Monday

Mpenzi aninyanyasa kisa Umasikini, sasa ataka ndoa, je atabadilika?

"Habari dada Dinah, Mimi ni msomaji mkubwa wa Blog yako na ninapenda Posti kwani zimetusaidia wengi. Mimi ni mwanamke wa miaka 23 natokea Mkoani Tanga lakini kwa sasa naishai Zanzibar na mpenzi wangu alienichukua nyumbani.

Ninamshukuru Mungu kwani mpenzi wangu ananijali na kunitimizia mahitaji yangu ikiwemo na kuwasaidia wazee wangu nyumbani. Lakini huyu mpenzi anasema kwa kila mtu alie karibu nae kuwa kwetu ni masikini na sote tunamtegemea yeye. Hali hii huzidi hasa tukiwa na ugomvi.

Nimewahi kumwambia mara kadhaa kwamba sipendi tabia yake hiyo, lakini bado hana dalili yeyote ya kuachana na tabia hiyo. Ikitokea ananigombeza basi huwatusi mpaka wazee wangu jambo ambalo hunitia uchungu sana.

Zaidi ya yote anasema hafurahii sana ladha ya tendo la ndoa kwa hiyo anataka tufanye kinyume na maumbile, kitu ambacho mie siwezi kuthubutu kukifanya.

Kwa bahatimbaya au nzuri nimekutana na Kaka mmoja Mzanzibari ambae anadai kuwa ananipenda sana na yupo tayari kufunga ndoa nami nikamwambia kuwa ninampenda lakini kuna mtu ninaishi nae.

Kusema ukweli ninampenda huyu Mkaka niliekutana nae, aliomba akanitambulishe kwao lakini mimi nikamuomba akanitabulishe kama rafiki kwani sikutaka wajue kutambulishwa kama mpenzi wakati niko kwenye uhusiano na mtu mwingine japo sina amani.Familia yake walionyesha kunipenda.

Tatizo linalonisumbua ni kuwa huyu mpenzi ninaeishi nae ametangaza ndoa, lakini mie sitaki kuolewa nae kutokana na tabia zake za kinyanyasaji, sasa sijui nimueleze mama yangu ukweli wa mambo ili nipate mawazo yake au nikubali kuolewa nae kwa kuamini kuwa atabadilika!!

Au nitafute njia ya kuachana nae ili niwe na Kaka wa Kizanzibari alienitambulisha kwao kama rafiki lakini nia yake ni kufunga ndoa nami?

Naombeni ushauri
Asante"

Pages