Friday

Nipo na Mpenzi alie-cheat on her X with Me, je anaweza kuni-cheat na mimi?

"Hallo dada Dinah, Nakupongeza kwa kazi nzuri ya kuelimisha jamii kwa maswala mbalimbali ya mahusiano na mapenzi. Hongera sana.

Mimi ni kijana mwenye miaka 33, nina mpenzi niliyekutana naye mwaka mmoja uliyopita na tumeanza kuishi pamoja tangia mwezi wa kumi mwaka 2010. Nina maswali mawili. Mpenzi wangu alishawahi ku-cheat na mpenzi wake wa zamani ambao waliokuwa pamoja miaka 7.

Kwa maelezo yake miaka miwili ya mwisho mpenzi wake wa zamani alikuwa anamdangaya mambo mengi na akapoteza trust kwake, mapenzi yakapungua na kwa kipindi hicho cha miaka miwili wakawa wanaishi nchi tofauti ila walikuwa wanakutana mara moja kwa mwaka kwa mwezi mmoja.

Swali la kwanza;Anadai alim-cheat jamaa yake na mimi na ndio ukawa mwisho wa mahusiano yao. Hivi mwanamke kama huyu anaweza kuaminika kwa mahusiano ya kudumu na mimi?

Mimi binafsi niko commited kuwa naye bila ya kuwa na mwanamke mwingine ila nahisi kama alivyofanya kwa wa zamani yanaweza kunitokea na mimi. vipi maoni yako na wachangiaji wengine kuhusu hili?

Swali la pili: Ninamridhisha mpenzi wangu huyu kwa ratio ya 6:10 yaani kwa kufanya mapenzi mara 10 mara 6 anakuja. Swali ili mwanamke kuridhika na mwanamme kabisa anapenda afike mara zote kumi? yaani kila mkifanya mapenzi lazima aridhike(akojoe)? ninakuwa sina furaha hizo siku ambazo hafiki.

Je mwanamke akiji-stimulate Clitoris akiwa on top huku uki-pump na akafika, itatafsiriwa kama amekuja kwa Vaginal orgasm au Clitoris Orgasm? mimi binafsi napendelea aje kwa Vaginal Orgasm zaidi.

Pia,Je mwanamke anaweza kufurahia ngono ukiishi naye zaidi ya miaka 3 sawa na jinsi mlivyokuwa ndani ya mwaka mmoja? je hamu ya mapenzi itapungua? haitasababisha kutamani new adventure?

Asante dada Dinah".

Sunday

Nilitalikiwa Kisa Usomi, sasa nimepata mpya lakini....Ushauri!

"Hi da Dinah!
Mimi ni msomaji na mfuatiliaji wa blong yako, shortly I like it and I you as well. Nina 30years nafanya kzi kama Mhasibu Ofisini kwa mkuu wa nchi hii! Dinah tatizo langu ni kutaka ushauri kuhusiana na mwanaume nilie nae, lakini kabla naomba nikupe hadithi ilivyokuwa.

Nilipokuwa na 25yrs niliolewa na mwanaume wa Kiislam kama mimi na nikaenda Chuo soon after ndoa! Baada ya kuanza chuo ikawa ni tatizo kwa wifi zangu na Baba mkwe that kwanini nisome kabla ya kuzaa alafu pia mume wangu ni Form 4? Kwa nini nimpite kielimu?

Tatizo likandelea na likawa kubwa, Baba mkwe alimwambia mwanae achague moja a Divorce au la yeye sio baba yake. Nilipokuwa mwaka wa pili mume wangu akanishauri niache chuo nami nikakubali lakini after 2 months mama yangu akaja juu kwanini niache chuo kisa shinikizo la baba mkwe?

Nikaenda kwa mshauri wa wanachuo Chuoni for ushauri, yeye ndio akanishangaa na kuiomba nirudi Chuoni ! In a dilema nikarudi chuo na within a week wifi yangu akaniletea Talaka Chuoni ! Nusu nijiue kwa kuchanganyikiwa ila kwa sababu ni Muislam tena safi sikufanya hivyo!

Niliumia kwasaabu yeye ndio alikuwa mwanaume wangu wa kwanza na sikuhitaji mtu mwingine tena maishani mwangu! Maisha yakapita na nikamaliza Chuo salama na kuanza kazi. Siku moja nikakutana na Ex baba mkwe akiwa na shida fulani, kwenye maongezi akaniambia "mwenzio anakuhitaji tena na bado hajaoa".

Mimi nikamsaidia shida yake bila kumjibu lolote, nilimsaidia kama binadamu lakini roho iliniuma sana kwa kusikia habari kuhusu Ex hubby wangu. Kwa bahati mbaya Baba mkwe alifariki Dunia mwaka 2009 na my Ex hubby akaja kutaka turudiane lakini mimi nikakataa.

Akaanzakunifanyia fujo wherever he sees me! One night nilikutana nae wakati narudi kutoka Kitchen party alinitolea Bastola , thanks God alikamatwa na kuswekwa rumande for a long time !Niliapa siitaji tena mwanaume, ila watu na wazazi hawakukubaliana na mimi , then nikaamua kuwa na mtu ingawa nilikuwa naogopa sana!


Sasa tatizo ni kitandani, yaani kuwa zaidi ya mara kumi nilizojaribu kuwa nae kitandani akitaka kugusa tu basii "kashacheka", akijitahidi na kusimamisha tena bado anaceka kabla hajagusa. Kaenda kwa daktari, kajaribu mazoezi , kasoma article zako nk ! imeshindikana !

NIFANYEJE? Je niachane nae na kusubiri mwingine au nivumilie?
jemmy, DSM "

Nampenda Mdada alienizidi miaka 9, je naweza kuoa?-Ushauri

"Dada Dinah pole na mihangaiko ya hapa na pale ya kila siku. Mimi ni mwanaume wa miaka 23 naenda 24 sasa. Nimetokea kumpenda dada wa miaka 32 ambaye ni rafiki yangu kipenzi. Lengo langu ni kutaka kumuoa kwani moyo wangu umeridhika juu yake.

Sijamtamani kingono but I feel that I am in love with her. Hajawahi kuolewa na wala hana mtoto. Bado sijamweleza nia yangu ya kutaka tuhame kutoka kwenye urafiki tulionao kwenda kwenye uhusiano wa kimapenzi. Kwasasa mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuo kikuu hapa Tz, mwenzangu yeye ni mwalimu.

Tumekuwa pamoja kama marafiki kwa mwaka mmoja sasa. Urafiki wetu ni zaidi ya urafiki kwani tushafanya romantic talk/romance kwa njia ya simu. Naogopa kumweleza nia yangu kwani nahofia kuumiza hisia zangu ikiwa atanikatalia.

Moyo wangu unapata faraja na mateso juu yake. USHAURI ninaoomba kwako dada Dinah na wanablog wengine ni, Je kuna athari zozote yinazoweza kujitokeza kutokana age gap iliopo ikiwa tutaoana?

Na je nimweleze nia yangu au nifute wazo hilo? Wanawake mnalichukuliaje swala la kuolewa na mume mdogo kuliko mke kwa gap kubwa? NAOMBENI MAWAZO YENU NA HEKIMA ZENU. Facts are sacred, opinion are welcome and ideas are respected.

I love u All,

NB. Kilichonivutia kwake ni akili yake iliyokomaa, upendo alionao juu yangu na uelewa mkubwa alionao. Sura huwa si kigezo cha muhimu sana kwangu".

Pages