Tuesday

Maeneo ya Kumshika Mwanaume...

Habari dada Dinah
Mimi ni binti mwenye umri wa miaka 28 na ni bikira tatizo  nimepata mchumba tumepima ukimwi na tuko kwenye process za ndoa.


Tatizo mimi ni mwembamba yeye ni mnene na mboo yake ni kubwa na ndefu akitaka kuanza kuniingilia kwa ajili ya kufanya mapenzi naumia mno anaishia kuingiza kichwa tu.

Hebu nisaidie nifanyeje na nakaribia kuingia kwenye ndoa. Pili nataka kujua sehemu zipi nimshike ili apate raha.

******************************


Dinah anasema: Kwanini unasema "tatizo nimepata mchumba"? Inamaana haukotayari kuolewa nae? Kwanini udhanie kuwa na mchumba ni tatizo?

Wembamba wako hauna uhusiano wowote na unene wake kwenye suala la kufanya mapenzi.


Kwa kawaida kuingiliwa kwa mara ya kwanza (tolewa Bikira) kunauma na sio wanawake wote wanaotolewa Bikira siku ya kwanza kwani hushindwa kuvumilia maumivu na hujawa na Uogoa hivyo misuli ya uke inashindwa kujiachia(relax).


Ndio maana zamani wakati Mabinti wanaolewa na Bikira walikuwa wanakaa ndani siku Saba, Usiku wa ndoa Bikira inatolea na siku saba baada ya hapo mwanamke "anazoeleshwa" uume(kuingiliwa ukeni) na yeye kuonyesha mambo mengine ya kimapenzi aliyofundwa kwao.


Ikiwa Mchumba wako amefanikiwa kuingiza kichwa ni wazi kuwa wewe sio Bikira tena, isipokuwa Uke wako haujazoea kuingiliwa na kitu kinene na kigumu + hofu ya kuumia.


Vilevile kichwa cha uume huwa kikubwa kiasi kuliko sehemu ya nyuma ya Uume, ikiwa kichwa kinaingia ni vema kama utavumilia ili aendelee kuingia taratibu na kwa hatua, sio anaingia moja kwa moja na kwanguvu na shauku zake zote....utaumia na kumchukia!!


Weka uaminifu kwa Mchumba wako na muombe aingie taratibu-taratibu, usiwe na haraka ya kuzoea leo au kesho! Unaweza kusubiri mpaka mtakapofunga ndoa na kwenye Fungate ndio mkazoeshane.


Wanaume wanatofautiana hivyo siwezi kusema umshike wapi ili afurahie kwani mie simjui(sijawahi kuwa nae hehehehehe)....anyway! Kuna maeneo ambayo ni General na mengine jaribu kubahatisha au kutafuta jinsi mnavyozidi kuzoeana.

--Kubusu shingo katika mtindo wa kuuma kwa mbaaali


--Busu au papasa juu ya Kinena(sehemu inayoota mavuzi) au niseme kiunoni kwa mbele hivi kama unaelekea chini ila usifike kwenye uume.


--Lamba katika mtindo wa kunyonya Chuchu, hakikisha unazinyonya kwa kupokezana, usibaki kwenye chuchu moja kwa muda mrefu kwani utampoteza "msisimko".


--Masikio, unaweza kuwa ni sehemu ya chini, kwa nyuma au kwa ndani kama sio sikio lote. Tumia midomo yako kulamba, busu, hemea na nong'oneza maneno matamu kumfanya Mchumba wako asikie raha na kuelewa hisia zako kwake.


--Busu katika mtindo wa kulamba sehemu ya ndani ya mapaja yake, pia busu sehemu ya nyuma ya kiuno(juu kidogo ya makalio yake).


--Shika Kende zake na kuzichezea(taratibu usimuumize) na tumia midomo yako kutumbukiza pumbu na kuzitoa kama vile unapuliza ki-slow-mo.

Anza na hivi, vingine tutaendelea kuelekezana jinsi unavyoendelea na maisha yako ya ndoa.


Maana ukionyesha mengi jamaa anaweza kukushangaa....Lol!


Hongera sana kwa kuchumbiwa na kila la kheri kwenye maandalizi ya Ndoa yenu. Mungu awaongoze na kuwalinda.
------------------

Sunday

Ndani ya Wiki mbili kesha "move on" na jamaa kwenye WhatsApp!

