Monday

Uhusiano una Mwaka, Ex wa Mpenzi amejifungua mtoto wake mwaka huu! Nifanyaje?

"Habari dada Dinah pole na majukumu ya kila siku,
mimi ni dada wa miaka 27 nina mchumba ana miaka 35 tumekuwa pamoja kwa muda
wa mwaka na miezi mitatu hivi. Nampenda sana mchumba wangu na yeye naamini ananipenda.

Tatizo limejitokeza hivi karibuni; ni kwamba kabla ya kuwa na mimi alikuwa na mwanamke ambaye alinishanitaarifu kuwa aliachana nae ndio maana mimi nikakubali na tukawa wapenzi. Sasa ananiambia kuwa huyo dada ana mtoto wake tena kamzaa this year, ina maana
hiyo mimba kapata wakati ndio tunaanza uhusiano wetu.

Sijasikia kwa mtu mwingine zaidi yake amesema eti nikisikia kwa watu na yeye
hajaniambia nitamuacha, amesema yeye ananipenda mimi na anataka niwe mke wake. Hapa nilipo nimechanganyikiwa mbaya zaidi badonampenda sana huyu kaka na sijui nifanyaje!

Yaani mpaka sasa sijamuelewa ananidanganya au ananipenda kiukweli, mwenyewe ananiomba msamaha sana kuhusiana na tukio la kuzaa na ex wake.

NAOMBA USHAURI WENU, nifanye nini?

Saturday

Nifanye nini ili mimi na mpenzi tukojoe pamoja?-Ushauri

"Hey Dinah pole sana kwa shughuli za mchana kutwa, pili asante sana kwa kutufundisha wenzangu na mimi ambao tumeanza malavidavi kabla ya kufundishwa Unyagoni. Wengine hatuna Mila za kuingizwa Unyangoni basi tuna taabu.

Mimi ni mwanamke wa miaka 29 nimeanza kungonoka nikiwa na miaka 26 na mwanaume wa kwanza ambaye ndio alinitoa Usichana wangu. Tulikuwa tunakutana kwa mwezi mara 2 hivyo tulikuwa hatuna muda wa kungoana vizuri.

Mwanaume huyu alikuwa anajipendelea yeye hana Commucation na mimi, alikuwa anataka anavyotaka yeye, baada ya muda fulani tukaachana. Sasa hivi niko na mwanaume mwingine ambae kwa bahati nina muda mwingi tu wa kungonoka naye ila tatizo langu kubwa mimi sijawahi hata siku moja kupata raha ya kungonoka.

Nasemea ile raha kama ninavyosikia kwa wenzangu au kwako unavyoandika ushauri kuwa unaweza mkakojoa kwa pamoja sijawahi hata siku moja! Mimi kukojoa kwangu mpaka mpenzi wangu anichezee K tena kwa muda mwingi sana mpaka namuonea huruma.

Basi kwa vile nadhania kuwa namchosha inabidi nimwambie tayari nimefika kumbe bado. Nashukuru sana mwanaume wa watu hapendi niondoke bila mimi kukojoa.Naomba ushauri nifanye nini na mimi niwe napata raha kama wenzangu?

Pili, nifanye nini ili na mimi niweze kumaliza pamoja na mwenzangu?"

Sunday

Nifanye nini ili nami nipate raha na Utamu wa Kungonoka?

"Hey Dinah pole sana ka shughuli na asante kwa kutufundisha wenzangu na mie ambao tumeanza malavidavi kabla ya kufundishwa Unyagoni, maana wengine hatuna Mila za kuingizwa unyagoni basi tuna tabu.

Mimi ni mwanamke wa miaka 29 na nimeanza kujihusisha na masuala ya kimapenzi na ngono na mwanaume wa kwanza nikiwa na miaka 26, tulikuwa tunakutana mara mbili kwa mwezi na hivyo hatukuwa na muda wa kungonoana vizuri. Mwanaume huyu alikuwa anajipendelea yeye kwani hakuwa na communication na mimi alikuwa anataka anavyotaka yeye.

Sasa hivi nimepata mwanaume mwingine na muda wa kuwa nae na kufanya mapenzi ni mwingi zaidi kuliko awali ila tatizo langu kubwa ni kuwa sijawahi hata siku moja kusikia raha ya kufanya tendo kama ninavyosikiwa kutoka kwa wenzangu au kwako Dinah hasa pale mahali ulipoandika kuwa "mnaweza kukojoa pamoja".

