Thursday

Baba kanilea na kunisomesha, Mama anasema si baba yangu!!

"Hi Dada dinah nina matatzo sana hivyo I need your advice. Mimi ni kijana wa miaka 21, it is a long story but I wil make it short and clear. Ni kwamba, mimi nimezaliwa Kenya when my dady met with Mum there but walikuwa ni wapenzi yaani hawakufunga ndoa.


Nilipofikisha miaka 2, baba alinichukua nikaenda kuishi Moshi na bibi, anadai kuwa matunzo kwa mama hayakuwa mazuri. Tangu alivyonichukua hadi nafikisha miaka 17 Mama hakuwahi kuja kuniona wala hakutaka kujua habari zangu japokuwa hakuwa mbali sana yaani ni kiasi cha kutumia Tsh elfu3 kama nauli.


Nilipofikisha hiyo miaka kumi na saba ndio akaja kuniona. Kipindi chote nilikuwa naishi na baba tu kwani alirudi nyumbani. Sasa baada ya Mama kuja anadai eti yule niliyekuwa naishi nae na kuamini kuwa ni Baba yangu was not my father na kwamba my father is from Uganda but huyu Baba ndio ninayemfahamu, ndiye aliyenilea na kunisomesha mapka nilipofikia na hajajua hilo, kwamba mimi sio mtoto wake. Je nifanye nini?"

Dinah anasema:Pole kwa mawazo yanayosonga akili yako hivi sasa kuhusiana na ukweli juu ya nani ni baba yako wa damu. Ukweli utabaki kuwa mama siku zote ndio anajua baba wa mtoto ni nani?

Nasikitika kusema kuwa kuna akina baba wengi tu walilea na wanaendelea kulea watoto ambao Kibailojia au kidamu sio wa kwao lakini kwa vile wanashiriki tendo la ndoa na wake/wanawake zao basi hujenga ukukaribu na mimba ile na mtoto anapozaliwa huona kabisa kuwa ni wa kwake na hivyo kujenda bond kama baba hali ambayo humathiri Kisaikolojia huyu baba na hatimae kuona mtoto huyo anafanana na watu wa karibu na familia yake kama sio yeye mwenyewe.

Pamoja na kusema hivyo, sina maana kuwa huyo si baba yako na wala siwezi kukubaliana wala kukataa kuwa yule Mganda pia ndio baba yako wa damu. Kama walivyogusia baadhi ya wachangiaji huenda hata huyo Mganda sio baba yako.

Kutokana na maelezo yako inaonyesha wazi kuwa hauko interested na mwanamke huyo japokuwa ndio aliyekuzaa hivyo huna budi kumpa heshima kama mzazi wako wa kike kwani hajui kuwa mama ni nini hasa kwani sio yeye aliyekulea bali bibi yako.

Sitokulaumu kwa kupoteza interest au hata mapenzi juu ya mzazi wako huyo wa kike kwani hakutaka kujihusisha na wewe, sasa kwa vile umekuwa mkubwa na yeye anazeeka ndio kashituka na kuona hakutakuwa na mtu wa kumsaidia hapo ndio akakumbuka ala kumbe nina mtoto Tz!

Inawezekana kabisa hakujua ni namna gani atakujia na hakutaka kuomba msamaha kutokana na kujiweka mbali na maisha yako wakati ulipokuwa ukimuhitaji zaidi (ulipokuwa mtoto) na njia pekee ya kujiweka karibu na wewe ili kupata atakacho ni kupandikiza uongo bila kujali (Again) kuwa akuwa atakupa msongamano wa mawazo (stress), kuumiza hisia zako (emotional) na Kisaikolojia.

Mimi nakushauri kama ifuatavyo,
Mosi, Kamwe tena mwiko kabisa kumueleza baba yako Mtanzania kuhusu hili suala, kwani litamuumiza sana na hata kusababisha matatizo makubwa (inategemea na atakavyolipokea) sio yeye tu bali Bibi yako, ndugu jamaa na marafiki.

