Monday

Baada ya Ultrasound na kujua umri wa mimba Mpenzi kaikataa!

Habari Dinah,

Mimi ni mmoja wa waenzi wa Blog yako ila leo ndio mara ya ngu ya kwanza kukuandikia nikihitaji ushauri au msaada wa kimawazo. Nina umri wa miaka 25, na ninamshukuru Mungu kuwa nina Ujauzito ambao siku yeyote naweza kujifungua kwani tayari niko kwenye my due date.

Tatizo ni huyu baba mtoto ambae anaumri wa miaka 28. Nilipokuwa na mimba yangu changa about a month nilitokea kumchukia sana na nikawa na hasira za karibu karibu kitu kilichopelekea mimi na yeye tukatengana.

Nikaendelea kutunza mimba yangu hadi ilipofikia miezi minne then nikataka kujua mwenzangu anampango gani, hivyo nikamuuliza. Yeye akaniita tukayaongea na kukubaliana kwamba tutalea mwanetu nahivyo penzi likaanza upya.

Tukaenda kuangalia Ultrasound ikawa inasema Mimba ina miezi mitano na sio minne, tukarudia tena ikasema hivyo hivyo, yule mwanaume akaanza ku-doubt nakujiweka mbali kidogo na mimi. Kumbe sisi tulivyokuwa tunahesabu ni tofauti na wanavyohesabu wataalam.

Kumbe mimba inahesabiwa kuanzia siku ya mwisho ya Hedhi (last date of period) na sisi tulikuwa tunahesabu kuanzia siku ya kwanza ya kukutana kimwili (Date of Conception) so ikawa inatusumbua ila mimi nilikuwa na hakika kuwa yeye ni baba kwa sababu yeye ni mwanaume pekee niliyefanya nae mapenzi, sina mwanaume mwingine.

Cha kushangaza mwenzangu akaanza visa na pia nikagundua kuwa anatoka na mwanamke mwingine, nilipouliza kulikoni? akanijibu kuwa yuko serious na huyo mwenzangu, pia akadai kuwa hana uhakika kama mtoto ni wake. Kaendelea kusema kuwa hayupo tayari kuzaa kwani hajajipanga.

Niliumia sana, nikatafuta Daktari nakumuelezea na yeye akanielewesha namna ya kuhesabu tarehe kwa mara ngingine tena nikagundua kuwa mimi na baba mtoto tulikuwa tunakosea kuhesabu tarehe, basi nikamuandikia Email ndeefu baba mtoto wangu na kumueleza yote na pia kumuomba aende kwa Daktari yeyote ampe tarehe zetu za kukutana kimwili then tarehe yangu ya mwisho ya kupata hedhi ili apate ukweli. Naamini kuwa alifanya hivyo ila hakutaka kuniambia ili akwepe majukumu.

Baada ya muda nikawa namcheki ili aniambie amefikia wapi? akadai hawezi kuamua sasa mpaka mtoto azaliwe, cha kushangaza kazini kwao na kwa marafiki zake anatangaza kuwa mtoto ni wake. Nimehangaika mpaka sasa nakaribia kujifungua bila msaada wowote kutoka kwake, nilipokuwa najaribu kuomba msaada alikuwa akinijibu kijeuri au kukaa kimya.

Kanifanya niwe mpweke sana kwani kipindi cha mimba ni kigumu na kinachohitaji support ya hali ya juu. Nasikia kutoka kwa watu wengine kuwa anataka kuja kuomba amjue mtoto atakapo zaliwa, ila mimi nina hasira sana na sitaki hata kumuona.

Naomba ushauri wa kujenga na sio kubomoa wala sio matusi, huyu mtu ni wa kumsamehe kweli? na je tunahitaji mtu kama huyu kwenye maisha yetu (mimi na mtoto)?

Asanteni"

Sunday

Nina Ujauzito wa Miezi 2, je haya ni ya kawaida?

"Kwenu wadau wenzangu, Kwa mara nyingine tena naleta swali langu nahitaji michango yenu,
Mimi ni mwanamke nimeolewa na baada ya miezi 7 ijayo natarajia kuitwa mama. Tatizo lilonifanya nije kwenu kuomba ushauri ni kwamba tangu nimegundua kua ni mjamzito nimekua katika wakati mgumu sana mpaka inafikia kipindi nashindwa hata kufanya kazi.

