Sunday

Zawadi ya kumpongeza Mke!

Da Dinah hi,

Pole na majukumu yako ya kila siku na hongera kwa moyo wako usio na kinyongo kwa ushauri katika kuboresha Penzi langu na laazizi wangu, MUNGU AKUBARIKI SANA KWA MOYO WAKO HUO.







Nimekuwa kwenye mahusiano na Mdogo wako wa kike kwa miaka takribani mitano na tuna umri unaokaribiana na tumeishi kwa upendo na Amani.









Kila mtu hubuni mbinu mpya ya kumshika vilivyo mwenzake ili afurahie umbaaji wake Mola kwa bidii na maarifa.







Kwa upande wangu huwa sipendi kwenda kumuona nikiwa mikono mitupu hasa nikiwa nina nafasi ya pesa mf. humnunulia Viatu kama Magauni, Nguo za ndani Peremende na kila aina ya zawadi ambayo moyo wangu utaniongoza.







Mke wangu huwa anashuru sana bila kujali ukubwa wala udogo wa zawadi kwa kweli namshuru MUNGU kwa hilo!







Sasa ni kwamba ameshika Mimba nami nataka nimpongeze kwa hatua hiyo je! ni zawadi gani ambayo wewe ungenishauri nimpe ambayo wanawake wengi huwa mnapendelea nawe ukiwa mmoja wapo?





Ni hayo tu kwa leo.





************



Dinah anasema: Hello! Ahsante kwa kujali na shukurani sana kwa ushirikiano.







Hongera kwako na kwa mkeo kwa kuwa wazazi wa kijacho, Mungu awakuzie na kuwalinda.





Mmh! Hilo litakuwa gumu kwani wanawake tunatofautiana, pia mimba zinatofautiana.







Mimi nadhani zawadi ambayo kila mwanamke mjamzito angependa kuipata ni Uelevu na uvumilivu (akinuna, akilia n.k), Ushirikiano(kwenda nae Kliniki n.k) Huruma(maumivu,kutapika n.k), Usaidizi na kuwa karibu kila anapokuhitaji.







Katika hali halisi sio zawadi bali ni jukumu lako kama Mume wake.





Vinginevyo Mnunulie nyumba au Shamba....



Kila la kheri!

Mapendo tele kwako...

Saturday

Nimeachana na Mume wangu bado nampenda.

Hi dada Dinah,
Ninaumri wa miaka 30 nina Watoto wawili niliolewa miaka mitano iliyopita.

Kiukweli mume wangu alikua na mapenzi makubwa sana kwangu hadi kufikia kuonewa wivu na majilani na baadhi ya ndugu hasa upande wa mumewangu.


Mimi na Mume wangu wote ni wafanyakazi, Matatizo yalianza baada ya mwaka mmoja kwenye ndoa baada ya mama mkwe na mawifi zangu walipokuja kututembelea na kukuta maisha ya amani na upendo tuliyokua tukiishi.


Kunakipindi mama mkwe alimwambia mwanae eti tuzae watoto wawili tu maana tayari kuna mtoto wa mdogo wake alishazaa so shuleni wamemuandikisha jina la mume wangu kama baba yake kwahiyo ni wetu na tumuweke kwenye mahesabu yetu.

Kwakweli sikukubaliana na hicho kitu, nikamshauri kuwa tutamsaidia kumsomesha na mambo mengine ila shwala la sisi kupunguza idadi ya watoto tuliopanga kuzaa hapana tukawa tumekubaliana.

*****************

Dinah anasema: What a bully Mkwe and Co! Kumsaidia mtu ni uamuzi wa Msaidizi (wewe na mumeo) na sio amri wala lazima hata kama msaidiwa ni Mdogo wako achilia mbali mtoto wake.

******************

Akamueleza mama yake, mama mkwe alibadilika kabisa na kudai eti mimi namnyanyasa mwanae  inakuje kila kitu anachoongea nae anieleze na kwanini hawezi kutoa maamuzi kama mwanaume hadi anishirikishe mimi.

Mwanzoni niliona kama utani mwisho ikawa majanga mume wangu akaanza tabia ambazo hakuanazo hapo nyuma, akawa anatoka nje ya Ndoa na wanawake tofauti tofauti.


Kukawa na kutokuelewana ndani ya nyumba, bila kujua chanzo ni mama mkwe nikawa namshitakia anamuonya mwanae na tabia hiyo inaisha nikamuamini sana mama mkwe nikidhani ndio mkombozi wangu kumbe ulikua ni mpango anaoufahamu vizuri na kukubaliana nao.

Nimejitaidi kuishi kwa mashaka hadi mwaka jana mume wangu alipo amua kuhama kabisa nyumbani na kuhamia kwa mwanamke mwingine.

Hakujua huku nyuma kaniacha na Ujauzito wa week moja baada ya week mbili nikajigundua ni mjamzito
nikamtalifu mama mkwe na shangazi yake nikijua kabisa watamtaarifu maana mume wangu alibadili namba ya simu nikawa sina mawasiliano nae.

Cha kushangaza mimba imefikisha
miezi sita mume wangu akanifuata Ofisini kwangu na kuanza kunieleza kwamba mimi nilimwambia dada yake kuwa ninamimba na mimba siyo ya mdogo wake, aliyenipa mimba yuko Dar.


Nikashangaa nikajaribu kumueleza hali halisi akagoma kabisa na akadai niwaambie kwetu waandae Mahali yake arudishiwe.


Miezi tisa baadae nikajifungua salama mtoto wa kiume  mtoto alifanana kila kitu na mume wangu nilifurahi nikijua suluhisho limepatikana.


Huwezi amini dada Dinah yule mwanamke anaeishi na mume wangu akajifungua pia mtoto wa kiume tarehe iliyofuata yani watoto wetu walipishana siku moja mimi nikianza yeye akifuata.


Siku zote hizo sikuwahi kujua kama yule mwanamke alikua ni Mjamzito baada ya week mbili mama mkwe alikuja kunisalimia  akakaa siku tano siku ya sita akaaga anaenda kijijini kwao.

Kumbe haikuwa kweli alikua anaenda kumsalimia mke mwenzangu na akakaa huko siku nne  akarudi kwangu bila kujua alivyokua huko alikutana
na watu wanao mfahamu na wananifahamu mimi maana alikua anakuja kila mara pale kwangu.

Alivyofika mimi sikutaka kumuonyesha kuwa najua alipokua nikamuuliza nyumbani hawajambo akasema hawajambo nilikuta kunawagonjwa huko ndio maana nikachelewa kurudi.

Mie uzalendo ukanishinda ikabidi nimuweke wazi kuwa najua kila kitu huko alikokua akabaki anajiuma uma tu na kesho yake wakaaga na kuondoka kwa aibu.

Baada ya hapo nilikuwa kama mwendawazimu nikizunguka kwa Waganga huku na huku na bila suluhisho cha zaidi niliambiwa mume wako anakupenda sana ila mbaya wako ni mama mkwe wako, amekutupia mkosi hadi mwanaume akahama nyumbani.


Siuamini kama kuna mzazi anayeweza kuharibu Mji wa mwanae, pamoja na majibu hayo lakini waganga wote hakuna aliyeweza kunisaidia.

Mwisho wa siku nimeamua  Kuokoka na ninampenda Yesu naamini mwisho wa matatizo yangu umefika nahitaji muungane na mimi katika maombi ili familia yangu irudi kama zamani.


Nafanyiwa maombi na Mchungaji  kunakitu aliniambia nikashangaa sana aliniambia "unajua kilichomtoa mume wako nyumbani?" Nikamwambia hapana mchungaji akaniambia
"nimefunuliwa wakati wa maombi ndugu wa mume wako walikukalia vikao sana hatimae wakafanikiwa kumgeuza akili mume wako ila Mungu ni Mwema muda si mrefu atarejea zidi kuomba na kufunga sana".


Kilichonifanya niandike haya ni kutaka kujua hivi ni kwanini wazazi hasa wa upande wa Kiume wanapenda kuharibu maisha ya watoto wao hasa  mama wakwe na mawifi?

Kwanini kama kunatatizo wasimueleze mtu hadi kufikia kumuendea kwa Waganga ili aachike ona sasa familia inavyotaabika.

Baba alishakataa kutoa matumizi na hataki kuwaona wala kuwasikia watoto wake kweli hii ni sahihi jamani?

Yaani huwezi amini kuanzia nimejifungua huyu mtoto baba mtu pamoja na kupata taarifa kafanana kila kitu lakini   hajawahi hata kujakumuona.

Naumia sana moyoni  nahitaji maombi yenu na ushauri wenu. Thanks dada Dinah.

****************

Dinah anasema: Gosh! mie nina Imani na Msimamo wangu kama mwanamke well kama Dinah.