Habari yako dada Dinah,

Mimi ni kijana Mtanzania, nina jambo ambalo ningependa ushauri wako. Jambo lenyewe ni kwamba nina mpenzi wangu ambaye tuligombana na tukakaa kama wiki mbili hivi hatuelewani...ndani ya hizo wiki mbili akafanya ngono na mwanaume mwingine.


Sasa baadae, baada ya hizo wiki mbili tulikuja kuelewana tukasameheana yale yaliyotugombanisha. Hapo bado sikuwa najua kama alifanya ngono na mtu huyo mwingine.


Sasa baada ya hapo tukarudiana na kuendelea na uhusiano kama mwanzo, Mpenzi alikuwa anatumia simu ya Blackberry ambayo baadae alinipa mimi niitumie kwasababu yeye tayari alishapata simu nyingine ambayo sio Blackberry lakini anaipenda zaidi. Nikaichukua ile simu nikaweka line yangu ya vodacom.

Cha kushangaza, baada ya siku kama mbili tatu hivi napokea Message kutoka kwa mtu ambaye walikuwa wakiwasiliana kupitia WhatsApp, hiyo message ilikuwa ya kimapenzi...then muda mfupi nikapokea picha mbili ambazo huyo jamaa alizituma.

Hizo picha zilionyesha walipiga wakiwa wote, moja wamelaliana yeye mpenzi akiwa amejifunga khanga moja tu, na nyingine wanakipeana busu yeye akiwa amemkalia huyo jamaa...


Nikaamua kumuuliza taratibu kwanza kabla hata ya kumuonyesha hizo picha, nikamuuliza kama anazijua namba za huyo jamaa nilimuonyesha maana kwenye whatsApp namba ya alietuma inaonekana, akasema anamjua.


Nikamuuliza wakoje naye, akasema ni rafiki tu japokuwa jamaa anamfuatilia mara nyingi kwani amekuwa akimtaka...akakataa kabisa kusema ukweli.


Baadae nikawa mkali na kumwambia tuachane kabisaa aendelee na huyo jamaa yake! Akawa mkali, hapo bado sijamuonyesha zile picha, akawa analia machozi kabisa kila siku ananibembeleza nimsamehe kwakuwa hakuwahi kuniambia kuwa huyo jamaa huwa wanatongozana japo bado hajamkubali.


Ndio siku moja nikamwambia upo tayari kusema ukweli ili nikusamehe?..akasema ndio! basi nikamwambia tukutane sehemu tuongee....ukweli ni kwamba hakuna alichokisema kipya zaidi ya kusisitizia kuwa huyo jamaa yeye ndiyo anaemfuatili (kumtongoza) lakini yeye hamtaki na wala hawajawahi kukaa au kukutana faragha popote.

Nikamuuliza je? nikikuonyesha ushahidi kwamba yule ni bwana yako, nimfanye nini?...akanijibu niachane naye nisimsikilize tena na akasema yeye atakuwa Malaya na hafai...


Mmh nikaguna kidogo, nikamuuliza tena kama kuna jambo ambalo amefanya nae halafu hajaniambia basi aseme lakini wapi...akang'ang'ania msimamo wake.


Ndipo nikamuonyesha hizo picha mbili. Alitahamaki, akaanza kulia na kuoba msamaha tena kwa kunipigia magoti, ila moyo wangu ulishakufa ganzi nilipomuona anajiamini baada ya kupinga maswali yote niliomuuliza wakati ni uongo ambao hata yeye alikuwa akiujua kuwa ni uongo.


Kwasababu baada ya kumuonyesha zile picha tu alianza kulia na kuomba samahani nisifanye yale aliyojiapiza, wakati nilitegemea angezikana zile picha au angalau abishe bishe kidogo lakini alizikubali pale pale na kuanza kulia na kuomba samahani akinisihi nisifanye yale aliyojiapiza...


Hapo mimi nilinyanyuka na kuondoka zangu nikimwambia tusijuane tena...aendelee na huyo jamaa yake...


Hivi ninavyoongea mpaka sasa bado hatuna mawasiliano mazuri, mimi ndio sitaki kuwa naye tena japo roho inaniuma lakini nikimuangalia nasikia hasira sana.


