Sunday

Nina Ujauzito wa Miezi 2, je haya ni ya kawaida?

"Kwenu wadau wenzangu, Kwa mara nyingine tena naleta swali langu nahitaji michango yenu,
Mimi ni mwanamke nimeolewa na baada ya miezi 7 ijayo natarajia kuitwa mama. Tatizo lilonifanya nije kwenu kuomba ushauri ni kwamba tangu nimegundua kua ni mjamzito nimekua katika wakati mgumu sana mpaka inafikia kipindi nashindwa hata kufanya kazi.

Yaani napata kichefuchefu cha ajabu ila sitapiki, nakuchagua baadhi ya vyakula pia harufu harufu hizi za manukato au chakula mara nyingine zinanipa shida kweli lakini najipa moyo kwani najua haya ni mambo tu ambayo humtokea mama mjamzito pindi mimba inapokua changa.


Ila kubwa zaidi ni kwamba sijisikii kabisa kufanya tendo la ndoa na Mme wangu kitu ambacho naona kama vile nanyima haki yake, ila najitahidi sana kujiweka katika fikra za kimapenzi lakini nashindwa.


Namshukuru Mungu kuwa yeye Mume wangu ni muelewa, anaelewa nikimwambia ila sasa naona hali mbaya kwani ni wiki ya pili sasa sijisikii kabisa kufanya mapenzi. Nahitaji msaada wenu wa mawazo ndugu wadau, nahisi nitaipoteza ndoa yangu.

Ningependa kujua kua Je hali hii iliyonikumba baada ya kushika ujauzito ni kawaida kwa wanawake au ni tatizo lingine linanikumba?
Asanteni"

No comments:

Pages