Thursday

Ushuhuda kutoka kwa Wakawe!

"Ni mimi wa KAWE, niliyekuwa nazinguliwa na demu!!!!!!!!!.Nimekubali wadau hapa panafundisha. Ktk maoni yenu nimejaribu kufanyia kazibaadhi ili nianglie matokeo.

Nilianza na kummchunia kama sipo naye hata kimawazo, nikawa naondoka simuagi tukikutana nampa hi halafu nakuwa sina time naye kwa story wala kwa ishu yoyote. Hapo hapo nikamwambia kwakuwa amenikataa natafuta demu mwingine.

Akaniambia tafuta! Sikumchelesha kesho yake nikaigiza demu chumbani na yeye akamuona lakini hakufanya lolote kwa muda huo. Siku hiyo usiku nilimuona anakuja na vazi la usiku hana hata chupi, akaniuliza aliyekuwa humu chumbani mchana ni nani?

Nikamjibu mpenzi wangu, akaangua kilio na kunirukia nilipokuwa hakuongea lolote ila nikutomasa na kuniambia TANGIA LEO NAOMBA TUWE WAPENZI. Hapo hapo kanipa mpaka sasa nimapenzi motomoto.

Ananiambia alikuwa ananipenda ndio maana aliHitaji nimsumbukie kumpata ili nikikumbuka nilivyosumbuka kumpata nitashindwa na nikweli siwezi kumuacha wala kuhangaika kwingine !Kama mungu atajalia nitarudi jamvini kuwajuza habari za ndoa.

SHUKRANI WADAU NYOTE.
NI MIMI WA KAWE.

Dinah anasema: Hiongera sana kwa kufanikiwa kupata mpenzi uliyekuwa ukimtaka baada ya kufanyia kazi ushauri wa wachangiaji. Mimi nasema asante sana kwa kurudi tena hapa na kutuambia unavyoendelea na kuahidi kuja tena mara baada ya kurekebisha masuala ya ndoa.

Mungu awabariki wote kwenye maisha yenu kama wapenzi na kila la kher kwenye maandalizi ya kutangaza ndoa.

Sijui nini cha kuongea nae, yaani nakuwa-blank-Ushauri.

"Da Dinah happy new year! Blog yako imenisaidia sana kwa mambo mengi ambayo nilikua siyajui na yale nilo kuwa nayajua nimeweza imarisha zaidi, shukrani sana na pia kwa wote wanao changia watoa msaada mkubwa pia.

Da Dinah mimi nipo nje ya nchi kwa ajili ya masomo boyfriend wangu wa miaka minne sasa yupo Bongo, tumesha kwaruzana sana kwa ajili ya mahusiano yetu lakini nampenda kweli huyu kaka. Hilo si swali langu lakini just to give you an insight.

Mwaka jana mwishoni nilikua Bongo kwa likizo fupi na nilimtambulisha kwa Mama yangu Mama akampenda na yeye alikwisha nitambulisha kwao muda kidogo japokuwa mama yangu alikuwa anamsikia lakini hatukuwahi kukaa sote.

Niliporudi masomoni tukawa tunaendelea kuwasiliana vizuri tu sema siku hizi anakuja mpaka mtandaoni tunaongea lakini ukweli sijui nini cha kuongea nae, does that make sense?? Yaani na baki kucheka na kukumbushia yalopita madogo madogo na yanayo endelea huku kiasi nitaongea nae kuhusu nini kingine jamani online?

I love the idea that we chat but I've never done that with him so am blank! niwe naongea nini online? msaada dada yangu mpendwa...asante. M"

Dinah anasema: M heri ya mwaka mpya nawe pia, naona sasa mwaka ndio unachanganya...nimekuwa napata shida sana kuandika 2010 na hivyo nikawa naishia kuandika 2001, ila sasa nimezoa...anyway!

Uhusiano wa mbali ni mgumu sana na wengi huishia njiani, lakini njia pekee ya kufanikiwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mtu aliye mbali ni mawasiliano. Kwa bahati nzuri vijana wa sasa tumekuwa na Teknolojia na hivyo kuturahisishia sana linapokuja suala la mawasiliano.

Natambua wakati mwingine inaweza kuwa ngumu sana ku-keep maongezi kwa vile yeye hajui nini kinaendelea huko uliko na wewe hujui nini kinaendelea huko aliko, sio hivyo tu pia sisi wanadamu tunatofautiana kuna baadhi yetu tunapenda kuzungumza na wengine sio wazungumzaji.