Ikiwezekana kaa mbali na huyo mama kwa kumwambia kuwa huitaji kuwa nae karibu kwa na asikutembelee wala kuzoea kuja hapo nyumbani na badala yake mwambie wewe utakuwa ukimtembelea huko Kenya kila unapohitaji kufanya hivyo kwani tayari wewe ni mtu mzima.

Pili, Ukisha muweka mbali tafuta wasaa na uzungumze nae hata kama ni kwa simu na umwambie yalioujaza moyo wako ikiwa ni pamoja na msimamo wako juu ya baba aliyekulea (hata iweje ndio unamtambua kama baba yako n.k) na juu yake(utampa heshima kama mzazi wa kike na hadithi za masiha yake ya ujana azi-keep mwenyewe).

Tatu, Kama unataka/ukipenda kuwa na amani moyoni juu ya Mzazi wako wa Damu basi utalazimika kum-bana mzazi huyo akupe ukweli halisi kama kweli anauhakika kuwa Mganda ndio Baba wa damu au anadhania tu lakini inawezeakana hata yeye sio baba na ukweli ni kuwa hajui baba ni nani na akaamua kusingizia wanaume wote aliotembea nao.

Usimuonee aibu wala usihisi Guilt kutokana na katabia kake kachafu ka kulala na wanaume ovyo tena bila kinga, hakikisha unam-bana akupe ukweli wote mpaka kwanini hasa akamsingizia huyu baba wa Tz na kitu gani kilimfanya asijihusishe na wewe na sasa nini kimemfanya akukumbuke (yote yalioujaza moyo wako yatoe) kwani unahaki zote za kujua kwa uhakika kama huyo Mganda ni baba wa damu au unaenda kubahatisha tu!

Akihakiki na kukupa maelezo ya kutosheleza na wewe kuhisi the argue ya kutaka kujua ukweli basi omba mawasiliano ya huyo Mganda ili ufanye nae mawasiliano na ikiwezekana kufanya vipimo vya DNA ili upate amani moyoni na sio kwenda kuanza kujipendekeza kwa mtu au hata familia ambayo huijuia achilia mbali Tamaduni zao za Kiganda.


Akisita nakuja na hadithi nyingine ambazo zinaashiria kuwa hana uhakika na Mganda, kwamba inawezekana pia sio baba wa damu basi achana na the issue na endelea na maisha yako na baba wa Tz. Wewe hautokuwa wa kwanza kulelewa na mzazi ambae sio wa damu kwani kuna watoto wengi tu wanalelewa na wazazi ambao sio wa damu lakini wanapendwa, kujaaliwa, kupewa msingi na mwanzo mzuri tu wa kimaisha kama ulioupata wewe.

Kuna watoto wanaishi na wazazi wao wa damu lakini hawapati ulichokipata wewe, kwa uzoefu wako umeona kabisa kuwa mama hakukutaka ulipokuwa mdogo na alikupa matunzo mabaya kiasi kwamba baba Mtz akahofia kuwa ungeendelea kuishi na mama huyo huenda usingefikisha miaka 21, ungejifia ktk umri mdogo sana.

Kumbuka kwenye suala la DNA, hakikisha humpi jukumu lakufuatilia kwani anaweza kuwa ana-demand pesa kwa kisingizo cha kufuatilia, hakikisha unalifanya mwenyewe na kama hakuna sababu ya wewe kufanya vipimo hivyo kwa vile una amani moyoni kuwa Baba Mtz ndio baba yako hakikisha unamuweka mama huyo mbali kabisa na familia yako ya Tz ili kuepusha matatizo ambayo yatakuathiri wewe na Baba mTz.

Kama nilivyosema awali kuwa kuna asilimia kubwa sana ya kina baba hapa Duniani wamelea na kusomesha watoto ambao sio wao wa damu, lakini kwa vile hawataki masumbuko ya akili, Saikolojia, hisia na hata kuharibu ukaribu wao wa kifamilia wanaamua kudharau maelezo ya watu wengine pia vipimo ya DNA na kuendelea na maisha yako kama kawaida.

Najipa matumaini kuwa umefanyia kazi maelezo na ushaurio kutoka kwa wachangiaji na utafanya uamuzi wa busara ili kuishi kwa amani na furaha.
Kila la kheri!

