Thursday

Nataka kuolewa lakini nashindwa kupenda kila anaenitokea-Nifanye nini?

"Hello dada Dinah mimi ni binti in early twenties, ninatamani sana kuolewa na kupata japo mtoto mmoja soon. Bado niko shule lakini sielewi why I feel this way now! kwasababu nilikua against kuolewa kabla ya kumaliza masomo.

Niliwahi kuwa na Mpenzi ambae nilimpenda sana ila nilimuacha kwasababu nilidhani hakunipenda kwani we were breaking up and makingi up all the time, yaani maisha yalikuwa ndio hayo kwa muda wa miaka mitatu mpaka nilipoamua kuwa sasa I have had enough and called it off.

The guy bado ananitafuta kwa simu akitaka tuonane lakini mimi namchunia. Baada ya kuachana na huyo nikaanza kutoka na mwanaume mwingine ambae amenizidi umri kwani anamika 37 sasa. Tatizo ni kwamba jamaa anataka tufunge ndoa haraka iwezekanavyo.

Nyumbani hawamfahamu kwani bado sijamtambulisha, nilihakikisha anamjua rafiki yangu mmoja tu ambae nae alibahatika kwani aliomba lift. Baadhi ya ndugu zake wananifahamu na kufahamu uhusiano wetu kwani huwa ananikaribisha kwao na mwezi wa Pili kwama huu alitaka tuvalishane Pete.

Sina mpenzi mwingine na ninataka kuolewa lakini kusema ukweli simpendi huyu jamaa kihivyo, sura yake, na anavyoongea kwangu ni kero na pia he's terrible in bed. Nimekuwa nae kwasababu ya pesa, na kila ninapohitaji hunipatia pesa. Jamaa amejijenga vizuri kwani ana Kampuni yake na nyumba nzuri tu, pia huwa ananiachia niendeshe gari yake.

Nikaamua nimwambie kuwa siwezi kuolewa nae kwa sababu ni mkubwa kwangu na some other reasons which I cooked up but they sounded concrete. Yeye hataki tuachane kwani anadai kuwa ananipenda na anataka kuishi maisha yake yote na mimi pia anasema kuwa familia yake itamuona muhuni kama tutaachana.

Mie nimeshangaa jamaa bado anang'ang'ania kuwa na mimi wakati tangu tumekuwa pamoja sijawahi kumuonyesha mapenzi, yaani hata kumpa K ni ishu!! Mpaka anibembeleze kwa Wiki na wakati mwingine miezi. Mfano mwaka huu tumefanya ngono mara tatu tu.

I mistreated him kwa kumponda, kumnunia hata miezi miwili bila sababu ya msingi ili aniache lakini wapi! Kila kitu anachonipa na kuahidi ni perfect isipokuwa yeye. Nipo nae kwa vile hivi sasa sina kitu na sina mtu wa kuniangalia (money wise) kwani nina mzazi mmoja na kipato chake ni kidogo na sijawahi kumuomba mzazi huyo pesa kwa vile namuonea huruma.


Wakati niko kwenye Dilema hiyo, kuna kaka wengine wawili wanaonyesha interest kwangu. Wote wanasura nzuri na wanavutia na pia wana kazi nzuri ila mimi sina hisia za mapenzi, napenda sura zao na kazi zao. Mmoja ndio anaonekana mwema na anaweza kunioa ila naogopa kutoka nae kwani sina uhakika kamanitawapenda au itakuwa kama huyu Mjamaa, sitaki kuumia.

Dada Dinah naogopa nitakosa mwanaume wa kunioa kwani umri nao unakwenda lakini kila anaenitokea sivutiwi na sina hisia za kimapenzi, lakini rafiki zangu wakiwaona jamaa wanapagawa kweli.

Najua Email yangu ni ndefu sana, lakini am in desperate need for help na nilitaka nigusie yaliyopita na ninayokabiliana nayo hivi sasa ili nieleweke.

Nifanyeje?"

Monday

Nimekuwa na Mchumba kwa Mwaka, nampenda lakini sina uhakika-Ushauri


"Pole Dada Dinah kwa kazi ya kutushauri, mimi ni mwanamke mwenye miaka 26 nina Mchumba wangu mwenye umri wa miaka 36. Tumekuwa pamoja kwenye uhusiano wetu kwa mwaka mmoja.


Mchumba wangu huyu kwa mujibu wake ni kuwa anaishi kwenye nyumba yake, lakini toka tuanze kuwa pamoja kwenye uhusiano hajawahi kunipeleka kwake japokua ameniambia sehemu anayoishi. Kwa kawaida huwa tunaonana kila siku na pia mara nyingi tunaenda out kwa ajili ya diner n.k.


