Wednesday

Pesa anazo lakini hanihusishi-Ushauri

"Mimi ni mwanamke wa 25 nimeolewa miaka 3 iliyopita kwasasa ni mjamzito hivyo niliacha kwenda kazini tangu mimba hii ilipoingia kutokana na matatito ya kiafya. Mume wangu ana nafasi nzuri kazini na kipato chake kinakidhi mahitaji ya familia yetu.


Baada ya matumizi muhimu kwa kawaida najua anabakisha kama laki 5 kila mwezi lakini hakuwahi kunijulisha kama ana pesa hizo au ana plan gani na mabaki hayo ya pesa, nikimuuliza anasema hana pesa.


Wakati huo mimi kuwa baada ya mahitaji muhimu najua pesa fulani hubaki na sasa amefikisha million 5 lakini hataki kusema ukweli, Pesa hizo zipo kwenye account nami najua password yake lakini yeye hatambui hilo.
Je mtu wa design hii nimchukulie kama alivyo au nimweleze ukweli"


Jawabu: Asante kwa ushirikiano wako, inaonyesha wewe ni mmoja kati ya wanawake wachache ambae ulikuwa ukijituma ili kuchangia kipato ndani ya nyumba na ninachokiona hapa ni ile hali ya "kujishitukia" kwa vile hufanyi kazi unafikiri mume wako atakunyanyasa na bila kujijua unaamua kuomba pesa ambazo pengine wala huzihitaji....kama ulivyosema mwenyewe kuwa anakamilisha mahitaji yote muhimu.


Kitu kingine ninachokionahapa ni kuwa na hofu kuwa anaweza kuwa anazitumia pesa zinazobaki kwa ajili ya mambo mengine kama vile "kuwekeza" kwenye Ulevi na wanawake nje ya ndoa yane kwa vile tu wewe ni mjamzito (kutokana na matatizo ya kiafya ni wazi kuwa tendo la ndoa halipo vile inavyotakiwa kitu ambacho kinaongeza hofu).


Lakini kutokana na maelezo yako ni wazi kuwa pesa zote zinazobaki baada ya mahitaji muhimu anazitunza Benk, hazitumii kivingine. Kumbuka wewe ni mjamzito which means kuna "mtu" mwingine ataongezeka kwenye familia yenu ndogo na badala ya kuwa wawili mtakuwa watatu nahivyo basi majukumu yataongezeka na kwa mshahara wa mtu mmoja tu mtoto hatokuwa na maisha bore.


Sasa ili mtoto kuwa na maisha bora au angalau "comfortable" ni wazi kuwa kuna ulazima wa ninyi kama wazazi kujiandaa na jukumu hilo jipya. Si hivyo tu bali kuna matukio ambayo hujitokeza bila mipango kama sehemu ya maisha yetu yanaitwa "udhuru" ni wazi kwa akiba inahitajika incase kitu kama hicho kinaibuka.


Sote tunapokuwa na mipango fulani na pesa tunazotunza ili kukamilisha jambo fulani alafu mtu akaibuka na kukuomba seti au kukuazima ni wazi kuwa utamwambia kuwa huna pesa....sio huna kabisaaa bali ulizonazo zinamipango yake muhimu na hutaki kuzigusa unless upate "udhuru" kama kuuguliwa, msiba n.k.


Umchukuliaje?-Since unalo neno/namba ya siri ya Benki Akaunti basi mchukulie kuwa ni mmoja kati ya mwanaume wachache wanaojua majukumu yao, anangalia mbele na sio pale mlipo (kuvaa miwani ya mbao) pia ni muaminifu na ndio maana akakupa neno/namba ya siri ya account (natumai hukuitafuta mwenyewe balia likupa baada ya kuomba).....vinginevyo mume wako anajaribu kufanya mambo yake kama mwanaume na wewe unapaswa kumuamini.


Nini cha kufanya-Hakuna ukweli wa kumuambia hapo kwasababu moja, Pesa ni zake, Pili hazitumii bali ziko pale zimetulia, tatu wewe unataka pesa za nini wakati kila kitu unatimiziwa ndani ya nyumba?


Kama unawasiwasi sana na wewe ni mwanamke kamilifu na mke hivi sasa ni lazima ulifunzwa namna ya kupata unachotaka kutoka kwa mume wako kwa kutumia lugha ya kimapenzi (siwezi kusema hapa kwani kaka zangu wakijua hatutopata kitu), sasa tumia mbinu hiyo kwa mume wako na hakika atakueleza mipango yake kuhusu pesa hizo (akiba) na hapo utapata amani moyoni mwako.

Acha kujishitukia kwa vile umeacha kazi, jiamini hali itakayokusaidia kumuamini mume wako.
Kila la kheri.

Tuesday

Ushuhuda wa Mama Johnson wa Mza!

Hi My Dear Dinah.
Its me again Mama Johnson From Mza.

How is Valentine 2 all Tanzanian?
Napenda kuwashukuru watanzaia na Non-tanzanian wote ambao mmenishauri hapo chini. Mimi ni Ma Johnson ambae nilituma mada yangu kwa da Dinah ikisomeka NAHISI MUME WANGU ANAJISAHAU. Especcialy my special thankfull to you Dear Dinah.

Let me tell u maana ilikuwa as a story what happened to me.
Baada ya kuwasilisha mada yangu hapa mezani sikuwa na jinsi ilinibidi ningoje matokeo kwa kujua kuwa ntapata challenges lakini na jibu litapatikana.


Nilivumilia na nikasitisha mawasiliano. Sikuwasiliana nae kwa njia yoyote ile. I was do as he do to me. Akinitumia sms nikawa simjibu. Akinipigia napokea namjibu in short kama niko kazini namwambia niko bussy kidogo ngoja ntakupigia. Na kama ni mida ya jioni namwambia ngoja ntakupigia mtoto ananisumbua mwisho wa yote sipigi wala sijibu sms zake.


Wakati huo nilikuwa nafatilia mawazo ya wanablog wenzanu ya kuwa nimfate dar bila taarifa yoyote wakati huo ndo tulikuwa tunaelekea kwenye Valentine Day. Nilifatilia maombi ya ruhusa ofisini angalau kwa siku tano ili nije dar boss wangu hakuniruhusu kwa sababu Mi ni Accounts Administrator na huwa tunafunga hesabu za mwezi tar ambazo nilikuwa nimeomba. So it was difficult to move.