Tuesday

SMS kwa jina la kike mhusika Dume-Ushauri!

"DEAR,
MImi ni kijana mwenye umri wa miaka 24, nina mpenzi ambaye hadi sasa nimekuwa nae kwa mda wa mwaka mmoja. Mpenzi wangu huyu ni msiri sana linapokuja suala la matumizi ya simu. Kwenye simu yake inaonyesha anamtu mwingine ambae anaishi Mtwara na huwa wanawasiliiana mara kwa mara, lakini kila nikimuuliza ni nani huyo? yeye anasema kuwa ni rafiki yake na ni mwanamke.

Lakini katika uchunguzi nilioufanya nimegundu mtu huyu ambaye ni rafiki yake ni Mwanaume kwani amekuwa wanawasiliana kwa sms, akitumiwa tu sms husoma na kuzifuta haraka sana. Sasa tarehe 16/9/2009, Tulitoka na kwenda Biashara Club kwa ajili ya msosi, Mpenzi akatoka kidogo na kwa bahati mbaya akawa ameissahau simu yake mezani.


Mara sms ikaingia, kwa sababu nilikuwa na wasiwasi na mawasiliano yake ya mara kwa mara nikaamua kuisoma ile sms ikisema wakutane mda wa saa mbili usiku, wakati ujumbe umeingia ilikuwa ni saa mmoja usiku.


Namba ya huyo mtuma ujumbe imetunzwa kwenye simu kwa jina la MASA, kutokana na sms niliyo soma na kupata uhakika zaidi ambao nilikuwa nautafuta niliamua kumwambia mpenzi kuwa na hitajika nyumbani kwani kuna tatizo, sikuweza kuendelea kuwepo pale, sasa ili nijue ukweli wake nifanye nini?
Naomba ushauri wako dada.
it's me Hassan"

Dinah anasema: Hassan, pole kwa mkasa huo. Hiyo ni tabia ya watu wengi ambao sio waaminifu, wanakuwa na wapenzi nje ya mahusiano yao na kutunza mawasiliano ya simu kwa majina ya ambayo sio halisi. Mf- Kamani mwanamke watatunza kwa jina la kiume na kama ni wa Kiume basi jina litakuwa la kike.

Jambo muhimu ni kwenda kufanya vipimo ili kujua kama uko huru kutoka HIV! Kwani hali ni mbaya sana na inatisha.

Katika hali halisi unapokuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi huitaji kuwa na siri, kila kitu unachodhani ni muhimu mwenzako kujua basi utaweka wazi jambo husika, hata kama mtu huyo anampenzi mwingine kwa sababu nyingine labda za kimapenzi au kiuchumi (wapo watu wanakuwa na wapenzi 2, mmoja wa kimapenzi na mwingine kwa ajili ya pesa) pia unatakiwa kuweka wazi hilo ili huyo anaetaka uhusiano na wewe aweze kufanya uamuzi wa busara.

Nasikitika kusema kuwa mpenzi wako sio mwaminifu na kuna uwezekano mkubwa anakuchanganya wewe na mwanaume mwingine. Ni vema kama utamueleza mpenzi wako ukweli wa nini kilichokufanya uondoke usiku ule mlipokuwa nje kwa ajili ya chakula, muulize kuhusu huyo Jamaa anaewasiliana nae na kama wanangonoana n.k.

Kisha msikilize anasemaje na umwambie uwazi kuhusu msimamo wako Mf- hutaki kum-share yeye na mwanume mwingine, hupendezwi na tabia yake ya usiri. Sasa kama hakuna kinachoendelea na huyo jamaa wa SMS (mana'ke inawezekana njemba inamtaka tu lakini hajafanya nayo ngono)....mwambie Demu abadilishe tabia yake ili uweze kumuamini.

Kama walikwisha ngonoka, ni wazi kuwa mdada huyo hakufai hivyo basi achana nae na subiri kupata binti mwingine atakaejiheshimu nakuheshimu uhusiano wenu na kukuthamini wewe kama mwanadamu.

Kila la kheri!