Naomba mnishauri, je anamapenzi ya kweli au ananidanganya tu, ningependa awe mume wangu Mungu akitujaalia. Asante"

Nashindwa kumuacha mume wa mtu-Nifanyeje?


"Natumaini wewe ni mzima na waafya. Mimi ni mwanamke wa miaka 24, naomba ushauri wako kama mdogo wako. Mimi nimetokea kumpenda mume wa mtu na nina amini ananipenda pia. Tumekuwa na mausiano kwa mwaka mmoja bila hata mke wake kujua na nina tamani sana kumjua mke wake.

Tatizo langu ni kuwa sijiamini kama huyu Mume wa mtu atakuja kuwa nami kama mpenzi wake wa kudumu, mimi binafsi nashindwa kumuacha kwasababu Jamaa mwenyewe ni innocent and very caring.
Naomba ushauri nifanye nini?."
Dinah anasema: Mie mzima wa afya namshukuru Mungu, Nashukuru sana kwa Mail yako na hongera kwa kuwa wazi pia kuwa na nia ya kuachana na huyo mume wa mtu lakini hujui uanzie wapi?
Ninaamini nia yako ni kuachana nae na labda ulipogundua kuwa ni mume wa mtu ulitaka kufanya hivyo lakini kutokana na hali ya kujali na upole anaokuonyesha unadhani kuwa ni mtu mwema na hivyo kuzidi kumdondokea kimapenzi. Ikiwa kama nia yako sio kuachana nae hakika usingekuja hapa kuomba ushauri na badala yake ungeendelea kivyako.
Uhusino wenu umekuwa kwa mwaka mmoja kwa vile mkewe hajui na wala hajahisi kuwa mumewe ana-cheat labda kwa vile anajali na amevaa ngozi ya kondoo hivyo mkewe anamuamini kupita kiasi na hivyo kutohisi kitu chochote kibaya.
Kama mkewe angejua au angehisi kuwa mumewe anagawa umasikini nje ya ndoa yao hakika angempa wakati mgumu sana na kupelekea Jamaa kuachana na wewe.
Sasa hebu tuambie kitu gani kinakufanya utamani sana kumuona mkewe? Ili umwambie kuwa mumewe ana-cheat (ni jambo jema japo ni ngumu kwa yeye kukuamini hasa kama mumewe atakataa na kudai kuwa wewe unamtaka) AU unataka kufanya ushindani ili kuzua ugomvi juu ya mumewe (sio vema kuumiza hisia za mwanamke mwenzio kiasi hicho).
Hisia za Mapenzi:
Kutokana na uzoefu hakika natambua kuwa ni ngumu sana kukabiliana na hii kitu kwani hupangi au kuchagua nani wa kumpenda, hisia za kimapenzi hujitokeza tu kwa mtu yeyote na wakati wowote, lakini kabla hisia hizo hazijaota mizizi (hazijakukaa sana) ni vema kuwa mdadisi kuhusu mtu uliempenda ili kujua ukweli kuhusiana na maisha yake ya sasa kimapenzi. Na mara tu baada ya kugundua kuwa amefunga ndoa ni vema kumkwepa.
Kutojiamini:
Ofcoz huwezi kuwa na hali ya kujiamini au kuwa na uhakika wa wewe kuwa mpenzi wake wa kudumu kwani huyo mwanaume sio wako na sio single ni mume wa mtu, siku yeyote ikiwa mkewe atagundua kuwa kajisahau na kuanza kurudisha yale yote ambayo labda mumewe anakosa na sasa kuja kupata kwako.
Vinginevyo, kama walivyogusia baadhi ya wachangiaji ni kuwa, ikiwa Imani zenu za Dini zinaruhusu na mkewe wa kwanza akaridhia then utakuwa mke wa pili.
Matokeo yake:
Wee bado ni binti mdogo wala huitaji kujiweka kwenye matatizo makubwa kama kuharibu ndoa ya mtu na vilevile kuishi na hatia ya kuharibu maisha ya watoto ambao ni matunda ya ndoa hiyo. Kumbuka watoto waliozaliwa kama matunda ya ndoa hiyo wataumia kama atakavyoumia mama yao.
Utakuwa umewanyang'anya baba yao, utakuwa umewaharibia maisha yao kwani hakuna mtoto anataka kumuona mama yake anaumia (unajua watoto tulivyo karibu na mama zetu). Huenda hujui yote haya kwa vile hukulelewa katika mazingira ya ndoa (kama mmoja wa wachangiaji alivyogusia), mazingira tuliokulia husaidia sana kwenye maamuzi yetu.
Nini cha kufanya:
Achana na huyu mume wa mtu kwania anakupotezea muda wako na kukuzibia bahati ya kukutana na wanaume, kwani kuna vijana wengi tu wenye umri mkubwa zaidi yako lakini hawajaoa na pia wapo vijana wenye umri wako (24-29) ambao wako huru.
Kila la kheri.