Nimejaribu kumuuliza maswali kadha wa kadha kwamba kwanini na ilikuwaje ndani ya muda mfupi vile alifikia umbali wote huo wa kufanya ngono na mtu mwingine?


Akanijibu eti frustration tu..ndio zimemchanganya akajikuta kafanya hivyo...Mh akilini kweli mimi hainiiingii...Frustration?...Sasa swali langu mimi kwako na hata wadau wengine wanisaidie mawazo.

Je! sio kwamba huyo mtu alikuwa naye muda mrefu tu?...au ni kweli inawezekana ndani ya hizo wiki mbili ndio wamekubaliana na kutiana kweli?...

Na je! ni vyema mimi kumkubali na kumsamehe turudiane kama mwanzo?....je! Inawezekana ndio tabia yake?, kwasababu nijuavyo mimi, mwanamke yeyote anaweza akatongozwa karibu kila siku na watu tofauti, lakini kukubali ndani ya muda mfupi hivyo kumvulia mtu chupi na kufanya naye mapenzi sio rahisi tena ukiwa katika kipindi kibaya umegombana na mpenzi wako ambaye leo au kesho unaomba akusamehe ili mrudiane?


Pamoja na maswali hayo ukweli ni kwamba nimemchukia sana yule dada.

Sasa dada Dinah na Wadau wengine naombeni ushauri...nini cha kufanya hapo?

Natanguliza shukrani zangu, Ahsanteni"

------------------

Thursday

Yeye 40s with 2 Kids, Mimi 27 anataka ndoa! Je nikubali?

Habari Dada Dinah!
Naomba ushauri wako lakini naomba usinitaje jina langu.


Awali nilikuwa na uhusiano na kijana mmoja ulidumu kama miaka saba hivi. Hatukuweza kuwa pamoja kwa sababu mwenzangu alikuwa anasoma hivyo tulivumiliana kwa shida na raha.

Kwa kweli kaka huyo nilimpenda kupita maelezo lakini alikuwa na tabia zake nyingi ambazo nilizivumilia nikitegemea kuwa ipo siku atakuja kubadilika na hata hivyo niliziona kama ni ndogo kwani penzi la dhati lilitawala juu yake.


Mimi nilianza kazi huku mwenzangu akiwa bado anasoma, hivyo nilikuwa nikimsaidia kwa vitu vidogo vidogo na hata kumnunulia zawadi hasa kila siku yake ya kuzaliwa. Hivyo vyote sikuvihesabu kwani nilikuwa natoa kwa mtu nimpendae.


Kuna kipindi alianzisha biashara mbalimbali na kuna wakati alihitaji msaada wa pesa na mimi bila kinyongo nilitoa kwa moyo. Lakini zile biashara zilikuja kuisha kimya kimya na nikimuuliza anasema eti hajapata kitu chochote.


Yaani kwa kipindi chote hicho sikuona wala kupewa zawadi ya mafuta ya kupaka kama moja ya kifaida alichokuwa anapata katika biashara hizo.


Akaanza kuwa rafu kweli kwani alikuwa anafuga mindevu na nywele ndefu na kila nikimshauri ananiambia hii ndio life style yake na mimi siwezi kumuambia kitu na bangi alikuwa anavuta.


Hayo mambo yote niliyavumilia japo yalikuwa yaniuma sana hasa ukizingatia unamshauri mtu kitu na yeye anakipinga. Yaani ni mambo mengi alinifanyia kiasi kwamba nikasema enough is enough japo yeye hakutaka tuachane kwa kigezo kuwa amebadilika lakini sivyo.

Mapenzi yetu tulianza mwaka 2002 hadi mwaka 2009 nilipotosheka na vituko vyake. Niliamua kujikalia peke yangu bila mahusiano ya kimapenzi na mtu yoyote hadi leo.


Japo kwa kipindi chote hiki cha ukimya wangu huwa ananitumia meseji za kuomba msamaha kwa mambo yote aliyonitendea na kusema amebadilika na ikitokea nimemwambie mimi sitaki mahusiano tena na wewe basi atatuma meseji za kashfa na matusi kibao then anakuja kusema nimsamehe tena eti ni hasira ndizo zinamsababisha afanye hivyo.