Kama wewe ni mzungumzahi basi mazungumzo huja yenyewe yaani jinsi unavyoongea ndivyo ambavyo "topics" zinazaliana basi mnajikuta mnapiga soga mpaka mmoja wenu anaamua kuaga(hela imeisha n.k).....na wengine ni wa kimya kwamba akikupa habari anazodhani kuwa ni muhimu basi maongezi yameisha, utabaki kuuliza maswali nkupewa majibu mafupi.

Unaweza ukawa unazungumzia tofauti ya tamaduni za huko na Nyumbani, ukazungumzia sinema, habari za kisiasa, maisha kwa ujumla, mipango ya maisha yenu ya baadae, ni namna gani unakabiliana na masomo, leo Chuoni kulitokea nini, amekula nini, nani alipika (kama bado anaishai kwa wazazi), n.k.

Ukiwa unapa stori za huko uliko ambazo zinavutia na kuozungumzia mipango ya maisha ya hata yale maisha mlioishi miaka minne iliyopita......yaani unachanganya maongezi. Ili kumfanya na yeye aongee basi wewe unamuulizia habari za hapo nyumbani na watu mnaofahamiana nao n.k.

Pia mnaweza kuzungumzia ngono na hata kuifanya ngono kwa kutumia simu. Hii itawasaidia sana kupata zile kuwa karibu zaidi kihisia na hivyo uhusiano wenu kutotetereka.

Natumaini maelezo ya wachangiaji na nyongeza yangu yatasaidia ideas za kuendeleza maongezi na mpenzi wako.

Kila la kheri.

Monday

Mchumba ana UTI isiyoisha-Ushauri!

"Pole na kazi dada Dinah
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27 sasa na nina mahusiano na nataka sasa nifanye maamuzi hasa kwenye maisha ili niweze kuoa, maana nafikiri kila kitu nimemaliza kwani nimeshapata elimu kwa kiwango cha degree moja na nimepata kazi nzuri .

Kwa sasa nimeshatoka nyumbani najitegemea na nimeshafikiria maamuzi ya kuoa, ila tatizo kubwa linaloniumiza kichwa ni huyu mpenzi wangu karibu kila baada ya miezi 2-3 lazima atalalamika kuwa tumbo linamuuma sana na akienda hospital anaambiwa kuwa ana UTI sasa mimi nashindwa kuelewa.

Tunakaa pamoja na nyumba ina choo cha kuflash na sasa ni zaidi ya mara 5 amepatwa na huo ugonjwa, napata wasi wasi sana japokuwa nilipomwambia tukapime HIV alikubali na wote tulikuwa safi, sasa najiuliza maswali haya

1.Huu ugonjwa ukiachilia uchafu wa chooni tatizo lingine linasababishwa na nini?

Dinah anasema: Maambukizo kwenye njia/mfumo wa Mkojo unasababisha na wadudu wanaoishi sehemu ya kutolea haja kubwa na sio uchafu wa chooni, japokuwa uchafu chooni unaweza kusababisha maambukizo mengine ukeni.

Mgonjwa akipata UTI na kuanza matibabu ni lazima amalize Dozi aliyoandikiwa na wakati akiendelea na unywaji wa dawa lakini akawa mzembe kunywa maji kwa wingi tatizo hilo litaendelea kujitokeza mara kwa mara kwa vile wakati alipokuwa akitumiia dawa alipaswa kunywa maji kwa wingi ili kusafisha njia yake ya mkojo kwa kukojoa mara nyingi.


Msemaji aliyesema kuwa UTI ni kichocho sio kweli, kichocho ni maambukizo mengine ambayo husababishwa na wadudu wanaishi kwenye maji yaliyotuwama/simama. Mtu mwenye kichocho hukojoa mkojo wa damu wakati mtu mwenye UTI anakojoa mkojo wenye rangi ya kama brauni hivi....yaani mkojo wake sio msafi na huto aharufu mbaya na kali sana.

2.Je akifanya ngono tatizo hili alimuathiri ?

Dinah anasema: Mhusika napopatawa na UTI hata kama ni mwanaume, unatakiwa kutumia Condom wakati wa kufanya ngono ili kuepuka maambukizo. Lakini ni vema kutofanya ngono mpaka mgonjwa amalize Dozi na kuponakabisa. Utajua umepona baada ya kwenda kumuona Daktari kwa vipimo vingine na pia mkojo kuwa msafi (unatakiwa kuwa kama maji).