Basi Mpaka ikafika tar 14 no call from me to him and no call from him to me. Roho iliniuma sana ukizingatia mi ndo nilianza kuuchuna. Siku hiyo ya tar 14 nikatoka kazini mchana as u know it was week-end. Nilipitiliza hadi home nikaandaa chakula mapema nikaoga na kujipumzisha.
Ikafika saa mbili yausiku sm yangu ikaita. Kupokea ni yeye akaniuliza uko wapi nikamwambia niko hm akaniambia toka unifungulie geti. It was supries. I felt like iwant to fall down.


Nikatoka nikamfungulia. Akaniambia samahani sana nimekuja bila taarifa. nikamwambia no worries its your home and am your married wife. Akasema nimeitahidi sana nije maana siku hiyo yaani tar 14 mwezi huu wa pili ndo tulifunga ndoa AICT na tulikuwa tunatimiza miaka 5 ya ndoa mwezi huu.


Baada ya yote akanilaumu nimebadilika nimekuwa mjeuri akinipigia sizunumzi nae akinitumia sms simjibu. Na mi nikamwambia na mi nilikuwa naumia hivyo wakati ule najitahidi kuwa karibu nae ye anakuwa mbali. Akanisihi nisifanye hivyo maana yuko mbali nipunguze mawazo he loves me sour much, hayuko radhi kunisaliti ila ni majukumu tena ya mda mchache tu.


Alikaa tarehe 16 alfajiri akaondoka. Sikumwamini hata kidogo nilijua ananipaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Yaani da Dinah ye aliondoka kwa flight ya saa mbili pass through Nairobi. Mi nikaondoka na Flight ya saa sita mchana.


Nilichukua chumba jirani na hotel anayoishi na kwa mda mfupi nikagundua kuwa chakula hula pale kila siku jioni. nilijenga mazoea na yule dada muudumu nikampatia cash kidogo. Akawa karibu na mimi mno. So kila nilichomdadisi alinipa ushirikiano wa kutosha bila chochote.


Pale pale kwa maelezo ya yule dada nikajua no one alse ila baadae niligundua yule dada alijua habari za pale wa kuwa house boy wa mr wangu ni jamaa bf wake. Nikamuuliza kwani huyo kaka yupo akasema alikwenda mza kuiona familia yake amerudi leo amefika tu nakuondoka ameenda kazini. Ilipofika saa mbili ya usiku alikuja pale hotelini akapata dinner akaenda nyumbani kulala. Saa tano ya usiku nikamtuma yule dada aniitie yule bf wake alishagaa sana nikamwambia aende.


Alipomwita nilimuuliza unanifahamu mimi akasema nahisi nilikuona seemu ila sikumbuki ni wapi. Nikamwambia kumbuka vizuri hapo hapo nikamwuliza na uyo mtoto je? Akamtazama kwa makini akasema huyu mtoto anafanana na bossi wangu theni akasema nimekutambua ni wewe ndopicha zako na mtoto zimetapakaa mle ndani. nikamuulizabosi wako yupo akasema yuko anaangalia tv.


Nikamwambia beba huyo mtoto twende hakuna kumshitua. Akaniongoza hadi ndani Da dinah, hakuwa na taarifa kama tuko pale lakini nilimkuta ameshika picha yangu niliopiga sku ya wapendanao akiitazama kwa hisia wakati huo alikuwa ametoka kunipigia sm nikamwambia niko home najiandaa kulala.


Alipata mshituko usiosemekana. Na mi nilipofika nilidhibiti sm yake vilivyo sikuona sms ambayo itanipa hofu ya kusalitiwa. & now i have find out the true. Kwa mda wa siku mbili nilikuwa pale kweli da dinna Mr wangu yuko bussy mpaka nilimwonea huruma. Napenda kuwashauri wanawake wenzangu tusiwalaumu wala kuwalaumu wapenzi wetu.

Tuwapende tuwe karibu nao, Na watuambiapo jambo lolote tusiwablame inatakiwa uvumilivu na maelewano.Thanks all for your information. And many thankis to You Dinah.
Samahani nimeandika marefu kama gazeti.

Regards.
Mama Johnson.
Mza.

Friday

Viagra!


Mambo vipi wewe!

Kwenye Topic ya 12 Feb 2009.
Naona watu wanashauriana vitu ambavyo inaonyesha kuwa vinafanywa na wengi kwenye mahisano ya kimapenzi bilakujua kwanini hasa Viagra ipo na inafanya kazi gani? Kama ilivyo kwenye matumizi ya karanga na korosho....wengi wanadhani inaongeza nyege lakini ktk hali halisi "nuts" zinaongeza uzalishaji mzuri na wenye afya wa Shahawa/Manii na sio nyege.



Kuna msemaji mmoja katoa actually "somo" (hehehehe nimecheka mpaka nimeanguka alafu ndio nikaanza kusikitika) kuwa unaisaga Viagra kisha unaichanganya na Juice na kumpa mumeo....sasa huoni kuwa huko ni kumbaka? Unamlisha dawa ya kusimamisha uume bila yeye kuandaa mwili na akili yake tayari kwa tendo hilo takatifu?



Come on wanadada, kama yeye akifanya hivyo wakati wewe huna hamu ya ngono kwa vile uwezo wako mdogo utajisikiaje? Hakika utaenda kumshitaki kuwa kakubaka kwa wakuu wa mtaa.



Itambulike kuwa Viagra haimpi mwanaume nyege bali inasababisha mapigo ya moyo kwenda kasi na hivyo kusukuma damu kwenye mishipa ya uume wake na kusababisha uume kusimama. Nyege inategemea zaidi akili/Saikolojia na kuachiwa kwa "homono" (wacha nitafute jina lake kwa kiswahili hapa) na sio mapigo ya moyo na msukumo wa damu.



Mwanaume kama anauwezo mdogo wa kungonoka hata ufanye nini hawezi kuwa na nyege unless zije zenywe pale mwili wake unapokuwa tayari....japo kuwa kuna dawa za kumfaya anyegeke lakini haiwi kama vile kunyegeka kiasilia.



Vilevile kutokuwa au kupungukiwa na nguvu za kiume kwamba mwanaume hawezi kusimamisha lakini anakuwa na nyege kama kawaida ila Mboo haidisi (hawa ndio wanahitaji Viagra) ni tofauti na mwanaume mwenye uwezo mdogo wa kungonoka a.k.a low sex drive.