Yaani napata kichefuchefu cha ajabu ila sitapiki, nakuchagua baadhi ya vyakula pia harufu harufu hizi za manukato au chakula mara nyingine zinanipa shida kweli lakini najipa moyo kwani najua haya ni mambo tu ambayo humtokea mama mjamzito pindi mimba inapokua changa.


Ila kubwa zaidi ni kwamba sijisikii kabisa kufanya tendo la ndoa na Mme wangu kitu ambacho naona kama vile nanyima haki yake, ila najitahidi sana kujiweka katika fikra za kimapenzi lakini nashindwa.


Namshukuru Mungu kuwa yeye Mume wangu ni muelewa, anaelewa nikimwambia ila sasa naona hali mbaya kwani ni wiki ya pili sasa sijisikii kabisa kufanya mapenzi. Nahitaji msaada wenu wa mawazo ndugu wadau, nahisi nitaipoteza ndoa yangu.

Ningependa kujua kua Je hali hii iliyonikumba baada ya kushika ujauzito ni kawaida kwa wanawake au ni tatizo lingine linanikumba?
Asanteni"

Tuesday

Mpenzi atishia kujiua Kisa sms ya Ex akiomba msamaha!-Ushauri

"Kwanza pole na hongera kwa kazi unayofanya ya kutoa ushauri kwa jamii. Mimi ni msichana mwenye miaka 23, nina mpenzi ambaye siku hizi ni kama kafichua makucha vile. Tumekuwa pamoja kwa muda wa mwaka mmoja.

Kilichonifanya niandike leo Dinah, ni huyu mpenzi wangu! mwanzo tulikuwa tunapendana sana na ahadi tele tele, yaani mikwaruzano haikuwepo na muda wote huo hatukuwahi kukosana. Basi siku moja tulikuwa tumekaa sehemu akaniomba nimuhamishie wimbo kutoka kwenye simu yangu kwenda kwenye simu yake.

Kwa utani tu nikamwambia nimeiacha simu nyumbani, jamaa akaja juu kwamba nimemdharau nikamuomba msamaha lakini wapi! akanipokonya simu huku akiuliza "unaficha nini?" Nikamwambia samahani lakini hakukubali na hivyo akachukua simu na akaenda nayo kwake.
Ile simu alikuwa kaninunulia yeye, kwenye simu hiyo kulikuwana sms za x- boyfriend akiniomba msamaha ili turudiane.

Mpenzi wangu akazidi kukasirika na kupandisha sana na akampigia huyo kaka nilieachana nae nakumpandishia aache kunifatilia. Kinachomuuma hasa ni bada ya kugundua kwenye zile sms kuwa Ex wangu anamzidi Elimu kwani kamaliza Chuo Kikuu na pia anamzidi kifedha. Lakini mimi sinampango nae huyo jamaa wala elimu yake wala fedha zake kwani niliisha achana nae na analijua hilo.


Sasa tatizo kubwa hapa ni kuwa mpenzi wangu huyu ananitishia kuwa atajiua na hatanii kweli, ni Mchaga alafu pia nimemzidi kielimu kwani hivi sasa niko Chuo Kikuu mwaka wa pili yeye aliishia Kidato cha 4 na kuanzisha Biashara zake zinazomuingizia hela.

Mimi kuwa Chuo Kikuu ndio limekuwa tusi tukiongea kidogo tyu utasikua "au kwa vile sijasoma najiua ili nikuache huru" Mpenzi wangu anamiaka 25 aliniambia hajawahi kuwa na mwanamke na mimi ni wake wa kwanza.

Dinah najieleza na kuomba kila kukicha na sasa ni miezi 3 imepita lakini msimamo wake ni ule ule wa kujiua, nikamwambia nirudishie simu lakini kila tukipanga kuonana anasema yuko busy. Nikimuomba ninunue simu nyingine hataki, ikabidi nijinunulie mwenyewe simu nyingine kama ile ile ili kuendeleza mawasiliano.

Sasa jamani huyu mwanaume niendelee nae? kama nikiendelea nae na nikajamkosea tena si atajiua!! na nisipoendelea nae na yeye akajiua mimi sinitakuwa matatizoni na Degree yangu ikaishie Segere?
Naomba ushauri kutoka kwa wachangiaji wote".