Ndoa ni uvumilivu sawa, nakubali na nitavumilia magonjwa, nitavumilia ukosefu wa pesa, shida na matatizo ya kibinaadamu LAKINI kutoka Nje ya Ndoa hakuvumiliki.....am gone!

Pole mwaya kwa yote na usiumie sana kwani sio Mwisho wa maisha yako bali ni mwanzo mpya.....ngoja niende tu kwenye NUKTA.


Kwa kawaida Walokole hupeana matumaini na Moyo mpaka wakati mwingine wanakuwa wajinga na kupotezeana mida bila sababu ya Msingi.


Don't get me wrong, nina amini katika Yesu, Maombi ni sehemu kubwa ya maisha yangu ya kila siku, Mungu katendea mambo mengi ya ajabu na Mazuri maishani mwangu ila mimi sio Mlokole na siwaamini wanaojiita WALOKOLE.


Mumeo anakula raha huko na kijifamilia chake kipya, wewe unashupaa kujibana, kulia, kuwaza, kuhuzunika, kujiuliza kwanini nyingi, kukasirika n.k.


Hayo yote yanazuia bahati ya kukutana na mwanaume mwema ili ufurahie maisha kama mwanamke na kama mama kwa kuamini " siku moja mume wangu atarudi na tutakuwa na furaha".....mumeo sio Yesu....move on Mdada.


Baada ya yote aliyokufanyia yeye na familia yake + kumkataa mtoto bado unataka arudi kwako ili uendelee kuishi na mijitu ileile iso na Utu, Hekima, Heshima wala Ubinaadamu.


Kwa bahati nzuri unakazi yako, endelea kuangaliwa watoto wako wawili na kuwaonyesha upendo na furaha.

Piga kazi kwa bidii, ongeza Elimu ya Ujuzi kipindi hiki watoto bado wadogo ili uwe na uhakika wa kusimamia Elimu yao hapo baadae (upande Cheo au kupata kazi inayolipa zaidi).

Simama kama mwanamke ili wanao waje kujivunia Mama yao sio kwa kuwazaa(hukulazimishwa) bali kwa kuwalea vema, kuwatimizia mahitaji yao, kuwapenda na kutumia muda mwingi ukiwa nao.


Hii ni 2014 hatuhitaji wanaume bali tunawataka ili kufurahia maisha sasa kama ulienae hataki kuwa na wewe ili mfurahi pamoja basi songa mbele na utakutana na mwingine (ila usizae tena).

Najua hii inakwenda kinyume na Imani yako ya Kilokole but trust me, Mungu anajua kuwa umejaribu na imeshindikana na am sure atakubariki zaidi kama unafuraha na mwanaume mwingine iwe kwenye ndoa au uhusiano wa kudumu.

"Mambo ya Mume wangu atarudi tu"....."ni mwanaume wangu wa kwanza siwezi kuwa na mwingine"....."Penzi la kwanza haliishi" ni upuuzi.

Kuna watu wamepoteza (fiwa) Wenza wao wakiwa bado wanawapenda lakini baada ya kuomboleza na kukubali kuwa "ndio imetoka hiyo" huendelea na maisha yao kama ifuatavyo.....

Kumbuka maisha hayakusubiri wewe umalize kwanza kusononeka na kulalamika...maisha yanaendelea nawe huna budi kusonga nayo.

Watoto wakikua watamtafuta baba yao, usitieshaka wala kupoteza muda kufunga na kuomba Mumeo arudi kwako. Nani anataka ku-share mwanaume? ewww!

Piga kiberiti kila kitu kinachomuhusu huyo mwanaume, choma moto Kitanda na Godoro mlilokuwa mki-share.

Ikiwezekana hama nyumba, kama mlijenga basi fanya mpango wa kuiuza alafu uhamie kwingine(jenga kwingine).

Nenda Mahakamani kuomba kumtaliki Mumeo (Kisheria Tz inaruhusiwa mwanamke kumtaliki mwanaume)....

Kisha nenda Ustawi wa Jamii ili wakusaidie kuhusu matunzo ya watoto kutoka kwa Baba yao (sio lazima kama mwenyewe unajiweza kiuchumi).

Endelea kuomba ila maombi yasihusu mumeo kurudiana na wewe (wacha kuishi kwenye maisha yaliyokwisha pita) na badala yake ishi maisha uliyonayo sasa na yajayo.

Omba Mungu akupe mwanaume mwema, atakaekujali, kukupenda na kukuthamini.

Omba Mungu akupe afya njema ili uendelee ku-provide kwa watoto wako, awape afya njema watoto na uelewa ili wasikusumbue kuulizia habari za baba yao.

Omba ili Mungu akusaidie kufuta "emotions" zote kuhusu mumeo ili uweze kusonga mbele kiurahisi zaidi...Ni ngumu sana tena sana lakini utaweza tu.

Hilo la "Kwanini Mama Mkwe na Ndugu wa mwanaume huwa na roho mbaya au waharibifu wa maisha ya ndugu zao?"....fufanye iwe Topic siku zijazo.


Tuone wengine watasemaje....

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Friday

Mume si Mtekerezaji...

Hi da Dinah mie na mume tunapendana sana lakini tatizo mwenzangu bado
hafikirii maisha.

Kila nikimshauri mambo ya maana huitikia lakini kutekereza hatekerezi. Tumejaaliwa mtoto Mmoja muda mwingine nawaza labda mwenzangu ana mwanamke mwingine.

Kila tukikubaliana tuweke pesa ili tuweze kufanyia vitu vya maana mwenzangu anakubali ila
utekezaji hamna naomba ushauri wako dinah.


************

Dinah anasema: Habari there!


Labda vitu vya maana na muhimu kwako, kwakwe sio hivyo....si unajua watu tunatofautiana!

Ila kuna wakati tofauti inawekwa pembeni na kukubaliana kufanya mambo kama Team(mke na mume) kwa faida yenu kama familia.

Kabla hatujamshutumu kuwa na mwanamke mwingine nje ya ndoa yenu....je? Unajua kipato chake na kama ndio kipato kinaendana na matumizi yenu?


Je? Wewe unashughuli inayoingiza pesa (kazi/biashara) na je? Kipato chake JUMLISHA Kipato chako TOA matumizi muhimu (Pango, Bills, Chakula, Mtoto) mnabaki na kiasi gani?


Inabidi mkae chini na mzungumze tena kwa kuhimiza na sio kwa hasira (usichoke wanaume wengine wanachelewa kukua kiakili)....muanze kubajeti matumizi yenu ili kupatikane pesa ya kutunza kwa ajili ya mambo muhimu kwa wote kama familia.


Mkubaliane kuwa mwenye Kipato kikubwa afanye arekebishe mahitaji yote ya mwezi na mwenye Kipato kidogo atunze (weka Akiba Benki) kwa ajili ya Emergencies na mambo mengine ya maana.

Mkubaliane kwenye matumizi yenu ya kila mwezi, mfano kwa miezi 3 hakuna luxuries (pombe, gauni jipya n.k) na senti itakayotunzwa muda huo itumike kununua Sementi...kwa mfano!


Kama mwanaume ni mzembe kwenye utekerezaji mwanamke inabidi uchangamke na umsukume kwa ushauri na wakati mwingine umuongoze au kumuonyesha mifano halisi.

Ikishindikana basi jaribu kubana matumizi kwenye pesa za matumizi anazokupa kila Siku/Mwezi/Wiki na utunze kibindoni.

Watu tumetofautiana kimalezi, huwezikujua alikulia mazingira gani....si unajua wale watu wa "kila mtoto anakuja na bahati yake, na tutajua hukohuko muda ukifika" sort of people.

Pamoja na kusema hivyo, kama hujui Kipato chake na hakuna cha maana anachokifanya kwa familia yake (wewe na mtoto) basi inabidi utafute ukweli wa wapi anapeleka kipato chake kila mwezi.


Ni mumeo, ninyi ni mwili mmoja lazima ujue kipato chake na yeye ajue chako eti!...Kama hujanielewa tafadhali usisite kunicheck tena.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Thursday

Ananipenda but ni Jobless....

Da Dinah mie ni msichana nipo katika mahusiano ya mwezi mmoja sasa na huyu boyfriend wangu but kinachonkira ni yeye kuaw jobless.

Kutwa yuko home, I know love is not money but money is the part of love ukitaka kustawisha penzi tumia vyote.

Sijajua ni kwanini hajishungulishi hata kutafuta kazi ya kujishikiza tangu mtokeo ya form 4, 2011. Sijajua ni wazazi au yeye kwasababu nikimuuliza huwa hanielezi anapotezea.

Mie nampenda lakini sidhani kama kutakua na future nzuri kati yetu so nifanyaje?


