Tuesday

Naomba Ufumbuzi wa Haraka nisimpoteze Mpenzi!

"Habari da Dinah? I hope wee mzima na unaendelea na shughuli nzito ya uelimishaji wa jamii. Am greatful topics zako nyingi zimenisaidia. Mimi ni mdada mwenye umri wa miaka 24, nina ujauzito wa miezi sita na nusu sasa.
Niliposhika mimba nilipata taabu ya kutapika na kushindwa kula kwa miezi kama 4 hivi. Mpenzi wangu alivumilia sana kwani nilimfanyia visa sana ingawa haikuwa makusudi.
Sasa shida ya kwanza ni kwamba anataka tufanye mapenzi lakini mimi nashindwa kwani uchafu umezidi kutoka na ni mwingi mno mpaka inakera, imefikia hatua navaa pantyliners kila siku.
Hii hali inanifanya nihisi kama vile mpenzi wangu hatosikia raha na mimi sipendi kuwa weti hivyo kwani nasikia kichefuchefu lakini wakati huohuo sitaki mpenzi wangu anaitelekeze.
Pili Sehemu zangu za siri zimebadilika rangi na kuwa nyeusi wakati rangi yangu ya ngozi ni lighter kiasi, pia nikinyoa natokwa na vipele vidogo vidogo, sasa sitaki mpenzi wangu anione nikiwa hivyo, je nitaondoaje vipele na kurudisha rangi yangu ya awali?
Nilikwenda kwa Gyno wangu kuangaliwa na sikuwa na maambukizo yeyote
Je kuna dawa asilia ambayo naweza kuitumia? maana hizi dawa za kizungu nyingi hazifai kutumiwa wakati wa ujauzito.
Tatu Matiti yangu yanauma na kuwasha sana, basi huwa najikuna mpaka najikwaruza ili kupoza napaka mild steroid lakini wapi!! Sasa how will we have sex when matiti yako hivyo?
Nne Mpenzi wangu hupenda mwili wangu ukiwa bonge kiasi, sasa kpindi cha miezi 4 nilipokuwa naumwa na kushindwa kula nimepungua sana, yaani na tumbo langu kubwa bado sijafikia mwili wangu kabla ya ujauzito kwani nilikuwa a bit kibonge.
Mpenzi kaniletea Dada zake waje kunisaidia kupika ili nile na kuwa na afya lakini wapi! alafu mbaya zaidi ni kuwa nikikonda naonekana so terrible na I really feel unattractive na i think nikikubali kumvulia nguo hatoniona navutia tena. Sitaki kumpoteza mpenzi wangu.
Kila siku natoa sababu za kuumwa, tafadhali naomba ufumbuzi wa haraka kwani mpenzi ameanza kuwa bitter and unhappy ninapomkwepa kwani anasema anataka kuwa karibu na mimi."

Sunday

Romance kuisha

Dada dinna hongera kwa ushauri wako mzuri,mimi naomba kuuliza mnaposema romance hufa kutokana na mwanamke kupoteza mvuto baada ya kujifungua au kuwa na watoto mbona unakuta mwanaume anatoka nje ya ndoa na anakuwa na uhusiano na mke wa mtu ambaye tayari naye ameshazaa na ana watoto je hiyo imekaaje?
Kwenye topic "Kwanini Romance hufa baada ya kipindi fulani kwenye ndoa"
Umesema b

Nimevumilia tofauti zake kwa Ex, ila hili lanishinda...

"Habari da Dinah!
Jamani nimeshawishika kukuchagua wewe kama msaada kwangu, umri wangu ni miaka 29ti mwenye jitihada sana katka maisha. Kinachonikatisha tamaa ni mpenzi wangu ambae simuelewi kama ana ugonjwa au la, maana ni miezi tisa sasa hanifikishi kila tukianza kufanya mapenzi.

Hali hii aliyonayo mpenzi wangu hakuwepo awali, imejitokeza mwaka huu na sasa ni mwezi wa tisa anawahi kukojoa sekunde chache tu tangu tuanze tendo. Imefikia hatua ya kujichua mwenyewe na hata kufikiria kutoka nje ya uhusiano wetu ili niridhike kingono...so horrible!

Licha ya tatizo hilo nimekuwa nikivumilia tofauti alizonazo compared to my ex relations, ukweli ni kuwa he is not smart as my either he is romantic, nimejaribu kum-pimp atleast aweze kunivutia  lakini habadiliki, yaani ni kama anapuuzia vile.


Tatizo ni uoga wa kumuacha kwani ataniona kama namkimbia kwa mapungufu aliyonayo kimwili na kikazi. Nisaidieni mwenzenu kwani nahisi nina mwanaume jina. Asanteni"

Nifuate ndoa nchi nyingine, niache ajira?-Ushauri

"Dada Dinah na wachangiaji wote, tafadhali naomba ushauri au mawazo kwani nipo kwenye kipindi cha kufanya maamuzi magumu.

Nina mchumba wangu ambae tunataka kufunga ndoa, lakini nitakapofunga ndoa nitalazimika kuhama kutoka Nchi moja kwenda nyingine na kuacha ajira yangu.

Kinachonichanganya hasa ni suala la kuacha kazi, yaani mawazo juu ya hilo hunipa maumivu ya tumbo na huonga huniingia.

Naomba ushauri kutoka kwa yeyote aliyepitia hii hali katika maisha yake, asanteni"

Pages