakuchukua muda ili kumsahau yeye kama Mtu na kusahau kile mlichokuwa nacho(Uhusiano).









Kuacha au kuachwa kote kunauma sawa kwani hivyo haijalishi kama umekubali kuwa hakufai na kumuacha au yeye kakuacha wewe....vyovyote vile Hisia(Moyo) na Akili vinahusika.











Maumivu ya Mapenzi hayana ujasiri....Unahitaji kujipa muda wa "kufanya Msiba wa Uhusiano wako" na kuzika yote yaliyopita ili uweze kusonga mbele ukiwa huru na mwenye furaha. (Rejea majibu yangu kwenye Post niliyoelezea namna ya kusonga mbele baada ya Ex Wiki 2 zilizopita).











Kama tayari Mwaka umepita tangu muachane basi jipe tena Miezi Sita au hata miaka mingine miwili ili kupona kabisa.









Pamoja na kujipa Muda, uponaji wako unategemea zaidi juhudi zako za kutaka kusahau yaliyopita ili uweze kuendelea na maisha yako kirahisi.











Jitahidi kutumia muda wako mwingi na watu waliokaribu na wewe na kufanya activities za pamoja, kucheka na kufurahi pamoja.











Hakikisha siku yako inakuwa imejaa shughuli ili kuepuka kukaa peke yako na ukifika nyumbani unakuwa hoi (hupati muda wa kumuwaza Ex).









Jipe muda na ifunze akili yako "kuzima" au "ku-switch" mawazo ya Ex kwenda kwenye kitu kingine.





Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Monday

Ananipenda au ananizingua?

Habari dada,
pole na hongera kwa kazi ya kuelimisha jamii. Mimi ni msichana na nipo kwenye uhusuano na mpenzi wangu kwa
miaka miwili sasa.

Mwanzo wa uhusiano tuliishi vizuri japo tulikuwa mbali mbali kwa muda wa mwaka mmoja kwa sababu yeye alikuwa anaishi Dar (akiwa
Chuoni) na mimi nilikuwa Singida (Shuleni-form6).

Mwaka jana mwishoni nilijiunga na Chuo fulani hapo Dar ndipo tukawa karibu. Miezi ya kwanza
alinijali kwa kila kitu lakini sasa hivi kabadilika yaani anaweza kukaa zaidi ya Wiki 2 asinitafute kwa Simu.



Kila nikimpigia Simu anakata na hata
Meseji hajibu, yale mambo aliyokuwa ananifanyia kama kunitembelea
ninapokaa hayapo tena. Siku akijisikia kunipigia simu haniulizi kama mimi
mzima au la! Ila anataka tukutane kwa ajili ya sex tu.

Nikimuuliza kwanini hapokei Simu zangu anasema eti nisimuwaze sana kwasababu yuko busy
na maisha yake. Hivi sasa wiki 3 zimepita hajanitafuta, sasa nashindwa
kuelewa nipo kwenye mapenzi ya aina gani?

Nisaidie dada yangu.


************


Dinah anasema: Habari ni njema tu, ahsante! Shukurani kwa Ushirikiano.

Sijui mlimudu vipi Uhusiano wenu kipindi cha mwaka mmoja mlipokuwa mnaishi Mikoa tofauti, ila nahisi umbali huo ndio uliomaliza Uhusiano wenu.


Mlichokuwa nacho pale ulipohamia Dar na kuwa karibu ni "Mazoea" na kufidia kipindi mlichokosana huku mwenzio akijaribu kuangalia kama hisia ni zilezile au hazipo tena.....wewe ukapata matumaini tofauti na kilichokuwa kichwani mwake.


Sioni Uhusiano hapo ila Jamaa anakutumia kwa Ngono pale anapojisikia, na wewe unakubali ukidhani unaomsogeza karibu kama mpenzi.

Mpaka kafikia mahali anakuambia usimuwaze sana kwani yupo busy na maisha yake...ujue haupo kwenye mipango yake na kwake wewe ni "kipoozeo" kwamba anakutafuta akibanwa na Nyege tu.