He is 22 and am 24 and am student at_______(Dinah kahifadhi).


************


Dinah anasema: Ahsante kwa ushirikiano.


Aliyekuambia kuwa "money is the part of love na ukitaka kustawisha penzi tumia vyote" ni MUONGO.


Pesa ni muhimu maishani lakini sio sehemu ya mapenzi. Huitaji pesa ili kumpenda mtu....unahitaji hisia (Moyo/Akili/Mwili) na Utu.

Ukitaka kustawisha uhusiano wa kimapenzi unahitaji mambo kibao kama vile Mapenzi ya kweli, Ushirikiano, Heshima, Uelevu, Uvumilivu, Maelewano, Mawasiliano, Uwazi, Ukaribu, Usikivu,Huruma,Usafi nakadhalika....pesa is none of them.

Unapomuona mtu na kuvutiwa nae kisha kumdondokwa kimapenzi huoni Bank account yake, huoni kazi aifanyayo wala uwezo wa wazazi wake. Unamuone yeye kama mwanadamu sio?!! Anyways...

Ndani ya Mwezi tu umeisha anza kuwa pushy.....wala hujamjua kijana wa watu vizuri, hujui hali ya kimaisha/kiuchumi aliyonayo na mipango yake huko baadae baada ya kumaliza Sekondari 2011.

Usikute anakupotezea kwavile bado hajakuamini, I mean...ndani ya mwezi mmoja nani anaweka kila kitu chake wazi?

Isitoshe wewe ni nani kwake mpaka uanze kumuuliza na kumsukuma atafute kazi? Unless otherwise anakuomba pesa....still huna mamlaka ya kumsukuma akatafute kazi baada ya kuwa nae mwezi mmoja tu.....subiri mwaka hivi labda!

Kutokana na maelezo yako inaonyesha huyo bado ni mtoto ambae yupo chini ya wazazi wake....sana sana anataka ku-have fun na wewe na sio kukufanya uwe wa kudumu (kuwa na future).

Unajua wanawake huwa tuna-mature kiakili haraka kuliko baadhi ya wanaume, mwanamke wa miaka 22 ni tofauti kabisa na mwanaume mwenye umri huo(kiakili).

Kama wewe unaumri wa miaka 24 na bado ni mwanafunzi, yeye wa miaka 22 pia anahitaji Elimu zaidi ya kumpa ujuzi ili kumuwezesha kufanya kazi au kuajiriwa.

Kama pesa ni muhimu sana kwako au kwenye uhusiano wowote utakaoingia basi ni vema umuache mtoto wa watu, maana asijeshindwa kukuridhisha kipesa ukamuweka kwenye "remix" na Njemba wenye mahela.

Tangu umeweka pesa mbele ni vema uongeze bidii kwenye Masomo yako, umalize upate ajira kisha uanze kujichanganya na Vijana ambao tayari wapo kazini au wanabiashara(wanapesa) na wakubwa kiumri angalau kuanzia miaka 26 kwenda juu.

Achana na watoto wa Shule/Chuo, ukishika Mimba mtapelekana wapi?

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Wednesday

Kitu cha Mviringo ndani ya K!

Mimi bado ni mchanga kwenye mambo ya sex kwasababu nina mda mfupi tangu nimeanza ngono.







Naishi mbali na boyfriend wangu na tunaonana baada ya muda mrefu ila kila tukikutana kwa sex napata maumivu mwanzo wa uke.







Pia nikiwa najisafisha ndani ya Uke nahisi kama uvimbe kwa juu (wa mviringo) sijui kama ni kitu cha kawaida ama vipi na kuna siku boyfriend wangu alinambia wakati yuko ndani ya uke alihisi kama kitu kinamsukuma na hata mie nilihisi hiyo hali pia na nilihisi maumivu kidogo.







Naomba kama unaweza nisaidia kwa haya please.





***********



Dinah anasema: Hello there!



Kupata maumivu mwanzo wa uke nadhani kunatokana na kukaa muda mrefu bila kufanya ngono mie huwa naita "second time virginity".....sio Bikira ila maumivu yake yanakaribiana kwa mbali.







Kutokana na uzoefu "kuna kitu kama kinamsukuma mwanaume" ni Cervix au shingo ya Uzazi/Mlango wa uzazi.







Kila mwanamke anayo hii sehemu ila ni wachache ambao wanaweza kuifikia kutokana na ukaribu wake au umbali wake(inategemea kina cha Uke).







Unajua ukifungua mdomo na kuangalia kwa ndani kule mwisho wa ulimi unaona kama "kidole" hivi eeh, basi na shingo ya Uzazi ipo hivyo.







Hii Shingo ya Uzazi hufunguka na kufunga, inategemeana na mzunguuko wa Hedhi na hali ya kuwa tayari kushika mimba.







Hiyo sehemu ikiguswa hutoa maumivu yenye mchanganyiko na utamu....utamu unatokana na kuta za kuke na ule wa mwanzo wa Uke.....(Inabidi uwe na uzoefu kwanza).







Lakini usichukue maelezo yangu haya ya kisha ukatulia kwani mie sijahisi unachohisi, nimeelezea kutokana na uzoefu.





Hivyo ni vema ukaenda kumuona Daktari ili akuangalie na kukupa all clear!





Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

how to stop being a one minute man

There are a number of ways to stop premature ejaculation available on the market. Men that suffer from this condition typically ejaculate sooner than they or their partners would desire. If you happen to be one of these men, you can at least take comfort in the fact, that you are not alone.
Research has revealed that as many as 3 in 10 men worldwide suffer from this embarrassing condition. It's not surprising that premature ejaculation is almost every woman's number one complaint when it comes to having sex.
The sad fact is that there are some men that do not seek help to cure their condition, as they find it too shameful to discuss it with anyone, not even their partners. They end up suffering in silence and it can have devastating effects on a relationship.
There are various ways to stop premature ejaculation available to men serious about finding out how to cure this condition. Like anything in life you need to have a better understanding of what really works. A very popular method that lots of men are choosing to use of recent are the natural home remedies.
Benefits of natural programs to compared to other methods are:

1. Many medical experts recommend the use of simple natural home treatments for certain conditions nowadays
2. Since it's 100% natural it's much safer to use
3. Natural cures for this condition have no side effects
4. Using pills, desensitize sprays or creams only treat premature ejaculation they are not a cure for the condition. Some pills contain chemicals that can be harmful to you
5. It's a one time payment that is much cheaper than pills or creams
6. Using a desensitize cream numbs the sensations you should feel during sex
7. It cures the condition permanently, so you can start enjoying sex like you never thought possible
Instead of worrying about the different ways to stop premature ejaculation your whole life, you can choose to do something about it. Sex should not be a shameful experience that you dread. Using a simple natural program is a method worth considering, it can be used in the privacy of your own home. The money back guarantee offered also makes it risk free to you.
If you would you like to discover more natural Ways To Stop Premature Ejaculation And start enjoying passionate, mind blowing sex for as long as you like. Then go to http://cureprematureejaculationnaturally.info to discover a simple natural home program that so many men have used to successfully cure their condition permanently. It's easy when you know what really works.

Tuesday

SAMSUNG GALAXY S5 and  RELEASE DATESamsung has launched its Samsung Galaxy S5 smartphone during the Mobile World Congress 2014. Despite the announcement, the device will not hit stores until April 11. The device will reportedly hit stores first in the UK before trickling to other regions.

 Full Image

Reuters

New Samsung Galaxy S5 smartphone (L), Gear 2 smartwatch (C) and Gear Fit fitness band are displayed at the Mobile World Congress in Barcelona February 23, 2014. Samsung Electronics unveiled a new smart watch and fitness band along with the latest version of its flagship Galaxy smartphone on Monday, demonstrating how the battleground for innovation is shifting from the hand to the wrist. Picture taken on February 23. REUTERS/Albert Gea

 

Recent reports suggested the Korean tech giant also plans on releasing a Prime version. What can Samsung Galaxy S5 Prime offer? 

Samsung Galaxy S5 will be available in a Prime version, according to a leak by @evleaks in February 2014. After that, several reports have sprung up about what people should expect from the official release of the upcoming flagship.

According to the full review reported by GSM Arena, while Samsung claimed the water will only be water-resistant, the review noted it might also be waterproof. 

The report showed a picture of the device under the faucet. Apparently, the unit has not been damaged even after all the water exposure. Samsung also transformed the display compared to previous models. According to GSM's review, the color accuracy appeared to be better. The report noted color accuracy is also good despite odd viewing angles. It is a big leap from Samsung Galaxy S4. 

The device will also come with a 16 MP camera featuring ISOCELL technology. According to Motoring Crunch, the camera on S5 will be fast featuring autofocus at 0.3 seconds. It is not clear yet whether it has some real good advantage over the technology in S4. 