Nafikiria kuachana nae lakini nashindwa, nifanyeje?

"Heshima yako dada Dinah.
Napenda kutoa pongezi kwako na kwa wachangiaje wote ambao wapo bega kwa bega kutoa ushauri katika topic mbalimbali. Mimi ni mmoja wa wapenzi wa blog hii, nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana mada mbalimbali na kujifunza mambo mengi kwakweli.

Dada dinah kama unavyojua matatizo tumeumbiwa nayo binadamu hasa katika barangeni hili la mapenzi. Mimi ni kijana mwanaume, umri miaka 22. Kusema kweli mpaka sasa mwenzenu nipo njia panda kuhusu msichana ambaye ninampenda sana ila simuelewi hata kidogo kama kweli ananipenda ama la.

Ni miezi sita tangu ni mueleze hisia zangu juu yake bahati nzuri alinielewa na akanipa jibu zuri ambalo lilinifanya nisijute kumpenda. Tangu hapo nilikuwa nimechizika kwake nilipenda kila wakati eidha nimuone au nisikie sauti yake tu. Hapo ndipo nilipo fikia uamuzi wa kumnunulia simu ili mawasiliano kati yangu na yeye yawe rahisi.

Tangu hapo nikawa nampigia simu mara kwa mara wakati mwingine anapokea wakati mwingine hapokei, basi ninaamua kumtumia sms ambazo pia hakuona umuhimu wake, nasema hivi kwasababu ninapo muuliza kama amepata sms yangu hunijibu sms ipi? Ilikua inasemaje? Basi tu ilimradi.

Haya yote sikuyatilia umuhimu kwa kuwa nampenda ila wasiwasi wangu umeanza kuja hapa, tangu niwe na mahusiano nae sijawahi kukaa nae tukajadili kuhusu mapenzi yetu kwa kuwa huwa anakataa na kudai kuwa anashughuli nyingi.

Pili sijawahi hata kumkiss shavuni achilia mbali romance nimejaribu mara kadhaa kumuomba tutoke out japo twende hata beach lakini huwa ana kataa sababu ni hizo hizo. Nimemjali kwa mengi bado haoni umuhimu wangu kama mpenzi wake. Pia nikakubaliana na yote hayo hivyo mapenzi yakawa ni ya kwenye simu tu hakuna kuonana.


Kikubwa kinacho niumiza mimi mara kadhaa ninaweza kukutana nae katika mizunguko lakini cha ajabu huwa hana muda na mimi hata salamu mpaka nianze mimi. Nikikaa kimya hunipita kama hanioni. Dada dinah kiukweli nimekuwa sina raha muda mwingi nawaza kwanini ananifanyia hivi lakini nakosa jibu, hata yeye mwenyewe ninapo muuliza huwa hanijibu chochote.

Sasa sijui amedhamiria au ndio mapenzi yenyewe! naweza kusema alibadilika pale tu nilipo mnunulia simu na ilikuwa ni wiki moja tu baada ya kunikubalia ombi langu. Anayo nifanyia ni mengi mno ila sipendi kuwachosha wachangiaji kwa kusema yote.

Hivyo mwenzenu mpaka sasa nipo njia panda, neno nakupenda limebaki kuwakumbukumbu kwangu. Nimeshajaribu kufikiria kumuacha niwe alone lakini nashindwa, je nifanye nini mwenzenu.
Ahsanteni".

Sunday

Nimerudi, samahani kwa kukutenga!

Habari za leo mpenzi msomaji, mtembeleaji na mchangiaji wa D'hicious, nafurahi kusema kuwa nimerudi tena mahali hapa baada ya kupotea kwa muda wa wiki chache kutokana na mishughuliko ya kikazi (safari za hapa na pale) ambazo zilininyima muda wa ku-publish post mpya na kujibu maswali yaliyokuwa published.

Naomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na kutokupatikana kwangu. Namshukuru Mungu nimemaliza salama na sasa nimepata muda wa kuwa nawe tena.

Vilevile napenda kukufahamisha kuwa sito-publish maswali yote yanayozungumzia au kugusia ngono kwa undani kwa muda (Mwezi huu Mtukufu) ili kuepusha vishawishi na pengine kuharibu Funga za wenzetu Waislamu.

Asante sana kwa ushirikiano wako.

Mwenye upendo na kujali,
Dinah.

Pages