Ukweli sasa.
Inasemekana kuwa Viagra ilibuniwa au tengenezwa maalumu kabisa kama dawa ya kutibu Ugonjwa wa moyo, sasa kusimamisha uume ilikuwa moja ya "side effect" ya dawa hiyo (kabla hawajaibadilisha jina na matumizi yake).


Sasa mwanaume yeyote mwenye tatizo la kusimamisha a.k.a ED iwe haisimami kabisa ua ule ugumu wake unakuw ahautoshi kuingia ukeni ndio huwa wanashauri wa Daktari husika kutumia "buluu" na hiyo hufanyika mara baada ya kuangaliwa afya yake nahivyo kupimiwa kiwango gani atumie.


Wanaume walio wahi kuzitumia au wale wanaozitumia wanaweza kueleza kwa kirefu zaidi.

Jaribu kufahamu mwili wa mumeo wako na namna gani unafanya kazi badala ya kuchanganya mambo kwa mfano wengi wanafikiri kusimamisha ndio nyege na nyege ndio kusimamisha.


Ili mwanaume asimamishe ofcoz anahitaji kusisimuliwa ili kunyegeka, mnyegeko ukitokea ndio anasimamisha....lakini kama anatatizo ED basi atasisimka (nyege kibao) lakini misuli ya uume itagoma kusimama na hapo ndio atahitaji msaada wa Daktari na hatimae kupatiwa kidonge buluu.


Tafadhali ongezea kutokana na uzoefu wako.

Ty.

Wednesday

M3 anaomba tufichue yale yanayoweza kuharibu ndoa!

"Moja ya dhumuni la kuanzisha blog hii (dada Dinah,kama nimekosea unisahihishe), ni kujaribu kufichua yale yanaharibu mahusiano na kuboresha yale yalipo, kwa kuyaweka wazi kwa kila mmoja, ili kama wewe hukuwa nalo utajifunza au utaliacha ili uende sambamba na mwenzako.


Kwahili la kutokujaliana, ni vyema sisi kama wanaume au wewe kama mwanamke ukasema nini hasa kinachokufanya usifanye hivi au ukafanya vile, kwani kusema ukweli huo, ndiko kunakoweza kutusaidia.


Mimi ningependa kufichua yale ambayo wanaume tunayo, na kawanini tunafanya hivyo. Kwa upande huo wa kutokuwasiliana, ipo dhana tumejijengea kuwa si vyema kumzoesha mkeo kila kitu, kwamba mimi nafanya hivi au nataka kufanya vile kwa mfano kukupigia simu mara kwa mara inaleta mazoea ambayo ukikosa kupigiwa utaleta dhana potofu, hii ni moja ya sababu.


Lakini ipo sababu kubwa ambayo hata nyie wanawake mnayo, ni ile ya kujisahau. Kwamba sinimeshaoa, sinimesha-olewa, kuna sababu gani ya kuhangaika mara simu mara nifanye hiki na kadhalika.


Wengi wanasema eti mkishaoana, mnazoeana kama dada na kaka. Wewe dada ni dada na mke au mume ni hivyo hivyo, havina mbadala. Jiulize kama ni dada yako unaweza ukaoga nae? Kwahiyo kila siku inapokwenda hakikisha unajiweka kama vile `unatafuta’.


Kila siku inapokwenda hakikisha hufanyi makosa ya kumfanya mwenzako ahamanike ni `vipita njia’ kwani jamani kila kukicha vinazaliwa vyombo…. Kwahiyo hasa kwa hawa wanaosafiri hukutana ni vishawishi hivyo ambavyo vinawaweka njia panda.


Jingine la muhimi ni mawasiliano. Hili ni tatizo, sugu,sisemi mawasiliano ya simu,nasema mawasiliana kama mke na mume. Sisi wanaume mara nyingi hatupendi kujadilia, hasa katika maswala ya ndani, ya kimahusiano, tunataka kufanya.


Mnapokuwa ndani mjaribi kujadili, kuelezena na kupeana ushauri kuhusu hili au lile. Nashangaa wengine wanasema maswala ya mapenzi hayahitajiki majadiliano mkiwa mumeshaoana,kwanii mnatafute nini zaidi! Inabidi tujadili, tuelekezaneni ka kuwekana sawa.

Unaacha bwana au bibi keshasafiri unaanza kulalamika huku nyuma. Pale mkiwa uso kwa uso ndipo pa kujadili. Mhh, yapo mengi ngoja niwaachie wenzangu, wenye nia ya kufichua uzaifu huu, ili tujenge mahusiano mema.
emu-three"

Nafichua, machache ya wanawake ambayo yanaweza kuharibu ndoa;
(1)-Kufunga ndoa bila kuwa tayari (kufuata mkumbo, kuamini ni baraka, kufuata pesa).

(2)-Wanawake tukipenda na kupendwa huwa na tabia ya kujisahau pale tunapojuwa tumeolewa, u dont put an effort anymore kwa kuamini kuwa amekuoa so hawezi kwenda popote.

(3)-Kutokujua tofauti kati ya Mpenzi na uhusiano......wengi hutegemea "hisia" kuboresha penzi hawajui kuwa unatakiwa kufanya kazi ya ziada kuwa na uhusiano udumu.

(4)-Kukimbilia kuzaa (kwa imani kuwa ni kukoleza mapenzi) bila kuwa tayari/kujua utajigawa vipi kati ya mapenzi, uhusiano na majukumu kama mama.

(5)-Kumtegemea mwanaume kwa kila kitu yaani kumfanya "ajira".

(6)-Kujiachia kwa maana ya kutojipenda tena na una"tilia" vivazi vizuri ikiwa tu unakwenda kwenye sherehe au unakoga na kujifukiza manukato siku ukiwa unataka tendo.

(7)-Kuchukulia Ngono kama wajibu.......uvivu wa kujifunza kupenda tendo hilo takatifu.

(8)-Kuamini ktk msaidizi (houseBoy/Girl)......kumpikia mwanaume ni alama ya upendo (kule nitokako mimi) hivyo Vigoli huwa hatupikii wanaume ovyo-ovyo unless njemba kama imekuja kuchumbia.

(9)-Heshima ya uoga....huna mpango wa kumheshimu mume wako lakini unamuogopa au unaogopa kuachwa.

