Thursday

U've made it! Heri ya mwaka Mpya!!

Hongera kwa kumaliza Mwongo (Decade) na Kila la kheri unapokwenda kuanza mwingine. Nakutakia afya njema, maisha ya Ndoa/Kimapenzi mazuri, marefu na yenye mafanikio zaidi ya 2000-2009.
Akupendae na kukujali,
Dinah.Xxx

Monday

Kaniacha, lakini bado ananijali...je Kukeketwa inaweza kuwa kikwazo?-Ushauri

"Kwanza napenda kukupa pole na kazi ambayo unatuelimisha, nilikuwa sifahamu mambo mengi lakini kupitia kwenye blog yako nimejifunza vitu vingi sana.

Naitwa Jack ninaishi Tanga, nina umri wa miaka 25. Tatizo langu ni kwamba nimekeketwa tangu nikiwa mdogo sana hata kujitambua ilikuwa bado kwani nimekuja kutambua nikiwa mkubwa kuwa nimefanyiwa kitu hicho.

Nilipomuuliza Mama kwa nini umenifanyia hivi? akasema nilikuwa nasumbuliwa na ugonjwa wa lawalwa nikawa sina jinsi bali kukubali jibu la mama. Baada ya kukua ndio naona umuhimu wa kuwa kama wenzangu ambao hawajakeketwa.

Nilikuwa na boyfriend nikamueleza suala hili akakubaliana nami nikawa naenjoy pale napo fanya mapenzi aliweza kunifikisha kileleni kama kawaida tulidumu na Mchumba kwa miaka 3 na nusu lakini baada ya kwenda Dar es Salaam kwa masomo Mpenzi wangu huyo akanichiti na msichana mwingine na hivyo aliniacha mwaka huu mwanzoni.


Mimi bado nampenda sana ila yeye hakutaka kurudiana nami tena, japokuwa alikuwa amekwisha achana na yule dada aliyenichiti nae muda mrefu lakini hakutaka kuwa na mimi. Sijui kama ana msichana mwingine ama la. Mpenzi huyo ni mwanaume pekee ambaye nilimwambia kuwa nimekeketwa!

Hivi sasa nimepata boyfriend mwingine lakini bado hatujafanya mapenzi na ninaogopa kumwambia kama mie nimekeketwa sasa nitafanyaje ili ajue?

Mtu ambaye aliyekuwa ananifikisha kileleni ni mwanaume wangu huyo niliyekuwa nae miaka 3 iliyopita na ndie alikuwa ananipa raha kuliko niliyekuwa nae mwanzo kabla ya yeye. Sisikii kabisa hamu ya kufanya mapenzi kwa sasa nilikuwa nampenda sana mpenzi wangu wa zamani.

Nimejaribu kumuomba turudiane hataki, ila kama nina tatizo hunisaidia pia kama ninashida labda ya fedha huwa ananitumia, na nilipokuja kusoma alikuwa ananisomesha yeye mwenyewe, Da Dinah kila nikijaribu kuwa na boyfriend mwingine nashindwa nisaidie Dada yangu?
samahani kwa email ndefu utanisahihisha pale nilipo kosea?"

Dinah anasema:Asante sana kwa ushirikiano, ningependa akina dada wote waliokeketwa wasijisikie au kuchukulia kuwa wao ni waathirika(Victims) kwani inaweza kuchangia (Kisaikolojia) kwa kiasi kikubwa kutofurahia ngono.

Natambua tendo lenyewe ni la kikatili hasa ukizingatia kuwa binti unafanyiwa hivyo ukiwa ktk umri mdogo, lakini kwa vile limekwisha tokea hauna budi kukubali maumbile yako na kusonga mbele na maisha yako.

Mimi binafsi sidhani kama kukeketwa ni tatizo kwani mwanamke kuwa au kukosa kisimi hamfanyi mwanaume ashindwe kukupenda na hata kufurahia ngono, Kisimi ni kwa ajili yako wewe mwanamke na si mwanaume. Hata kama ni suala la kushukiwa chini bado kuna maeneo mengine anaweza kufanyia kazi na wewe ukafurahia kama ifuatavyo......

Kwa bahati nzuri wanawake tumeumbwa na maeneo mengi ya kusikilizia nakupata utamu, hii inategemea na utundu wako lakini mimi binafsi nimegundua maeneo sita tangu nimeanza kushiriki uhusiano wa kingono.

Maeneo 5 tayari nimekwisha changia hapa na Radioni ili wanawake wengine waweze kufurahia na wanaume kuyafahamu ili waweze kuyafanyia kazi vemana hilo eneo la sita nimegundua miezi michache iliyopita (nitachangia siku zijazo ili na wengine mkafurahie).

Uhusiano ule na wasasa: Kwavile uliamini tangu mwanzo kuwa kukeketwa ni jambo la ajabu (huenda ni kutokana na linavyolaaniwa kupitia vyombo vya Habari ) basi ilijengeka akilini mwako kuwa mwanaume atakae kuwa na wewe ukamwambia kuwa umekeketwa na akakukubali basi ndio atakuwa THE ONE.

Ulimuamini na kumpenda mpenzi wa zamani ambae inawezekana kabisa kuwa ndio alikuwa mwanaume wa kwanza kumpenda, kumuamini, kutoa "siri" yako na kufanya nae ngono, kutokana na kuhisi kukubalika kwa Jamaa huyo Kisaikolojia ukaamini kuwa hakutokuwa na mtu mwingine atakaekuparaha au hata kukupenda na kukubali japokuwa huna "Vikorombwezo" huko nyetini.

Sote tumepitia huko kwa mpenzi wa kwanza maishani, ni kweli kwa wanawake wengu huwa sio rahisi kumsahau yeye kama mtu, kusahau uhusiano ulivyokuwa na kutompenda mtu mwingine kama ulivyompenda yeye. Hakika unaweza penda mtu zaidi yake lakini mapenzi hayatokuwa enjoyable kama yale ya mtu wa kwanza), hii haina maana kuwa umg'ang'anie tu kwa vile ni 1st love hata kama yeye hataki.

Suala la yeye kukujali na kukusaidia haina maana kuwa anakutaka au anakupenda kimapenzi kama unavyompenda wewe, bali anakujali kama ex na angependa uendelee kuwa rafiki na njia peke ya kuendelez aurafiki huo ni kukusaidia na kuwa karibu kila unapomuhitaji labda kwa vile ni binti mwema, mzuri, unajiheshimu n.k.

Linapokuja suala la mpenzi uliyenae hivi sasa, huna haja ya kumwambia kuwa huna "vikorombwezo" kunako K na badala yake acha agundue mwenyewe na kama akiuliza mbona uko hivi hapo ndio utamwambia kuwa kwenu (kabila lako) huwa/walikuwa wanatahiri wanawake n.k

Huenda pia unahofia kuwa jamaa naweza asikufurahishe kingono ikiwa hutomwambia, unadhani kuwa ulipokuwa na yule wa kwanza alikuwa akikufikisha kwa vile alikuwa akijua....si ndivyo unavyodhania? Ukweli ni kuwa ulikuwa unasikia raha na utamu wa ngono kwa vile ulijiamini, ulikuwa unampenda na ulikuwa comfortable wakati wa tendo.

Mwanaume yeyote anaeujua mchezo (namna ya kufanya ngono ipasavyo) atakufikisha na kukupa raha isiyo kifani. Kitu muhimu ni wewe na yeye kujua kona nyingine za ume ambazo zinamsababishia mwanamke utamu (tafuta topic isemayo maeneo 5 ya kusikilizia utamu kwa mwanamke).

Kushindwa kupenda Bf mwingine: Ni kawaida kwa mtu yeyote anaetoka kwenye uhusiano wa kimapenzi wa muda mrefu kama wewe. Huwa ni ngumu sana kuanzisha uhusiano mwingine au niseme kupenda mtu mwingine. Baadhi hutumia muda huo kukusanya hisia zao na kuzi-review ili asirudie makosa pale atakapokuwa tayari kupenda tena.

Kwa kesi yako hakika itakuchukua muda mrefu kidogo mpaka utakapokubali kuwa umeachana na jamaa, hii ni kutokana na ukweli kuwa hujui kwanini hasa kakuacha na hivyo kila siku unapata matumaini ya Njemba hiyo kurudiana na wewe.

Kama unataka (sio lazima) kujisaidia ili kuondokana na hayo matumaini ambayo ni wazi yanakupotezea muda wa kuendelea mbele na maisha yako ya kimapenzi, ni vema kumuuliza mpenzi wako kwanini hasa ameamua kukuacha? Je ni kutokana na umbali kati yenu? Je ni aibu yake kuwa aliku-cheat? Je ameambukizwa HIV ndio maana hataki kuwa na wewe kwa vile anahofia kukuambukiza? n.k......kutakuwa na sababu moja inayomfanya ashindwe kurudiana na wewe.

Mimi kama Dinah nakushauri ujitahidi kumsahau kama mpenzi na jaribu kuji-keep busy na rafiki, ndugu na jamaa. Furahia maisha yako na kama huyo kijana uliyenae sasa unampenda basi focus kwenye penzi lenu na achana na ile njema ya zamani, kwani wakati wake umepita.

Ukiamua kupata ukweli:
Mara tu baada ya kujua ukweli kwanini alikutema, iwe ni Hasi au Chanya itakusaidia kusonga mbele na maisha yako. Kumbuka penzi ni hisia na hazilazimishwi bali hujitokeza zenyewe. Vilevile sio lazima hisia hizo zilingane bali kuzidiana na wakati mwingine kutokuwepo kabisa kutoka upande wa pili.

Kila la kheri!

Binti kaniacha...je nichukue gari langu n.k?-Ushauri

"Habrai yako Dinah,
Hebu tusaidiane hapa, nilikuwa na mpenzi wangu kwa miaka 4 hivi, na nia yetu ilikuwa tufunge ndoa mwaka huu. Baadaye binti alihama mji na kuishi mji mwingine kikazi, hivyo nikawa namtembelea mara mbili kwa mwezi, na nikafanya hivyo kwa takriban miaka miwili.

Kidogokidogo nikaanza kuona tofauti za mawasiliano na sikusita kumwambia, japo sikuona mabadiliko tofauti na hali kuzidi kuwa mbaya, nami nikaendelea kumueleza na kujaribu kuongeza mapenzi kwake ili nisimpoteze.

Baada ya kuona haitoshi nikaamua kumshawishi tufunge ndoa ili awe wangu kabisa na ikiwezekana nimrudishe mji ninaoishi mimi. Kwa kuwa dini zetu ni tofauti tukakubaliana kila mmoja akaongee na familia yake ili tuoane kila mtu na dini yake.

Mimi nikafanikiwa ila yeye akasema kwao hawataki kusikia eti mototo wao anaolewa na Muislam. Basi nikamshauri tuendelee tu kuwa wapenzi kwa muda zaidi kama hawataki tuoane kwa sasa.

Yeye akasema hana jibu maana anahisi anachanganyikiwa tu. Kuanzia hapo hali ikazidi kuwa mbaya mawasiliano ni tabu, sms nikituma asubuhi atajibu jioni, simu mpaka nipige mara 10 ndio ipokelewe nk. Hata nikisafiri kumfuata huko aliko ngono sipewi kwa kisingizio kuwa matatizo tuliyonayo yanamkosesha hamu ya ngono.

Hivyo nikakaa zaidi ya miezi 8 bila ngono japo tunaonana na kulala pamoja mara mbili kwa kila mwezi.Ghafla siku moja baada ya kutopokea simu zangu nyingi sana ndio akanambia alikuwa ananifanyia hivyo visa makusudi ili nimchukie alafu nimuache, maana anaona uhusiano wetu hauto work out as wazazi wake hawanitaki.

Katika kipindi chote hiki cha mapenzi kulikuwa na kusaidiana kwa hapa na pale na niliwahi kumuachia gari atumie. Jee ni haki niendelee kumuachia gari yangu atumie hata baada ya kuniacha?

Jee jamii itaniona nina roho mbaya, na nitajisikiaje siku nikikuta mwanaume mwingine anaye mtomba anatumia jasho langu? Nisaidieni mawazo yenu, kumbukeni kuna vingi nilivyomfanyia kama furnitures, Ada ya Pango etc.

Kindiki"

Dinah anasema:Kindiki asante sana kwa ushirikiano, Hakika kuna wanaume wenye mapenzi ya kweli na wavumilivu sana hapa Duniani. Nimesoma comments na nikagundua kina kaka wamekupa ushauri mzuri ambao natumanini umesaidia wewe kufanya uamuzi mzuri.

Hili liwe fundisho kwa kaka zangu, acheni tabia ya kuwafanyia kila kitu wanawake. Kwani nyie ni baba zao? Kama ni mapenzi mnapendana wote wawili, kama ni ngono mnaifanya wote wawili na kama ni utamu wote mnaupata, sasa inakuaje wewe umfanyie kila kitu yeye na yeye hakufanyii lolote zaidi ya kukuchanganya na Midume mingine?

Sisemi kuwa usimsaide au kumnunulia zawadi mpenzi wako au usimjali kiuchumi kama anahitaji msaada huo, la hasha! Linapokuja suala la kufanyiana mambo makubwa kama kununua Kiwanja, nyumba, gari n.k mnatakiwa kufanya hayo mkiwa na uhakika na uhusiano wenu, kwamba ni wa kudumu/wachumba mnaelekea kufunga ndoa hivyo sio tu unamsaidia yeye bali wewe pia kwani mtakuwa mnaishi pamoja au kwenda kuishi pamoja.

Mf. kwa kulipa pango la nyumba na kununua vitu muhimu kama fenicha, gari n.k itakuwa kwa ajili yenu wote wawili na sio yeye peke yake....sijui mnanielewa? Kuna wanawake ukiwa nao basi utasomesha wadogo zake wote na kujengea wazazi wake nyumba na ukikamilisha yote hayo anakutema vilevile. Wapo wanawake siku hizi wanachukulia wanaume kama ajira, yaani akiwa kwenye uhusiano ndio kapata ajira.

Mimi binafsi nakushauri uchukue Gari lako na uliuze ili kuondoa mikosi na kumbukumbu za huyo mdada. Vingine ambavyo havishikiki achana navyo. Next time unajiingiza kwenye uhusiano hakuna kununulia mtu gari, mtafutie Dereva.

Mungu atajaalia mwaka huu mpya utaanza maishamapya na mpenzi mpya atakae kupenda kwa dhati, kukuthamini na kukuheshimu. Hakikisha hurudii makosa.

Kila la kheri!

Wednesday

Siko Comfortable kuwa karibu na Ma'mkwe-Ushauri

"Hongera sana dada Dinah kwa jinsi unavyotusaidia kwenye mambo mbalimbali, nimeshapost maswali yangu mawili lakini umeyatia kapuni dada yangu kulikoni?? chonde chonde usilitie na hili kapuni.

Dinah anasema: Mama M, sijapokea swali lolote kutoka kwako, hili ni la kwanza. Kwa kawaida kila swali linanolifikia ni muhimu na huwa nali-publish kwa kufuata lini nimepokea.

****************************************************************************

Mimi ni mwanamke niliyeolewa na nina watoto wawili, mume wangu alishawahi kunicheat hapo awali na nikagundua lakini bado aliendelea. Mpaka sasa bado sijatulia kutokana na kutendwa na mume wangu.