3.Kwanini hiyo UTI inamtokea mara kwa mara?

Dinah anasema: Kuna sababu chache ambazo nimezigusia hapo juu na nyingine ni kwa vile anaendelea kungonoka wakati wewe ambae nadhani utakuwa umeambukizwa. Mlipaswa wote kupimwa na kutumia dawa za kutibu UTI.....ugonjwa huu sio kwa wanawake tu, bali hata wanaume.

4.Ni njia zipi zinaweza kuchukuliwa ili asipate tena ?

Dinah anasema: Kuhakikisha anapimwa tena, anatumia dawa na kumaliza Dozi yote bila kuruka siku, masaa. Kujenga tabia ya kunywa maji kwa wingi kila siku, kujifunza kuwa msafi na kujua namna yakujisafisha sehemu zake nyeti.

Kutokubana mkojo kwa muda mrefu, wanawake tunauwezo wa kubana mkojo kwa zaidi yamasaa manne na huwa tunajisifu sana kwa hilo lakini kama umewahikuwa na UTI hakikisha ukibanwa tu mkojo unaenda kukojoa haraka.

Vilevile kukojoa kila baada ya kufanya ngono ( ni muhimu kunywa kimiminika) sio uji, Soda wala pombe bali juisi iliyochanganywa na maji mfano maji ya Ukwaju, Ubuyu, Squash (hii lazima uzimue na maji) au aina yeyote ya kinywaji ambayo inachanganywa na maji asilia. Yote kwa yote maji ni mazuri zaidi ya vimiminika vingine.

Anapojisafisha baada ya kunya asijisafishe mpaka ukeni kwa wakati mmoja. Kama amekojoa wakati anakunya na anataka kujisafisha "kwa mpigo" ni vema kuanza kujiswafi uke na kumalizia sehemu ya kunyea kwama viungo viwili vinavyojitegemea kwamwe asisafishe kwa wakati mmoja. Pia kuepuka kuchangia vyombo/vifaa/sehemu za kuongea au kujisafishia nyeti zake.

Ikitokea amjemaliza kujisaidia (kunya) kisha akaenda kuoga (baada ya kuchamba) ahakikishe kuwa amesafisha mikono yake kwa sabuni kabla hajagusa uke wake nakujisafika ukeni (kuondoa utoko).

5.Madhara gani makubwa yanaweza kutokea baadae?

Dinah anasema: Kama ataendelea kutumia aina ya Antibaotics kutibu UTI kwa muda mrefu, inasemekana dawa hizo husababisha tatizo lingine la kiafya, pia kama UTI itafikia kwenye kiwango cha mgonjwa kukojoa mkojo mzito (uliochanganyikana na usaa) au usaa kuteremka wenyewe kama Utoko basi ni wazi kuwa mrija wake wa mkojo unaweza kuzima na hivyo kushindwa kutoa mkojo kawaida.....unabanwa mkojo lakini huwezi kukojoa.

Ikifikia hatua hii mhusika tahitaji kufanyiwa upasuaji ili asafishe na pengine kuwekewa Catheter (mrija wa mpira) kwenye Kibofu cha mkojo nahivyo kutumia Mfuko wa nje wa kutunzia mkojo.

Nitashukuru sana nikipata majibu kutoka kwako hili nitoe wasiwasi wangu
Ni mimi nduguyo Jm."

Dinah anasema: Asante sana JM kwa uwazi na ushirikiano. Ni matumaini yangu maelezo ya wachangiaji na haya yangu niliyo ongezea yatasaida wewe na mpenzi wako kwa pamoja kwenda kwa Daktari ili kupata matibabu na kutibu tatizo.

Kila la kheri.

Wednesday

Sitaki kuudhi mke na Familia yangu, nitaachaje?-Ushauri

"Habari dada Dinah, Mimi nijiite Elly. Umri wangu sasa ni 34yrs, naishi scandinavia countries.
Leo ndio mara yangu ya kwanza kuandika humu japo kwa suala la kupitia mana nyingine najikuta nimerudi kama mara mbili kwa siku kuona kama kuna jipya.

Ni ukweli nisiouficha kuwa nimekuwa nikijifunza mengi kupitia hapa.
Nimeona niandike humu kwani naamini kwa ushuri wanaopewa waliopitia hapa kuomba ushauri kwa kweli naona wanasaidiwa. Kwani wengi wa watembeleji wa humu ni watu wazima.

