Sunday

Mkwe anataka nimuache mwanae ni Hanithi, lakini tumesha-do mara kibao na yuko sawa-Nifanyeje?

"Habari Aunt? Mimi ni mwanamke wa miaka 24,nina boyfriend wangu ambae tumedumu kwa miaka mitatu na plan yetu ni kufunga ndoa. Alipanga kuleta Posa baada ya Mwezi wa Ramadhan lakini cha ajabu mama yake aliwafuata mama zangu wakubwa na kuwaambia kuwa huyo boyfriend wangu si mwanaume, kwamba ni hanithi.

Pia mama yake alinifuata mimi na kunambia kuwa mwanae hana uwezo wa kiume. Lakini mimi na boyfriend wangu tayari tumekutana kimwili mara kadhaa na mimi namuona yuko sawa ila huwa anapiz nje kwa kuwa tulipanga tusizae nje ya ndoa.

Siku nyingine Mama yake kanambia kama siamini basi nijarbu kumtega kwa kumwambia kuwa anipe mimba, nilipomwambia boyfriend wangu anipe mimba alinijibu kuwa yeye yuko tayari. To be honest nampenda kutoka moyoni na yeye ananipenda pia.

Hivi sasa niko njia panda kwani pande zote mbili wanataka niachane nae lakini mimi sijaona tatizo au mapungufu ya mpenzi wangu yako wapi. Kwangu mimi ngumu kuachana nae kwa kuwa tunapendana na tuna plans nyingi tulizopanga na ni za muda mrefu.

Naomba watanzania wenzangu mnisaidie kwa hilo niko njia panda.

Asante."

Dinah anasema:Habari ni njema tu lovey, asante sana kwa ushirikiano. Pole kwa misukosuko ya soon to be mother in law, hapo ni sawa na kujitukana na kujidhalilisha mbele ya wazazi wenzie. Yeye amejuaje kama mwanae hawezi au hana uwezo wa kuzaa? Hata kama huo ni ukweli yeye anahusika vipi na maisha yenu ya ndani ninyi wawili kama wapenzi?

Anyway, Kama walivyo akina mama wengi wenye watoto wa kiume hupenda sana kupata mjukuu pale wanapotaka wao, wengine hutumia neno "sitaki kufa kabla sijaona mjukuu) hivyo hufanya kila jambo ili mtoto wa kiume kuzaa iwe kabla au baada ya ndoa.

Utagundua kuwa, kuna baadhi ya kina mama wakishajua mtoto wao wa kiume anauhusiano utasikia anataka kijana huyo afunge ndoa (hata kama hayuko tayari) na ikitokea akafunga ndoa kutokana na matakwa ya mama, soon baada ya ndoa mama mkwe ataanza kudai mjukuu, akipata wa kike, atataka wa kiume n.k yaani ni kama vile wana-control maisha ya watoto wao wa kiume.

Huyu mama anaposema mwanae ni Hanithi anamaanisha mwanae ni Tasa (hana uwezo wa kuzaa), labda kwa vile kila msichana alietoka nae kabla yako hakushika mimba kwa vile Mwanae alikuwa mwangalifu au hakutaka kuzaa kabla ya ndoa.

Vilevile inawezekana Mama mkwe huyo anadhani wewe ni Tasa kwani umekuwa na mwanae kwa muda mrefu bila kushika mimba (si unajua wazazi wetu wao walitumia Majira na hivyo waume zao walikuwa wanamwaga ndani tu hakuna cha nje wala Condoms)huenda anajiuliza "kulikoni hawa watu hawapeani mimba miaka yote hii" hivyo anataka ushike mimba kabla mwanae hajakuoa.

Sasa huyu mama anachojaribu kukifanya hapa ni kutaka wewe uwe forced na wazazi wako kushika mimba kabla ya ndoa ili ukifunga ndoa baada ya muda mfupi wewe na mumeo mmpatie mjukuu. Kumbuka amekuambia kama "huamini mwambie akupe mimba".

Alafu kwanini wazazi wako wakatae kupokea posa wakati sio wao wanaokwenda kuolewa na huyo Kijana, kwa kawaida binti ndio huwa na uamuzi huo. Kwamba mtu akija kuchumbia kwenu wazazi wanasema watamjibu baada ya muda fulani, then unaitwa alafu unaambia kinachoendelea na wewe kukubali au kukataa (kizamani).

Kisasa wengi tunakuwa tunawajua wachumba (vishwa Pete) kabla ya posa hivyo hata posa ikipelekwa wewe unakuwa wa kwanza kujua na huenda ukawaambia wazazi kuwa wazee wa kadhaa wa kadhaa watakuja kuposa n.k. hivyo wazazi kukataa Posa kwa sababu ya majungu ya mzazi mwenzao sio haki.

Nini cha kufanya:
Hebu kaa chini na mama yako mazazi na uwaambie ukweli kuwa Mchumba wako anauwezo wa kufanya mapenzi kwani tayari mmekwisha fanya mara kadhaa ndani ya miaka 3.

Mwambie "tunapendana na niko tayari kufunga nae ndoa. Sielewi mama mkwe(sijui unamuitaje) anataka nini kutoka kwetu kwani hivi majuzi (itaje siku) alinifuata na kuniambia nimtege mchumba wangu ili anipe mimba, inamaana huyu mama anadhani ukoo wetu ni Tasa?!!"

"Mimi sitaki kushika mimba kabla ya ndoa na ndio maana nimekuwa mwangalifu na kujikinga kwa miaka yote mitatu" (hii trick ya kujifanya victim huku unatoa CHOZI siku zote hufanya miujiza).

Enedelea "Mama naomba mkubali posa ya mpenzi wangu kwani ni mwanaume pekee ninae mpenda na tumepanga kufanya mambo mengi kwa ajili ya maisha yetu na familia zetu, nisingependa kumpoteza mwanaume anaenijali, mwenye nia njema nami na mwenye upendo wa dhati".

Mama yako anakupenda, hakika atakuelewa na atafikisha ujumbe kwa Baba. Ikiwa bado wanashupalia uachane nae basi uamuzi ni wako, Funga ndoa na Mchumba wako bila ya kuwaharifu wazazi wenu na baada ya ndoa ndio wapewe taarifa.

Fanyia kazi maelezo ya wachangiaji wengine pia,
Kila la kheri!

No comments:

Pages