Motoring Crunch also noted consumers can expect impressive computing performance because of the Snapdragon 801 processor. This is despite the lower RAM compared to Note 3 and Xperia Z2. Samsung Galaxy S5 will only have 2 GB whereas Note 3 and Xperia Z2 come with 3 GB RAM. The Snapdragon processor will be clocked at 2.5 GHz. The device will be shipping with 16 GB internal storage plus SD card support. 

According to reports, Samsung Galaxy S5 will have 5.1-inch display plus FHD Super AMOLED display. It will have resolution of 1920 x 1080p plus pixel density at 432 ppi. Other features include 2,800 mAh, Android 4.4 KitKat and TouchWiz.

For more information about the Samsung Galaxy S5 handset, check out this video. 

To contact the editor, e-mail: editor@ibtimes.com

Sunday

Hedhi kigeugeu, nashindwa kushika Mimba.

Jambo da Dinah first of all pole kwa kazi. Nimeijua blog yako for a long time now and it taught me a lot of stuff.





So dada swali langu is I have been in my marriage for long now bila kupata bahati ya mtoto na tatizo langu kuwa ni kwamba sijui kuhesabu mzunguuko wangu kwani tarehe zinabadilika sana.







Hata sielewi kama ni tatizo au ni normal hii inashifanya nisijue ovulation days zangu.







Mwezi wa Sept niliingia tarehe 7, October nikaingia 5, November it was 7, December was 15, January was 18 and February was 14.







Tafadhali naomba unisaidie, nasubiri majibu yako. Thanks sana Mungu awe nawe and your family.



*************



Dinah anasema: Ahsante kwa kujali na shukurani kwa ushirikiano.





Uzoefu wangu ni wa mzunguuko wa kawaida wa siku 28, nikianza kuelezea na kutoa mahesabu hapa kuhusu mzunguuko wa kubadilika-badilika (siku 24-35) nitakuwa nakudanganya tu mdogo wangu.





Hata hivyo sidhani kama mzunguuko wako unafanya usishike mimba hasa kama mnafanya mapenzi zaidi ya mara 3 kila wiki...kwa mfano.







Kumbuka Manii hudumu kwa siku tatu na hata zaidi (inategemea na afya yake) hivyo kama mnafanya mapenzi ya kutosha ndani ya Mzunguuko bila kujali tarehe ni wazi mimba itanasa tu.







Unless otherwise kuwa na mambo mengine yanayoingilia au kuchangia kutoshika Mimba.







Suala muhimu ni ku-relax maana stress huwa zinaingilia utungwaji wa mimba. Natambua kuwa unapokuwa unahitaji sana mtoto unajipa mawazo na pressure za hali ya juu hali ambayo hupaswi kuwa nayo wakati unajaribu for a baby. Hilo moja.







Pili, angalia mtindo wa maisha yako, kama ni mwembamba sana mambo ya diet nini na nini....acha kama unafanya hivyo.....kula balanced diet sio Junk (chips, pizza, soda n.k)







Tatu, Unene....kama mwili ni mkubwa pia inaweza kusumbua, fanya utaratibu wa kupungua kiasi.







Ikiwa hujashika mimba baada ya Mwaka moja tangu ufanye mabadiliko basi wewe na mumeo muende kwa Daktari kwa Uchunguzi na Ushauri wa kitaalam.





Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Saturday

Shoga kipenzi hajui nimezaa na BF wake, nimwambie au niuchune?

Habari za kazi dada, nasoma makala zako sana, nna tatizo nahitaji
ushauri wako.

Nimekuwa na rafiki yangu wa muda mrefu sana kama best friend tunapendana sana kama miaka 4, ana mpenzi wake ambaye nilimfahamu
kupitia yeye, tumezoeana kupita kiasi.


Nilianzisha uhusiano wa siri na shemeji yangu kwa muda wa miaka 3 na
mpaka sasa nimezaa nae mtoto 1 na anamhudumia mtoto.

Rafiki yangu hatambui kama nimezaa na mpenzi wake mpaka sasa na pia bado tunawasiliana sana tu.

Mzazi wake baba wa mtoto anajua mimi ni rafiki wa mwanamke na nimezoeleka sana na mzazi wa mwanaume, anajua nimezaa lakini hatambui kama nimezaa na mtoto wake.

Naumia sana kila nikifikiria hili kwani natambua nimemkosea sana huyu rafiki yangu sielewi siku akijua haya yote itakuaje. Naomba ushauri dadangu.

*************

Dinah anasema: Habari ni njema na shukurani sana kwa ushirikiano.


Duh! Aren't you fast?!! Baada ya mwaka tu ukajisevia mpenzi wa mwenzio....alafu watu wananishangaa kwanini sina marafiki na inakuaje sina hata best friend!

Wala humpendi na hujawahi mpenda rafiki yako bali unadhani kuwa unampenda. Ungekuwa unampenda usingezoeana na Mpenzi wake hivyo na ungeheshimu mipaka ya urafiki na upendo kati yenu.

Basi ungetumia kinga usishike mimba angalau (labda angekusamehe)....au ilikuwa mambo ya PMU(Pata Mimba Uolewe), ukampiku mwenzio eti?!

Je bado unaendeleza uhusiano na huyo bwana au uhusiano umeisha baada ya Mimba....huyo bwana nae the shenzi kabisa.


Mwambie huyo mwanaume amuambie Mpenzi wake (rafiki yako) alichokuwa akikifanya kwa miaka yote 3 mpaka kuzaa na wewe.

Au wewe mwenyewe umwambie moja kwa moja kuwa kwa miaka 3 uhusiano wake ulikuwa wa watu watatu, yaani wewe, yeye na huyo mwanaume.

Usimwambie katika hali ya kujidai au kumnanga, kumbuka umemkosea mwenzio sana tena SANA.....go to the point...Mf: "nimeficha siri kwa muda mrefu, nisamehe kwa hilo! Huyu mtoto nimezaa na bf wako".

Na huko kwa mkwe wala usijipendekeze, mwenye kwao akitaka mzazi wake ajue basi atamwambia.

Fanya haraka ili mwenzio afanye uamuzi muhimu wa maisha yake kuliko kuendelea kupoteza muda na ninyi wanafiki.


Kila la kheri!

Mapendo tele kwako...

Friday

Nimtokee bila taarifa!

Da dinah shikamoo.! Pole na majukumu ya kusaidia mapenzi ya watu kila
uchao!

Da dinah nina age ya 22 nipo kwenye relationship na mwanaume kama miezi 3 saizi tatizo limeanza baada ya mimi kuwa mbali kama 3weeks hivi.


Nahisi anamwanamke zaidi yangu kwasababu hata namna ya kuongea
inanitia mashaka.

Kuna wakati akiongea na mimi anaongea vizuri sana but sometimes nikimpigia simu anaweza akaongea haraka haraka and mda huo najua yupo nyumbani kwahivo hayupo bize.


Nkimuuliza mbonahivo upo na nani? anakata simu then anafunga simu kabisa, kesho yake anaweza kuniambia simu imezima haikuwa na chaji au hapendi maswali yangu kwani
naonyesha kama simuamin.

Da dinah nataka nimfanyie suprise visit, sababu nimesharudi safari naye hajui kama nipo hapa mjini ili nijue kama kweli anakua bize au maswali yangu yanamkera na hamna kingine.


Je hii suprise ndio itaua kabisa mapenzi au nifanyaje da dinah.


**********


Dinah anasema: Marhaba mrembo, hujambo?


Haka kaumri huwa kanasumbua sana, high expectations na hofu nyingi kwenye uhusiano kabla uhusiano haujawa UHUSIANO.

Huyo nae wa wapi? Au ni utoto unaulizwa swali....unakasirika na kumkatia mtu simu...so rude!

Miezi mitatu ni mapema mno kuanza kumfuatilia bf....sana sana utakuwa unaumia na kupoteza muda kuwaza na kuwa paranoid kuhusu bf ambae uwezekano wa kuwa mumeo ni mdogo au haupo kabisa.

Sina maana usiwe na bf, la hasha! Bali ni kutomchukulia huyo mjamaa kuwa ndio atakuwa mumeo na badala yake enjoy ujisia wako kama mwanamke na ukumbuke kutumia Kinga ili usikamate Mimba au magonjwa ya zinaa.

Umri huu ndio mzuri kuanza kufurahia uanamke wako, kuzingatia masomo kama upo Chuoni au kuanza kutafuta namna ya kujikomboa kama mwanamke, sio kupoteza muda kuwaza na kuwazua kuhusu bf.

Hakuna sababu ya kumtokea kwake bila taarifa, isipokuwa ukipata nafasi zungumza nae kuhusu tabia yake ya kukukatia simu au kukuzimia kabisa it's kind rude.

