Tuesday

Ushuhuda wa Mama Johnson wa Mza!

Hi My Dear Dinah.
Its me again Mama Johnson From Mza.

How is Valentine 2 all Tanzanian?
Napenda kuwashukuru watanzaia na Non-tanzanian wote ambao mmenishauri hapo chini. Mimi ni Ma Johnson ambae nilituma mada yangu kwa da Dinah ikisomeka NAHISI MUME WANGU ANAJISAHAU. Especcialy my special thankfull to you Dear Dinah.

Let me tell u maana ilikuwa as a story what happened to me.
Baada ya kuwasilisha mada yangu hapa mezani sikuwa na jinsi ilinibidi ningoje matokeo kwa kujua kuwa ntapata challenges lakini na jibu litapatikana.


Nilivumilia na nikasitisha mawasiliano. Sikuwasiliana nae kwa njia yoyote ile. I was do as he do to me. Akinitumia sms nikawa simjibu. Akinipigia napokea namjibu in short kama niko kazini namwambia niko bussy kidogo ngoja ntakupigia. Na kama ni mida ya jioni namwambia ngoja ntakupigia mtoto ananisumbua mwisho wa yote sipigi wala sijibu sms zake.


Wakati huo nilikuwa nafatilia mawazo ya wanablog wenzanu ya kuwa nimfate dar bila taarifa yoyote wakati huo ndo tulikuwa tunaelekea kwenye Valentine Day. Nilifatilia maombi ya ruhusa ofisini angalau kwa siku tano ili nije dar boss wangu hakuniruhusu kwa sababu Mi ni Accounts Administrator na huwa tunafunga hesabu za mwezi tar ambazo nilikuwa nimeomba. So it was difficult to move.


Basi Mpaka ikafika tar 14 no call from me to him and no call from him to me. Roho iliniuma sana ukizingatia mi ndo nilianza kuuchuna. Siku hiyo ya tar 14 nikatoka kazini mchana as u know it was week-end. Nilipitiliza hadi home nikaandaa chakula mapema nikaoga na kujipumzisha.
Ikafika saa mbili yausiku sm yangu ikaita. Kupokea ni yeye akaniuliza uko wapi nikamwambia niko hm akaniambia toka unifungulie geti. It was supries. I felt like iwant to fall down.


Nikatoka nikamfungulia. Akaniambia samahani sana nimekuja bila taarifa. nikamwambia no worries its your home and am your married wife. Akasema nimeitahidi sana nije maana siku hiyo yaani tar 14 mwezi huu wa pili ndo tulifunga ndoa AICT na tulikuwa tunatimiza miaka 5 ya ndoa mwezi huu.


Baada ya yote akanilaumu nimebadilika nimekuwa mjeuri akinipigia sizunumzi nae akinitumia sms simjibu. Na mi nikamwambia na mi nilikuwa naumia hivyo wakati ule najitahidi kuwa karibu nae ye anakuwa mbali. Akanisihi nisifanye hivyo maana yuko mbali nipunguze mawazo he loves me sour much, hayuko radhi kunisaliti ila ni majukumu tena ya mda mchache tu.


Alikaa tarehe 16 alfajiri akaondoka. Sikumwamini hata kidogo nilijua ananipaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Yaani da Dinah ye aliondoka kwa flight ya saa mbili pass through Nairobi. Mi nikaondoka na Flight ya saa sita mchana.


Nilichukua chumba jirani na hotel anayoishi na kwa mda mfupi nikagundua kuwa chakula hula pale kila siku jioni. nilijenga mazoea na yule dada muudumu nikampatia cash kidogo. Akawa karibu na mimi mno. So kila nilichomdadisi alinipa ushirikiano wa kutosha bila chochote.


Pale pale kwa maelezo ya yule dada nikajua no one alse ila baadae niligundua yule dada alijua habari za pale wa kuwa house boy wa mr wangu ni jamaa bf wake. Nikamuuliza kwani huyo kaka yupo akasema alikwenda mza kuiona familia yake amerudi leo amefika tu nakuondoka ameenda kazini. Ilipofika saa mbili ya usiku alikuja pale hotelini akapata dinner akaenda nyumbani kulala. Saa tano ya usiku nikamtuma yule dada aniitie yule bf wake alishagaa sana nikamwambia aende.


Alipomwita nilimuuliza unanifahamu mimi akasema nahisi nilikuona seemu ila sikumbuki ni wapi. Nikamwambia kumbuka vizuri hapo hapo nikamwuliza na uyo mtoto je? Akamtazama kwa makini akasema huyu mtoto anafanana na bossi wangu theni akasema nimekutambua ni wewe ndopicha zako na mtoto zimetapakaa mle ndani. nikamuulizabosi wako yupo akasema yuko anaangalia tv.


Nikamwambia beba huyo mtoto twende hakuna kumshitua. Akaniongoza hadi ndani Da dinah, hakuwa na taarifa kama tuko pale lakini nilimkuta ameshika picha yangu niliopiga sku ya wapendanao akiitazama kwa hisia wakati huo alikuwa ametoka kunipigia sm nikamwambia niko home najiandaa kulala.


Alipata mshituko usiosemekana. Na mi nilipofika nilidhibiti sm yake vilivyo sikuona sms ambayo itanipa hofu ya kusalitiwa. & now i have find out the true. Kwa mda wa siku mbili nilikuwa pale kweli da dinna Mr wangu yuko bussy mpaka nilimwonea huruma. Napenda kuwashauri wanawake wenzangu tusiwalaumu wala kuwalaumu wapenzi wetu.

Tuwapende tuwe karibu nao, Na watuambiapo jambo lolote tusiwablame inatakiwa uvumilivu na maelewano.Thanks all for your information. And many thankis to You Dinah.
Samahani nimeandika marefu kama gazeti.

Regards.
Mama Johnson.
Mza.

No comments:

Pages