Anafanya hivyo kwasababu hayupo tayari kuwa na Uhusiano mpya na hataki kuwa na Uhusiano na wewe lakini ni rahisi kufanya Ngono na wewe anaekujua na amekuzoea kuliko mwanamke mwingine mpya....sijui unanielewa Mrembo?!!


Sasa hebu Mchunie, kwamba usimtafute na usipokee simu zake wala kujibu Meseji(ikiwezekana poteza mawasiliano yake).


Kuwa Imara kama mwanamke na anza maisha mapya bila yeye. Wanaume wapo wengi tu, muda ukifika utakutana na mwingine mwema.


Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Sunday

Tofauti ya Dini yaweza kuwa kikwazo

shikamoo da Dinah,
pole na hongera kwa majukumu. Nimerudi tena baada ya
kunufaika na ushauri wako wa kwanza. Naomba nsaidie katika hili.


Hivi karibuni nimekutana na mwanaume ambaye ni 10 yrs older than me na
mimi ni 22, ana mtoto mmoja. Nikamuuliza kuhusu mama wa mtoto, akanambia ilishindikana kumuoa kwasababu za kiukoo tu so mpaka sasa imeshindikana.

Sasa he is too fast! kantongoza tu next week anataka nimpe penzi eti
atajisikia vizuri na atakuwa na uhakika na mimi. Nikajiuliza kwani sex
ndio kipimo cha upendo? Sababu kuna vijamaa vishawahi kunambia hivo
nikavitolea nje lakini mpaka sasa vinanisumbua.


Sasa kuna mwanaume ambaye nampenda ila ni Islamic na mimi Christian na familia yangu
haitaki kusikia habari za mahusiano kama hayo.


Nikionana na huyu jamaa
baada ya salam automatically kifuatacho ni romance but bila sex, zaidi
ya nakupenda hajawahi nambia chochote kuhusu mimi na yeye.


Nishawahi kumuuliza akanambia a better future awaits, hakusema kingine tena mpaka leo na sasa ni zaidi ya mwaka. Kiukweli nampenda Dini inanipa shida.


majukumu mema!


**********


Dinah anasema: Marhabaa mrembo, shukurani kwa ushirikiano na Karibu tena.


Huyo mwenye Mtoto ambae sababu za kiukoo ni Muhimu kuliko hisia za mwenzie hafai kabisa! Bora hata angesema "things didn't work out".....kwani kuzaa na mtu sio Tiketi ya kufunga Ndoa.....Mwache AENDE.

Dini: Mrembo sote tumelelewa katika Mzingira ya Dini/Imani fulani lakini sio lazima kufuata Dini/Imani hizo bali unachagua kufuata na kuishi maisha ya kufuata Dini/Imani husika.

Suala la Dini ya familia yako lisikusumbue kwenye "stage" hii (liache) muhimu ni hisia zako kwa sasa. Tukisha pata commitment na kujua kama kuna "future" na Muislam then tutatafuta namna ya kushauriana(kutegemeana na uamuzi wako sio Wazazi wala huyo mkaka).

Pamoja na kuwa Muislam analeta matumaini ila nae haeleweki (kutokana na maelezo yako), ni vema kwamba hasumbui kuhusu Ngono, anakupenda na wewe unampenda, Chemistry yenu ni MOTO, nakubaliana nae mambo mazuri hayataki haraka....lakini nisichoelewa ni kutokuonyesha commitment kwako.



Nijuavyo mimi kwa Muislam wa kweli(alieamua kufuata Imani kwa kuipenda, sio kwa kurithi), Uislamu wa mwanamke ni muhimu zaidi kuliko hisia za kimapenzi, na uislamu huo usiwe wa kulazimishwa.....mf; wewe uamue kuwa Muislamu sababu ya kumfurahisha au Ndoa bali kwa faida yako na Moyo wako.

Mwaka ni muda mzuri wa kuhoji "uhusiano" wenu ambao unaonyesha kuwa sio rasmi.

Sio mbaya kama utamuuliza....tumuite Mahmood sawa?!! "Mahmood tuna chemistry nzuri, tunaelewana na ninakupenda, ila sina uhakika kama tupo kwenye uhusiano au tunapotezeana muda".