Saturday

Namuonea huruma Soon to be Ex Wife-Ushauri

"Heloo dada Dinah, pole sana kwa kazi. Nimeona nikutumie hii mail kwa ajili ya ushauri.
Tatizo langu ni kwamba dada, mimi ni mdada wa miaka 24 nimeajiriwa. Huwa napenda sana kutembelea blogs mbali mbali na kuchat katika pita pita hizo nikakutana na mtu (Mwanaume) tukawa tunawasiliana aliniambia kuwa ana mtoto ila mama wa mtoto wametengena na yuko nje ya Tanzania kaolewa na Mwanaume mwingine na wamezaa.

Tuliendelea kuwasiliana kwa simu na kuchat kupitia internet hadi ilipofika siku tukaonana. Baada ya kuonana siku ya kwanza tuliendelea kuwasiliana kwa simu na pia kupanga miadi ya kuonana tena na tena hadi siku aliponitamkia kuwa anapenda niwe mpenzi wake.

Kiukweli nami pia nilimpenda ila kwa wakati huo nilikuwa kwenye matatizo na mpenzi wangu wa awali so nikaona haina haja ya kuendelea kuteseka wakati tayari kuna mtu anaonesha kunipenda kwa dhati.Basi tukawa wapenzi.


Tatizo lilianza pindi mpenzi wangu wa awali alivyogundua kuwa nina ukaribu na huyo mjamaa ambae kumbe anamfahamu. Siku moja akanipigia na kuniambia kuwa yule mtu ameoa tena kwa ndoa ya Kanisani na wanaishi wote na mkewe, nikamwambia mbona mimi ameniambia tofauti.

Basi ikabidi nimbane kweli huyu jamaa mpya nae akaniambia kuwa ameoa ila yeye na mkewe wana matatizo ya muda mrefu sana ambayo sio rahisi kusameheka na isitoshe huwa hawalali pamoja! na anachosubiri yeye ni ruhusa ya kupeana Talaka kwani swala lao limeshafika mbali.


Kwakuwa alikuwa ananionyesha mapenzi ya dhati, nikawa niko tayari kuendelea naye hapo nakiri kweli nilikuwa mdhaifu kwani nilistahili kuachana naye baada ya kugundua ukweli lakini tatizo ni kwamba tulishakula kiapo kuwa hatutaachana kwa namna yoyote ile.

Hadi sasa tuna muda wa miaka miwili. Ushauri niutakao ni je, niendelee na huyu mtu au niachane naye??? kwanini nataka ushauri wa hivyo ni kwa sababu nafsi inamuonea huruma sana mkewe ingawa kiukweli anaonekana wazi kuna kitu kikubwa alimkosea mumewe kwani mara nyingi huwa anamuomba msamaha naona hayo kwenye simu yake na pia huwa anapiga na huyu kaka huwa anaweka loudspeaker nami nasikia.


Ameahidi pindi atakapotengana na mkewe yuko radhi kunioa, hilo pia nahofia kwa kuwa sijui namna ya kuieleza familia yangu kwani itabidi niweke wazi kuwa alikuwa mume wa mtu kabla hawajasikia kwa watu.

Kwetu mimi ni mtoto wa pekee wa kike. Samahani kwa mail ndefu, na sijui kama nitakuwa nimejielezea vizuri ukanielewa ila kama utakuwa na maswali ya kuniuliza ili uweze kunisaidia sawa unaweza kuniuliza nitakuwa tayari kujibu ili nisiendelee kuteseka.

Asante sana, kazi njema.
Lizzy"

Dinah anasema: Mdogo wangu Lizy, mtu akishindwa kuwa mkweli mwanzoni kabisa mwa uhusiano ni wazi kuwa daima hatokuwa mkweli kwako. Kutokana na maelezo yako huyu Jamaa alikuwa anam-cheat mkewe via internet (wako wengi sana hawa viumbe wake kwa waume wanao abuse maendeleo ya mawasiliano).