Mimi na mama mke hatupatani kutokana na yeye mama kumtetea mume wangu alivyonicheat. Mama huyu alinifokea sana na kuniambia nimuache mume wangu, Yaani alinijia juu mpaka wake wa mashemeji zangu wakawa wanamsema kwa kumwambia anavyofanya sio vizuri.


Nimejifungua hivi karibuni na mtoto sasa anamiezi saba, sijawahi kuwasiliana na mama mkwe wangu tangu mwezi wa kumi na mbili mwaka jana alipokuja kwangu hapa Dar ambapo aliondoka vibaya na hata kusema kuwa kamwe hata kanyaga kwangu.


Mama mkwe yeye anaishi Mkoani, na kiukweli mimi nilikuwa nikimuonyesha heshima zote wala sijawahi kumchukia wala kujibishana nae sembuse kubadilishana maneno makali. Nakumbuka kuna wakati nilimpelekea nguo za Christmass, lakini aliziponda sana akasema atazitupa "nguo gani mbaya hivyo"? japokuwa ilikuwa ni suti nzuri tu jamani! mpaka wifi yangu (mtoto wake) akajisikia vibaya akaja kuniambia mbele ya mama yake ambaye aliona aibu na kuanza kukana.


Tatizo kubwa naona kama huyu mama mkwe anachuki binafsi na mimi japokuwa ndio mchezo
wake kwani keshawakorofisha sana hata hao wake wengine wa mashemeji zangu ila naona kwangu kazidi.

Sasa hivi niko kwenye uhusiano mzuri kiasi na mume wangu japo bado machungu hayajaisha ila anajitahidi, aliniita akaniomba nimsamehe mama yake akidai kuwa "nyie wanawake mnajuana wenyewe sijui kwa nini anakuchukia hivyo" akaniomba nimsamehe na niwe nampigia simu na niwe karibu nae. Siku mjibu kitu mume wangu na wala sikumpigia huyo mama mkwe kwani mimi nimejifungua hata yeye angeweza kuja au kunipigia simu naa kuulizia mtoto lakini anaongea na mwanae tu.

Swali: Mume wangu anataka tukambatize mtoto wetu mkoani (kwa mama mkwe) Xmass hii na mimi sijisikii huru kwani sitamani hata kumuona yule mama kwa alivyonipa stress kwenye maisha yangu, yani hapa sijaandika yote, hata watu baki na ndugu zangu wanajua matatizo niliyoyapata kutokana na chuki ya mama mkwe.

Naomba ushauri kwanza, nikubali nikambatizie mtoto huko kwa mama mkwe au la, na kama nikikubali kwenda huko je nimnunulie huyu mama zawadi kama nguo?? kwani mume wangu huwa hana utaratibu wa kununua nguo za mama yake kabisa!! tafadhali nisaidieni nideal vip na huyu mama??
Wenu mama M"

Dinah anasema: Pole sana kwa kukabiliana na chuki ya mama mkwe wako, hili ni tatizo kubwa linalowakabili wanawake wengi sana hapa Duniani. Hata mimi sijui ni kwanini hasa mtu umchukie mkweo kiasi hicho. Tena mbaya zaidi ni pale Mumeo akiwa ndio mtoto wa Kiume kwa kwanza/mwisho/mtoto wa kiume pekee kwenye familia yao.....hapa mama wakwe/wifiz huwa hawataki mchezo!

Tatizo letu wanadamu huwa tunategemea kupendwa mara tu baada ya kuungana na familia nyingine (kufunga ndoa), Jamani! Mtu mmoja kukupenda haina maana Ukoo mzima ukupende. Kama ikitokea kwa bahati nzuri mkapendana poa, ikitokea hawakupendi safii tu au kama wewe huwapendi ni kawaida vilevile (kwani mlizaliwa pamoja bwanaaa!).....kitu muhimu ni kuheshimiana na kila mmoja wenu kujua mipaka yake kati ya yule aliye waunganisha in ur case mumeo.


Unachotakiwa kuzingatia ni Kumpa heshima lakini kamwe usijipendekeze kwa mama mkwe huyo, usijilazimishe kumpenda (huwezi kulazimisha hisia kama hazipo kubali kuwa hazipo), kutokumchukia (mchukulie kama alivyo na dharau uchokozi na chuki zake kwako), hata siku moja usimzungumzie vibaya kwa watu wengine (kwa kufanya hivyo itakufanya ujenge chuki dhidi yake) kumbuka kuwa huyo ni bibi wa watoto wako hivyo kubali kuwa hakupendi na muache kama alivyo aili mradi tu hamkai nyumba moja.

Ni kama kuwa Kazini/Shuleni, kutakuwa na watu wanakupenda na wengine hawakupendi(ni nature ya mwanadamu)....... lakini huwezi kuacha kazi au masomo kwa vile tu watu fulani wanakuchukia. Unawadharau na kufanya kazi/masomo yako kwa bidii.

Ukiangalia kwa undani asilimia kubwa ya wanawake huwa na tabia ya kuchukiana kweli kweli bila sababu, inawezekana kabisa mtu humjui lakini unajenga chuki. Sasa mimi nadhani hii asili ya baadhi ya wanawake kuwa na chuki za ovyo-ovyo ndio husababisha baadhi ya wakwe zetu kuwa hiyo kwani uanamke hauwatoki hata kama ni watu wazima sana.


Wataalam wa Saikolojia wanadai kuwa mama na mtoto wa kiume huwa na bond maalum, ukaribu huo kati ya mama na kijana wake kuendelea kwa muda mrefu sana. Mama huyu huendelea kudhani kuwa Kijana anahitaji kumsikiliza na kufanya maamuzi ambayo yeye mama anakubaliana nayo kama akipinga basi Kijana hapaswi kuendelea na maamuzi hayo na kiendelea basi atakumbwa na mabaya (si umewhai kusikia kuwa Radhi ya mama ni Kali kwa mtoto wa kiume kuliko wa kike? Jiulize kwanini iwe kwa mtoto wa kiume tu?).


Sasa Kijana anapokuwa na kuanza kujitegemea mama hupata hisia za kupoteza sehemu kubwa maisha yake na hivyo ataendelea kujiweka karibu na kutaka kujua kila kitu ambacho Kijana wake anakifanya. Ikitokea Kijana kaamua kuchumbia Binti ampendae mama huyu anaweza kukubali au kupinga (huwezi kuambiwa hili ni suala la familia yao).


Mama akikubali basi ataanza kujiweka sana kwenye uhusiano wenu na kuhoji vitu kama vile mtafunga ndoa lini? nani asimamie, aina ya nguo zitakazo valiwa, sherehe iwe wapi na iwe vipi? n.k. Baada ya kufanikiwa kufunga ndoa mama huyu ataanza "nataka mjukuu" wakati tayari wapo wengine waliozaliwa na dada/kaka wa mumeo....

Hii yote ni katika kutafuta ushindi na kukuonyesha wewe Mkwe (anakuona kama mwanamke mwingine unaechukua nafasi yake kwa mwanae) kuwa yeye ndio mwenye sauti na mamlaka kwani huyo Mumeo ni mtoto wake hivyo anatakiwa kufanya akisemacho yeye na sio wewe.

Kutokana na maelezo yako inaonyesha kuwa Mama mkwe wako hakupewa nafasi sana kwenye uhusiano wenu na ndio maana anakuwa bitter kila kukicha, na kilichonifanya nigundue hilo ni kutokana na maelezo yako kuwa alimtetea mwanae alipotoka nje ya ndoa.....alimtetea mwanae ili aweze kum-win back Kijana wake na wewe ubaki mwenyewe na maumivu yako moyoni.....alitaka Ushindi kwani wewe ndio unaemjali kwa kumnunulia zawadi na si mwanae......kwa mama mkwe huyu hili ni pigo kubwa kwani anadhani kuwa wewe as "mwanamke tu" ndio una-control kila kitu kwenye maisha ya mwanae.


Nini cha kufanya: Mimi binafsi sioni sababu yakwenda kumbatiza mtoto huko Mkoani unless otherwise kuna sababu za msingi kama vile Kabila la Wachaga (Xmas kuliwa Nyumbani Moshi kind muhimu), mnamtegemea yeye Mama mkwe kiuchumi, labda ndugu wengi wako huko Mkoani na wanataka kushuhudia Ubatizo na ili ku-save ni bora ninyi muende huko kuliko wao kuja Dar, Mama mkwe huyo mgonjwa na hawezi kusafiri lakini anataka kumuona mtoto n.k.

Ili kuondoa vurugu, wewe kubali kwenda kubatiza mtoto huko aliko mama mkwe lakini hakikisha unaelewana na mumeo kuwa hamkai sana ili kuepuka "chokochoko" za huyo mwanamama. Utakapo kwenda huna haja ya kumnunulia chochote huyo mwanamama asie na shukrani.....ili apate ujumbe kuwa kuponda zawadi =hakuna zawadi.

Baada ya shughuli ya Ubatizo kuisha ni vema wewe na mumeo kuwasiliana kwa mara nyingine tena kuhusiana na unavyojisikia kwa mama mkwe wako. Usipozungumza na mumeo na kuliweka hili wazi na kumfanya akuelewe ili asaidie kumaliza chuki za mama yake kwako.

Mumeo mpenzi ataendelea kudhani (mwanaume akisema "sijui kwanini mnachukiana, ni mambo yenu wanawake...naomba umsamehe mama") yaya tachukulia kuwa yameisha, kuwa umemsamehe mama yake na hivyo kuendelea kufanya mambo ya kumhusisha mama yake na wewe mara kwa mara hali itakayosababisha maumivu makali ya hisia kwa vile utadhani kuw amumeo hakujali pia hautokuwa comfortable na mkweo.


Liweke wazi suala la wewe kujisikia huna thamani kwa mama mkwe huyo kutokana na dharau zake, kutetea usaliti wa ndoa...tena sisitiza hapa kuwa ukimuona mama mkwe huyo unakumbuka uchafu aliokufanyia mumeo (umesema kuwa bado unamachungu/hujasahau japokuwa unajitahidi kusamehe....itachukua muda mpaka kurudia hali yako ya kawaida). Mwambie yote yalioujaza moyo wako bila hasira wala chuki.

Muombe mumeo amwambie na ikiwezekana amsaidie mama yake abadilishe tabia yake mbaya, na mara baada ya kubadilisha tabia yake basi anza kumnunulia/tumia zawadi lakini sio ktk kujipendekeza bali kumjali.

**Nani alisema maisha ya ndoa ni rahisi eei? Ni magumu ila ukijua namna ya kukabiliana na wanawake (mama mkwe/wifi) kila kitu kina kinaenda vema na kila mmoja wenu anafurahia maisha yake kivyake na familia yake.

Natumaini kuwa maelezo ya wachangiaji na haya yangu yatakuwa yamekusaidia kufanya uamuzi wa busara.

Kila la kheri!

Friday

Ndoa na Kaka wa kambo (step Brother) ni sahihi?

"Mimi ni msichana wa miaka 23, nina kaka yangu baba mmoja na mama tofauti. Yeye ananipenda na mimi nampenda na tumekwisha wahi kufanya mapenzi mara kadhaa. Yeye ameahidi kuwa atanioa. Sisi ni Waislamu, je ni sawa tunachokifanya kama sio sawa tufanyeje?"

Dinah anasema:Inasemekana na kuaminika kuwa Kibaiolojia na Kiuumbaji ( Mungu alivyotuumba ) mtu na ndugu yake hawawezi kutamaniana, ndugu kwa maana ya kuwa mmechangia damu ya mzazi mmoja. Lakini ndugu wengine kama Binamu, wapwa n.k. wanaweza kutamaniana na hata kupendana kwa vile hawachangii damu moja bali wazazi wao ndio wanaochangia damu.

Pia inasemekana watoto waliochangia sehemu moja ya damu (kama wewe na kaka yako wakambo) wakitamaniana ina maana kuwa uwezekano mmoja wenu sio toto halisi (Kibaolojia) wa baba. Yaani huenda wewe baba yako ni mwingine na sio huyo unaeamini kuwa ndio baba yako au kama wewe ni mtoto wa huyo Baba basi kuna uwezekano kuwa huyo kaka yako sio mtoto wa kweli wa Mzee wenu (mama zenu ndio wanajua ukweli halisi ktk hili au mfanye vipimo vya DNA kujua ukweli).

Kwenye jamii yeyote ile Duniani bila kujali Imani zao za kidini mtu na kaka yake waliochangia damu hawaruhusiwi kuwa wapenzi achilia mbali kufunga ndoa na kuzaa, kwa baadhi ya nchi za Ulaya ndugu kupendana ni kosa la jinai.

Kama hisia za mapenzi ni kali sana miongoni mwenu (which sio kawaida kwa ndugu) basi ni wazi kuwa ninyi sio ndugu na hivyo mnapaswa kuanza mikakati ya kutafuta ukweli kuhusu baba yenu na njia pekee ni either kuongea na mama zenu ili kuwapa ukweli halisi au kufanya DNA test.

Namna ya kupata ukweli:
Msikurupukie mama zenu na ku-demand bali mnahitaji kuwa na mipango nakujua namna za kupata ukweli bila wao kujua kama mmekwisha wahi kungonoana, mana'ke wakijua tayari mnamahusiano mtarushiwa shutuma na mtashindwa kujitete na wao kina mama watakuwa saved kutokana na "kutokujua baba yako au baba wa kaka yako".

Wewe na yeye kwa nyakati tofauti na kila mtu kivyake zungumzeni wazazi wenu wa kike......mwambie "mama mimi nahisi kama vile huyu sio baba yangu! Sina mapenzi wala hisia za baba na mtoto, unadhani kuna uwezekano kuwa huyu sio baba yangu?"......atakupa jibu, hakikisha majibu yake sio ya kusita na wala haonyeshi mshituko pia ukali lakini kama atashituka, kuwa mkali na kusita ujue kuna walakini.

Mwambie kwa kusisitiza kuwa " nataka kujua ukweli kwanini napata hisia hizi, hivyo nitaenda kufanya vipimo vya DNA ili nijue kama kweli huyu ni baba yangu"......mpe muda!

Sisemi kuwa huo ndio ukweli kuwa huyo Mzee sio baba yenu halisi bali kuna uwezekano mkubwa sana kuwa ninyi wawili sio ndugu! Nadhani mmoja wenu huyo sio baba yake mzazi bali ni baba mlezi (alisingiziwa au mama alikuwa hana uhakika na aliyem-mimba).

Kumbuka kuna asilimia kubwa ya akina baba ndani na nje ya ndoa nchini Tanzania wanalea au walilea watoto ambao sio wao. Ili kujua ukweli, ni mama pekee anatakiwa kutoka msafi au kufanya vipimo vya DNA.

Vinginevyo Ni mwiko kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu yeyote ambae mmechangia damu. Toka kwenye uhusiano huo mara moja na usirudie tena.

Kila la kheri!

Sunday

Mikono mikubwa kuliko mwili....nitapendeza gauni la Harusi?







"Pole kwa kwa ngumu dada Dinah.
Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 24 tatizo nililonalo ni kwamba, mikono yangu ni minene kuliko mwili.