Mume kung'ang'ania picha za Ex wake ni kawaida?-Ushauri

"Habari Dada Dinah, Mimi ni mwanandoa ambaye nakaribia kumaliza mwaka sasa kwenye ndoa yangu. Tatizo langu ni kuwa mume wangu ana picha alizopiga na wapenzi wake wa zamani na hataki kabisa ziondolewe kwenye albam.

Ukigusia hilo suala ni ugomvi mkubwa, je Dada Dinah hiyo ni haki? au nichukue maamuzi gani? Nizitoe tu hapo na kuzichoma moto au nijifanye sijaziona na akiniuliza nimjibu kuwa sijui zilikokwenda na kumbe najua?

Maana yake kwa kweli zinanitia kichefuchefu. Tena kibaya zaidi ni za wasichana wa kizungu wawili tofauti, Je ndoa ndiyo zilivyo Dada Dinah au huyu mwenzangu ana lake jambo? Hao wasichana wako Ulaya yeye aliendaga kusoma huko siku za nyuma kama miaka mitatu ilopita na ndipo aliporudi akakutana na mimi tukaanza mahusiano na mpaka kufikia ndoa.
Naomba ushauri wenu jamani mnisaidie."

Dinah anasema: Ni njema tu Mdada, Unauhakika kuwa ni wapenzi wake au walikuwa marafiki tu wa Chuoni? Maana kuna Watanzania wengi wajinga wajinga wanadhani ni sifa kuwa waliwahi kutoka na Wakoloni (Wazungu) kimapenzi au kuthibitisha kuwa alisoma nje basi anatunza Picha za wanafunzi wenzake.


Ikiwa ni kweli ni wapenzi wake hakika anachokifanya sio haki, si hivyo tu mumeo hana heshima na wala hajali hisia zako kama mkewe. Katika hali halisi unapokuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi wa kudumu na mtu hapaswi kuwa na Picha za wapenzi wake wa zamani let alone kuwa kwenye ndoa.

Picha za maisha ya shule/chuo yaliyohusisha wapenzi huwa tunaziacha nyumbani kwa wazazi, album za wanandoa huwa na picha zenu mlipokuwa wapenzi na zile za ndoa, za wazazi wenu ndugu, jamaa na marafiki sio exes.

Unapoingia kwenye ndoa unaacha kila kitu huko nje na kuanza maisha upya, ndio maana huitwa maisha mapya ya ndoa. Wote wawili mnaanza upya sio tu kama wapenzi/familia bali pia kama individuls.

Kama umejaribu kumuomba kwa ustaarabu aziharibu Picha hizo na yeye kuwa mkali na hata kuibua ugomvi basi kuna mawili ya kufanya;

(1)~Ziondoe na uzifiche mahali kisha tafuta njia ya kumfanya aongeze picha kwenye album ambayo ilikuwa na hizo Pics za Exes. Asipoziona ni wazi kuwa atakuuliza au kukushutumu kuwa umezitupa na kuibua ugomvi kama kawaida au anaweza kuuliza tu picha fulani ziko wapi? Mwambie ukweli kuwa Picha hizo zinakunyima raha, zinakufanya usijiamini n.k.

Kama ugomvi utakuwa mkubwa sana, basi mwambie "naona hili suala la picha za wapenzi wako wa zamani limekuwa ni tatizo kubwa kwenye ndoa yetu, hivyo naomba tuliwakilishe kwa wazazi wa pande zote mbili" katika hali halisi ni jambo dongo sana kulipeleka kwa wazazi wenu sio hivyo tu litamfanya asikie aibu na ku-give up....then acha siku mbili zipite alafu zipige kibiriti.

(2)~Tafuta picha za the hot guys kuliko yeye lakini wabongo na wewe ziweke kwenye album yenu. Au kama kuna picha ambazo ulipiga zamani ukiwa na wanaume ambao sio ndugu na yeye hawajui ziweke kwenye album hiyo....so he can learn the hard way.

Natumaini unafanyia kazi ushauri wa wachangiaji wengine.
Nakutakia kila la kheri

Pages