Kukojoa kwangu ni mpaka anichezee K kwa muda mrefu wakati mwingine huwa namuonea huruma kwani nahisi kama vile namchisha na hivyo naishia kumwambia "tayari nimefika" kumbe bado. Nashukuru Mkaka huyu najali na huwa hapendi kuacha mpaka ahakikishe nimekojoa ilandio hivyo tena.

Naomba ushauri kutoka kwenu kwenye haya mawili: (1)-Nifanye nini ili na mimi angalau nifurahie ngono kama wenzangu?

(2)-Niifanye nini ili niweze kumaliza na mwenzangu kwa wakati mmoja?

Asanteni.

Natafuta njia ya kushika na kubemba mimba-Nifanyeje?

"Dada Dinah, umri wangu ni miaka 33 miaka miwili tangu nimefunga ndoa nilibeba mimba lakini kwa bahati mbaya iliyoka baada ya miezi mitatu tu, mpaka leo sijashika tena mimba. Nimeenda Hospitali zaidi ya mara moja kwa ajili ya uchunguzi lakini nimeambiwa sina tatizo lolote.

Vilevile nimejaribu kutumia dawa za Kienyeji lakini sijafanikiwa kushika mimba mpaka leo, je kuna njia nyingine yeyote inayoweza kunisaidia kushika mimba tena bila kunywa dawa za Clomid? Naomba mnisaidie....

Nimefurahi sana kupata email yako.

Asante."

Mume Mzinzi lakini hataki kunipa Talaka, nifanyaje?

"Habari dada Dinah pole na majukumu, naomba mnisaidie niko njia panda, mimi niliolewa miaka mitatu ilipota histori fupi ya mimi na huyu mume dada Dinah ni hivi: Tulikuwa wapenzi toka tuko shule, baada ya kumaliza mwenzangu akapata kazi kwenye hotel kubwa tu hapa dar.

Wakati huo mie nikawa niko field Airport tukawa tunaishi pamoja kam amume na mke, visa vikaanzia hapo. Mwanaume akawa anapigiwa siku na wanawaka mara akanza kuwa anarudi nyumbani asubuhi. Ikafikia hatua ya kunifukuza pale na kuanza kubadilisha wanawake dada dinah.

Vitu vilivyoko pale nyumbani vingi tulishirikiana kama wapenzi kwakweli niliumia sana kwasababu nilikuwa nampenda. Basi tulitengana nikarudi kwetu na nikapata ajira baadaya Field. Baada ya miezi kama sita hivi akaja kunibembeleza huku akiniahidi hatarudia tene na amekuja kwa ajili ya kunioa.

Nilikubali dada, tukafunga ndoa na tukabahatika kupata mtoto wa kike, ndungu zangu wakanisaidia kunishughulikia tukapata nyumba ya NHC naye pia alitoa pesa zake ila hati zote ziliandikwa jina langu.

Kama ilivyokuwa kabla ya ndoa akaanza visa tena, sasa akawa ananitukana matusi makubwa mbele ya h/girl mpaka majirani wanasikia mara aniambie "wewe mwanamke gani mie sinimekusaidia tu kukuoa", mara anipige, anarudi Alfajiri akiwa amelewa.

Nimejaribu kumwambia nataka Talaka yangu hataki kunipa, sasa nilichoamua mwezi wa tatu sasa sitaki kabisa kushare nae love. Kinachonikera kwasasa ni kwanini hataki kunipa Talaka yangu aendelee kufanya mambo yake!

Naombeni mnishauri, nitaipataje Talaka yangu kutoka kwa huyu mume ili na mimi niwe huru?
Asanteni.

Saturday

Je kuna namna ya kuamua jinsia ya mtoto?-Msaada

"Hi Dada D,
Naomba ushauri kutoka kwa mtu yeyote mwenye utaalam wa kujua jinsi ya kuamua kupata mtoto wa kiume au wa kike. Cha muhimu ni kujua wakati gani nikikutana na mke wangu atakuwa na mimba ya mtoto wa kiume au wa kike?

Asanteni.

Pages