(10)-Kutokuwa na tabia ya kum-challenge mumeo, kila asemacho wewe ni "ndio bwana"...challenge him, onyesha kuwa u r smart woman!

(11)-Kutokumpa mume wako muda wa kutosha....unakuwa busy na marafiki/shoga au familia yako kila wiki.

(12)-Kujihusisha sana kwenye familia yake hasa kama kuna migogoro kati ya ndugu na ndugu. Unatakiwa kuwa upande wa mume wako lakini jua ur limit, kamwe usiponde ndugu zake hata kama yeye anawaponda.

(13)-Ile kaingia tu unamuwahi na nini kilitokea b4 hata hajanywa chai/kaa chini nakutuliza akili...hujui siku yake ilivyokuwa mama, ongea nae lugha ya mapenzi kumlainisha, mkande ili awe relax kabla hujamshitaki mwanao kuwa aligoma kwenda shule au kafeli jaribio la hisabati.

Yapo mengi ila kwa sasa wacha nitunze ndoa yangu.
Midas.

Sunday

Nilitoka na mume wake,nimesaidia wamerudiana lakini....

"Hey Dinah, natumai kuwa wewe ni mzima kabisa. Mie nina changamoto ambayo naamini kabisa wanablog wenzangu wanaweza kunisaidia kwa ushauri.

Nina BF ambaye nimekuwa naye kwa miaka mitatu sasa, kwa vigezo nilivyonavyo ni kwamba nampenda sasa kabla sijakutana naye sikuwahi kufikiri wala kutamani kuolewa. Isipokuwa niliwahi kuwa na BF ambaye tulikuwa marafiki wa kawaida kwa muda mrefu kabla ya kuamua kungonoana then we parted ways.

Mapenzi yetu yalikolea na kuwa matamu zaidi automatically tukajikuta tunakaa pamoja. Kwa kweli sikuwahi kusikia raha ya kuwepo dunia kama wakati huo. Lakini wakati sisi tukiendelea kufaidi maisha kwa kiwango hicho BF wangu alikuwa ametengana na mke wake kwa mifarakano ambayo wenyewe wanaijua na kwa muda mrefu wamekuwa wakikaa mikoa tofauti mpaka sasa.


Nadhani mke wake alikuwa akitufuatilia na kujua kuwa tupo pamoja. Asili ya kazi zangu ni safari, hivyo katika safari zangu nilikwenda Mkoa ambao mkewe anaishi. Nikakutana naye akanifanyia bifu baadae tukapata audience akaniuliza kama nipo na mumewe mie nikatoa nje kwani niliogopa mkono maana nilimwona mshari kama nini.


Kwa bahati mbaya au nzuri nikaenda tena katika Mkoa ule tukaonana akanihadithia mambo mengi kuhusu mume wake ambaye mimi ni BF wangu. Alinieleza walianzia mbali katika maisha na kwamba sasa wamefika pazuri mume wake ndio anamfanyia hivyo.


Nilimwuliza kama mumewe anatunza watoto wao 2 akasema ndiyo lakini anataka arudi kwake kwani anampenda sana. Nilimwonea huruma na ikanigusa sana kwa sababu mimi ndiye ninayesababisha hivyo.


Niliporudi home nilimketisha BF nikamwambia situation na kwamba uamuzi wangu ni kwamba kwa kuwa sina mpango wa kuolewa basi we could be together while she is with his wife and everything will be ok.


To my surprise alikataa katakata kwamba yeye hamtaki na wala hana mpango wa kumrudia. Mimi nilihisi kwamba inawezekana anahisi namtega but I was very sincere. Siku zikapita na mimi huruma ikaendelea kunishika lakini mume wa mtu nampenda.


Tukawa tunapanga mikakati mingi na mke wake ili nimsaidie mumewe arudi kwake kumbuka kwamba nimekataa katakata kwamba mimi sipo na mume wake. Kwa bahati mbaya sana alikuja mkoa tunaoishi kwa majukumu ya kifamilia (msiba).


Kama baba wa watoto iliwajibika kumfariji na nadhani hapo ndipo walipo ombana radhi na kusameheana , wakaanza upya. Mimi pia nipo pembeni nafurahia mafanikio yao. Mke wake akaendelea kunisisitiza nimsaidie ampate mwanamke aliyemkamata mume wake. Kwa mara ya kwanza niliona kuwa ananitega lakini moyoni nikasema mtego huo hauwezi kunikamata.


Naomba nikufahamishe kwamba aliponiuliza mara ya kwanza nilikataa kushirikiana na mumewe lakini nilikiri kumfahamu na kwamba huwa tunawasiliana isipokuwa ni nyanja za kazi tu. Nilipoona anazidi kusisitiza nimsaidie nikamua kufikia maamuzi magumu sana ya kumwacha mpenzi wangu huyo.


Ilikuwa ngumu sana kwani nampenda sana huyu mwanaume. Nilijaribu kumwambia kwa lugha ya taratibu na upole sana lakini hakuwa tayari kabisa. Nilimwambia nafanya hivyo kwa ajili yake na mke wake. Bado akakataa.


Nilimtoa nyumbani kwa nguvu na kwa ugomvi mkubwa sana. Ilikuwa vibaya kwa sababu tulikuwa tukiishi nyumbani kwangu. Aliona kama nimemnyanyapaa. Baadaye alifanikiwa kuondoka na kurudi kwake. Hata hivyo alikuwa anakuja nyumbani kwangu mara nyingi tu.


Baada ya muda mrefu wa mawasiliano ya mbali hivyo akaanza kukata mawasiliano kwa muda mrefu kama wiki mbili tatu hivi simsikii. Akiibuka anasema atakuja nyumbani anataka kungonoka. Tukingonoka anapotoea tena kwa muda wa mwezi or so na akirudi anataka kungonoka.


Hiyo tabia ikanichosha nikaamua kumwambia kwamba ilipofika panatosha kwa sababu naona kama ananifanyia mzaha na kutaka kuniumiza roho. Yeye akasema kwamba nilimuumiza sana kwa kumfukuza nyumbani kwangu na kwamba jeraha nililosababisha litachukua muda kupona.

Mimi nimechoshwa na hiyo tabia na kila ninapojaribu kumwacha nashindwa kwani akitokea nasahau kwamba nilitaka kumwacha tunaendekeza libeneke.