Nae (kama ana kerwa) ataweka wazi kuhusu tabia yako ya maswali mwengi ya kijinga/kitoto....upo wapi? Upo na nani? Mbona unaongea hivyo kuna mtu hapo?....hivi unanipenda kweli n.k

Wote kwa pamoja mfanye mabadiliko ya tabia zenu kwa wakati wenu.


Nakubali maswali mengi yanaweza kuudhi hasa kama mtu kachoka au ana-stress za mizunguuko yake, lakini hiyo sio sababu ya kumkatia mtu simu na kumuacha kwenye limbo!



Kwa sasa mchunie (tufanye umekasirika), subiri mpaka yeye akutafute. Ni ngumu sana kama unampenda lakini itakusaidia huko mbele.


Wewe mwanamke bwana, unawindwa....hawindi. Hakuna sababu ya kupigapiga simu kila mara


Uhusiano sio lelemama, na at 21! Safari ni ndefu...


Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

WIFE MATERIAL

14 ways to tell she's wife material.


SHE DOESN'T SMOTHER YOU. She knows you have friends and need your "guy time." What's more, she happy that you go out and have fun with your buds.

Girls just wanna have fun. She's able to let her hair down and just have a good time. But...

...she's also responsible. She's not a non-stop party girl.


SHE'S A GREAT COOK and ENJOYS IT. There's a lot of truth behind that whole "The way to a man's heart is through his stomach" line.


SHE PUTS UP with YOUR TRAP. Guys do a lot of stupid things. Apparently it's in our genes. (Or is that jeans?) Rather than just bail or call it quits, she tolerates some of the more idiotic things you do. But then again...


SHE's NOT a DOOR MAT. She may let you get away with something once or twice, but she'll most definitely let you know she's not happy about it.


SHE's SELF CONFIDENT. Nothing, as in nothing, is sexier on a woman than self-confidence. Which reminds me of another good point.


SHE'S SEXY. Hey, guys are 95 percent visual creatures, so if just looking at your huge... tracts of land helps him stand at attention, that's a good thing.


SHE'LL WATCH DIE HARD WITH YU. Granted, you'll probably have to suck it up and see some Renee Zellweger flick, but compromise is the strongest pillar in any marriage.


SHE's GOOD WITH MONEY. Good at making money is even better, but it's great if she can keep her eye on the checkbook and make educated purchasing decisions. Somebody has too, right?


SHE HAS a SENSE OF HUMOR. Whether she's cracking jokes or laughing it up at yours, she definitely knows that, as Oscar Wilde put it, "Life is too important to be taken seriously."


SHE PUTS FLORENCE NIGHTINGALE TO SHAME. When you're home sick, she'll race over with a container of chicken soup. She'll cover you with blankets, prop your head up with pillows, and rent your favorite movies. She'll do everything she can to nurse you back to health.


SHE HAS GOALS. Doesn't matter if it's career goals, life goals, or wanting to climb Mount Everest, she has dreams and isn't afraid to go after them.


SHE MAKES YOU A BETTER PERSON. She makes you want to do more, be more. When you're with her, you really work at becoming a better man all around.

HUSBAND MATERIAL

 husband material. Qualities that anyone might notice and say, "Wow, what a mensch!" but that one lucky woman recognizes as reasons to marry the man!


In an effort to nail those reasons down, our friends at YourTango actually surveyed mental health professionals about what actually makes a man husband material. While the ability to communicate, honesty, and reliability came out as top traits, and those make perfect sense, there are many of other characteristics that make a guy a keeper. Without further ado ...

HE'S SUPPORTIVE no MATTER WHAT. Whether you're struggling with your career or health or any other personal challenge, we all want a man who is going to be encouraging, stick by our sides, and want to support us financially, emotionally, etc. even when he would have no need to.

HE's LOYAL. Obviously someone who would never cheat or sell you out, but also ...
... NOT A MAMA'S BOY. No one wants to spend a lifetime with a man who will repeatedly put his mom before you.
But he's not disrespectful of his mom. YourTangoExpert Jennifer Elizabeth Masters warns, "If a man is disrespectful of his mother, he will disrespect you. If he does not get along with his mother, he is a bad risk."

HE's FAMILY ORIENTED. Even if you don't necessarily want to have kids, you probably want to marry a guy you can build a home and a life with. And who prioritizes togetherness with loved ones. Every time I see how important it is to be close with his family, I'm reminded what a wonderful husband my fiance will be.
HE'S PATIENT. File a guy with a hair-trigger temper under "do not want."

HE WOULD DROP WHAT HE's DOING to HELP LITTLE OLD LADIES or CHILDREN or anyone in need cross the street. Self-explanatory.

HE'S FUN to BE AROUND. Life's short, but also too long to be bored by your partner.

HE'S SEXY. It never hurts to find your man irresistibly attractive.

HE'S FLEXIBLE. Some people are just naturally more stubborn, but a marriage is a two-way street, so he's gotta be willing to compromise.

HE'S COMPASSIONATE. Being able to sympathize and empathize with others proves he's got a huge heart.

HE'S INTELLECTUALLY CURIOUS. Gotta love a man who never wants to stop learning. Keeps the conversation flowing and life exciting!

HE'S MOTIVATED and STRONG. Conviction, drive, passion, etc. isn't just hot but it'll help him push through life's adversities.

HE HELPS YOU TACKLE YOUR TO DO LIST WITHOUT BEING ASKED. He'll take your little fluffy lap dog out for a walk or go get your car's oil changed, just to make your life less stressful.

What are some other traits do you think make a guy husband material?x

This are best five sex position .........which It's time to upgrade your sex life, and to get your partner turned on like never before.


 




We already knew that women love sex, but have we ever thought of sex positions wome

Mpenzi kaacha wivu, karelax ile mbaya!

Dinah habari za kazi na pole sana. Mimi ni Mwanamke mwenye umri wa miaka 32 na Mume wangu anakaribia 42. Ndoa yetu imejaaliwa mtoto Mmoja wa Kiume mwenye umri wa Miaka 4.

Tangu urafiki, uchumba na ndoa mume wangu alikuwa ni mwenye wivu wa mapenzi, sio wa kufokeana na kugombana.

Nikitoka lazima apige simu kuangalia kama nipo salama, kama nipo na wenzangu alikuwa akitaka kuongea nao ili kuhakikisha kuwa kweli nipo nao kama nilivyomuaga.

Tulipokuwa pamoja alikuwa ananishika Mkono kama vile anaonyesha kuwa mimi ni wake na nilikuwa nafurahi sana na kujisikia napendwa, nalindwa na ananijali.

Kuanzia mwaka jana, Mume wangu kaongeza mazoea na mmoja wa marafiki zangu lakini kwa vile nawaamini wote sina mashaka nao.

Kinachonitia mashaka ni mume wangu kuacha kuonyesha wivu, yaani karelax mno hadi nahisi kama vile hanipendi tena.


Je ni utu uzima unamnyemelea au kuna zaidi? Naomba ushauri. Asante.


************


Dinah anasema: Ahsante na shukurani kwa ushirikiano.

Unapofundwa unaambiwa wazi kuwa usimuamini sana mumeo (kwa asilimia zote) na ukiona ana-relax, mtingishie kiberiti makusudi (mfanye apate Wivu).

Kutokana na hali ya maisha ilivyo sasa mie ninasema Usimuamini Mpenzi wako kwa asilimia zote iwe ni Mwanamke au Mwanaume.

Kuna baadhi ya watu wanadhani kumuamini mtu ni sifa za Mke/Mume mwema, na baadhi hufikiri kuwa ni hali ya kujiamini wao kama wao.

Utasikia, kwanini uwe na wivu bwana? Kwani huna "confidence" mbele ya wanawake/wanaume wengine?....kakuchagua wewe, relax!

Kwamba wewe uwe huna habari hata kama mwenza achelewe, ashikane na kucheka na watu wengine, akae mahali kazunguukwa na marafiki zako/zake Watanashati/Waarembo....kwavile tu unamuamini kuwa hawezi kufanya kitu "stupid" na wewe unajiamini.

Wanasahau kuwa mara zote watu huwa hawaterezi na watu wageni au kutoka mbali....hao hao kwenye mzunguuko wenu ndio rahisi kushawishika au kushawishi mwenza wako.

Pia wanasahau (au hawajui) kuwa Wivu ni hisia kama zilivyo hisia za mapenzi na kwamba zinategemeana/shirikiana....Bila mapenzi hakuna Wivu na bila Wivu hakuna mapenzi.

Mtu haitaji kwenda mbali kutereza (cheat) na haitaji siku nzima, sekunde chache tu zinatosha kujenga mazoea alafu tabia na baadae uhusiano wa nje ya ndoa/uhusiano wenu.