Nina umbo zuri, sura nzuri lakini mikono imezidi. Nahofia siku ya harusi yangu sintapendeza, kwa kawaida huwa sivai nguo za mikono mifupi au midogo. Nimekaribia kufunga ndoa na wasi wais wangu ni mikono, je kuna namna yeyote ya kuipunguza au hata kama kuna dawa yoyote unayoijua ya kupaka naomba unisaidie au kama kuna mazoezi yoyote ya kupunguza mikono. Mpenzi wangu huwa ananiambia huna mikono minene basi mimi sipendi, wakati najua ni minene"



Dinah anasema: Hey mtarajiwa, hongera sana na kila la kheri ktk maandalizi ya kufunga ndoa. Hakika suala la kutafuta na kupata gauni litakalokupendeza kutokana na umbile lako sio kazi rahisi, hata hivyo shukrani kwa wabunifu wa mitindo yanguo za kufungia ndoa kwani wanabuni kutokana na maumbile ya watu.



Ukubwa wa mikono itakuwa ni sehemu ya umbile lako na hivyo sio rahisi kuifanya iwe midogo au miembamba, pamoja nakusema hivyo kuna aina ya mazoezi ya kuifanya mikono yako kuwa "firm" na hivyo kuonekana minene lakini haijajitokeza kwa nyuma au kwa chini (kama mbawa), tafadhali kama utakuwa tayari mimi kukuelekeza namna ya kuzoezika basi usisite kuniandikia.



Vinginevyo mimi nakushauri uchague Gauni ambalo litaficha mikono yako (angalia picha hapo juu), usifuate trend kwamba kila mtu anavaa gauni bila mikono basi na wewe utake hivyo (mara nyingi huwa too common) na badala yake nenda kwa a classic one lakini inayoendana na umbile lako.


Kila la kheri na furahia siku yako ya ndoa.

Tuesday

Sitaki kumpotezea muda na nimekuwa honest,lakini hanielewi-Ushauri

s"Dada Dinah, ni mara yangu ya kwanza kukuandikia lakini nimekuwa nafuatilia sasa blog yako hii na kwa kweli ni kitu ambacho tunakihitaji sana kwani inasaidia sana kufumbua matatizo mbalimbali ya kimapenzi.

Sasa mimi nina mpenzi wangu ambaye tumekuwa mbali kwa muda wa miaka mitano hivi, kutokana na mimi kuwa nje ya nchi. Katika kipindi chote hiki tumekuwa katika mawasiliano ya mara kwa mara ambayo kwa kweli yamesaidia kuweka live penzi letu.

Sasa kwa jinsi mambo yalivyo ukiwa nje ya nchi ni kwamba mambo yanaweza kuwa unpredictable sana, kwani kutokana na mambo yanavyokwenda sioni kama nitaweza kurudi nyumbani hivi karibuni, kwa kuzingatia hilo na pia kwa kuzingatia kwamba umri unakimbia sana mimi nina miaka 31 na mpenzi wangu ana miaka 30 nikaona kuwa itabidi kuchukua maamuzi mazito.

Kwahivyo nikamwambia mpenzi kuwa mimi naona kuwa ni vizuri kama kila mmoja wetu akaamua kumove on ikitokea kuwa atapata wa kumfaa ili isije ikafika kesho na kesho kutwa tukaza kupeana lawama kutokana na ukweli kuwa labda nikarudi nyumbani tukakuta kuwa hatuwezi kuishi pamoja sababu labda wote wawili tumebadilika sana kwani tumekuwa mbali mbali kwa muda wote huu kufikiria kuwa tungeishi pamoja.


Nilipomueleza hivyo mwenzangu aliumia sana na ikawa akinitupia lawama mimi kuwa eti labda nimepata mwingine na ndio maana naamua kumtosa, lakini kwa ukweli ni kuwa mimi nilikuwa naangalia picha nzima kwamba tusiwe tunapotezeana wakati kwani umri wetu ndio unakimbia.

Kwa jinsi mwenzangu alivyo react ni kwamba hakubaliani na hilo na kwakweli ameumia sana kitu kilichonifanya nijidoubt labda uaamuzi niliochukua si sahihi kwani imefikia mahali inaniumiza kichwa sana. Ukweli ni kuwa I do care for her lakini inabidi mara nyingine uangalie jinsi hali halisi inavyokwenda katika maisha.

Sijui wewe na wadau wengine mnaonaje kuhusu swala hili, naomba msaada na mawazo yenu wote. Ahsante sana na samahani kwa mail ndefu kama hii, tuendelee kuelimishana katika swala zima la mahusiano"

Dinah anasema:Asante kwa kuniandikia, nadhani kosa ulilofanya hapa ni kufanya uamuzi ulioegemea upande mmoja tu (upande wako peke yako) bila kumuhusisha yeye (mpenzi wako), umefanya uamuzi kisha ukampa matokea....yaani hamkuzungumza na wote wawili kukubaliana kumaliza uhusiano au kutafuta namna nyingine ili uhusiano wenu uendelee.

Mwanamke yeyote mwenye mwanaume Ulaya anatarajia Big, sasa unapomuibukia na kumaliza uhusiano ktk mtindo huu, kidogo inakuwa ngumu kuamini, kuelewa na kukubali.

Kumbuka mko kwenye uhusiano na kama walivyogusia baadhi ya wachangiaji, inawezekana katolea nje wanaume wengine wengi tu kwa ajili yako kwa vile aliamini kuwa siku moja mtakuja kuishi pamoja.

Mimi nakushauri, uzungumze nae na umpe picha kamili ya maisha ya huko uliko. Kwasababu, watu wengi hapa nyumbani hawajui ni kiasi gani maisha yanaweza kuwa magumu huko Ughaibuni (ugumu interms of kutoruhusiwa kutoka nje mpaka wakurudishie kitabu chako, unaweza ukasubiri milele*).

Ukiweka wazi ni nini hasa kinakuzuia wewe kusafiri au hata kurudi nyumbani kwa sasa na hujui lini utaweza kufanya hivyo, akikuelewa ndio uanze kuzungumzia suala la uhusiano wenu. Hakikisha unampa nafasi yeye kukuambia msimamo wake na nini hasa anataka out of uhusiano wenu....msikilize kwa makini. Kisha mpe maelezo kutokana na matarajio yake au atakayo out of uhusiano huo.

Weka kila kitu wazi, kama kuna uwezekano wa yeye kukufuata uko nini afanye na kama hakuna mwambie kwa uwazi kabisa kwanini haiwezekani, kwa sababu kibongobongo wapenzi hutegemea sana kupandishwa majuu lakini hawajui urahisi na ugumu wake.....sasa mpe hali halisi.

Hakuna uwezekano wa kukufuata na huna mpango wa kurudi Bongo sasa:
Mwambie hali halisi kuwa, umri aliofikia wanawake wengi hupenda kuanza kujiandaa na ndoa, kuanza familia n.k. na wewe ungependa kufanya hivyo lakini unasikitika kuwa hutoweza kutimizia hayo kutokana na umbali na mambo yanavyokuendea huko uliko. Muombe radhi kwa kumpotezea muda kwani mipango haikuwa kama ulivyotarajia.

Akikubaliana na wewe, ahidi kuendeleza urafiki na wasiliana nae kila upatapo muda. Akiendelea kutokukuelewa na kukutupia lawama then punguza mawasiliano kama sio kuyakata kabisa.

Kila la kheri!

Monday

Anataka nifanye Masters pia niwe msiri-Ushauri

"Mpendwa dada Dinah. Mimi ni mwanamke wa miaka 23 naishi jijini DSM. Nimekuwa nikifuatilia na kusoma mambo mbalimbali na ushauri wako na comments za washirika tofautitofauti. Nimeona bora nije na hii yangu ambayo kwa ukweli inanichanganya kichwa.

Ninae boyfriend kwa hapa nitamwita X mwenye miaka 26, nimekutana nae chuoni mwaka 2006 nikiwa naingia mwaka wa kwanza na hadi sasa tumeshadumu miaka 3. Tulikuwa darasa moja huko chuoni ila yeye kwa sasa anaendelea na Masters ambapo kwa mimi plan ni next year ndiyo niisome hiyo masters kwani sikupenda kuunganisha.

Mwanzo alipoanza kunidate alikuwa mtu mzuri sana, muda wote alikuwa karibu na mimi na tulipoanza mahusiano mambo yalibadilika kidogo japo aliniambia kuwa yeye ni busy person. Tulikuwa tunaonana kwake siku za weekend tu tena mchana. Siku za kawaida na hata kama ni darasan ni salaam tu basi then kila mtu na muda wake.

Nilipomuuliza alinijibu kuwa yeye ni mtu anaependa privancy hasa kwenye mambo yake ya binafsi kama mahusiano. Tuliendelea hivyo japokuwa alinitambulisha kwa baadhi ya marafiki zake wa chuoni na hata wa kazini kwake akiwemo Boss wake. Kitu ambacho kilinishangaza katika usiri wake ambao ulikuwa ni chuoni tu, kwani tukishatoka chuoni alijitahidi kuwa close na mimi.

Mara moja moja tulipokuwa darasani alikuwa anakuja kukaa na mimi na mda mwingine hapana, japokuwa darasa zima lilikuwa likikujua kuwa tunadate na walikuwa wanatushangaa tunavyoact kama hatujuani.


Hapo ndipo mambo mengine yakaanza, akaniambia anataka watu wachanganyikiwe kwamba wasiwe na uhakika kama tunadate kweli au la. Akawa akiulizwa "mkewako mzima?" anawajibu "sina mke mimi" na baada a hapo anawaacha kwenye mataa na kuondoka.


Kitu kingine ambacho kiliniuma sana ni kuwa hata kwenye party za chuo kama za darasa ambazo ni za usiku alikuwa haongozani na mimi, bali na marafiki zake 3 wa kiume na msichana mmoja. Ndani ya party anakaa na hao watu ila mda mwingi anatoka nje na kurudi


Wakati party inaendelea msg zake kwangu haziishi kutumwa kuwa nisijali nivumilie na niact kiutu uzima. Ukicheza mziki na mkaka anakuja kukutoa na kuniambia nijiandae tunarudi nyumbani. Kwa maana hiyo party ndio inaishia hapo.


Siku zilienda mara nyingine alikuwa na mikutano ya kikazi mpaka saa sita za usiku ndio anaweza kuniambia anatoka kikaoni, nilikuwa najiuliza ni kazi gani usiku? Nijuacho mimi ni kuwa anafanya kazi kwenye makampuni 2 ambayo kote kuwili alinipeleka.

Hatimae nikaja kusikia tetesi kwa watu wengi wa darasani kuwa X anafanya kazi ya upelelezi, tena na hivi alikuwa anasafiri sana kwenda nchi tofauti na hamna anayemuaga zaidi ya mimi tu basi mi ndio nikawa nasumbuliwa "vipi mumeo kaenda kufanya upelelezi?" na maswalimengine mengi.

Siku moja nikamuuliza, akaniambia "kazi zangu zote mbili unazijua haya ya upelelezi sijawahi kukuambia na wala siyajui ndio mana nikakwambia watu wambea sana wanaongea mno, wewe nisikilize mimi na si wao".

Kwa kweli haya yote yalinisumbua sana kichwa changu na mara kwa mara niliongea nae ila jibu lake ni kuwa eti nahitaji kumwelewa na tupeleke mahusiano kiutu uzima na si kitoto. Basi kwa vile nilimpenda nikaka kimya.

Ilimradi mapenzi niliyapata, nikiumwa yupo,nikiwa na shida ananisaidia, akiwa less busy naenda kwake na hata nikitaka kulala huko yeye sawa tu, pia yeye alikuwa anakuja kunitembelea nilikokuwa naishi na wakati mwingine analala. Marafiki zangu walimjua na aliwajua vizuri japo alikuwa ananiambia nisiongee nao kila kitu kuhusu mapenzi yetu kwani hataki umbea.


Siku moja nikamuuliza hivi una mpango gani na mimi wa mbeleni? akanijibu "nataka usome hadi masters mana kamwe sitaoa mwanamke asie na masters" na akaniambia kwa yeye ana plan ya kumaliza masters na kuendelea kusoma na ana mpango wa kuoa mwaka 2015 ila kwa sasa nijue tu kuwa sisi ni wapenzi mungu akipenda basi tutafika mbali.


Ila akaniambia ukitaka tuwe wapenzi zaidi inabidi ujifunze kuwa privancy person hiyo ndiyo sheria yangu,ukianza kuongeaongea sana mambo yetu na mengineyo tutaishia hapo.

Kwa saa tupo mbalimbali na huwa nafunga safari kumfuata chuoni na ninakaa nae siku tatu au mbili kisha narudi kazini. Mambo si rahisi kwa huu umbali ila najitahidi kumtembelea na hata mapenzi ya simu yanachukua nafasi kubwa zaidi kama nikiwa nimekosa kisingizio cha kuomba ruhusa kazini, maana kazi nazo si kila mara uombe ruhusa.

Basi mara nyingi mimi ndio nikawa nampigia simu kila siku jioni, inaweza kupita hata siku mbili kama sijapiga basi tena. Siku moja nikamwambia sipendi hiyo tabia kwa nini hapigi simu?akanijibu kuwa huwa anasahau kuweka credit basi nikamwambia "kama hunipendi uniambie kuliko kunipotezea muda".Tukaagana.

Kesho yake yeye akapiga simu ila sikuchangamka kama siku nyingine.Siku iliyofuata usiku akanitext "hujambo umeshindaje?usiku mwema", mimi nikamwendea hewani tukaongea vizuri tu mwisho nikamwambia "i love u",akanijibu "me too".


Nikamuliza "una uhakika?" akanijibu "sina budi ya kurudia kitu kwa miaka yote 3 tuliyokuwa pamoja hujakua tu?kua basi tuwe na mapenzi ya kiutu uzima" na akaniambia "kusema i love u kila siku haimaanishi ndo unapendwa naweza nikakuambia hivyo na bado nisimaanishi. Kwa kweli sikumwelewa, akaniambia mwisho tukagombana bure na yeye hataki hilo litokee bora tulale,basi tukaagana.

Huyu ndie mwanaume ambae ninae dada Dinah kwa miaka 3 sijapata jibu ni mwanaume wa aina gani huyu na kama kweli ananipenda na ana mpango na mimi. TAFADHALI NAOMBA UNISAIDIE KWA USHAURI NIFANYAJE.
Na washiriki wengine nahitaji maoni yenu tafadhali.

Ni mimi dada F"

Dinah anasema: Dada F, shukrani kwa ushirikiano na uvumilivu wako as nachukua muda mrefu kujibu kutokana na uwingi wa majukumu mengine ya kikazi na maisha. Nimefurahishwa na maelezo yako ya kina na kumfanya yeyote kuelewa picha nzima bila kuwa na maswali.....hongera kwa hilo.

Suala la Ushushushu sio muhimu sana as long as wewe unajua kazini kwake, na akitoweka siku zote huwa anakuambia kuwa anasafiri hivyo huitaji kujipa hofu na mimi binafsi sina uzoefu na masuala ya wapelelezi. Nitakupa maelezo kuhusiana na issue ya uhusiano wenu wa kimapenzi ambayo naamini yatafungua macho yako kwa kiasi fulani.

Mimi binafsi ninaamini kuwa sisi wanadamu lazima tupitie hatua sita za maisha ya kimapenzi na mahusinao. Ila tatizo la wengi huwa tunakurupuka na kutaka/kutegemea jambo fulani kabla ya wakati.