Wanawake wenzangu nisaidieni lakini pia wanaume naomba ushauri kwani tabia zenu zinafanana.
Kim from Atown"

Jawabu:Hi Kim, hapa kila kitu kiko sawia kabisa. Kwanza napenda kukupa pongezi kwa kutokuwa mbinafsi na kumsaidia mwanamke mwenzio kurudiana na mume wake. Hongera sana kwa hilo.


Ni kawaida kwa wake na waume ktk umri fulani kutojiona au kufikiria kama sio kutamani kuolewa au hata kuzaa (muda ukifika utalifikiria hilo na kutenda kama ifuatavyo), natambua uamuzi wako wa "kutojikita" kwenye ndoa ulikufanya uone kawaida kutoka na mwanaume yeyote utakae mpenda bila kujali kaoa na familia au la, nafahamu uamuzi wako ulikupa hali ya kujiamini sana kama mwanamke kitu ambacho ni kizuri...i mean kujiamini.


Lakini katika hali halisi no matter how unajiamini na kujitegemea usithubutu kutoka na mume wa mtu kwa kudhania kuwa hutoruhusu akuoe au kumuacha mkewe kwa ajili yako......kwani kwa kufanya hivyo sio tu utakuwa unaumiza mwanamke mwenzio bali pia utakuwa unaharibu mpangilio mzima wa maisha ya mtoto au watoto waliozaliwa kwenye ndoa hiyo na vilevile kufanya watu ktk jamii kutothamini ndoa(kitendo chako kinatoa ujumbe kuwa huthamini ndoa za watu).


Kutokana na sehemu ya maelezo yako inaelekea huyu bwana pamoja na matatizo mengine ya kindoa kama vile kuzozana mara kwa mara kitu kinachoweza kusababisha asipate ngono na mapenzi ya kutosha kutoka kwa mkewe.


Huyu bwana sio tu alikuwa akihitaji hifadhi kutoka kwako ili apumzike kiakili (kutokana na matatizo ya kindoa) bali na ngono pia. Unajua, linapokuja suala la ngono, akili kutulia na kuwa "comfy", hakuna maswali ya kipuuzi-puuzi, lawama za kizembe na malalamiko ya ajabu-ajabu kama sio kusingiziwa, mwanaume wanaweza kuhamia na kusahau familia yake kama unavyo "blink" vifuniko vya macho yako......bila shaka umeshuhudia hilo na unauzoefu mzuri tu.


Kuachana na mtu unaempenda ni ngumu sana na ndio maana huwa nawashauri "wateja wangu" kama kweli wanania ya kufanya hivyo lakini upande wa pili bado unasumbua kama huyo Ex bf wako ni kukata mawasiliano kwa kubadilisha nambari za simu na anuani ya makazi. Vinginevyo kila mkionana utahisi kutaka kuwa karibu nae na kufanya chochote na hivyo uhusiano wenu utakuwa ule wa on and off kwa vile wewe bado unampenda na yeye bado anapata ngono tamu na ya bure kutoka kwako.


Lakini kwa vile mkewe anamtafuta "mwizi wake" ambae ndio wewe lakini yeye hajui kuwa wewe uliyesababisha mumewe arudi nyumbani ndio "adui" ni vema kuachana kabisa na huyo bwana kwani huwezi kujua huyo Mdada anataka kumfanya nini huyo aliyemlia mumewe.....well huenda anataka tu kujua nini ulikuwa ukimfanyia mumewe ili na yeye afanye (fanya utafiti ujue anataka nini hasa kutoka kwa mwizi wake kwanza hehehehe unaweza kutolewa macho kama sio roho.......mtu chake atii).

Sasa mimi nakushauri utumie nguvu (kibali cha Polisi) ili kuzua huyo bwana asije tena kwako, kwa kufanya hivyo itasaidia wewe na yeye kuepuka "ngono chafu" na mume wa mtu. Natambua kuwa unampenda huyo mume wa mtu lakini kumbuka sio wako na kamwe hawezi kuwa wako.

Pamoja na uamuzi wako wa kuwa mwenyewe for life haina maana basi utembee na mwanaume hata kama ni mume wa mtu, jaribu kuwa mchunguzi unapotaka kuanzisha uhusiano ili usirudie kosa. Hakikisha unamfahamu mhusika kabla hujaji-comminte kwake kama mpenzi, hakikisha unakujua kwake, anaishi na nani n.k.

Wapo wanaume wengi tu ambao hawana wake kwa vile hawako tayari kuoa kuoa kwa mara ya pili baada ya Talaka au wake zao wamefariki dunia, nadhani wanaume wa namna hiyo wanakufaa zaidi na mtakuwa compartible in a way.

Kila la kheri.

Thursday

Hivi huyu ananipenda au Mchunaji?-Ushauri!

"Hi Dinah mdogowangu hujambo?
Naomba msaada wa ushauri kwa wanablog wenzangu. Mie ni mama mkubwa kiasi kwa umri, Nilikua na mwanaume tuliokua dini tofauti na tumeachana kwa miaka miwili sasa.


Kuna kijana ambae nimemzidi kwa takriban miaka miwili alivyosikia kama niaeachiaka tu, hapo hapo akaniambia yeye ananitaka na dakika hiyohiyo akaniambia kama niko tayari basi anaweza kufunga ndoa hata kesho, nilibaki nashangaa kwa nini haraka?


Mie sikumpa jibu la ndio wala hapana lakini nikabaki kumuambia labda ananijoke asingeweza kunioa kwa kua mie mkubwa kwake. Hali yangu kiuchumi na hata assets sio mbaya sana, Yule kijana ana kazi , ila kiuchumi nimemzidi ana mke na watoto watatu, ni muislam ndoa ya pili inaruhusiwa.


Alikua anamwamko sana wa kwenda kuongeza shule (degree ya pili) lakini hakua na sponsor na mwajiri alimkatalia ruhusa na akataka kuacha kazi, nilimshauri asiache ambembeleze mwajiri ruhusa. Sasa nikajiuliza ana mapenzi huyu au anataka kunituma nimsomeshe?


Baada ya mawasiliano, tukapoteana kwa kipindi kirefu kidogo kwa kuwa nilikua nje ya nchi. Tumeonana mwezi wa kwanza ki-accidental, ile mada imeanza tena, Na sasa ameshapata admission IFM hana sponsor, mimi niko nje ya nchi tena ila yeye anasisitiza anataka kuowa hata kwa remote, (kwa waislamu inaruhusika).