Yeye kutokuwa au kuonyesha wivu ni dalili kuwa mapenzi yake kwako yanaanza kubadilika na kuwa "heshima" bila yeye kujua.

Anaweza kusema anakupenda sana lakini kama ghafla tu haonyeshi hisia alizokuwa nazo awali ni wazi kuna kitu kinaendelea.


Labda na wee ume-relax, huonyeshi mapenzi kwake hivyo inampunguzia nguvu na kujihisi ni yeye tu ndio anaependa.

Inasemekana mwanaume akifikia umri wa miaka 40+ huanza kujihisi kama vile alivyokuwa na miaka 25. Anahitaji kuhakikishiwa na kuonyeshwa kuwa anapendwa, anahitaji attention n.k.

Wanawake huwa tunadhani kuwa wanaume hawahitaji hizo mambo, ukweli ni kuwa wanahitaji ila approach yao ni tofauti na sisi wanawake.


Isije kuwa Shoga yako ndio anatoa attention, anamsifia, anamhakikishia kuwa bado "wamo"....

Hebu anza kufanya uchunguzi wa karibu kuhusu uhusiano wa Mumeo na huyo rafiki yako ili ujue kinachoendelea. Hilo moja.

Pili, mapenzi ni ya wawili na yana Nguzo zake. Nguzo muhimu zinazokosekana kwenu (kwa mujibu wa maelezo yako) ni Mawasiliano na Ushirikiano.

Zungumzeni kama wapenzi na kila mmoja wenu aweke wazi hisia na hofu zake ili iwe rahisi kwenu wote kujirekebisha na kuongeza ishirikiano ili kusonga mbele mkifurahia ndoa yenu.

Tatu, Punguza ukaribu na huyo rafiki yako mwenye mazoea na mume na kamwe asiguse tena nyumbani kwenu.

Nne, Ongeza effort kwenye kuonyesha mapenzi, kujali na kumhakikishia mumeo kuwa unampenda.


Kila la kheri!

Mapendo tele kwako...

Wednesday

Mume wangu ataka Ex awe mke wa Pili kwavile alizaa nae!

Dada Dinah pole kwa kazi ngumu ya kuelimisha na kutatua matatizo ya kijamii kwa kiasi kikubwa.

Binafsi nimepitia makala zako karibia zote only last month baada ya kupata link ya web yako nilipokuwa nasearch kitu fulani mtandaoni!

Nami leo nikaona ni vyema nitoe ya moyoni yanayonitatiza kwa muda mrefu na ambayo sijawahi kuomba ushauri kokote wewe ndio wa kwanza.

Mimi ni binti wa miaka 26, nimeolewa miaka 4 iliyopita ila bado sijabahatika kupata mtoto kutokana na mipangilio ya Mungu na ya kimaisha.

Wakati naanza uhusiano na huyu mume wangu alinieleza kuwa ana watoto 2 kwa mama tofauti ila alishaachana nao wakiwa kwenye mazingira ya uchumba na those pregnancies were a mistake he regrates!

Na kwamba kutokana na hilo hatafuti tena girlfriend bali mke wa kuoa, na alinieleza mazingira yaliyopekekea kuachana nao na nikaridhika.

Ex wake wa kwanza alishaolewa ila huyo wa pili bado yupo single to date. Hao ma-ex siwafahamu zaidi ya kuwaona kwenye picha.

Wa kwanza yeye alikata mawasiliano kabisa ila huyu wa pili huwa wanawasiliana kwa ajili ya mtoto. Mwanzoni sikuwa na tatizo na hilo, ila baada ya mwaka tangu tuoane akaanza kusafiri kwenda huko kwa Ex ambaye anaishi Nje ya Mkoa kwa madai ya kumtembelea mtoto na ndipo tatizo lilipoanza kutokea.


Kwani baada ya kuwa anawatembelea mara kwa mara akaanza kusema kwamba hajisikii vizuri kutengana na huyo Ex kwani mtoto anakosa matunzo ya baba na mama hivyo anataka nayeye awe mke wa pili ili mtoto akue katika misingi mizuri.

Anadai kwamba mwanaume akishazaa au kutembea na  mwanamke basi huyo ni mke wake.

Mimi nilipinga vikali swala hilo na nikamwambia imani yangu ya kikristo hairuhusu ndoa za wake wengi kwani sote ni wakristo na kama ingekuwa mtu kuzaa na mwanamke ndio mkeo basi wanaume wote wangetakiwa kuwaoa maEx zao.

Naisitoshe kama ndo hivyo iweje unataka kuoa huyu wa pili tu mbona yule wa kwanza humzungumzii!

Nikamwambia ni heri ungeniambia hivyo wakati tuko wachumba mimi ningekupisha tu muendelee lakini sasa siwezi kwani mimi ni mkeo halali wa ndoa ambaye ulioa pasipo kulazimishwa.

Nikamwambia siku zote tulikuwa sawa ila tatizo lako hilo limeanza baada ya kuanza kwenda kumtembelea Ex hivyo kinachokusumbua siyo mapenzi ya dhati bali ni guiltiness unapokuwa mbele ya Ex so ni bora ukate mawasiliano.

Baada ya malumbano ya mda mrefu ambayo alikataa katakata tusishirikishe watu hasa kwa ushauri hatimaye akatulia kwa muda na kusitisha mawasiliano.

Baada ya kipindi kupita akaanza tena yaleyale but this time bila kwenda huko ila anadai anataka tu kujua maendeleo ya mtoto.

Kinachonishangaza ni kuwa huwa hafanyi mazungumzo na huyo ex nikiwepo kitu ambacho si kawaida yake kwa simu nyingine.

Kwakweli tangia matukio hayo yalipoanza sina amani kabisa na mume wangu kwani huwa nahisi kama kulikuwa na kitu kilichoendelaea kati yao wakati alipokuwa akiwatembelea.

Kwakweli kwa sasa sina amani tena na mume wangu kufanya mawasiliano na huyo Ex wake ambaye amezaa naye.


Nina mpenda pia sina shaka na upendo wake kwangu ila ninahisi kuna kitu kina mvuta arudishe mahusiano ya kimapenzi na huyo Ex, kwani nikishaongea nae hunielewa na kutulia then akiongea tu na huyo Ex ndio hayo mambo mengine ya kurudiana nae hutibuka so nashindwa kuelewa kuna nini nyuma ya pazia.

Ninaomba ushauri wako dada yangu nifanyeje ili kuwe na amani kwa wote! Maana hivi sasa akishataja tu jina la huyo mtoto nakosa amani ya roho kabisa na hata siwi tena comfy kuzungumza naye masuala ya watoto maana naona nakumbushia huko! asante.


*************


Dinah anasema: Ahsante kwa ushirikiano. Pole nawe kwa unayokabiliana nayo.


Enzi za Bibi zetu walikuwa wanawachukua watoto na kuishi nao pale inapojulikana mwanaume alizaa kabla ya Ndoa.


Hii ilikuwa inaondoa matatizo kama haya kwenye ndoa na inamfanya Ex asipate "matunzo" kwa kumtumia mtoto.

Hali hii iliwafanya Bibi zetu waonekane kuwa walikuwa na roho nzuri sana kwa vile wanakusanya watoto wa nje wa waume zao na kuishi nao nyumba moja. Nia ilikuwa kumuondoa Ex kwenye maisha yao ya ndoa zao....anyway!

Mumeo hakutaka mshirikishe watu wengine (mostly wazazi na aliewafungisha Ndoa) kwenye tatizo lenu kwa vile anajua wazi anachokifanya sio sahihi.

Maswali mengi yanajitokeza hapa:-

1)-Huyu bwana aliachana na Exes wake walipokuwa wachumba alafu Mimba zote zilikuwa mistake, well ya kwanza tukubali....na ya pili? Hakujifunza tu?


2)-Huyu Ex king'ang'anizi ni wa kwanza au wa Pili?


3)-Alafu kwanini anatunza picha za Ex zake? Umesema huwajui ila umewaona kwenye picha tu! Kuzaa nao sio sababu ya kutunza picha zao.

4)-Mtoto anaumri gani?


5)-Kwanini ulimruhusu aende peke yake kwa Ex?


6)-Kutokuzaa ni uamuzi kutokana na Maisha yenu yalivyo au mmejaribu lakini bado hamjafanikiwa?.....maana isijekuwa anaku-push makusudi ili uzae nae haraka.

Kama walifikia hatua ya Uchumba ni wazi kuwa walikuwa wakipendana tofauti na wale wa "usiku mmoja" baada ya pombe mara boom "nina mimba yako" sort of thing.

Naelewa Jina la mtoto likitajwa kwenye mazungumzo kinachokujia kichwani ni Ex na mumeo kama wapenzi in which inakufanya usitamani hata kulala kitanda kimoja na huyo Mumeo.