-Uzoefu/kutambua ujinsia wako kwanza (hapa unakuwa kwenye umri mdogo so jaribu kufurahia maisha na kupata uzoefu zaidi wa kimaisha na wakti huohuo unazingatia masomo/kazi, sio lazima ungonoke).

Pili:-Unapenda na ku-commit (hapa utakuwa mkubwa kiumri na umetulia kiakili).

Tatu:-Chumbia na Ndoa (kuwa na uhakika wa kuishi na huyo mmoja tu maisha yako yote).

Nne:-Familia(Uamuzi au kukubaliana kuzaa).

Tano:-Kufanya uhusiano wenu wa kimapenzi na ndoa kusimama Imara.

Mf-ninyi wawili bado wadogo, mnapendana sana tu (kutokana na maelezo yako bado mko hatua ya kwanza)...ila wewe unategea au unataka zaidi ya unachokipata kutoka kwenye uhusiano wenu, huenda ungependa siku moja ufunge ndoa na huyo mpenzi X hasa ukizingatia kuwa owte mnafanya kazi na mmeshakuwa pamoja kwa muda mrefu. Lakini yeye hayuko tayari kufanya hivyo kwani anachotaka yeye kwa sasa ni kurekebisha maisha yake na wakati huohuo kuongeza Elimu.

Kitu ambacho sisi wanawake huwa tunakikosea ni kuharakisha mambo, labda kutokana na " msukumo" kutoka kwa jamii inayotuzunguuka kuwa ukiwa kwenye uhusiano baada ya muda fulani basi lazima uolewe au hata kuzaa.

Lakini katika hali halisi tunatakiwa kujua nini hasa wapenzi wetu (wanaume) wanakitaka kutoka kwenye uhusiano husika na je ni hatua gani hivi sasa uhusiano wetu upo? kabla hatujaanza kurukia/harakisha hatua inayofuata kama sio kuziruka zote na kwenda hatua ya mwisho.

Sasa ninachokiona hapa ni wewe kutaka commitment na kuhakikishiwa nafasi yako, wakati yeye bado anajaribu ku-have fun. Kweli anakupenda lakini hiyo hamfanyi yeye kuwa na uhakika kwa 100% kuwa wewe ndio mke wake.......anahitaji muda.

Kwenye suala la wewe kuwa msiri, mimi sioni tatizo kwani naelewa kuwa kuna baadhi ya watu wanaaibu sana yanapokuja masuala yao ya kimapenzi.....yaani hawapendi kujionyesha wa watu wengine kuwa wao ni wapenzi. Sasa kwa vile mpenzi X ni mmoja kati ya hao watu ni vema wewe kuheshimu takwa lake hilo.

Nini cha kufanya: Jiulize nini hasa unataka out of the relationship with X, mawasiliano yenu yako bomba kama wapenzi, unapewa mapenzi yake yote, mnaonana kila mnapohitajiana, anakujali, kila mtu yuko huru kwenda kwa mwenzie, mnaoneana wivu (which ni dalili nzuri) X anaonyesha ameji-commit kwako.......nini kingine unataka?

Kama ni ndoa ndio utakayo ni wazi hutompata kwa sasa kwani yeye anadhania takuwa tayari akiwa na miaka 31 (2015) which wanaume wengi ndio hupenda kujipangia hivyo kuanzia 31-36 wawe wamefunga ndoa, huamini by that time wanakuwa somehow wamekamilisha "mipango" yao kimaisha.

Hivyo hapo kuna maamuzi 3 tofauti;
(1)-Endela na uhusiano huku ukimsubiri tumia muda huo kwenda kufanya hiyo Master yako au

(2)- Endela na uhusiano, furahia maisha yako na chukulia kila siku kama inavyokujia (mkifunga ndoa poa isipotokea ndoa poa).

(3)-Toka kwenye uhusiano ili kupata utakacho kwenye uhusiano mwingine (kama unaharaka sana na maisha ya wawili).

Nakutakia kila la kheri.

Thursday

Mume ni mwema lakini hataki kazi wala hatoi Unyumba-Ushauri!

"Habari mpenzi,
nimevutiwa sana na blog yako, kwa kweli ina story za kusikitisha na ukweli kuhusu maisha. Mimi ni mwanamke niliyeolewa naona nina matatizo ambayo nimekaa nayo kimya kwa muda mrefu bila kujua nimwombe nani msaada.

Nimejaribu kuongea na Mama yangu mzazi lakini nimepewa ushauri wa kuvumilia, nimejaribu kuongea na Mama mkwe wangu ushauri ni huo huo sasa sijui labda nipate ushauri toka kwa watu wengine sasa.

Story inaanza hivi; tumependana na mume wangu bila kuwa na kasoro, baada ya mwaka wa uchumba tukafunga ndoa Kanisani. Baadaya ya kuoana tu mungu akanijalia ujauzito nikazaa mtoto wa kike mwaka uliofuata, basi ilikuwa ni furaha tu.

Baada ya miaka miwili nikajaliwa mtoto wa pili wa kiume sasa, basi nayo ilikuwa heri. Sikuwahi kugombana na mume wangu wala kukosana kwa aina yoyote, maisha yalikuwa ni matamu haswa kwani ni msikivu kweli kweli. Chochote ukimwambia anafanya hata kupika hata kufua nguo zangu za ndani.....duuuh hadi wengine walikuwa wananiambia nimempa limbwata.


Basi baada ya kuzaa mtoto wa pili nikashangaa mwenzangu hana time na mimi si kwamba halali nyumbani laah anakula na tunalala wote, watoto anaangalia na matumizi yote anatoa lakini penzi kitandani hakuna, basi ikapita miezi kadhaa bahati mbaya kazi yake aliyokuwa anafanya ikaharibika.

Akawa hana kazi lakini hatukukata tamaa ya maisha tulianza kutafuta tukisaidiana maisha na tulikuwa na miradi yetu midogomidogo ilikuwa inatusaidia. Lakini bado pamoja na yeye kushinda nyumbani tu labda akihangaika kuomba kazi huku na huku mimi nikirudi kutoka kazi hana time ya kufanya mapenzi ila kuongea tunaongea vizuri na hatugombani hata siku moja.

Nikapata woga wa kumuuliza mwenzangu kama ana tatizo maana naona jogoo huwa anasimama kama kawa hasa wakati wa asubuhi lakini hajawahi kunitamkia ananitamani au kunitaka kuwa anataka tufanye mapenzi, mhhhh nikaja nikaona hii kweli kali.


Miezi sita ikapita hatujagusana ila tunakaa vizuri sana kula wote, kulala wote na kushare vitu vingine tu kama kutoka out n.k. Sasa limekuja suala la kazi, kila ninapomuombea kazi kwa watu na kuitwa kwa ajili ya mahojiano hapati. Juzijuzi nilimuombea kazi mahali nifanyapo kazi na akaitwa lakini akakataa kwenda akadai yeye hawezi kwenda kufanya kazi mahali ambapo mimi nafanya kazi.

Hapo mhh sikumuelewa nikajaribu kumueleza vizuri kuwa hatutakuwa ofisi moja ila jengo moja hakukubaliana na mimi . Sasa dada dinah, mtu kama huyo unamfanyaje?

Mwaka mzima umekaa ukishikilia familia na ukisali Mungu ampe kazi, ukimvumilia na kumpenda ingawa hakupi unyumba bila sababu maalum, sasa na kazi hataki kufanya anachagua badala ya kufanya yoyote for the sake of the kids, je nifanyeje? tafadhali naomba msaada hapo kama ni wewe ungefanyaje?-Magy"

Dinah anasema: Mpendwa Magy asante sana kwa ushirikiano na uvumilivu as nimechelewa kujibu, lakini natumaini maoni na ushauri wa wasomaji umesaidia wakati unasubiri kutoka kwangu.

Nitakupa maelezo na ushauri katika sehemu mbili, moja kuhusu kutokufanya Mapenzi na pili suala la yeye kugoma kufanya kazi sehemu moja na wewe.

Kwanini hafanyi mapenzi na wewe lakini anasimamisha!!
Kuna sababu nyingi ambazo zinaweza kumfanya mwanume apoteze hamu ya kufanya mapenzi, kumbuka hamu na nguvu ni vitu viwili tofauti tena kwa wanaume kusimamisha pia kuko kwa aina mbili kusimamisha kwa vile wako tayari kungonoka na kusimamisha kwa vile ni sehemu ya ujinsia wao kwa maana kuwa kuna aina mbili za mwanaume kusimamisha:- (1)-kutokana na mawazo ya kingono (2)-kutokana na kuwa stimulated kwa kushikwa au kuguswa na kitu kama vile shuka, chupi, mkono n.k


Mfano ni mwanaume kusimamisha asubuhi, ile haina maana kuwa anataka ngono japokuwa inaweza kufanyika ngono kama akikuona ukopembeni na ukamvutia then akapata mawazo ya kingono on top of msimao ambao ulisababishwa na mzunguuko wa damu wakati kalala......


Hivyo basi yeye kutokufanya ngono na wewe haina maana anamatatizo ya nguvu za kiume. Nadhani tatizo kubwa linaweza kuwa moja kati ya haya :-

Mosi, Hofu ya kuachishwa kazi (katika hali halisi unapewa taarifa mapema kuwa utapunguzwa/fukuzwa kazi), sasa ile hofu ilisababisha msongamano wa mawazo (stress) na hivyo kupoteza hamu ya kungonoka.

Pili, mabadiliko ya mwili wako baada ya kujifungua mtoto wa pili (Chunguza hapa), na jitahidi kurekebisha.....jipende na hakikisha unavutia zaidi, fanya mazoezi ya misuli kuanzia ya ulimi mpaka ya Uke.

Tatu, hapati attention ya kutosha kutoka kwako kama mpenzi labda kwa vile wewe huna muda as una-deal na watoto bila ushirikiano wake kutokana na stress.......(peleka watoto kwa bibi yako au kwa ndugu yeyote mnae muamini) mara moja kila baada ya wiki 2.

Nne, Yeye kuwa muanzilishi wa kutaka/kufanya ngono kitu ambacho huwa kina udhi/kera na kuchosha na hivyo mtu anaamua kutokufanya kabisa......(Kuanzia sasa usisubiri yeye aanze, anzisha wewe). Hii itamfanya ajiamini na kuhisi kuwa anavutia pia anafurahi kuona kuwa mkewe sio Gogo, pia mara moja kwa wiki mfanyie mumeo jambo litakalo mfurahisha, pagawisha na kumridhisha kingono).

Nini chakufanya kwa ujumla: Mumeo anahitaji ushirikiano mkubwa kutoka kwako, ushirikiano huo sio wa kumtafutia kazi au kumsukuma atafute kazi (kitu ambacho anakijua wazi yeye kama mwanaume) kwani kwa kufanya hivyo unamfanya apoteze ile hali ya kujiamini kama mwanaume na pia unasumbua Ego yake kwani yeye kama mwanaume kamili najaua kuwa ni wajibu wake kuwa provider kwa familia yake, sasa unapo-take over nakujaribu kumtafutia kazi inaweza kuchangia kumfanya azidi kuhisi kuwa yeye ni useless.

Natambua unafanya hivyo katika harakati za kumpa ushirikiano, kuonyesha uko pale kwa ajili yake na tayari kumsaidia mumeo kwa faida ya watoto wenu, yote haya wewe kama mwanamke ungefurahi kuyapokea kutoka kwa mumeo kama ungepoteza kazi......lakini sio mwanaume. Mwanaume anapewa ushirikiano kivingine.

Huyu mumeo anamengi sana akilini mwake hivyo hakuna nafasi kabisa ya kuweka mawazo ya kingono (kama unawajua wanaume vema utanielewa ninachokisema hapa). Sasa ili kumsaidia arudie hali yake ya kawaida unatakiwa kufanya kazi ya ziada......


Mf: kuongea nae vizuri, kumshauri/kumpa matumaini, kumshirikisha kwenye maamuzi (japokuwa hawezi kuchangia kwa sasa), kuonyesha unampenda na kuvutiwa nae zaidi sasa hana kazi kuliko alivyokuwa na kazi(anzisha ngono, cheza na mwili wake na kuwa mtendaji mkuu), kuonyesha kuwa unaweza kusimama wewe kama mama bila kuonyesha stress au kuzidia (anajua kuwa unazidiwa lakini sio lazima umuonyeshe au kulalamika kwani itamuangamiza kiakili), usionyeshe kukerwa na yeye kutokuwa na kazi, kumpa matumaini kuwa kazi ni kazi tu as long as senti zinaingia n.k.


Kwa kufanya hayo niliyogusia na mengine ambayo baadhi ya wachangiaji wameshauri hakika mumeo atakuwa comfortable na mawazo yanaweza kupungua na hivyo kuanza kupata nafasi ya kufikiria ngono akilini mwake na hata kuanza kuona kuwa unamvutia tena.


Kufanya nae kazi Jongo moja: Ukiachilia mbali matatizo mengine yanayoweza kujitokeza kwa kufanya kazi sehemu moja (unless otherwise Taaluma zenu zinafanana na mnawekeana mipaka vinginevyo sio nzuri/afya kwa uhusiano wenu wa kimapenzi.


Kama nilivyogusia hapo juu, kwa baadhi ya wanaume kusaidiwa na wake zao ktk mtindo wa ku-take over kama ulivyofanya wewe huwapotezea hali ya kujiamini na kuhisi kuwa "wameolewa" achilia mbali mwnaume huyo aende kufanya kazi Jengo moja na mkewe ambae ndio actually kamtafutia hiyo kazi na usikute kazi yenyewe ni ya kiwango kidogo kuliko mkewe........hapo haji mtu!

Uless kuna matatizo mengine kwenye ndoa yenu ambayo hukutaka kuyaweka hapa, lakini tatizo lako sio kubwa kiasi cha kutishia uhai wa ndoa yenu. Hakikisha unafanyia kazi ushuri uliopewa na nina kuhakikishia kila kitu kitakuwa safii na Unyumba utaupata lakini kwa sasa jitahidi ku-initiate ngono kila unapojisikiwa kutaka kufanya hivyo, usisubiri yeye akufuate au akuombe!....ni mumeo huyo hivyo unamfanya atake kufanya kwa kutumia uanamke wako au yeye anakufanya wewe utake kufanya kwa kutumia uanaume wake.

Kama ingekuwa mimi ningefanyaje: Mimi kama Dinah, kwanza kabisa ningekubali mabadiliko na kujaribu kubadili mtindo wa maisha yetu kama familia ili ku-save. Ningeonyesha mapenzi kwa mume wangu kuliko mwanzo, ningehakikisha namuondolea stress kwa kutumia mbinu mbali mabali za kumkanda na kuongea nae bila kulalamika wala kuonyesha kuwa nimezidiwa na majukumu.


Kila wakati ningemfanya aone kuwa niko nae sambamba ktk hardship na sio yake peke yake bali yetu sote. Ningempa support na kumshauri kuhusiana na kazi/biashara (sio lazima kuajiriwa) kwa kumpa mawasiliano au kumuonyesha sites/magazeti lakini sio kwa ku-take over na kuingilia Ego yake.