Najaribu kumsihi kwamba sasa hivituwasiliane tu na tuchunguzane, lakini yeye ameng'ang'ania antaka jawabu la kukubaliwa tuoane au laa ajikate. Hakuwa moyoni mwangu sana lakini nilikua nahisi with time hasa ukizingatia umri wangu naweza kumpenda.


Lakini ameng'angania ananipenda na anataka jawabu. Kwa tabia kama mme ndani simjui vizuri, nilijaribu kumuuliza kijana anaefanya nae kazi akaniambia kazini hayuko-organized na yuko hash, kwa nyumbani sijuiiii.

Wana blog naomba mnisaidie mawazo huyu kijana ananipenda kweli, au anataka kunitumia? lugha zake za kusisitiza hilo suala sikuzipenda sana kwani kunasiku ashaniambia ukinikataa mimi hutapata tena mtu kama mimi au hutapata mtu atakae kupenda kama mimi, au kwanini hujiulizi ni nini nilikupendea nisipende wanawake wenzio.nk.

Naomba ushauri jamani, ananipenda huyu? nimkubali? nimemwambia tusubiri kwa kua sipo nchini hadi november tuyazungumze yeye kagoma. Ushauri jamani hili jamaa linataka nini?"

Jawabu:Mimi sijambo Dada'ngu, habari za wakti kama huu mpendwa!
Huyo isije kuwa ni mmoja kati ya wale "wezi watupu", dada unajua siku hizi hata wanaume tena walio na familia zao(wake na watoto) wanachuna wanawake ambao mambo yao ni safi kiuchumi?.

Tena siku hizi nasikia wanawake walio nje ya Bongo au wenye kujiweza ndio wanaoibiwa kweli kweli, unaweza teremka pale Yapoti (airport) ukapokelwa na vijana/babaz watanashati wakitoa "offers" tofauti tofauti za ndoa hihihihihi.....turudi kwenye somo.


Kwenye maelezo yako tangu mwanzo mpaka mwisho hakuna mahali umeelezea hisia zako juu ya huyo kijana. Huyu kijana ni kweli anataka mdhamini kwa ajili ya masomo yake ya juu na ndio maana akakurukia mara tu alipogundua kuwa wewe na mumeo/mpenzi mmeachana.


Inawezekana kabisa kutokana na "kasumba" alidhani wewe utakuwa "desparate" kuwa na mwanaume au kuolewa kama inavyoaminika kwa wanaume wengi kuwa unapokuwa mdada mkubwa na kisha kuachika basi unakuwa huna "bahati", hivyo pamoja na kuwa ni mdogo kwako aliona utamkubali tu bila mizengwe.


Kwa upande wa pili huenda kijana kweli anakupenda, lakini je wewe unampenda? Tangu umetoka kwenye uhusiano mwingine ambao naamini ulikuwa wa muda mrefu na "serious" ni wazi unahitaji muda kuchuja hisia zako ili kuwa na uhakika vilevile kuwa tayari kujiingiza kwenye uhusiano mpya wa kawaida wa kimapenzi acha ndoa.


Kutokana na maisha ya sasa hakuna kitu kinaitwa kuchunguzana ili kufunga ndoa(ilikuwa miaka hiyo), siku hizi kupendana kwanza, ndio majuana taratibu na kuchunguzana na kuerekebisha kama inawezekana alafu unamalizai nakufanya maamuzi ya busara baada ya kugundua kasoro zake na yeye kugundua zako na kisha kujitoa mhanga na kukubali kuishi maisha yako yote (kufunga ndoa) bila kuzijali kasoro zake na utakachokifanya ni kumpenda mwenzio kila siku kama ndio mmeonana wiki iliyopita.....vinginevyo ndoa itakuwa ndoano.


Sasa, suala hapa sio kama yeye ni mchunaji au lah, kitu muhimu hapa ni wewe na hisia zako juu yake. Je unahisi kumpenda? kama sio je unadhani unaweza kurafikiana nae kikawaida tu? Vilevile unadhani siku moja unaweza kupendana nae na kuwa zaidi yamarafiki wa kawaida?

Nakuja....

Tuesday

Tuliachana, sasa nusu anitaka nusu hanitaki-Ushauri!

"Mambo vipi Dinah,
Mimi ni kijana wa miaka 29. Nimekuwa na mahusiano na msichana mmoja wa miaka 25. Kwa sasa tumeachana kwa takribani miezi sita. Tatizo nililonalo ni kuwa tangu tuachane baadae niliona kuwa bado namfeel na yeye alionyesha kuwa bado ananifeel hivyo niliamua kumueleza dukuduku langu.


Yeye akaniambaia kuwa niendelee na maisha yangu, ghafla baada ya wiki mbili akanitumia msg kuwa anani-miss sana kuwa nae na kuwa bado ananipenda na ataendelea kunipenda daima. Mimi nikaamua kumuuliza kuwa yeye hisia zake kwangu zikoje? Jibu alilonipa ni kuwa nusu anataka kuwa nami na nusu hataki kuwa nami.


Pia ameniambia kuwa bado ananipenda sana na hajapenda mwanaume yeyote so far. Pia hajatembea na mwanaume yeyote tangu tuachane.Sasa wandugu hapa huyu mrembo anania gani na mimi? Kama still ananipenda and half anawish niwe nae then kwa nini hataki au kusita niwe nae?


Maana hata nikimwita tu anagoma kuja. Yaani kwa kifupi haeleweki msimamo wake kuwa nini hasa anataka. Mawasiliano yetu sio mabaya. Tunasalimiana kama kawaida.

Dada Dinah na wanablog naombeni ushauri."

Jawabu:Mambo ni mazuri kabisa Kaka, nafurahia likizo baada ya kuwa kule "busy" kwa taribani mwezi na nusu.


Sasa rafiki hujaeleza sababu ilisababisha wewe na binti huyo kuachana kitu kitakachofanya watu, well labda mimi tu kushindwa kukupa maelezo ya kutosheleza na yenye uhakika. Unajua, unapotoka kwneyeuhusiano kutokana na tofauti fulani fulani haina maana kuwa na mapenzi yamekwisha juu ya yule mpenzi wako.


