Thursday

Nataka kuolewa lakini nashindwa kupenda kila anaenitokea-Nifanye nini?

"Hello dada Dinah mimi ni binti in early twenties, ninatamani sana kuolewa na kupata japo mtoto mmoja soon. Bado niko shule lakini sielewi why I feel this way now! kwasababu nilikua against kuolewa kabla ya kumaliza masomo.

Niliwahi kuwa na Mpenzi ambae nilimpenda sana ila nilimuacha kwasababu nilidhani hakunipenda kwani we were breaking up and makingi up all the time, yaani maisha yalikuwa ndio hayo kwa muda wa miaka mitatu mpaka nilipoamua kuwa sasa I have had enough and called it off.

The guy bado ananitafuta kwa simu akitaka tuonane lakini mimi namchunia. Baada ya kuachana na huyo nikaanza kutoka na mwanaume mwingine ambae amenizidi umri kwani anamika 37 sasa. Tatizo ni kwamba jamaa anataka tufunge ndoa haraka iwezekanavyo.

Nyumbani hawamfahamu kwani bado sijamtambulisha, nilihakikisha anamjua rafiki yangu mmoja tu ambae nae alibahatika kwani aliomba lift. Baadhi ya ndugu zake wananifahamu na kufahamu uhusiano wetu kwani huwa ananikaribisha kwao na mwezi wa Pili kwama huu alitaka tuvalishane Pete.

Sina mpenzi mwingine na ninataka kuolewa lakini kusema ukweli simpendi huyu jamaa kihivyo, sura yake, na anavyoongea kwangu ni kero na pia he's terrible in bed. Nimekuwa nae kwasababu ya pesa, na kila ninapohitaji hunipatia pesa. Jamaa amejijenga vizuri kwani ana Kampuni yake na nyumba nzuri tu, pia huwa ananiachia niendeshe gari yake.

Nikaamua nimwambie kuwa siwezi kuolewa nae kwa sababu ni mkubwa kwangu na some other reasons which I cooked up but they sounded concrete. Yeye hataki tuachane kwani anadai kuwa ananipenda na anataka kuishi maisha yake yote na mimi pia anasema kuwa familia yake itamuona muhuni kama tutaachana.

Mie nimeshangaa jamaa bado anang'ang'ania kuwa na mimi wakati tangu tumekuwa pamoja sijawahi kumuonyesha mapenzi, yaani hata kumpa K ni ishu!! Mpaka anibembeleze kwa Wiki na wakati mwingine miezi. Mfano mwaka huu tumefanya ngono mara tatu tu.

I mistreated him kwa kumponda, kumnunia hata miezi miwili bila sababu ya msingi ili aniache lakini wapi! Kila kitu anachonipa na kuahidi ni perfect isipokuwa yeye. Nipo nae kwa vile hivi sasa sina kitu na sina mtu wa kuniangalia (money wise) kwani nina mzazi mmoja na kipato chake ni kidogo na sijawahi kumuomba mzazi huyo pesa kwa vile namuonea huruma.


Wakati niko kwenye Dilema hiyo, kuna kaka wengine wawili wanaonyesha interest kwangu. Wote wanasura nzuri na wanavutia na pia wana kazi nzuri ila mimi sina hisia za mapenzi, napenda sura zao na kazi zao. Mmoja ndio anaonekana mwema na anaweza kunioa ila naogopa kutoka nae kwani sina uhakika kamanitawapenda au itakuwa kama huyu Mjamaa, sitaki kuumia.

Dada Dinah naogopa nitakosa mwanaume wa kunioa kwani umri nao unakwenda lakini kila anaenitokea sivutiwi na sina hisia za kimapenzi, lakini rafiki zangu wakiwaona jamaa wanapagawa kweli.

Najua Email yangu ni ndefu sana, lakini am in desperate need for help na nilitaka nigusie yaliyopita na ninayokabiliana nayo hivi sasa ili nieleweke.

Nifanyeje?"

No comments:

Pages