Ningemshawishi kwa maneno na vitendo kuwa kufanya mapenzi kunasaidia kuondoa au kupunguza stress, nikifanikiwa basi nitahakikisha namfanyia mambo hadimu ambayo najua yanaondoa stress hata kwa masaa mawili (which itamfanya anitake kingono mara kwa mara).

Kwa vile naelewa kuwa kipindi hiki cha hardship kinamfanya mume wangu kushindwa kutumia akili yake kufikiria/taka ngono na kusimamisha, basi ningetumia njia ya kumsisimua kwa kufanyia kazi mwili wake na kuhakikisha akili yake ime-relax kabla sijaanza zoezi zila la kumsisimua kingono.

Nakutakia kila lililojema!

Baba kanilea na kunisomesha, Mama anasema si baba yangu!!

"Hi Dada dinah nina matatzo sana hivyo I need your advice. Mimi ni kijana wa miaka 21, it is a long story but I wil make it short and clear. Ni kwamba, mimi nimezaliwa Kenya when my dady met with Mum there but walikuwa ni wapenzi yaani hawakufunga ndoa.


Nilipofikisha miaka 2, baba alinichukua nikaenda kuishi Moshi na bibi, anadai kuwa matunzo kwa mama hayakuwa mazuri. Tangu alivyonichukua hadi nafikisha miaka 17 Mama hakuwahi kuja kuniona wala hakutaka kujua habari zangu japokuwa hakuwa mbali sana yaani ni kiasi cha kutumia Tsh elfu3 kama nauli.


Nilipofikisha hiyo miaka kumi na saba ndio akaja kuniona. Kipindi chote nilikuwa naishi na baba tu kwani alirudi nyumbani. Sasa baada ya Mama kuja anadai eti yule niliyekuwa naishi nae na kuamini kuwa ni Baba yangu was not my father na kwamba my father is from Uganda but huyu Baba ndio ninayemfahamu, ndiye aliyenilea na kunisomesha mapka nilipofikia na hajajua hilo, kwamba mimi sio mtoto wake. Je nifanye nini?"

Dinah anasema:Pole kwa mawazo yanayosonga akili yako hivi sasa kuhusiana na ukweli juu ya nani ni baba yako wa damu. Ukweli utabaki kuwa mama siku zote ndio anajua baba wa mtoto ni nani?

Nasikitika kusema kuwa kuna akina baba wengi tu walilea na wanaendelea kulea watoto ambao Kibailojia au kidamu sio wa kwao lakini kwa vile wanashiriki tendo la ndoa na wake/wanawake zao basi hujenga ukukaribu na mimba ile na mtoto anapozaliwa huona kabisa kuwa ni wa kwake na hivyo kujenda bond kama baba hali ambayo humathiri Kisaikolojia huyu baba na hatimae kuona mtoto huyo anafanana na watu wa karibu na familia yake kama sio yeye mwenyewe.

Pamoja na kusema hivyo, sina maana kuwa huyo si baba yako na wala siwezi kukubaliana wala kukataa kuwa yule Mganda pia ndio baba yako wa damu. Kama walivyogusia baadhi ya wachangiaji huenda hata huyo Mganda sio baba yako.

Kutokana na maelezo yako inaonyesha wazi kuwa hauko interested na mwanamke huyo japokuwa ndio aliyekuzaa hivyo huna budi kumpa heshima kama mzazi wako wa kike kwani hajui kuwa mama ni nini hasa kwani sio yeye aliyekulea bali bibi yako.

Sitokulaumu kwa kupoteza interest au hata mapenzi juu ya mzazi wako huyo wa kike kwani hakutaka kujihusisha na wewe, sasa kwa vile umekuwa mkubwa na yeye anazeeka ndio kashituka na kuona hakutakuwa na mtu wa kumsaidia hapo ndio akakumbuka ala kumbe nina mtoto Tz!

Inawezekana kabisa hakujua ni namna gani atakujia na hakutaka kuomba msamaha kutokana na kujiweka mbali na maisha yako wakati ulipokuwa ukimuhitaji zaidi (ulipokuwa mtoto) na njia pekee ya kujiweka karibu na wewe ili kupata atakacho ni kupandikiza uongo bila kujali (Again) kuwa akuwa atakupa msongamano wa mawazo (stress), kuumiza hisia zako (emotional) na Kisaikolojia.

Mimi nakushauri kama ifuatavyo,
Mosi, Kamwe tena mwiko kabisa kumueleza baba yako Mtanzania kuhusu hili suala, kwani litamuumiza sana na hata kusababisha matatizo makubwa (inategemea na atakavyolipokea) sio yeye tu bali Bibi yako, ndugu jamaa na marafiki.

Ikiwezekana kaa mbali na huyo mama kwa kumwambia kuwa huitaji kuwa nae karibu kwa na asikutembelee wala kuzoea kuja hapo nyumbani na badala yake mwambie wewe utakuwa ukimtembelea huko Kenya kila unapohitaji kufanya hivyo kwani tayari wewe ni mtu mzima.

Pili, Ukisha muweka mbali tafuta wasaa na uzungumze nae hata kama ni kwa simu na umwambie yalioujaza moyo wako ikiwa ni pamoja na msimamo wako juu ya baba aliyekulea (hata iweje ndio unamtambua kama baba yako n.k) na juu yake(utampa heshima kama mzazi wa kike na hadithi za masiha yake ya ujana azi-keep mwenyewe).

Tatu, Kama unataka/ukipenda kuwa na amani moyoni juu ya Mzazi wako wa Damu basi utalazimika kum-bana mzazi huyo akupe ukweli halisi kama kweli anauhakika kuwa Mganda ndio Baba wa damu au anadhania tu lakini inawezeakana hata yeye sio baba na ukweli ni kuwa hajui baba ni nani na akaamua kusingizia wanaume wote aliotembea nao.

Usimuonee aibu wala usihisi Guilt kutokana na katabia kake kachafu ka kulala na wanaume ovyo tena bila kinga, hakikisha unam-bana akupe ukweli wote mpaka kwanini hasa akamsingizia huyu baba wa Tz na kitu gani kilimfanya asijihusishe na wewe na sasa nini kimemfanya akukumbuke (yote yalioujaza moyo wako yatoe) kwani unahaki zote za kujua kwa uhakika kama huyo Mganda ni baba wa damu au unaenda kubahatisha tu!

Akihakiki na kukupa maelezo ya kutosheleza na wewe kuhisi the argue ya kutaka kujua ukweli basi omba mawasiliano ya huyo Mganda ili ufanye nae mawasiliano na ikiwezekana kufanya vipimo vya DNA ili upate amani moyoni na sio kwenda kuanza kujipendekeza kwa mtu au hata familia ambayo huijuia achilia mbali Tamaduni zao za Kiganda.


Akisita nakuja na hadithi nyingine ambazo zinaashiria kuwa hana uhakika na Mganda, kwamba inawezekana pia sio baba wa damu basi achana na the issue na endelea na maisha yako na baba wa Tz. Wewe hautokuwa wa kwanza kulelewa na mzazi ambae sio wa damu kwani kuna watoto wengi tu wanalelewa na wazazi ambao sio wa damu lakini wanapendwa, kujaaliwa, kupewa msingi na mwanzo mzuri tu wa kimaisha kama ulioupata wewe.

Kuna watoto wanaishi na wazazi wao wa damu lakini hawapati ulichokipata wewe, kwa uzoefu wako umeona kabisa kuwa mama hakukutaka ulipokuwa mdogo na alikupa matunzo mabaya kiasi kwamba baba Mtz akahofia kuwa ungeendelea kuishi na mama huyo huenda usingefikisha miaka 21, ungejifia ktk umri mdogo sana.

Kumbuka kwenye suala la DNA, hakikisha humpi jukumu lakufuatilia kwani anaweza kuwa ana-demand pesa kwa kisingizo cha kufuatilia, hakikisha unalifanya mwenyewe na kama hakuna sababu ya wewe kufanya vipimo hivyo kwa vile una amani moyoni kuwa Baba Mtz ndio baba yako hakikisha unamuweka mama huyo mbali kabisa na familia yako ya Tz ili kuepusha matatizo ambayo yatakuathiri wewe na Baba mTz.

Kama nilivyosema awali kuwa kuna asilimia kubwa sana ya kina baba hapa Duniani wamelea na kusomesha watoto ambao sio wao wa damu, lakini kwa vile hawataki masumbuko ya akili, Saikolojia, hisia na hata kuharibu ukaribu wao wa kifamilia wanaamua kudharau maelezo ya watu wengine pia vipimo ya DNA na kuendelea na maisha yako kama kawaida.

Najipa matumaini kuwa umefanyia kazi maelezo na ushaurio kutoka kwa wachangiaji na utafanya uamuzi wa busara ili kuishi kwa amani na furaha.
Kila la kheri!

Tuesday

SMS kwa jina la kike mhusika Dume-Ushauri!

"DEAR,
MImi ni kijana mwenye umri wa miaka 24, nina mpenzi ambaye hadi sasa nimekuwa nae kwa mda wa mwaka mmoja. Mpenzi wangu huyu ni msiri sana linapokuja suala la matumizi ya simu. Kwenye simu yake inaonyesha anamtu mwingine ambae anaishi Mtwara na huwa wanawasiliiana mara kwa mara, lakini kila nikimuuliza ni nani huyo? yeye anasema kuwa ni rafiki yake na ni mwanamke.

Lakini katika uchunguzi nilioufanya nimegundu mtu huyu ambaye ni rafiki yake ni Mwanaume kwani amekuwa wanawasiliana kwa sms, akitumiwa tu sms husoma na kuzifuta haraka sana. Sasa tarehe 16/9/2009, Tulitoka na kwenda Biashara Club kwa ajili ya msosi, Mpenzi akatoka kidogo na kwa bahati mbaya akawa ameissahau simu yake mezani.


Mara sms ikaingia, kwa sababu nilikuwa na wasiwasi na mawasiliano yake ya mara kwa mara nikaamua kuisoma ile sms ikisema wakutane mda wa saa mbili usiku, wakati ujumbe umeingia ilikuwa ni saa mmoja usiku.


Namba ya huyo mtuma ujumbe imetunzwa kwenye simu kwa jina la MASA, kutokana na sms niliyo soma na kupata uhakika zaidi ambao nilikuwa nautafuta niliamua kumwambia mpenzi kuwa na hitajika nyumbani kwani kuna tatizo, sikuweza kuendelea kuwepo pale, sasa ili nijue ukweli wake nifanye nini?
Naomba ushauri wako dada.
it's me Hassan"

Dinah anasema: Hassan, pole kwa mkasa huo. Hiyo ni tabia ya watu wengi ambao sio waaminifu, wanakuwa na wapenzi nje ya mahusiano yao na kutunza mawasiliano ya simu kwa majina ya ambayo sio halisi. Mf- Kamani mwanamke watatunza kwa jina la kiume na kama ni wa Kiume basi jina litakuwa la kike.

Jambo muhimu ni kwenda kufanya vipimo ili kujua kama uko huru kutoka HIV! Kwani hali ni mbaya sana na inatisha.

Katika hali halisi unapokuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi huitaji kuwa na siri, kila kitu unachodhani ni muhimu mwenzako kujua basi utaweka wazi jambo husika, hata kama mtu huyo anampenzi mwingine kwa sababu nyingine labda za kimapenzi au kiuchumi (wapo watu wanakuwa na wapenzi 2, mmoja wa kimapenzi na mwingine kwa ajili ya pesa) pia unatakiwa kuweka wazi hilo ili huyo anaetaka uhusiano na wewe aweze kufanya uamuzi wa busara.

Nasikitika kusema kuwa mpenzi wako sio mwaminifu na kuna uwezekano mkubwa anakuchanganya wewe na mwanaume mwingine. Ni vema kama utamueleza mpenzi wako ukweli wa nini kilichokufanya uondoke usiku ule mlipokuwa nje kwa ajili ya chakula, muulize kuhusu huyo Jamaa anaewasiliana nae na kama wanangonoana n.k.

Kisha msikilize anasemaje na umwambie uwazi kuhusu msimamo wako Mf- hutaki kum-share yeye na mwanume mwingine, hupendezwi na tabia yake ya usiri. Sasa kama hakuna kinachoendelea na huyo jamaa wa SMS (mana'ke inawezekana njemba inamtaka tu lakini hajafanya nayo ngono)....mwambie Demu abadilishe tabia yake ili uweze kumuamini.

Kama walikwisha ngonoka, ni wazi kuwa mdada huyo hakufai hivyo basi achana nae na subiri kupata binti mwingine atakaejiheshimu nakuheshimu uhusiano wenu na kukuthamini wewe kama mwanadamu.

Kila la kheri!

Saturday

Namuonea huruma Soon to be Ex Wife-Ushauri

"Heloo dada Dinah, pole sana kwa kazi. Nimeona nikutumie hii mail kwa ajili ya ushauri.
Tatizo langu ni kwamba dada, mimi ni mdada wa miaka 24 nimeajiriwa. Huwa napenda sana kutembelea blogs mbali mbali na kuchat katika pita pita hizo nikakutana na mtu (Mwanaume) tukawa tunawasiliana aliniambia kuwa ana mtoto ila mama wa mtoto wametengena na yuko nje ya Tanzania kaolewa na Mwanaume mwingine na wamezaa.

Tuliendelea kuwasiliana kwa simu na kuchat kupitia internet hadi ilipofika siku tukaonana. Baada ya kuonana siku ya kwanza tuliendelea kuwasiliana kwa simu na pia kupanga miadi ya kuonana tena na tena hadi siku aliponitamkia kuwa anapenda niwe mpenzi wake.

Kiukweli nami pia nilimpenda ila kwa wakati huo nilikuwa kwenye matatizo na mpenzi wangu wa awali so nikaona haina haja ya kuendelea kuteseka wakati tayari kuna mtu anaonesha kunipenda kwa dhati.Basi tukawa wapenzi.


Tatizo lilianza pindi mpenzi wangu wa awali alivyogundua kuwa nina ukaribu na huyo mjamaa ambae kumbe anamfahamu. Siku moja akanipigia na kuniambia kuwa yule mtu ameoa tena kwa ndoa ya Kanisani na wanaishi wote na mkewe, nikamwambia mbona mimi ameniambia tofauti.

Basi ikabidi nimbane kweli huyu jamaa mpya nae akaniambia kuwa ameoa ila yeye na mkewe wana matatizo ya muda mrefu sana ambayo sio rahisi kusameheka na isitoshe huwa hawalali pamoja! na anachosubiri yeye ni ruhusa ya kupeana Talaka kwani swala lao limeshafika mbali.


Kwakuwa alikuwa ananionyesha mapenzi ya dhati, nikawa niko tayari kuendelea naye hapo nakiri kweli nilikuwa mdhaifu kwani nilistahili kuachana naye baada ya kugundua ukweli lakini tatizo ni kwamba tulishakula kiapo kuwa hatutaachana kwa namna yoyote ile.

Hadi sasa tuna muda wa miaka miwili. Ushauri niutakao ni je, niendelee na huyu mtu au niachane naye??? kwanini nataka ushauri wa hivyo ni kwa sababu nafsi inamuonea huruma sana mkewe ingawa kiukweli anaonekana wazi kuna kitu kikubwa alimkosea mumewe kwani mara nyingi huwa anamuomba msamaha naona hayo kwenye simu yake na pia huwa anapiga na huyu kaka huwa anaweka loudspeaker nami nasikia.