Huenda kilichotokea au kusababisha muachane au namna ulivyomuacha au alivyokuacha ilimuuma sana na kumfanya apunguze hali ya kukuamini tena au kujiamini mwenyewe kwenye suala zima la mahusinao ya kimapenzi na hilo likitokea ni wazi kuwa atahitaji muda ku-sort out kichwa chake na hisia zake kabla hajawa na uhakika wa nini anakitaka ktk maisha yake ya kimapenzi na ngono ofcoz.



Sheria moja kuu ya kurudiana baada ya kuachana (well sio sheria inayojuliakana bali huwa naitumia mimi kwa wateja wangu kama wewe leo hapa) ni kuwa unapoachana na mpenzi wako kisha ukagundua kuwa bado unahisi nae za kimapenzi ni kupigania penzi hilo kwa kuonyesha mapenzi ya kihisia ya hali ya juu kuliko mwanzo.........
badala ya kucheza ule mchezo wa "kutegeana".


You just go for it full speed, viginevyo wajanja watakuwahi na watapenda binti kuliko ulivyokuwa unapenda na hilo likitokea ujue wazi kuwa binti hatokuwa na mapenzi na wewe tena kwani mapenzi ya mpenzi mpya yatafunika penzi lako la kusua-sua.


Fafanua akisemacho-Wanawake wengi huwa hawako wazi kusema ukweli, wanakuachia wewe ung'amue anachomaanisha hasa kama anataka wewe umuonyeshe kuwa "unamuhitaji". Sijui nini kilitokea na kuwafanya ninyi wawili kutengana lakini ninachokiona hapa kutokana na maelezo yako ni kupimana misimamo au hisia.


Huyu binti alipokuambia uendelee na maisha yako ni wazi kuwa alikuwa anataka kusikia ukisema "siwezi kuendelea kuishi bila wewe, maisha yangu hayatokuwa kama yalivyokuwa bila wewe mpenzi".....sasa baada ya wewe kuuchuna na kuendelea na maisha yako kiukweli (ulidhani ndivyo alivyomaanisha).

Si umeona mwenyewe akaona hujapata "meseji" akaamua kukumbusha kwa SMS na kusema kuwa anaku-miss, anakupenda na atakupenda daima.....hapo alikuwa anasema ukweli ulio wazi kwa vile wewe hukupata ujumbe wa "endelea na maisha yako".

Kosa kubwa ulilifanya-Alipokuwambia kuwa ameku-miss, bado anakupenda na atafanya hivyo daima, hukupaswa kumuuliza hisia zake juu yako!! Ulitakiwa kumkumbatia na kumwambia kuwa unapenda pia na ungependa mrudiane au kujaribu tena uhusiano wenu.


Mwanamke anapokuwa wazi hivyo ujue kazidiwa na mapenzi(katumia mbinu zote umeshindwa kuelewa), binti anakuhakikishia kabisa kuwa uko peke yako moyoni mwake pale aliposema kuwa hajapenda wala kutoka na mwanaume mwingine (kumbuka ni miezi sita imepita), mwanamke akikaa miezi sita bila kuingia kwenye uhusiano mpya hata kama sio wa kimwili na bado anarudi kwako na kudai anakupenda ujue huyo ni 4 the keep hehehehe sio lazima iwe hivyo, usiogope my broda!.


Nia yake ni kutaka kurudiana na wewe lakini kwa bahati mbaya wewe huonyeshi kutaka kurudiana nae sina hakika ni kwavile huelewi anachokisema kwako au na wewe huna uhakika na hisia zako za kimapenzi juu yake??!!. Ile nusu anakutaka (ni hisia zake juu yako) na nusuhatakikuwa na wewe (ni kwavile hujamuonyesha kuwa unamtaka back).


Sasa skia, inakwenda hivi, sawa!......Muombe msamaha kwa kutokuwa nae kwa muda wa miezi sita (kwamwe usigusie nini kiliwaachanisha), mwambia hisia zako bila kumuuliza yeye anajisikiaje juu yako. Mwambie kuwa unampenda sana na ungependa kuishi maisha yako ukijuwa kuwa yeye ni mwanamke wako peke yako, mueleze kuwa utafanya kile uwezacho ili kufanya uhusiano wenu uwe mzuri, wenye mapenzi ya dhani na wenye afya.


Mwambie tangu mmekuwa mbali-mbali maisha yako yamekuwa sio kama vile yalivyokuwa mlipokuwa wote, mhakikishie kuwa utamuonyesha mapenzi motomoto ambayo hujawahi kumuonyesha hapo awali (hakikisha unafanya hivyo.....hata kama ni kumshukia chini au kumla denda kwa mtindo tofauti).....ongeza na mwengine ujuayo wewe kama mwanaume.


Usitegemee jibu la papo kwa hapo (hii inategemea na ufundi wako wa kubebembeleza, ikiwezekana toa chozi mshikaji...it'll work).....asipokubali on spot mpe muda na wewe kuwa kwenye mawasiliano mara nyingi kuliko kawaida.


Unapowasiliana hakikisha unamsalimia kikawaida nakuonyesha kuwa unajali, lakini kama vipi fanya mawasiliano ile mida ya "chombeza" hakikisha una-flirt(hata kama ni kwa SMS), unamkumbusha mlipokuna (ruka matatizo mliyokutana nayo au mlivyoachana), zungumzia maisha yako ya baade na yeye...Mf-Kama tungekuwa wote sasa hivi tungefanya hivi-vile nakadhalika.

Kila la kheri!

Monday

Umewahi kuhisi ukamilifu kama mwanamke?

Mambo vipi wewe?

Ni muda mrefu umepita bila kukupa somo, natambua kuwa ulikuwa una-miss mambo fulani, sasa leo rafiki napenda ku-share hisia ambazo sina uhakika kama ni mimi tu ndio huwa nazipata au vinginevyo. Kama hujawahi kuzipata basi endelea kusoma ili ujue kwa undani.


Nafahamu kuwa unafahamu kwamba mwanamke siku zote anachelewa kufika kileleni hali inayofanya waume/wapenzi wetu kufanya wawezalo ili mwanamke uanze kisha yeye amalizie....awe wa mwisho.