Nahisi Ex anatumia mtoto ili kurudiana na Mumeo au mtoto mwenyewe ndio anataka baba na Mama yake wawe pamoja na akamwambia baba yake live, baba akapata hatia.

Hakuna mtoto anaetaka wazazi wake wakae mbali-mbali, na mara nyingi mtoto hudhani "mke" wa baba wa sasa ndio aliesababisha mimi na mama kuachwa.


Sote tumewahi kuwa watoto na hakika hufurahi kuona baba na mama wakiishi pamoja.

Lakini mazingira ya upatikanaji wa baadhi ya watoto inakuwa ngumu kwa mama na baba zao kuishi na kuwalea pamoja kama familia.

Pamoja na kusema hivyo haina maana nakubaliana na uamuzi wa mke wa pili ila ni vema kuwa open kuishi na mtoto (ikiwa atakubali kuja ishi nanyi).


D'oh! Nimeenda kwa mtoto nimekusahau wewe....samahani!

Nini cha kufanya: Weka mumeo chini na mzungumze kwa upole lakini kuwa firm ili yamuingie na ajue wewe sio "ndio" bwana kind of a woman.

Mwambie unatambua umuhimu wake kama baba kwa mtoto na mtoto kwa baba yake na huna tatizo na hilo.

Mueleze kuwa nia yako ambayo ni amani kwa pande zote, Mtoto na ninyi kama wanandoa, Mama mtoto hausiki hapa.

Mkubaliane kama mawasiliano ni kuhusu mtoto basi yawe wazi na wewe kama mke hupaswi kufichwa.


Pia ongeza kuwa Ex asipige simu unless mtoto anamatatizo vinginevyo mumeo ndio apige kum-check mtoto na moja kwa moja aombe kuongea na Mtoto wake, hakuna stori na Ex baada ya salamu na hakuna Text.

Inategemea na umri wa mtoto, mkubaliane kwenda kumuona mtoto kila anapokuwa likizo (kama mdogo), ikiwa mtoto ni mkubwa basi awe anakuja kumtembelea baba yake hapo kwenu.

Ikiwa mtoto anamiaka 10 au zaidi basi Mumeo amnunulie Mtoto simu ambayo atakuwa akiwasiliana na mtoto wake mara kwa mara kabla ya ninyi kwenda kumuona.

Mnapokwenda kumuona hamfikii kwa Ex na wala Ex hapaswi kuambatana nanyi. Anakabidhi mtoto kisha anaishia kwa muda mliokubaliana kumrudisha mtoto.

Ni wewe, Mumeo na Mwanae.....nia na madhumuni hapa ni mtoto kuwa him/herself kwako na kuanza kukuzoea taratibu.

Usikubali kuitwa Mama Mdogo kwa vile Baba yake anataka hivyo, mwambie akuite jina lako. Mtoto akiwa comfy huko baadae mwenyewe ataamua kukuita anti au mama mdogo.

Usiahidi kuwa utampenda kama mwanao (wanaotoa ahadi hii kabla hawajaishi na mtoto huwa waongo) ila ahidi kuwa utam-treat kama mtoto anavyostahili kuwa treated.

Anza na haya, alafu tuone itakuaje.....kama hujanielewa tafadhali usisite kuni-check tena.

Tuone wengine watashauri namna gani.

Kila la kheri!

Mapendo tele kwako...

Monday

Simpendi kihivyo na siwezi kumuacha kutokana na mapenzi yake!

Hello natumai hu mzima na afya tele.

Mie ni msichana nina mpenzi ambaye ananipenda sana yaani yupo tayari kufanya lolote kwa ajili yangu na ninaamini hivyo kwa sababu kasha nifnyia mengi.

Kiufupi ni nilikua natafuta mwanamme anipendaye na nimempata lakini hana sifa za nje ninazo zihitaji.  

Tuna miaka 2 katika mahusiano, nina hisia kwake lakini sio kama anavyonipenda yeye.


Ni mwanamme ambaye anajua kumjali mwanamke ambae kwa sasa sio rahisi kumpata kama yeye.

Natamani niachane nae but siwezi na hata kama nikimwambia hawezi kuniacha japo kashajua kuwa yeye si chaguo langu.


Nifanyeje? nisaidie.

***********

Dinah anasema: Mzima wa afya tele namshukuru Mungu, ahsante kwa ushirikiano.


Natambua unadhani nitakuambia "ng'ang'ania baraka za bwana" kwavile ni vigumu kupata mwanaume anaejali, penda na kufanya kila kitu kwa Mwanamke wake.

Siamini katika kuishi na mtu kwa vile ni vigumu kumpata kama yeye na sipendezwi na watu wanaopotezea wenzao muda na pengine bahati ya kukutana na watakaopendana nao kwa dhati.

Mimi naamini katika mapenzi ya kweli, kwamba kama humpendi anaekupenda ni vema kuachana nae ili umpe nafasi ya kukutana na mtu atakae mpenda.

Hakika huwezi kupendana na mtu kama kwa kiwango kimoja, lazima upande mmoja uwe zaidi....lakini bado kuna mapenzi kati yenu.

Kutokana na maelezo yako umesema una hisia kwake lakini sio kama anavyokupenda wewe, hujasema unampenda ila sio kama akupendavyo.

Huenda hizo hisia zinasababishwa na matendo mazuri na hali ya kukujaali na kukuheshimu kama mwanamke, yaani unapenda mambo anayokufanyia na unapendezwa na hisia unazozipata kutokana na mapenzi yake kwako.

Hakuna mtu anaekubali kuachwa lakini at the end huwa wanakubali kuwa hawatakiwi na hivyo wanaendelea na maisha yao.

Jinsi unavyozidi kumpotezea muda ndivyo unavyomzidishia machungu, sasa tangu unajua anavyojisikia juu yako kwa miaka yote miwili, anza kumuacha taratibu.

Ukimuacha ghafla kwa kumuambia inaweza ikagharimu maisha yako, maana Dunia ya sasa sio ile ya 1990.

Kama hamuishi pamoja, kwa nyakati tofauti punguza mawasiliano ya simu na ya ana kwa ana, badilisha makazi, mwambie badilisha mawasiliano.....


Ikiwa mnaishi pamoja, rudi nyumbani kwa muda alafu utafute chumba/nyumba kisha badilisha mawasiliano, badilisha kazi ama hama na usimwambie mtu yeyote anaemfahamu huyo jamaa yako.


Tafuta sababu ya kumfanya aelewe...well huna sababu ya kumuambia kwani hamjafunga ndoa. Mwambie tu nahitajika nyumbani hivyo nitakuwa huko kwa muda halafu anza kupunguza mawasiliano.

Muache mkaka wa watu ili apate nafasi ya kupenda na kupendwa kwa dhati na wewe upate nafasi ya kumpata atakae TICK mahitaji yako mengi iwe ya kiutu au kimuonekano.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Friday

Nampenda, ila ananifanyia Visa!

Hi dinah!
I am a big fan of your blog napenda ushauri unaotoa kwa sababu unajenga na unaelimisha hiyo ndiyo sababu iliyonifanya nikuandikie ili wewe na wadau wengine wa blog hii wanisaidie

Dinah me ni msichana, and am at my early 20's and niko kwenye mahusiao kwa muda wa miaka mitatu sasa i trully love this guy (i mean i'm so madly in love) at first ilikuwa kama a passing fantancy 2 but this time round imekuwa so serious that i feel like i wanna be his saa yoyote ile(hiswife) lol.

But the problem it's self comes here.. This guy is so ignorance nw days, i might text him but he replies late au hajibu kabisaaa he goes silent for over a week and forth(this is really killing me) what runs kwenye akili yangu ni kwa nini ananifanyia hivi?

Hana hisia na mimi tena? Ana msichana mwingine au what exactly is going on.

Dinah this guy never seezes to amaze me coz when i talk to him kuhusu ku end this relation hataki hata kusikia and yet bado ana nifanyia visa.

Nashindwa cha kuamua hadi dakika hii coz bado nampenda as i said before i am willing to do anything yes! Anything so as to save this relation but nashindwa coz cjui nianzie wap and ukizingatia he's my first guy plz dinah nisaidie..

Thanks in advance dada dinah and wadau!


**********


Dinah anasema: ah! Hii ndio sababu ya mimi kuendelea ku-blog, ahsante sana kwa ushirikiano na Ushabiki kwa Blog yangu.


Upo in your early 20's ambayo ni kati ya 21-24 baada ya hapo ni Middle then late inaanzia 28.

Umekuwa kwenye uhusiano na Jamaa kwa miaka Mitatu, nae pia atakuwa kwenye 20's (I guess).

