Monday

Mume kung'ang'ania picha za Ex wake ni kawaida?-Ushauri

"Habari Dada Dinah, Mimi ni mwanandoa ambaye nakaribia kumaliza mwaka sasa kwenye ndoa yangu. Tatizo langu ni kuwa mume wangu ana picha alizopiga na wapenzi wake wa zamani na hataki kabisa ziondolewe kwenye albam.

Ukigusia hilo suala ni ugomvi mkubwa, je Dada Dinah hiyo ni haki? au nichukue maamuzi gani? Nizitoe tu hapo na kuzichoma moto au nijifanye sijaziona na akiniuliza nimjibu kuwa sijui zilikokwenda na kumbe najua?

Maana yake kwa kweli zinanitia kichefuchefu. Tena kibaya zaidi ni za wasichana wa kizungu wawili tofauti, Je ndoa ndiyo zilivyo Dada Dinah au huyu mwenzangu ana lake jambo? Hao wasichana wako Ulaya yeye aliendaga kusoma huko siku za nyuma kama miaka mitatu ilopita na ndipo aliporudi akakutana na mimi tukaanza mahusiano na mpaka kufikia ndoa.
Naomba ushauri wenu jamani mnisaidie."

Dinah anasema: Ni njema tu Mdada, Unauhakika kuwa ni wapenzi wake au walikuwa marafiki tu wa Chuoni? Maana kuna Watanzania wengi wajinga wajinga wanadhani ni sifa kuwa waliwahi kutoka na Wakoloni (Wazungu) kimapenzi au kuthibitisha kuwa alisoma nje basi anatunza Picha za wanafunzi wenzake.


Ikiwa ni kweli ni wapenzi wake hakika anachokifanya sio haki, si hivyo tu mumeo hana heshima na wala hajali hisia zako kama mkewe. Katika hali halisi unapokuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi wa kudumu na mtu hapaswi kuwa na Picha za wapenzi wake wa zamani let alone kuwa kwenye ndoa.

Picha za maisha ya shule/chuo yaliyohusisha wapenzi huwa tunaziacha nyumbani kwa wazazi, album za wanandoa huwa na picha zenu mlipokuwa wapenzi na zile za ndoa, za wazazi wenu ndugu, jamaa na marafiki sio exes.

Unapoingia kwenye ndoa unaacha kila kitu huko nje na kuanza maisha upya, ndio maana huitwa maisha mapya ya ndoa. Wote wawili mnaanza upya sio tu kama wapenzi/familia bali pia kama individuls.

Kama umejaribu kumuomba kwa ustaarabu aziharibu Picha hizo na yeye kuwa mkali na hata kuibua ugomvi basi kuna mawili ya kufanya;

(1)~Ziondoe na uzifiche mahali kisha tafuta njia ya kumfanya aongeze picha kwenye album ambayo ilikuwa na hizo Pics za Exes. Asipoziona ni wazi kuwa atakuuliza au kukushutumu kuwa umezitupa na kuibua ugomvi kama kawaida au anaweza kuuliza tu picha fulani ziko wapi? Mwambie ukweli kuwa Picha hizo zinakunyima raha, zinakufanya usijiamini n.k.

Kama ugomvi utakuwa mkubwa sana, basi mwambie "naona hili suala la picha za wapenzi wako wa zamani limekuwa ni tatizo kubwa kwenye ndoa yetu, hivyo naomba tuliwakilishe kwa wazazi wa pande zote mbili" katika hali halisi ni jambo dongo sana kulipeleka kwa wazazi wenu sio hivyo tu litamfanya asikie aibu na ku-give up....then acha siku mbili zipite alafu zipige kibiriti.

(2)~Tafuta picha za the hot guys kuliko yeye lakini wabongo na wewe ziweke kwenye album yenu. Au kama kuna picha ambazo ulipiga zamani ukiwa na wanaume ambao sio ndugu na yeye hawajui ziweke kwenye album hiyo....so he can learn the hard way.

Natumaini unafanyia kazi ushauri wa wachangiaji wengine.
Nakutakia kila la kheri

No comments:

Pages