Ni wazi kabisa wakati unakutana na huyu jamaa kwenye mtandao ulikuwa kwenye wakati mgumu kimapenzi hivyo kuwa Vanulable hali iliyopelekea huyo mpenzi mume wa mtu kuchukua advantage na kukulubuni. Ili aku-win akaamua kukupa mapenzi ya dhati ambayo alijua kabisa unayahitaji kwa vile ulikuwa huyapati kutoka kwa Mpenzi wako wa awali.

Kama walivyosema baadhi ya wachangiaji na pengine wewe pia unajua hasa kama ni Mkristo, kwamba Ndoa ya kikristo daima huwa haivunjiki unless mmoja wa wanandoa hao afariki. Hata kama wametengana bado hawatoruhusiwa kufungandoa tena unless mmoja wako kafa......vinginevyo labda Serikali iingilie na Talaka itolewe kwa amri ya Mahakama lakini hata hivyo mpaka Hakimu anakubali kuamrisha Talaka inatakiwa kuwe na vithibitisho kuwa wanandoa hao wametengena kwa muda gani na lini hasa ilikuwa mara ya mwisho kufanya ngono.

Kama bado wanaishi pamoja lakini "hawalali kitanda kimoja" bado haitoshi kumshawishi mtu yeyote kuwa wawili hao hawana ndoa. Ndio maana siku zote wanandoa wakitengana hushauriwa kuishi mbali-mbali kwa muda fulani (nadhani miaka miwili or something) ili Talaka yao Kisheria baade ije kuwa Valid.


Kama Jamaa hampi mapenzi, attention wala affection kutokana na kutumia muda mwingi kwenye Internet na pengine nje ya nyumbani pale anapokuwa na wewe ni wazi kuwa huyu mwanamke anahai ya kudai au hata ku-demand vitu hivyo na kila akifanya hivyo mumewe anakuwa mkali na kuzusha mabaya juu ya mkewe kwa vile tayari amejenga mapenzi na wewe hali inayomfanya mwanamama huyo kuomba msamaha kwa mumewe.


Mimi na wewe hatujui undani wa maisha yao ya kindoa as hayatuhusu, lakini kama kweli huyu Jamaa angekuwa hana nia na mkewe na anataka kweli kumtaliki basi angekuwa muwazi tangu mwanzo kuwa anafamilia lakini uhusiano wao sio mzuri na sio kukudanganya kuwa Mkewe kaolewa nje ya nchi.....hilo Mosi. Pili, angekuwa anaisha pake yake mahali, Tatu angekuambia tangu awali kosa alilofanyiwa na mkewe ambali anashindwa kumsamehe.

Mmekuwa kwenye uhusiano kwa muda wa miaka miwili ikiwa na maana ulinza na huyu Baba ukiwa mtoto wa miaka 22. Ktk umri wa miaka 24, mimi binafsi nisingekushauri kujikita na kuendelea na uhusiano na mtu ambae tayari alioa/ameoa na watoto kwani haitokupa Amani kwenye maisha yako yote, hasa ukizingatia kuwa sasa umekwisha anza kuhisi guilt kila unaposikia sauti ya mke wa jamaa akiomba msamaha n.k.

Sio tu utakuwa unadhurumu ujana wako bali utakuwa umeumiza mwanamke mwenzio na watoto ambao walikuwa matunda ya ndoa yao. Si huyu jamaa wala yule wa zamani...wote hawakufai.

Nakushauri umalize uhusiano na huyo Mume wa mtu kisha anza maisha yako upya, kumbuka kuwa unahitaji mwanaume ili ku-share nae mapenzi na sio mwanamke mwingine wala watoto wao.

Kitu cha mwisho ningependa kukisema ni kuwa, huyo jamaa sio tu kuwa anaroho mbaya kiasi cha kushindwa kumsamehe mkewe kwa kosa analolijua yeye pia hana heshima kwa wanawake wote kwa ujumla kwa sababu zifuatazo:-

-Kukudanganya wewe mwanamke on your face.
-Kumuweka mkewe kwenye loudspeaker.
-Kukuonyesha sms za mkewe.

Ukiangalia points hizi kwa undani ni kuwa alikuwa anajionyesha kwako ni namna gani basi "anatakiwa na mkewe" hivyo ukileta ujinga wakati wowote atarudi kwa mkewe.