Sidhani kama uhusiano wenu unahitaji kuokolewa kwani hakuna kitu kinachoashiria kuwa kuna matatizo makubwa...kutokana na umri wenu na urefu wa uhusiano wenu.

Kuna umri fulani (mara nyingi kati ya 24-30) baadhi ya wanaume huamua kuweka mapenzi pembeni na kuwekeza muda mwingi kwenye "kurekebisha" maisha.

Hiyo haina maana kuwa hakupendi/hana hisia nawe (kutokana na maelezo yako) bali hana muda.....inawezekana anatumia muda kukutana na watu anaodhani kuwa watamsaidia kuweka sawa mambo kimaisha/maendeleo.

By the time kafika nyumbani anakuwa hoi, ili usilazimishe kwenda au kukutana nae....anaona ni bora akujibu late au akae kimya which is wrong na hapo ndio Nguzo ya Mawasiliano inapoingia.

Achana na vitisho vya "kama ni hivyo tuachane basi" sort of thing....kama nia yako ni hiyo ni vema kutopetezeana mida.


Siku ukipata muda na kukutana nae ana kwa ana, ongea nae kuhusu mambo yanayokukera kuu ni "kuchuniwa" kwa wiki nzima.

Mwambie Mpenzi najua maisha/masomo yanakupeleka mbio na wakati mwingine unaona mie ni msumbufu....nasumbua kwa vile nakupenda.

Ongeza, huwa napata hofu unapokaa kimya kwa muda mrefu kwani sijui kama ni mzima au unatatizo, naomba tuboreshe mawasiliano yetu.

Mengine ongezea mwenyewe kulingana na unavyomjua mpenzi wako na jinsi alivyo serious na Uhusiano wenu.

Bila shaka nae atajieleza na kuweka wazi kitu kinachomfanya wakati mwingine akae kimya....

Baada ya maongezi hayo, jitahidi kupunguza mawasiliano, yaani usimtumie text wala kumpigia simu kwa siku 3, then msalimie kisha Uchune tena.


Hakikisha unapowasiliana nae unapunguza maswali au ulalamishi....


NYONGEZA: Tatizo kuu la mabinti wengi kwenye 20's ni haraka, too demanding, lazimisha mambo, kutegemea mengi kutoka kwa mwanaume na sio mchango wako (mwanamke) kwenye uhusiano husika .

Tatizo lingine ni kale kaimani ka' "mwanaume wangu wa kwanza" hawezi kunitenda na siku moja atanioa!

Ukitunza Bikira fanya hivyo kwa ajili yako binafsi na sio kwa ajili ya mwanaume au kama mtego wa kuolewa na atakae kuwa wa kwanza kwako.

Kwavile ni mpenzi wako wa kwanza haina maana kuwa ndio atakuwa mumeo.....Ukwanza/Bikira haina maana kwa mwanaume zaidi ya kuongezea kiburi Ego yake.

Pamoja na kusema hivyo, anza kumchunguza nyendo zake ili kujua ukweli (hii ni risk, akikubamba unalo).


Haya, tuone wengine watakushauri vipi.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Thursday

Umbo la Mchumba halinivutii, nivunje Uchumba?

Sorry madam dinah na pole kwa shughuli zote za kuielimisha jamii ya tz
juu ya mahusiano.

Nina mchumba ambaye tumemaliza chuo pamoja na ananipenda sana tena kwa dhati na pia tunatarajia kufunga ndoa Novemba 2014.

Shida niliyonayo kwa mwenza wangu huyu wa kike ni mwembamba sana, nami nikikutana na vibiti namba 8 nachanganyikiwa kabisa.


Je kunahaja ya kubadilisha mwelekeo wakati huyu mpenzi wangu ananipenda sana na teyari kanitambulisha kwa nduguze.

Swali la pili nikiwa naye huyu mpenzi wangu na kuishi naye kama mke umbo lake litabadilika na kuvutia macho yangu?

Maana watu wengine hudai kuwa
mwanamke mwembamba pia flat akiolewa anaweza kuwa na figure nzuri
baadaye hasa akizaa. Samahani nitoe ktk utata huu.

****************


Dinah anasema: Aii Madam tena? Tafadhali niite Dinah inatosha....


Kutokana na maelezo yako inaonyesha kuwa huna mapenzi nae na wala hakuvutii kwa asilimia zote.

Umemchumbia kwa vile kupendwa feels good au kwa vile kakutambulisha kwao hang on!!! Mchumba wako ni mwanamke alafu yeye ndio kakutambulisha kwako?!!

Ni kweli baadhi ya wanawake kama sio wote wakishika mimba huongezeka na wakizaa hurudia maumbile yao ya awali (wakitaka iwe hivyo).

Hiyo sio guarantee ya Mchumba wako "kuota" makalio na kiuno chembamba ili kutengeneza namba Nane ikiwa hana asili hiyo.

Chunguza wanawake upande wake na wa Baba yake, ikiwa kuna waliojaaliwa basi uwezekano ni mkubwa umbo lake linaweza kufanana. Upande wa mama sio mara zote Binti anachukua Umbile (Baba ndio husababisha mbegu za mtoto wa kike).

Ni vema umekuwa muwazi kwangu, ila ingependeza zaidi kama ungekuwa muwazi kwake na kumwambia kuwa unapenda umbile la namba Nane na sio namba Tisa ikiwa anamatiti makubwa na ni bapa kama ulivyosema au namba Moja (mwembamba kote).

Au uvunje uchumba kwa kumueleza kuwa unahisi kuwa haupo tayari kuoa kwani bado unatamaa.


Weka wazi kwamba ukiona mwanamke mwenye umbile la Namba nane unaheuka na kulitamani.


Mwambie mkifunga ndoa unaogopa kuwa utam-cheat (obviously).

Kama huna moyo wa kuvunja moyo wa mwenzio ana kwa ana basi tumia watu waliopeleka Mahari(walioenda kuchumbia) kwao au ndugu zako ama mtu yeyote ambae anafaa kwenda kuvunja Uchumba.

Sio sahihi kufunga ndoa na mtu kwa kigezo cha yeye kukupenda kwa dhati, wakati hakuvutii na wala huna mapenzi ya dhati kwake.


Fanya, haraka kabla muda haujafika na watu kuanza vikao vya Ndoa.


Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Monday

Nashindwa kumtongoza!

Habari yako dinah.

Mimi ni Msomaji mzuri wa Makala zako kwenye blog yako muda mrefu.







Kuna mwanamke nimetokea kumpenda sana ila naomba nijulishe kwa uchache nifanyaje ili niweze kumpata mwanamke ninayempenda baada ya kuchukua namba yake ya simu.







Ili asinione mimi ni muhuni na nisingependa nimpoteze huyu dada. Mimi naamini kutongoza kuna utalaamu wake  na ndio hapo panaponishinda mimi....ahsante.



****************





Dinah anasema: Habari ni njema kabisa, shukurani kwa Ushirikiano. Mail yako imenifanya nicheke kwanza, maana mie sijui mbinu za kutongoza mwanamke kwani mimi ni mwanamke.







Hata hivyo, kuwa na namba yake ya Simu ni mwanzo mzuri, itumie hiyo namba kumsalimia/julia hali asubuhi na jioni (kabla ya muda wa kulala).







Kitendo cha yeye kuamka/kulala na kusoma ujumbe wako au kusikia sauti yako kitaanza kumfanya ajihisi kuwa unamjali.







Inabidi ufanye uchunguzi ili ujue mida yake ili uwe wa kwanza kumjulia hali anapoamka na wa mwisho kusikiwa kabla hajalala.







Hii itasaidia wewe kubaki kichwani mwake akijiuliza maswali, kama yupo interested na wewe hatokukatisha tamaa, ila kama hana interes ni wazi utakuwa msumbufu hehehehe usikate tamaa though.







Akianza kuonyesha interest ongeza mawasiliano ya kumjulia hali na maongezi yawe marefu zaidi kiasi.







Maongezi yasihusu Ngono lakini yanaweza kuhusu upendo, maisha, kazi, familia, watu, celebs hobbies n.k (inategemea na yeye/wewe).







Muhimu ni kuhoji anapendelea nini ili ujue namna ya kuanzisha maongezi, then omba makutano siku ya kawaida na muda wa kawaida sio Mwisho wa Wiki na isiwe Usiku.







Tengeneza Msingi wa urafiki na kuaminiwa kabla hujaanza kumwambia unampenda n.k.







Ukifanikiwa, omba kutoka nae (a date) weekend kwa ajili ya Chakula au kinywaji, Sinema, Muziki...







Mpaka hapo atakuwa kajua kuwa unamtaka/penda na wewe utajua....!



Ikitokea vinginevyo basi kumbuka Penzi halilazimishwi.





Tuone wanaume wenzio watakusaidia zaidi.....



Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

Pages