Wednesday

Kitu cha Mviringo ndani ya K!

Mimi bado ni mchanga kwenye mambo ya sex kwasababu nina mda mfupi tangu nimeanza ngono.







Naishi mbali na boyfriend wangu na tunaonana baada ya muda mrefu ila kila tukikutana kwa sex napata maumivu mwanzo wa uke.







Pia nikiwa najisafisha ndani ya Uke nahisi kama uvimbe kwa juu (wa mviringo) sijui kama ni kitu cha kawaida ama vipi na kuna siku boyfriend wangu alinambia wakati yuko ndani ya uke alihisi kama kitu kinamsukuma na hata mie nilihisi hiyo hali pia na nilihisi maumivu kidogo.







Naomba kama unaweza nisaidia kwa haya please.





***********



Dinah anasema: Hello there!



Kupata maumivu mwanzo wa uke nadhani kunatokana na kukaa muda mrefu bila kufanya ngono mie huwa naita "second time virginity".....sio Bikira ila maumivu yake yanakaribiana kwa mbali.







Kutokana na uzoefu "kuna kitu kama kinamsukuma mwanaume" ni Cervix au shingo ya Uzazi/Mlango wa uzazi.







Kila mwanamke anayo hii sehemu ila ni wachache ambao wanaweza kuifikia kutokana na ukaribu wake au umbali wake(inategemea kina cha Uke).







Unajua ukifungua mdomo na kuangalia kwa ndani kule mwisho wa ulimi unaona kama "kidole" hivi eeh, basi na shingo ya Uzazi ipo hivyo.







Hii Shingo ya Uzazi hufunguka na kufunga, inategemeana na mzunguuko wa Hedhi na hali ya kuwa tayari kushika mimba.







Hiyo sehemu ikiguswa hutoa maumivu yenye mchanganyiko na utamu....utamu unatokana na kuta za kuke na ule wa mwanzo wa Uke.....(Inabidi uwe na uzoefu kwanza).







Lakini usichukue maelezo yangu haya ya kisha ukatulia kwani mie sijahisi unachohisi, nimeelezea kutokana na uzoefu.





Hivyo ni vema ukaenda kumuona Daktari ili akuangalie na kukupa all clear!





Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

No comments:

Pages