Kwa kifupi Dada Dinah mimi kwake ni basi tena japo bado ananitumia meseji za kuniomba msamaha.

Sasa Dada kuna hili ambalo limenifanya niombe ushauri kwako, ni kwamba kuna Baba mmoja tulianza kufahamiana katika kazi niifanyayo japo nilianza kuona dalili za kunitaka kimapenzi lakini hakuwahi kuniambia hata siku moja.


Basi akawa anakuja kama kawaida kufanya kazi zake kunipigia simu kunisalimu. Ikatokea kipindi fulani akawa haonekani nina maana mkoa nilipo mimi yeye amekuja kusoma masters lakini makazi yake ni mkoa mwingine kabisa.

Siku moja akaniomba akutane na mimi na majibu yangu nikamwambia mimi sipendelei kutoka na mume wa mtu yaani kukaa nae sehemu. Akanijibu mimi nina watoto lakini sina mke nikamwambia mtu mzima kama wewe utawezaje kukaa bila mke? Akanijibu naomba utafute muda nikwambie maana ni story ndefu.

Basi tukaa akaniambia yeye ana watoto wawili wakike (darasa la saba) na wakiume (chekechea) na mkewe amefariki kama miezi minne iliyopita. Nikamwambie wanaume mara nyingi mnaweza kumuua mtu akiwa bado mzima.


Basi siku nyingine akaniletea mikanda ya video ya mazishi na nikagundua kweli amefiwa na mke.

Dhumuni lake kubwa anataka kunioa na sasa imepita kama mwaka mmoja tangu mkewe afariki. Nikamwambia swala la kupima amesema hamna shida twende tena mara tatu.


Yeye ni mwajiriwa wa Serikalini na tena ni Afisa Kitengo fulani huko mkoa anaofanyia kazi.

Dada Dinah, Mwanzoni nilikuwa najisemea mwenyewe kuwa mimi siwezi kuwa na mwanaume anayenizidi miaka saba na kuendelea maana nilikuwa nawaona ni rahisi sana kudanganya binti kwa upeo wangu.


Sasa huyu baba kiumri yeye amesema ana miaka 40 na kitu na mimi nina miaka 27 Je, hii ni sahihi kwa yeye kunioa mimi? na je kwa mtazamo wako huyu baba ana msimamo wa dhati kwangu?
*******************************


Dinah anasema: Habari ni njema tu, asante. Pole kwa kusumbuliwa na Ex, kuna Ex wengine wasumbufu sana. Hongera kwa kuwa na Msimamo ulionao mpaka sasa.


Kutokana na maelezo yako imeonyesha umakini na kutaka kujua "mzigo" alionao huyo Baba (Mjane). Inaonyesha anahitaji "mother figure" kwa ajili ya watoto wake na ndio maana amekuwa wazi tangu mwanzo.


Kitendo cha kuwa wazi na kukuonyesha mkanda wa mazishi ambao atakuwa kakuonyesha watoto wake na kuna maelezo yanayo-support maelezo yake kuwa ndio alikuwa Mfiwa, sioni tatizo hapo.


Umegusia kupima na yeye amekubali kufanya hivyo mkiwa wote nayo pia inatia moyo lakini hakikisha mnapima kweli Usiridhike na kukubali kwake haraka.


Pia ni vema wewe ukachagua pa kwenda kupima bila yeye kujua (kuna watu huonga Madaktari kutoa vyeti "fake").


Tofauti ya Umri sioni kuwa ni tatizo, kutokana na maelezo yako inaonyesha kabisa umekomaa na unajitegemea kiuchumi na kiakili (katika kufanya maamuzi).


Hayo hapo juu yakiwa sorted (ukiwa comfortable) kitakacho fuata ni kuendeleza uhusiano na kujuana zaidi, wewe uwajue wanae na wanae wakujue wewe na wakuzoee/kukubali.


Usiharakishe wala kulazimisha wakupende, kumbuka wamepoteza Mama yao mzazi hivyo wanaweza wakafurahi kuwa na "mama" au kukasirika kuwa umechukua nafasi ya mama yao....yote ni sawa tu, kuwa mvumilivu na muelevu.

Tuone nyongeza ya wachangiaji wengine.

Nakutakia kila la kheri!

------------------

Pages