Ameahidi pindi atakapotengana na mkewe yuko radhi kunioa, hilo pia nahofia kwa kuwa sijui namna ya kuieleza familia yangu kwani itabidi niweke wazi kuwa alikuwa mume wa mtu kabla hawajasikia kwa watu.

Kwetu mimi ni mtoto wa pekee wa kike. Samahani kwa mail ndefu, na sijui kama nitakuwa nimejielezea vizuri ukanielewa ila kama utakuwa na maswali ya kuniuliza ili uweze kunisaidia sawa unaweza kuniuliza nitakuwa tayari kujibu ili nisiendelee kuteseka.

Asante sana, kazi njema.
Lizzy"

Dinah anasema: Mdogo wangu Lizy, mtu akishindwa kuwa mkweli mwanzoni kabisa mwa uhusiano ni wazi kuwa daima hatokuwa mkweli kwako. Kutokana na maelezo yako huyu Jamaa alikuwa anam-cheat mkewe via internet (wako wengi sana hawa viumbe wake kwa waume wanao abuse maendeleo ya mawasiliano).

Ni wazi kabisa wakati unakutana na huyu jamaa kwenye mtandao ulikuwa kwenye wakati mgumu kimapenzi hivyo kuwa Vanulable hali iliyopelekea huyo mpenzi mume wa mtu kuchukua advantage na kukulubuni. Ili aku-win akaamua kukupa mapenzi ya dhati ambayo alijua kabisa unayahitaji kwa vile ulikuwa huyapati kutoka kwa Mpenzi wako wa awali.

Kama walivyosema baadhi ya wachangiaji na pengine wewe pia unajua hasa kama ni Mkristo, kwamba Ndoa ya kikristo daima huwa haivunjiki unless mmoja wa wanandoa hao afariki. Hata kama wametengana bado hawatoruhusiwa kufungandoa tena unless mmoja wako kafa......vinginevyo labda Serikali iingilie na Talaka itolewe kwa amri ya Mahakama lakini hata hivyo mpaka Hakimu anakubali kuamrisha Talaka inatakiwa kuwe na vithibitisho kuwa wanandoa hao wametengena kwa muda gani na lini hasa ilikuwa mara ya mwisho kufanya ngono.

Kama bado wanaishi pamoja lakini "hawalali kitanda kimoja" bado haitoshi kumshawishi mtu yeyote kuwa wawili hao hawana ndoa. Ndio maana siku zote wanandoa wakitengana hushauriwa kuishi mbali-mbali kwa muda fulani (nadhani miaka miwili or something) ili Talaka yao Kisheria baade ije kuwa Valid.


Kama Jamaa hampi mapenzi, attention wala affection kutokana na kutumia muda mwingi kwenye Internet na pengine nje ya nyumbani pale anapokuwa na wewe ni wazi kuwa huyu mwanamke anahai ya kudai au hata ku-demand vitu hivyo na kila akifanya hivyo mumewe anakuwa mkali na kuzusha mabaya juu ya mkewe kwa vile tayari amejenga mapenzi na wewe hali inayomfanya mwanamama huyo kuomba msamaha kwa mumewe.


Mimi na wewe hatujui undani wa maisha yao ya kindoa as hayatuhusu, lakini kama kweli huyu Jamaa angekuwa hana nia na mkewe na anataka kweli kumtaliki basi angekuwa muwazi tangu mwanzo kuwa anafamilia lakini uhusiano wao sio mzuri na sio kukudanganya kuwa Mkewe kaolewa nje ya nchi.....hilo Mosi. Pili, angekuwa anaisha pake yake mahali, Tatu angekuambia tangu awali kosa alilofanyiwa na mkewe ambali anashindwa kumsamehe.

Mmekuwa kwenye uhusiano kwa muda wa miaka miwili ikiwa na maana ulinza na huyu Baba ukiwa mtoto wa miaka 22. Ktk umri wa miaka 24, mimi binafsi nisingekushauri kujikita na kuendelea na uhusiano na mtu ambae tayari alioa/ameoa na watoto kwani haitokupa Amani kwenye maisha yako yote, hasa ukizingatia kuwa sasa umekwisha anza kuhisi guilt kila unaposikia sauti ya mke wa jamaa akiomba msamaha n.k.

Sio tu utakuwa unadhurumu ujana wako bali utakuwa umeumiza mwanamke mwenzio na watoto ambao walikuwa matunda ya ndoa yao. Si huyu jamaa wala yule wa zamani...wote hawakufai.

Nakushauri umalize uhusiano na huyo Mume wa mtu kisha anza maisha yako upya, kumbuka kuwa unahitaji mwanaume ili ku-share nae mapenzi na sio mwanamke mwingine wala watoto wao.

Kitu cha mwisho ningependa kukisema ni kuwa, huyo jamaa sio tu kuwa anaroho mbaya kiasi cha kushindwa kumsamehe mkewe kwa kosa analolijua yeye pia hana heshima kwa wanawake wote kwa ujumla kwa sababu zifuatazo:-

-Kukudanganya wewe mwanamke on your face.
-Kumuweka mkewe kwenye loudspeaker.
-Kukuonyesha sms za mkewe.

Ukiangalia points hizi kwa undani ni kuwa alikuwa anajionyesha kwako ni namna gani basi "anatakiwa na mkewe" hivyo ukileta ujinga wakati wowote atarudi kwa mkewe.

Kila la kheri ktk kufanyia kazi yote uliyoshauriwa na kwenye kufanya maamuzi ya busara.

Friday

Nimetambulisha mchumba via simu, sasa hapatikani-Ushauri

"Nina msichana wangu nasoma naye chuo kimoja nje ya nchi na tumekuwa na mahusiano ya kimapenzi kwa kipindi cha miaka miwili sasa. Nampenda na yeye anaonyesha dalili zote za kunipenda mimi. Kila kitu nikimwambia huwa ananielewa haraka kitu ambacho ni muhimu sana kwangu.

Mwezi huu wa Tisa amepata likizo ya kurudi Tanzania, ndipo nikachukuwa nafasi hiyo kutaka uchumba wangu ujulikane kwa wazazi hivyo nikamuelekeza kwetu na akafika. Mimi nikawatambulisha wazazi wangu kwa njia ya simu kuwa huyo ndie chaguo langu yaani ndie atakuwa mke wangu baadaye.

Wazazi waliniunga mkono!! ila kuna kitu nashindwa kukielewa naomba ushauri wenu, tangu mpenzi amefika kuna line ya simu anaitumia ambayo ina tatizo la kutopiga huku nilipo hata kutuma message. Yaani akitaka kupiga au kutuma message hadi atumie namba ya mama yake au ya dada yake sasa sometime ikitokea watu hao wanakuwa na shughuli zao au hawapo ndio hatuwasiliani kabisa hadi mimi nimpigie.

Nilimwambia mchumba abadilishe hiyo line akaniambia atabadilisha, sasa ni Mwezi umepita line bado anayo ileile na sidhani kwamba hana hela. Je hapa kulikoni? naomba ushauri wenu wadau."

Dinah anasema: Hongera sana kwa kuchumbia! Asante kwa mail na uvumilivu wako pia. Tatizo lako ni kutojiamini hali inayopelekea wewe kushindwa kumuamini mwenzio. Natambua ugumu wa kuwa na mpenzi mbali na wewe, lakini ukiwa na ukosefu wa kujiamini inakuwa even harder!

Ni kweli mawasiliano kwa baadhi Network Bongo huwa magumu kwani ni lazima vyombo hivyo vya mawasiliano kuwa na "ubia" na vyombo vya mawasiliano vya nchi husika ambayo wewe unaishi ili kufanikisha mawasiliano(nilipata usumbufu huo nilipokuwa nawasiliana na mtu aliyekuwa akitumia Zantel). Hivyo hili lisikupe hofu sana au hata kumfikiria mwenzio mabaya.


Huenda suala la yeye kubadilisha mtandao/line ni rahisi sana kulifikiria, lakini tambua kuwa huyu Binti kaenda nyumbani kuonda ndugu zake baada ya muda mrefu kuwa mbali nao, wewe ulikuwa nae kila siku na baada ya muda huo mfupi utaendelea kuwa nae.


Kibongo-bongo, unapokwenda nyumbani kila mtu anapenda ku-spend muda na wewe kwa vile hawajakuona kwa muda mrefu hivyo inatokea kuwa unakuwa busy sana na shughuli za kifamilia na suala la kubadili nambari ya simu ili kukuondoa hofu wewe mpenzi linakuwa la mwisho kwani anajua moyoni anakupenda na anawasiliana na wewe kupitia Mama na ndugu zake wengine, ktk hali halisi hii ingekufanya uwe na Amani myoni kuwa yupo na watu unaweza kuwaamini, imagine angekuwa anawasiliana na wewe Via rafiki au kibanda cha Simu?

Ni matumaini yangu ulifanyia kazi vema maelezo ya wasomaji wangu. Naamini Mpenzi sasa amerudi na kila kitu kiko sawa, nawatakia maisha mema yenye amani na furaha na Mungu awajaalie mfunge ndoa na kuishi maishamarefu ya ndoa.

Pamoja na mambo mengine mengi Uamininifu ni nguzo muhimu ili kuwa na uhusiano bora wenye kuzaa ndoa thabiti.
Kila la kheri.

Sunday

Je anaweza kumsamehe Ba'Mkuu?-Ushauri.

"Dada Dinah mie nakuja tofauti kidogo. Nimekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Kijana mmoja kwa mwaka na nusu sasa. Nampenda na pia nadhani yeye ananipenda kwani huwa ananifanyia yote ambayo mimi nahisi ni kwaajili ya mapenzi yake kwangu.


Kipindi cha mwaka tumeishi pamoja baada ya yeye kuja na idea ya kusave ili tufunge ndoa mwakani, maana yake huku tunakosihi maisha ni ghali sana. Kwa vile ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuishi na mwanaume nyumba moja nikamuomba mpenzi ahamie kwangu badala ya mimi kuhamia kwake na akakubali.


Nilifanya hivyo kwa vile nilikuwa naogopa kunyanyaswa kama uhusiano wetu hautofika mbali. Namshukuru Mungu tangu tumeanza kukaa pamoja maisha yamekuwa mazuri ukiachilia migongano ya hapa na pale na kupishana kwenye baadhi ya mambo. Tumefanikiwa kusave kiasi cha kutosha kwa ajili ya kufunga ndoa kuanza maisha kama mke na mume.

Kitu cha kushangaza Mpenzi wangu hajawahi kuzungumzia wanafamilia yake, mwanzoni nilidharau tu kwa vile sikutaka kumkorofisha japokuwa kuna donge linanikaa rohoni nikitaka kujua kwanini hazungumzii familia yake wala kunitambulisha kwao kwa simu!

Huwa nafikiria vitu vingi sana juu ya mpenzi wangu huyu lakini kwa vile nampenda huwa najipa moyo maisha yetu ya ndoa ni kati yangu mimi na yeye na sio watu wengine. Siku moja nikaamua kukaa nae chini na kuuliza kama utani tu.

Mpenzi wangu alicheka alafu akaniambia, alikuwa anasubiri mpaka baada ya kufunga ndoa ndio aniambie ukweli kuhusu maisha yake lakini kwa vile nimeuliza basi atasema na lolote nitakaloamua basi ataliheshimu. Akaendelea kuwa yeye hana ndugu wala wazazi na alilelewa na baba yake mkubwa ambae alimtesa sana.

Nilimuonea huruma sana na nikatamani kumkatisha lakini pia nilitaka kujua mwisho wa story yake. Mpenzi wangu ilimbidi atoroke pale nyumbani na kudandia treni kwenda kijijini ambako kulikuwa na bibi na babu yake, alipelekwa shule na kufanikiwa kufaulu na kuendelea na Sekondari lakini baada ya tu ya kumaliza kidato cha nne Babu akafariki Dunia.

Maisha yalikuwa magumu kwani bibi hakuwa akifanya kazi na wala hakupokea msaada kutoka kwa baba mkubwa. Akaamua kuacha shule na kuanza kufanya kazi ya kulimia watu mashamba ili aweze kupata hela ya kula yeye na bibi.

Baada ya miaka michache kupita bibi nae akafariki na yeye akabaki mkiwa, hivyo akaamua kurudi Dar ili kutafuta kazi na kwa bahati nzuri alipata kazi kwenye Ubarozi fulani kama mlinzi. Akajiandikisha Chuo cha ufundi lakini masomo ya jioni na kujilipia mwenyewe. Alifanikiwa kumaliza na kufaulu, akiwa na kiu ya kwenda Chuo Kikuu aliomba Udhamini kutoka kazini kwake kwani gharama za masomo zilikuwa juu sana.

Boss wake baada ya kusikia historia ya maisha yake na kugundua kuwa hana ndugu akamdhamini akasome nje ambako ndio tumekutana. Baada ya kuniambia yote hayo nilijisikia vibaya na kujuta kwanini niliuliza, nilimuonea huruma mwanaume mzima kutoa machozi.

Nilipomuuliza kwanini hakuwa wazi tangu mwanzo? akasema hakutaka niwe nae kwa kumuonea huruma kutokana na maisha yake ya zamani bali niishi nae kwa vile nampenda.

Je! Ni sawa kama nitamshauri mpenzi wangu amsamehe baba yake mkubwa na kurudisha uhusiano?"

Dinah anasema: Nimepitia ushauri na maelezo ya wachangiaji na wamegusia vitu muhimu ambavyo natumaini umevifanyia kazi. Nakubaliana na imani yake kuwa hakutaka umuoenee huruma kutokana na hadithi ya maisha yake ya zamani ambayo inauzunisha na alitaka umpende.

Kuna watu wanajenga mahusiano na hata kufunga ndoa na kuendelea kubaki kwenye ndoa kwa vile wanawaonea huruma na sio kuwa wanawapenda. Nikirudi kwa past yake nadhani naungana na wote waliosema chunguza ili kujua ukweli na kama kuna ndugu (watoto wa baba Mkubwa'ke) basi unaweza k uanza kuzungumza nao bila kuwajulisha wewe ni nani (unaweza kujifanya ulisoma nae n.k) ili kujua ukweli wa mambo.

Kama asemayo ni kweli basi heshimu uamuzi wake wa kujiweka mbali na Mzee huyo (kama bado yupo hai) lakini jitahidi kutafuta namna ya yeye kurudisha uhusiano na watoto wa mzee huyo aliyemnyanyasa ili kuepusha watoto wao na wenu kuja kutengeneza mahusiano ya kimapenzi n.k si unajua Dunia ni ndogo hii.

Mimi binafsi sina uzoefu sana na matatizo ya kifamilia lakini nashukuru wasomaji wamekushauri vema kabisa.

Kila la kheri!