Hali hii ikizoeleka inakuwa "boring", yaani kila siku wewe unakuwa wa kwanza! Inakuwa routine kitu ambacho mimi binafsi nakipiga vita kutokea kwenye mahusiano ya kimapenzi kwani kinaweza kufanya ule msisimko wa uhusiano wenu kuwa "butu" yaani uhusiano hauna masham-sham a.k.a hauna "makali"



Licha ya hivyo, kuna wakati wewe mwanamke unatakakuhisi "uanamke wako" yaani kama ni mwanaume basi atasema mwanaume aliyekamilika. Ukamilifu wa mwanamke sio tu kujua aina za mapishi, kutoa penzi, kuwa mwepesi wakati wa kungonoana, mwenye kulipenda umbile lake zuri alilojaaliwa na M' Mungu, usafi na mwenye kuvutia bali pia uwezo wa kujua kumuwahisha mpenzi hasa kama mpenzi wako ni mmoja kati ya wale waliojaaliwa kwenda "mwendo mrefu" au kazoea kujizua na hivyo anashindwa kujiachia ili awahi....


Au inawezekana kabisa bao la kwanza kutoka kwake mpenzi wako linakuja haraka (kwaida kwa wanaume wengi hasa kama ananyege sana)lakini yatakayofuatia yanachukua "mwaka" hali inayoweza kukufanya utake kumuona mpenzi wako anakuja tena na tena....si wajua kale kasura ka “nakojoa” au “nakuja”...aah mimi huwa nakazimia sana na kaniniamshia hisia....wanasema “turn on”.


Unaweza kujitahidi kumfanyia manjonjo na masham-sham ili ashindwe kujizuia na kumaliza mapema lakini njema haifiki walanini.....hii ikitokea usikate tamaa na kujishtukia kuwa huwezi "game"...."game" unaiweza ila hujampatia tu......sasa nitakupa kambinu ambayo mwanaume yeyote hawezi kujizuia ikiwa utakapatia kambinu haka.


Kumbuka unapofanya hii mbinu lengo ni wewe na yeye kufurahia hivyo haijalishi ikiwa mtafika wote au yeye kuanza.........utahisi mchanganyiko wa hisia za raha, furaha, ukamili kama mwanamke na mapenzi ya dhati kwa mpenzi wako......inategemea zaidi na unavyolichukulia tendo hili takatifu, kama ni mpenzi wa tendo hili kama mimi basi utakuwa umenielewa vema.

Mkao-Kama kawaida mkao ni kifo cha mende na mtindo ni mwanamke chini.....kifo chamende ni mkao wenye mitindo mingi ambayo haichoshi na inakuwezesha wewe mwanamke kuwa incontrol na kuwa huru kumfanyia mume/mpenzi wako mambo mengi kwa kutumia uke wako kuliko mikao migine.


Si kwa vile nimesema kifo cha mende basi wewe unakimbilia kitandani na kujilaza chali na kujipanua.....hapana! cheza-cheza nae mpe ile inaitwa "stata", au "hapitaita" kabla ya mlo kamili(hajalishi ni mzunguuko wa ngapi)....si unajua kuwa kila bao linautamu tofauti??


Ili asijue nia yako ni nini basi unapaswa "kuzuga" na kumlaza yeye pale kitandani na kuanza kumfanyia "uchunguzi wa kina" kwa kutumia mikono/vidole, matiti, midomo, ulimi, mashavu ya uke.....na hakikisha unagusa kila kona ya mwili wake ambayo wewe unajua anapenda kuguswa.....


Baada ya hapo, jilaze pembeni yake na kumvuta ili aje juu yako au njia rahisi ni kukalia uume wake na kuhakikisha umeingia vya kutosha ndani yako alafu jilaze (full) juu yake bila uume kuchomoka kisha mkumbatie alafu jibilingishe nae.....hapo atakuwa juu yako moja kwa moja.....panua miguu yako vya kutosha ili kukuwezeza kuzunguusha kiuno cha ngono (sio kile cha ndombolo....bali kile nilichokizungumzia ktk Makala za nyuma).


Akisha kuwa juu yako muachie apige "tako" zake mbili/tatu yaani aende juu-chini au nje-ndani mara chache huku wewe ukizunguusha kiuno taratibu kutafuta kona nzuri ya kukibana kichwa......kisha mwambie atulize “ball” yaani hakuna ku-move.....no more takoz!


Alafu sasa, shikilia makalio yake na jaribu kuyakandamiza dhidi ya sehemu ya juu ya uke wako ili kumfanya asi-move(akitaka anaweza) lakini hiyo itakusaidia kumkumbusha kwa kumrudisha ndani kila akitaka kutoka kutokana na utamu.....na vilevile kukupa balance ya kufanya ukifanyacho.

Sasa anza kuzunuusha kiuno chako cha ngono ambacho kitakufanya uhisi kichwa cha uume kinasugua kona ya uke wako pale ulipoubana ktk mtido wa kuzunguuka, kubana na kuachia......endelea kuzunguusha kiuno chako cha ngono ktk nusu mzunguuko/duara yaani degree 180.....yaani huendi mzunguuko mzima unaenda nusu kisha unarudi ulikotoka nusu nyingine....kulia na kushoto.....


Uhatahisi jamaa anataka ku-move au atakushikilia kimtindo kama sio kutoa mihemo na miguno Fulani ya raha.......hatua hiyo ikifika ndio wakati wa kwenda mzunguuko mzima kwa kuongeza speed na kuipunguza.....Mf kukata kiuno cha ngono kutoka kulia kwenda kushoto ni rahisi na unakwenda haraka kuliko kile cha kutoka kushoto kwenda kulia. (inategemea kama wewe ni left heanded au vinginevyo)


Sasa unapobadilisha "rythim" kutoka haraka kwenda taratibu hakikisha unafanya kwa mpangilio huo, kwamba kutoka kulia kwenda kushoto haraka na kutoka kushoto kwenda kulia taratibu.....Hakika ile hali atakayokuwa akionyesha kuwa anafurahia itakufanya wewe ufurahie zaidi na utahisi utamu unakaribia.....

Hapa njemba itapagawa na kupiga "tako" mfurulizo ktk harakati za kufika kileleni.....wakati anafanya hivyo "relax" kiakili lakini kimwili endelea kufanya mambo uliyoanzisha ili mfike wote.

Kunauwezekano mkubwa kabisa akakuacha njia panda....hey ndio nia na madhumuni kumuwahisha......hii yote inachukua dakika dk 10 mpaka 20 ukiunganisha na romance (kuandaana) lakini kwa tendo peke yake ni dk 8-10 tu kitu na box......

Jaribu leo, ili kumpa mpenzi wako mwanzo mzuri wa mwezi.....kila la kheri.

Pages