Akijibu ki-hasi kwamba haonyeshi ku-commit na kuwa na uhusiano aka exclusive lakini anataka muendelee na mlichonacho....Muulize "unadhani tutaendelea hivi mpaka lini? na je hiki tulichonacho kwa mwaka sasa ni nini hasa?"

Jibu lake hapo ndio litakufanya ufanye uamuzi wa kuachana nae au kuendelea na kufurahia hicho mlichonacho bila kuwa na haraka wala Matumaini ya "siku tutafunga ndoa"....enjoy yourself as a woman....ikitokea Ndoa safi, isipotokea Ndoa poa vilevile.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Thursday

Nakuwa Moody na Mkali kwa Mpenzi...

Naomba ushauri kuhusu haya mambo nifanyaje ili niweze kuyabadilisha
kwasababu mpenzi wangu hajaridhishwa nayo.


Ni kwamba huwana change mood
ghafla na pia huwa nakuwa mkali asa sijajua nifanyaje nahitaji msaada
wenu.

***************

Dinah akauliza: G (Sio jina kamili),

Nahitaji maelezo zaidi ya hayo ili iwe rahisi kwangu kujua kama unahitaji Ushauri wa Kitibabu au Ushauri wa Kibinaadam.

Unabadili Mood ghafla na unakuwa mkali wakati gani hasa?


Unadhani ni kitu gani kinapelekea wewe kuhisi hasira, na kubadilisha mood huko hukutokea wakati gani?....nini hasa kina- triger?

***********

G(Si jina kamili) akajibu: ninapoona hali ya utofauti kwa mpenzi wangu au nikiona sms za mwaume mwingne au ataponijibu tofauti tu nabadilika mood na kuwa na hasira.

Dinah anasema: Ahsante kwa ushirikiano.

Kutokana na maelezo yako inaonyesha wote mnamatatizo ya kitabia na wote mnapaswa kujirekebisha na kuelewana ili kila mmoja wenu aepuke "kumtuma" mwenzie kuwa au kufanya afanyavyo.


Kitu gani hasa kinamfanya mpenzi wako afanye mawasiliano na wanaume wengine ambayo yanakukera? Umewahi kujiuliza?


Huenda humpatii mahitaji kihisia, kimapenzi au labda hakuna commitment anayoitaka na hivyo ameacha "mlango" wazi ili kuona kwa watu wengine kuna offer nini?.

Kumbuka mahitaji hayo yanaweza kupatikana kutoka kwa mwanaume mwingine via sms au njia nyingine ya Mawasiliano, na hufikia mahali mtu anahisi kupenda/vutiwa hali inayoweza kusababisha Usaliti kimapenzi.

Hasira au kubadilisha Mood kwako kunasababishwa na vitendo(tabia) ya mpenzi wako, sina uhakika kama anajua kuwa mawasiliano yake na wanaume wengine au majibu yake kwako ndio sababu kuu ya wewe kukasirika au kuwa na Mood mbaya.


Kwenye uhusiano wowote wenye matatizo ni muhimu kujua chanzo cha tatizo na kujaribu kurekebisha kwa kumshirikisha mwenza wako kabla hujaomba ushauri nje ya Uhusiano wenu.


Umesema mpenzio haridhishwi na tabia yako ya kuwa Moody na Hasira, ni wazi hajui sababu ni ipi hasa inapelekea wewe kuwa hivyo.


Sasa rudi kwake na mkae chini na kuzungumzia issue yenu kwa upendo bila kubishana wala kulaumiana na wote kwa pamoja mkubaline kufanya mabadiliko.


Maisha ya mahusiano ya kimapenzi ni kama Bustani ya Maua, ukitaka Maua yaonekane na afya na yaendelee kunawiri basi utahakikisha unamwagilia maji na kuweka Mbolea kila inapohitajika.

Kila siku unayatazama mauwa yako unafurahi kutokana na kunawiri kwake, unasogea karibu ili kuona kama kuna Gugu (majani ambayo sio sehemu ya maua yako)....unatafuta chanzo chake na kukiteketeza ili Bustani ya Maua yako isiharibike.


Nadhani umenielewa,

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Pages