Saturday

Mume to be anuna kwa vitu vidogox2-Ushauri

"MAMBO VIPI JAMANI?
MIE NI MDADA WA MIAKA 29, NATARAJIA KUFUNGA NDOA HIVI KARIBU MUNGU AKITUJALIA TUNA MUDA WA MIAKA 6 SASA NA TUNAISHI PAMOJA KWASASA YAANI DADA TATIZO NILILO NALO NI HUYU MWANAUME ANAPENDA KUNUNA KWA VITU VIDOGO YAANI UKIKOSEA KITU KIDOGO ANANUNA NA ANAWEZA KUONGEA MANENO YA KASHFA MPAKA NAOGOPA YANI MIMI HATA SIJUI NIFANYAJE JAMANI ANAWIVU SANA YANI NIKIPIGIWA SIMU AU KUTUMIWA MSG KOSA UNAKUTA KANUNA MARA HANIAMINI YAANI MPAKA NAKEREKA YANI NI VILE BASI TU EMBU NISHAURI DADA NIMFANYAJE HUYU MTU JAMANI MAANA ANANIKWAZA MPAKA BASI."

Dinah anasema: Mambo poua tu mdada, hujambo? samahani kwa kuchelewa kujibu. Binaadamu tumeumbwa tofauti hali kadhalika ninyi wawili ni tofauti sana kitabia, kimalezi hata matakwa yenu ni tofauti natumaini hilo unalifahamu.


Huyu mchumba wako inawezekana hajiamini hali inayopelekea yeye kushindwa kukuamini wewe hasa unapopokea sms au hata kupigiwa siku, mara nyingi mtu mwenye au alikuwa na tabia chafu kupitia simu au hata Internet huwa anakereka "Kisaikolojia" (kwa vile anajua ndio zake au zilikuwa zake yaani anauzoefu fulani hivi ) na kuumia balada ya kuuliza kwa upole na upendo "ni nani huyo ulikuwa unaongea nae" au "nani amekutumia ujumbe.


Mmekuwa pamoja miaka 6, mnapendana na mnakwenda kufunga ndoa ili kuishi pamoja maisha yenu yote hivyo basi ni vema kuanza kurekebishana sasa. Natambua kila mmoja wenu anavijikasoro ambavyo havirekebishiki so u live with them na viji-habit vyake ambavyo vinarekebishika ikiwa mhusika atakubali kuwa anavyo na vinamkera mpenzi wake.

Nini cha kufanya:
Ni ngumu sana kuwakilisha issue hiyo kwake (Kwa wanaume wengi lawama zote anabeba mwanamke) hivyo unapaswa kutumia UANAMKE wako kuandaa namna/mazingira ya kuwakilisha issue, unaweza kutumia mapenzi ya hisia na mwili, unaweza kumromantisha (kumfanyia kitu romantic), unaweza kubadili mwenendo kwamba kila unapopokea sms unasoma kisha unamuonyesha au unaifugua karibu yake ili aione, na kama ni simu basi hakikisha unamhusisha.....MF-unaulizwa simuni, "unafanya nini" unaweza kusema nipo tu hapa na Mchumba/mwenzangu/mume wangu tunapumzika. N.k

Vilevile kama unajua kuna vitu vidogo vidogo vinamuudhi na vitu hivyo wewe ndio unaevisababisha basi unapaswa "kupumzika" yaania cha kuvifanya. Baada ya muda (wiki nne mpaka miezi 2) unaweza kuwakilisha tatizo lako kwake kwa upole na upendo, hapo hatoweza kukurushia lawama zozote kwa vile tayari ulimhusisha kwenye txts msg na simu unazopokea na ukaacha vile vitu vidogo vidogo vinavyomfanya anune.


Kule kwetu tunapofunzwa huwa tunaambiwa kuwa mwanamke ndio pekee mwenye uwezo wa kubomoa au kujenga nyumba yako (not exactly ila wanatumia hii ili wewe mwanamke ujue nafasi yako na kuwa mwangalifu kwenye uhusiano ili kupunguza matatizo), Pia kumbuka maisha ya kimahusiano na ndoa sio lelemama, yanahitaji kufanyiwa kazi kila siku.


Bibi yangu aliwahi kusema kuwa "kukitokea tatizo ndani ya ndoa jiangalie wewe kwanza na jirekebishe kabla hujaomba mwenzio ajirekebishe"RIP........alitumia kuomba rather than kumtaka mwenzio ajirekebishe.

Usitegemee mabadiliko ndani ya siku au wiki moja bali muda zaidi kwa kuwasiliana, kushirikiana, kukumbushana na kuongozana.

Kila la kheri ktk kuweka sawa hili na kwenye kufunga ndoa.

Thursday

Nahisi naibiwa-Ushauri

"Nafikiri upo salama na unaendelea vizuri na shughuli zako.
Mimi ni mvulana 24, nina girlfriend ambaye tumeanza mahusiano yetu tangu tukiwa form One katika shule moja huko Kibaha mwaka 2002.

Tumeanza mahusiano ya kimwili tukiwa kidato cha tatu mwaka 04 kipindi hicho mwenzangu akiwa na miaka 16, nami nikiwa na miaka 19, nilifurahi sana siku hiyo kwani nilikuwa nakata utepe wa mpenzi wangu .

Tangu hapo ilikuwa kila baada ya mwezi tunakula goodtym mpaka tulivyomaliza kidato cha 4. Matokeo yalipotoka mimi nilichaguliwa kuendelea na kidato cha 5 ktk shule ya Azania mwenzangu hakupata nafasi na pia familiya yake haikuwa na uwezo wa kumsomesha zaidi.

Huku tulipunguza mambo flani kwakuwa elimu ilikuwa ngumu ukilinganisha na ile ya O-level, lakini tulikuwa tunawasiliana kama kawaida na mambo flani ya kizidi tulijiburudisha. Baada ya kumaliza kidato cha sita 6 mwaka 08 nilipata nafasi ya kuendelea na Elimu ya juu katika chuo cha Uhasibu Tanzania Institutes of Accountancy (TIA) tawi la mbeya.

Tangu nijiunge na chuo kila nikikutana kimwili na mwenzangu naona tofauti na nilivyozoea awali kwani sasa ukipiga goli moja tu mambo yanabadilika uke wake unakuwa na maji na mda mwengine naona kama size imeongezeka.

Sielewi kabisa dada inakuaje, najiuliza au ameshaanza kugawa mali yangu?. Nikimuuliza anasema kwamba hiyo ni kawaida kwa msichana kuna kipindi huwa inatokea hivyo, nashindwa kuelewa ukizingatia sijawahi kuingiliana na msichana mwingine zaidi yake nami ndiye niliye fungua mlango wake.

Naomba unisaidie dada angu kwani naogopa asije kuniuwa na Magonjwa. Sasa nafikiria kuachana naye lakini nashindwa ukizingatia nimemzoea, nimvumilivu na tumefanya mambo mengi ya hatari ila kwa hili nashindwa kuvumilia na roho inaniuma sana, huwa najiuliza kwanini size iongezeke wakati mi ndo mfunguzi wa uke wake?.

Naomba unisaidie kwa hili dada Dinah ili nijue ukweli wa mambo ili nifanye uamuzi sahihi.Ahsante!!
HO"

Dinah anasema:Mie niko salama kabisa hapa "naholideika" tu kimtido sehemu sehemu. Asante kwa mail yako na kunivumilia pia as nilikuwa "nabizika". Sasa wewe HO rafiki yangu ulianza uhusiano wa kingono yeye akiwa na miaka 16, ni mtoto na mwili wake ulikuwa bado unajengeka.

Wakati mwili wake unaendelea na mabadiliko ya ukuaji mlikuwa mnaendelea kula good tyme kama ulivyosema mwenyewe hiyo inaweza kuwa sababu ya kwanza. Sababu ya pili nadhani hakuwa akifika kileleni alipokuwa mdogo, sasa amekuwa mdada (mwanamke) anapata kusikilizia utamu na hatimae kukojoa......tuanze na sababu ya kwanza, sawa?

Sababu za Ukuaji:-
Hivi sasa huyu binti atakuwa na miaka 21 kama bado nakumbuka hesabu vema, umri ambao mwili wa mwanamke unakoma kukua yaani yale madadiliko kutokana kuvunja ungo yanakuwa yamekamilika na sasa anakuwa mwanamke kamili yaani mwili wake uko settled...umetulia.

Kwavile alikuwa akingonoka mara kwa mara akiwa ktk kipindi cha ukuaji mwili wake ukatend kukubali mabadiliko ya kingono yaliyosababishwa na uume wako na kuendelea kufanyia kazi sehemu hiyo kama ilivyo, sasa baada ya kuwa mwanamke wa miaka 21 ni kawaida kabisa kwako kugundua mabadiliko kama hayo na kwa kifupi wewe ndie uliyesababisha.......wazazi huwa wanasema acha kuharibu watoto wa wenzako that is what they mean.

Sababu ya kutofikia Mshindo (sitokwenda kwa undani kwa sababu ya Mwenzi mtukufu):-
Jinsi mwanamke anavyofurahi tendo ndivyo ambavyo ute unaongezekana na anapofikia mshindo(kilele) basi mwanamke huyu huzalisha ute mwingi zaidi hali inayoweza kusababisha yeye na wewe mtiaji kuhisi kama vile uke umepanuka kimtindo.

Ndio maana huwa nashauri wapenzi wanaokerwa na hili kubadilisha mkao/mdindo au kumpa muda mwanamke huyo apumzike (sio lazima utoke, unaweza kubaki ndani bila kufanya kitu) mpaka mwanamke huyo atakapo kuwa tayari kuendelea na ute utakuwa umepungua au unaweza kumfuta na kujifuta uume wako kisha mkaanza upya.

Mwisho kabisa napenda kukuhakikishia kuwa binti huyo hakuchezi shere na hata kama angekuwa kifanya hivyo wala usingegundua kwa kumtia, sio rahisi hasa kama anaotoka nao wanauume wenye ukubwa kama wakoa u chini ya hapo.

Ondooa hofu na endelea kupiga kazi kwa bidii.

Kila lilojema HO.

Wednesday

Dating online bila ngono, Mume kagundua-Ushauri

"Habari za leo Dinah, Mimi ni mama Samirah wa Briton-UK nimefurahishwa na kipindi chako leo (12 -07-09). Cheating inaweza kutokea ikiwa owte au mmoja wenu anakuwa bored na hapewi attention.

Mimi nimeolewa miaka 25 iliyopita na nina watoto wakubwa tu, lakini kutokana na shughuli zangu nyingi za kikazi sikuwa na muda wa kuipa Ndoa yetu attention na matokeo yake tukawa tunaishi kama mtu na flatmate wake.

Mimi nikienda kulala mume wangu anaendelea kufanya shughuli zake kwenye Comptuter au kuangalia TV, yeye akiwa amelala mie nakuwa macho nikifanya shughuli zangu. Maisha yetu yakawa hivyo kwa muda mrefu sana.

Ikafikia wakati nikawa nakosa the attention kutoka kwa mume wangu lakini yeye akawa hajali kabisa, mwishowe nikaamua kujiunga na dating site ya wanandoa ambao wako bored (nilipewa habari na co-worker hapa kazini). Huko nilikutana na wake kwa waume na wote ni wanaume na wake zao nyumbani.

Nilikuwa muoga lakini baadae nikawa nafurahia attention kutoka kwa wanaume hao kupitia emails na hatimae nikaamua kukutana nao moja baada ya mwingine na nilikuwa nafurahia sana jinsi walivyokuwa wakinijali na kunipa the attention na sifa lukuki nyingine hata mume wangu hakuwahi kuniambia.

Kwakweli nilibadilika na kuwa mwanamke mwenye furaha sana na nikabadilika kimavazi kwani zile sifa zilinilevya ukizingatia wengine walikuwa wakiniambia nikivaa magauni ya hivi napendeza zaidi na umbile langu linaonekana vizuri zaidi, basi mie nikawa nanunua nguo kwa mitindo hiyo ili kupendeza zaidi kwa nje na kujisikia vizuri kwa ndani.

Pamoja na kukutana nao hao wanaume kwenye dates sikuwahi kushawishika kufanya nao ngono, siku zote niliishia kuongea kuhusu maswala ya kimaisha, matatizo ya ndoa zetu, wale wanaume waliokuwa wakijaribu kutaka kwenda zaidi ya maongezi mara nyingi nilikuwa siwapi nafasi ya kukutana na mimi tena na wala sikuwa nikiwajibu.

Kwa bahati mbaya Rafiki wa Mume wangu alijiunga kule na ndio ukawa mwisho wa maisha yangu ya ndotoni kwani aliliona profile langu na moja kwa moja akaenda kumueleza mume wangu. Mume wangu alikasirika sana na tukagombana sana siku hiyo, lakini mie nikamuambia mume wangu kuwa yeye ndio chanzo kwani alikuwa akiniona kama vile fenicha ndani ya nyumba, nimpikie, nimfulie, nimuandalie mahali pa kulala na yeye anachofanya ni kula, kulala, kwenda kazini nakurudi.

Mume wangu akaondoka kwa hasira huku akisema tunahitaji kupeana nafasi na atakuwa Hotelini, mume wangu tangu atoweke hapa nyumbani hajaongea na mimi bali watoto wake wetu tu ndio anaongea nao na huenda kumtembelea huko hotelini. Watoto wetu hunipa habari baba yao anaendeleaje.

Dinah mdogo wangu, mume wangu nampenda sana japokuwa alikuwa nakasoro zake na kweli nilijibu kwa hasira nikidhani kuwa atakubali kosa na kunipa nafasi nimueleze ukweli wa ile dating site, lakini hakunipa nafasi hiyo.

Namtaka mume wangu kuliko nilivyokuwa nikimtaka mwanzo, sasa ni heri niwe nae nyumbani na sipati attention kuliko kukosa vyote. Yeye simuoni na attention haipo mara saba zaidi.

Naomba wanablog na Dinah mnipe ushauri ili mume wangu arudi nyumbani."

Dinah anasema: Habari ni njema tu Mama Samirah, asante kwa mail yako. Natambua pea nyingi sana hujisahau au niseme husahau kuwa kuna uhusiano wa kimapenzi ndani ya ndoa yao mara wanapozingwa na shughuli nyingi za kikazi.


Kutokana na maelezo yako nimegundua makosa mawili, Mosi ni uamuzi wako wa kumsaliti mumeo na kwenda kukutana na wanaume wengine, haijalishi kama uliwapa mwili (ngonoana) au la! Muda ulioutumia kwenda kutafuta, kujiandikisha na hatimae kuwa unakutana na hao wanaume nje ya ndoa yako ndio muda ambao ulipaswa kuutumia kurudisha romance ambayo ingeokoa ndoa yako.


Pili ni kumsukumuzia mzigo wa lawama yeye mumeo wakati unajua kabisa kuwa wote wawili mlijisahau au mlikuwa mnategeana au oengine mlikuwa mnadhani kuwa mmekuwa wazee kupeana attention kama wapenzi.

Badala ya kumuambia kuwa yeye ndio chanzo ulitakiwa kumuomba msamaha kwani wewe ndio uliyemtenda mwenzio, hata kama alikuwa hakupi attention bado alikuwa anakuheshimu na kukuthamini na kutumia muda wake nyumbani.


Ni wazi kuwa Mumeo amehama hapo nyumbani baada ya kugundua kitendo chako ili kupata nafasi ya kufukiri kabla hajafanya uamuzi kwa faida yake na watoto wenu, sasa unachotakiwa kufanya ni kama ifuatavyo:-

Mosi, ni kuomba msamaha kwa kumsingizia kuwa yeye ndiye aliyesababisha wewe kuibua tabia chafu na kumsaliti. Kama alivyoshauri mmoja kati ya wachangiaji, unaweza kutumia Kadi, Emails au barua (kizamani) ambayo actually siku hizi ni more romantic kuliko emails na Kadi. Hakikisha unaandika maneno yako kutoka moyoni na sio kuCopy na kuPaste kisha unaPrint.

