Tuesday

Mume aki-cheat na mwenye umbo tofauti na lako anaweza akawa bado anakupenda kama zamani?

"Dada Dinah mie naomba kuuliza,hivi kweli mumeo akitembea nje ya ndoa na mwanamke ambae hamfanani kabisa ikimaumbile anaweza akawa bado anakupenda?

Nimeuliza hivyo kwa kuwa mimi ni size 12 though kabla sijajifungua nilikuwa navaa chini saizi 14 juu saizi 12 kwa sasa nimepungua sana (na nimependa mwenyewe kupungua). Mwanamke ambae mume wangu alikuwa na affair nae for almost two months (kama ni mkweli) ni wale ambao ni ngumu hata kupata saizi dukani, yaani ni bonge la mtu lakini ni namba nane.

Inanifanya nisijue mume wangu anapenda miili gani? That is why I am not feeling like staying married to someone that am not sure anymore that he still loves me. Na wakati mwingine tukiwa kwenye gari wakipita wanawake wakubwa wenye namba nane huwa namcheki anavyowaangalia japo kwa wizi sana. Ingawa hata mimi huwa sometimes nawashangaa wanawake wenzangu. Sasa sijui nina wivu na sina Imani kwa sababu ameshani-cheat au ni normal"?

Naomba mnipe ukweli, je mume wako akitoka nje ya ndoa yenu na mwanamke ambae ni tofauti na wewe na baadae kukubali makosa na kurudi kwenye ndoa, je ataendelea kukupenda?

Asante".

No comments:

Pages