Kila la kheri ktk kufanyia kazi yote uliyoshauriwa na kwenye kufanya maamuzi ya busara.

Friday

Nimetambulisha mchumba via simu, sasa hapatikani-Ushauri

"Nina msichana wangu nasoma naye chuo kimoja nje ya nchi na tumekuwa na mahusiano ya kimapenzi kwa kipindi cha miaka miwili sasa. Nampenda na yeye anaonyesha dalili zote za kunipenda mimi. Kila kitu nikimwambia huwa ananielewa haraka kitu ambacho ni muhimu sana kwangu.

Mwezi huu wa Tisa amepata likizo ya kurudi Tanzania, ndipo nikachukuwa nafasi hiyo kutaka uchumba wangu ujulikane kwa wazazi hivyo nikamuelekeza kwetu na akafika. Mimi nikawatambulisha wazazi wangu kwa njia ya simu kuwa huyo ndie chaguo langu yaani ndie atakuwa mke wangu baadaye.

Wazazi waliniunga mkono!! ila kuna kitu nashindwa kukielewa naomba ushauri wenu, tangu mpenzi amefika kuna line ya simu anaitumia ambayo ina tatizo la kutopiga huku nilipo hata kutuma message. Yaani akitaka kupiga au kutuma message hadi atumie namba ya mama yake au ya dada yake sasa sometime ikitokea watu hao wanakuwa na shughuli zao au hawapo ndio hatuwasiliani kabisa hadi mimi nimpigie.

Nilimwambia mchumba abadilishe hiyo line akaniambia atabadilisha, sasa ni Mwezi umepita line bado anayo ileile na sidhani kwamba hana hela. Je hapa kulikoni? naomba ushauri wenu wadau."

Dinah anasema: Hongera sana kwa kuchumbia! Asante kwa mail na uvumilivu wako pia. Tatizo lako ni kutojiamini hali inayopelekea wewe kushindwa kumuamini mwenzio. Natambua ugumu wa kuwa na mpenzi mbali na wewe, lakini ukiwa na ukosefu wa kujiamini inakuwa even harder!

Ni kweli mawasiliano kwa baadhi Network Bongo huwa magumu kwani ni lazima vyombo hivyo vya mawasiliano kuwa na "ubia" na vyombo vya mawasiliano vya nchi husika ambayo wewe unaishi ili kufanikisha mawasiliano(nilipata usumbufu huo nilipokuwa nawasiliana na mtu aliyekuwa akitumia Zantel). Hivyo hili lisikupe hofu sana au hata kumfikiria mwenzio mabaya.


Huenda suala la yeye kubadilisha mtandao/line ni rahisi sana kulifikiria, lakini tambua kuwa huyu Binti kaenda nyumbani kuonda ndugu zake baada ya muda mrefu kuwa mbali nao, wewe ulikuwa nae kila siku na baada ya muda huo mfupi utaendelea kuwa nae.


Kibongo-bongo, unapokwenda nyumbani kila mtu anapenda ku-spend muda na wewe kwa vile hawajakuona kwa muda mrefu hivyo inatokea kuwa unakuwa busy sana na shughuli za kifamilia na suala la kubadili nambari ya simu ili kukuondoa hofu wewe mpenzi linakuwa la mwisho kwani anajua moyoni anakupenda na anawasiliana na wewe kupitia Mama na ndugu zake wengine, ktk hali halisi hii ingekufanya uwe na Amani myoni kuwa yupo na watu unaweza kuwaamini, imagine angekuwa anawasiliana na wewe Via rafiki au kibanda cha Simu?

Ni matumaini yangu ulifanyia kazi vema maelezo ya wasomaji wangu. Naamini Mpenzi sasa amerudi na kila kitu kiko sawa, nawatakia maisha mema yenye amani na furaha na Mungu awajaalie mfunge ndoa na kuishi maishamarefu ya ndoa.

Pamoja na mambo mengine mengi Uamininifu ni nguzo muhimu ili kuwa na uhusiano bora wenye kuzaa ndoa thabiti.
Kila la kheri.

Pages