Pili, kubali kuwa ulikuwa mjinga, mbinafsi na mwepezi kushawishika kirahisi na kufanya ulichokifanya, jutia kosa lako na kubali lawama zote ikiwa atazitoa juu yako (kumbuka you want him back ukianza ubishi utakuwa unamuongezea hasira)

Tatu, wakati unakili kuwa wewe ndio wa kulaumiwa, tumia nafasi hiyo kusema ukweli kuhusu kile ulichokuwa unakikosa lakini pangilia maneno ambayo hayatamfanya ajisikie alikuwa kajisahau (again, kumbuka wewe ndio unamtaka Mume asikutaliki hivyo kuwa mwangalifu), Mf: badala ya kusema kuanzia sasa tupeane attention.....unaweza kugeuza kibao na kuahidi kuwa utajitahidi kugawa majukumu na muda wako kati ya kazi na yeye n.k

Nne, kamwe usizungumzie wanaume wangapi umekutana nao na wapi mlikuwa mkikutana au nini walikuwa wakikuambia. Lakini ikiwa atataka kujua kama ulifanya ngono nje ya ndoa yenu basi sema ukweli (hapa umesema hukukutana nao kimwili) mhakikishie hilo kwa kusema wazi hisia zako juu yake, namna unavyomthamini kiasi kwamba huwezi kutoa mwili wako kwa mwanaume mwingine yeyote, sema hakuna mwanaume yeyote anaestahili mwili wako bali ni yeye mumeo na mengine yote ujuayo kuhusu kumfanya mwaname ajisikie Safiii!

Tano, mpe muda wa kufikiri mara baada ya kumuomba msamaha na kumueleza ukweli. Usilazimishe aje nyumbani haraka na badala yake muonyeshe namna unavyompenda kwa vitendo zaidi (kumbuka ahadi ulizompa), hakikisha yote uliyosema unayafanya kwa vitendo.

Kuwa mvumilivu kwani haweza akaamua kukusamehe na kusahau hapo hapo, atahitaji muda. Pia kumbuka kuna mtu wa tatu hapo anahusika ambae ni rafiki yake. Huyu rafiki (inategemeana na urafiki wao) anaweza akajenga au kubomoa ndoa ambayo tayari inaufa.

Hivyo basi, kama unauhakika kuwa huyu rafiki ni wa Damu basi unaweza kumtafuta huyu Bwana na kumueleza ni jinsi gani unampenda mumeo na watoto, ni namna gani ungepeda ndoa yenu iendelee kuwepo. Mwambie ni vipi unajisikia vibaya kwa kitendo ulichokifanya kwa rafiki yake ambaye ni mumeo, Weka wazi hisia zako za kimapenzi kwa mumeo mbele ya huyu bwana.

Hii itasaidia sana kufikisha ujumbe kwa mumeo ambao utajazaia yale uliyokwisha mueleza mumeo, hasa ukizingatia yeye ndiye aliyepeleka ujumbe wa dating site.

Baada ya hapa, watumie watoto ili kupata date ya familia ikiwa ni pamoja na baba yao, watoto siku zote wanapenda baba na mama kuwa pamoja hivyo haijalishi ni uchafu gani umefanya na utawaumiza lakini kama nia ni kurudiana watoto watasaidia kwa kiasi kikubwa sana kufanikisha hilo.

Kwa sasa nikuachie hapa ili ufanyie kazi Ushauri wa wachangiaji wengine na ule kiasi niliokupatia live kwenye radio siku ya Kipindi.

Kila la kheri.

Tuesday

Nafasi ya Wife, Unapogundua mtoto si wako-Ushauri

"Mie nafurahia sana jinsi unavyosaidia watu sijui ni kipaji au ulisomea haya mambo ya kushauri watu. Leo na mie natoa uzoefu wangu wa maisha ya ndoa naamini kuwa utasaidia wanablogu hii na wasomaji wengine kuwa makini na wapenzi wao.

Mie nimeolewa miaka saba iliyopita na tumebarikiwa kupata watoto wawili. Wakati tunachumbiana na mume wangu aliwahi kuniambia kuwa alizaa na mwanamke mwingine na waliachana miaka michache kabla hajakutana na mimi.

Ukweli sikujisikia vizuri kuwa na mwanaume aliyezaa na mwanamke mwingine lakini alinihakikishia kuwa haikuwa wazo lake kuzaa na yule mwanamke ila mwanamke yule alijilengesha ili Mume wangu asimuache wakati ule wako pamoja. Nilijitahidi kumuamini lakini bado nyuma nilikuwa nasumbuliwa na maswali kibao.


Mume wangu hakuwa akijihusisha sana na mwanamke yule isipokuwa kama mtoto anahitaji mahitaji muhimu ambayo yule mwanamke hawezi kutimiza au kama mtoto anaumwa, basi mume wangu akiwa kwenye heka heka za kumshughulikia mtoto wake mimi nilikuwa naumia sana nikifikiria mambo mengi ya kimaisha na uhusiano kati ya watoto wetu na mtoto huyo wa nje ya ndoa wa mume wangu.


Siku moja nikamuomba mume wangu amlete mwanae hapa nyumbani ili ajenge uhusiano na wanangu, lakini mume wangu alikataa kwa madai kuwa ni mapema kwake kufanya hivyo. Nilimuelewa na nikaheshimu uamuzi wake. Siku zikapita na sasa inakaribia mwaka mume wangu hajagusia lolote kuhusiana na mtoto wake huyo wala mama wa mtoto huyo kama ilivyokuwa zamani.

Juzi juzi hapa basi tukapata wageni kutoka upande wa mume wangu, kwa bahati nzuri tunaelewana sana na tunaongea mambo mengi tu kuhusu maisha. Mmoja kati ya mawifi zangu akagusia kuhusiana na mtoto wa nje wa mume wangu akaniuliza kama najua kuwa mume wangu alizaa nje. Mie nikajifanya kuwa sijui ili nipate umbea zaidi manaa yake wao walikuwepo na kaka yao na huyo mwanamke kabla mimi sijatokea kwenye maisha ya kaka yao.

Wifi yangu alizungumza mambo mengi ya kutisha na kusikitisha kuhusiana na uhusiano wa kaka yake na mwanamke aliyezaa nae. Kilichonitisha ni mwanamke yule kwenda kwa mganga ili mume wangu wakati huo alikuwa bwanake wafunge ndoa.

Wifi alinisimulia harakati zote walizozifanya mpaka kumpeleka kaka yao kwenye maombi na kufanikiwa kumtoa kaka yao kwenye maisha ya mwanamke yule na mwaka jana wakaamua kufunga safari na mtoto yule mpaka Afrika ya Kusini na kufanya vipimo vya DNA na kugundulika kuwa mtoto yule kumbe hakuwa wa damu wa mume wangu.

Baada ya maelezo hayo nikakumbuka safari ya mume wangu kwenda Afrika kusini kwa wiki moja na aliporudi alikuwa kama mgonjwa mie nikadhani ni uchovu wa safari. Pia nikagundua kwanini mume wangu alikataa kumleta mtoto yule pale nyumbani na kwanini siku hizi hazungumzii kuhusu huyo mwanamke wala mtoto wake wa nje.

Nashukuru Mungu nimejua ukweli kuhusu lakini nasikitika na kushangazwa na kitendo cha mume wangu kukaakimya kipindi chote cha mwaka mzima bila kunieleza lolote juu ya DNA au kuniambia tu kwa kifupi kuwa yule mtoto sio wake. Kwanini ananichunia kuhusu suala hilo wakati mwanzo alinihusisha?

Je itakuwa sahihi kama nitamuuliza? Kama ndio je nitaanzaje kuuliza ili aseme mwenyewe badala ya yeye kuja kugundua kuwa dada yake ndio aliyetoboa siri kwangu?

Mwenzeni hapa nilipo sielewi nini cha kufanya pia namuonea huruma mume wangu kwani najua kabisa anaumia na kujuta ndani ya moyo wake kutokana na muda alioupoteza kwa mtoto yule.
Mrs Mwilima, Dar es Salaam."

Dinah anasema:Mama Mwilima shukrani zikufikie kwa ushirikiano wako. Mimi binafsi sidhani kama ni sahihi kwa wewe kumuuliza mumeo kitu ambacho hakipo tena kwenye maisha yake. Hata mimi nahisi kuwa Dada mtu ambae ni wifi yako alitumwa na familia ya mumeo kukueleza wewe ukweli huo ktk mtindo wa siri, hii inawezekana ni ktk harakati za kuzuia mumeo kuumia zaidi kwa kujibu maswali mengi zaidi kutoka kwako kama mkewe (una haki zote za kujua kila kitu kuhusu mumeo).

Nini cha kufanya:Sahau kuwa mumeo alikuwa na mtoto kwani imejulikana sio wake, hivyo hakuna sababu ya kushupalia kitu ambacho hakipo tena na badala yake zingatia hali ya sasa ya mumeo. Natambua mumeo anahitaji muda ili kupona maumivu hayo (mwaka mmoja hautoshi kuponya maumivu yaliyowekwa kila siku ndani ya miaka yote aliyoishia kidhani mtoto ni wake), na wewe mkewe ndio mtu pekee utakaefanikisha uponaji wake wa haraka ili wote kwa pamoja muanze kuishi maisha yenye furaha na amani kama zamani.

Mpe ushirikiano mumeo, muonyeshe mapenzi ya kihisia zaidi na kumjali ktk kipindi hiki kigumu cha kukabiliana na masumbufu ya Kiakili na Kisaikolojia usikute hata Kiuchumi kwani Miaka yote hiyo alikuwa akipenda, kujivunia, kujali na akihudumia mtoto wa mwanaume mwingine akidhani ni wake.

Wewe pia unatakiwa kuwa mvumilivu kwani kipindi hiki mumeo anaweza akawa na hofu juu ya watoto wenu hao, inawezekana kabisa akawa anajiuliza mara nne-nne kama kweli ni wake au analelea mtu mwingine?

Ukiona hali yake inaendelea kuwa hivyo basi nakushauri wewe na wanafamilia kushirikiana na kumtafutia msaada wa Therapy ili kukubali ukweli, kusahau yaliyopita ili aweze kuendelea na maisha yake.

*****Haya mambo yapo sana na yanasikitisha lakini ukweli unabaki pale pale kuwa mama ni mtu pekee anaejua baba wa mtoto, Mtu unapoambiwa "huyu mwanao/mwanangu" Kisaikolojia watu wanaweza kuona mtoto kafanana sana na wao au babu, bibi, baba, shangazi yake n.k. lakini ukweli ni kufanya hiyo DNA Test kama unawasiwasi.

Kila la kheri Mrs Mwilima.

Sunday

He's too busy kuwa na mimi, nampenda-anipenda-Ushauri

"Hi dinah,

Mimi ni msichana wa miaka 27, nina mpenzi ambaye tulianza mahusiano yetu tangu 2007. Tulipoanza mapenzi yetu yalikuwa motomoto, tulionana mara kwa mara na tulielewana vizuri tu. Ilifikia mahali na kunitamkia kwamba ifikapo October 2009 tutafunga ndoa.

Kwa kweli nilifurahi sana, kwasababu ni mtu ambaye ananijali sana. Chakushangaza kadri siku zinapozidi kwenda amekuwa bize sana na promises zimekuwa nyingi. Tunapopanga kuonana au kutoka out mara nyingi hatokei, nikimtumia sms anaweza asijibu kabisa, then baadaye anatoa sababu zisizokuwa za msingi na kusisitiza kwamba bado ananipenda sana.

Isitoshe sijamuuliza kuhusu ahadi aliyoitoa ya ndoa maana naona kama nitamforce. Kwa kweli naumia sana moyoni kwa sababu hana muda na mimi yuko bize kupita kiasi, lakini anadai ananipenda.

Sitaki kumjibu vibaya wala kumtamkia its over kwasababu nampenda nataka aje kuwa baba watoto wangu lakini ananiumiza kwa sababu ya the way he treats me. Naomba ushauri wako kwasababu kuna kitu kimenikaa moyoni nashindwa hata la kufanya.

Nimejitahidi kukaa kimya lakini wapi bado ananipigia simu na kunitumia sms bado kuwa bado
ananipenda. Sasa najiuliza mapenzi gani haya wakati mtu mwenyewe hana muda na mimi, muda wote ni wakazi ambayo anafanya hapahapa Dar.

Ni mimi mdau,
mery."

Dinah anasema: Hello Mery, asante kwa mail na ufafanuzi kuhusu umri wa mpenzi wako ambao hakika ni umri ambao vijana wehu huanza kutulia kiakili (anakaribia miaka 31). Nakubaliana na wewe kwenye swali la "mapenzi gani haya wakati yeye hana muda na mimi?".

Kutokana na tabia yake (kwa mujibu wa maelezo yako) kuna mawili-matatu yanawezekana:-
(1)-Inawezekana ni kweli anashughuli nyingi za kikazi zinazomzuia kukutana na wewe.

(2)-Vilevile kuna uwezekano mkubwa tu kuwa anaendesha maisha kivingine na anakuweka wewe kama spare tire incase huko aliko hakutokwenda atakavyo.

(3)-Hana mpango wa kuwa na wewe tena ila hajui namna gani ya kumaliza uhusiano hivyo anafanya hivyo ili wewe ukate tamaa na uchoke kumsubiri na hivyo u call it a day.

Kwanini basi nimedhania hivyo? Kwa sababu huyu bwana alikutamkia kuwa atakuoa au mtafunga ndoa mwezi wa Kumi mwaka huu lakini hakuchukua hatua zozote zinazoendana na matamshi yake Mf-Kujitambulisha kwenu na kupewa utaratiubu wa kufunga ndoa na wewe na hatimae kuanza maandalizi...mwezi Octoba sio mbali na nijuavyo mie maandalizi ya kufunga ndoa hasa kwa kufuata taratibu za kijamii Tanzania huchukua muda mrefu.

Kwenye uhusiano wenu kuna ukosefu wa mawasiliano, kwa maana kwamba hamzungumzii maisha yenu kama wapenzi kwa uwazi, wewe unadhani kuzungumzia ahadi yake ni kama kumlazimisha na yeye huenda anahisi kutokuzungumzia kwako suala la ndoa ni dalili kuwa huna mpango wa kuolewa nae au hauko tayari.

Unajua, kuna tofauti ya kati ya kukumbushia jambo ktk mtindo wa kuzungumza na kukumbushia jambo hilohilo ktk mtindo wa kudai/lazimisha (demand).....napata picha hapa kuwa hukujua tofauti hizo na wewe ukadhania kuwa kukumbushia ni ku demand yeye afunge ndoa nawe.

Nini cha kufanya: Kwa unampenda mpenzi wako na unaamini kuwa na yeye anakupenda lakini kwa bahati mbaya hatujui ni nini hasa kinasababisha yeye kuwa hivyo alivyo, fuata haya nitakayokueleza ili kupata ukweli utakao kusaidia kufanya uamuzi wa busara....

Naja midaz....

Pages