Kifupi Dinah, mie nimekuwalia mazingira ya dukani tangu nikiwa Primary hadi Secondary, kipindi hicho chote cha kuuza duka kuna wateja hasa Arusha , Mererani na Mbeya ambako nimeuza duka nyakati tofaui (sio yangu ni ya kaka zangu) wakinunua sigara basi wana kuambia "niwashie" na mimi kuwawashia kama kawaida. Tangu kipindi hicho basi ndio mwanzo wa kujua sigara.

Sikuwa mvutaji yule wa viile, Ila pale ninapohitaji kuchangamka kama wanywa pombe ama wala ndumu, mie steam zangu ni sigara moja nachangamka.Tabia hii nimekuwa nayo kwa miaka 17 sasa. Miaka sita iliopia nilifunga ndoa na tumejaliwa mtoto mmoja ambae nilimuacha Bongo kwa miaka 3 sasa na mwanetu ana 4yrs.


Wakati wa kudate na ma wife hakuwahi gundua kuwa mara nyingine huwa navuta sigara, nasema mara nyingine maana kama nilivyotangulia kusema mie nilikuwa sivuti kila siku.
Pamoja na kutokujua ila kati yetu kuna kipindi fulani tuliambiana what I like and don't.

Yeye cha kwanza ni uvutaji na pombe, katu hatopenda wala kutamani mwenzie atumie. Pombe kweli Sijawahi kutumia kwani ladha yake tu inatosha kuninyima raha ya kunywa. Tabu yangu tangu nimekuwa huku Ughaibuni, Unajua tena kutimiza ndoto kwanza naona sio kama nilivyotarajia.

Maana nilitegemea ningeweza kuileta family huku ktk kipindi cha 1 year kitu ambacho kinaonekana ni kigumu hivyo napigana pengine kupata mtaji nirudi ku-join family ama kama yeye atapaa skuli basi aje. Ila hili sio ilionileta hapa ktk blog.


Sasa kipindi chote cha 3years nimekuwa nikivua takriban sigara 10 kwa siku, ila cha ajabu siwezi vuta waziwazi hadi nikiwa mwenyewe hivyo hata marafiki hili nao hawajui. Dinah sigara siipendi na sipendi kuwa mvuaji bali najikuta tu navuta.

Nimejaribu kuacha nimeshindwa, najua hata wife akijua japo nitajitutumua ka kidume ila ukweli hili litanipunguzia heshima nilionayo kwa mke wangu na jamii ya kwatu ambao hakuna hata mmoja mvutaji, sijui nimetokea wapi maana huu si utoto tena kwa umri huu.


Tafadhali msinishambulie jamani bali mnipe ushauri kama kuna mwenye kujua mbinu yoyote ya kuepukana na sigara.
Shukrani sana kwa ushauri mtakao nipa maana nitaufanyia kazi"

Dinah anasema: Elly asante sana kwa ushirikiano wako pia uvumilivu. Inapendeza kuona watu wamechangia uzoefu wao kuhusu matumizi ya sigara, mimi binafsi nitakupa ushauri wa uhakika wa kuacha "habit" yeyote mbaya inaweza kuwa kujichua, kutokuoga, ngono na watu tofauti kila siku (ngono zembe) kula sana, uvivu, kujamba, kutumia psa ovyo, kunywa pombe n.k

Ninachojaribu kusema hapa ni kuwa mtu anaweza kuzoea kitu fulani na kukitumia kitu hicho kama "kiondoa" mawazo au kwa case yako kukuchangamsha, mazoea hayo yanaweza kujenga tabia na tabia ikazaa tatizo liitwalo addiction kwa kitaalam.

Kama huko Ughaibuni ni pande za Uingereza, basi nafurahi kukuhabarisha kuwa NHS wanatoa huduma ya bure na baadhi hupewa malipo fulani ili waache kuvuta sigara, hivyo basi unaweza kufanya mawasiliano na wahusika ili kupata msaada wa kitaalam zaidi na support ili uache kabisa kuvuta Sigara.

Vinginevyo ni kujiwekea mikakati mwenyewe ya kujaribu kuacha tabia ya uvutaji, natambua kuwa ni ngumu sana kuacha kufanya jambo ambalo umelizoea ghafla, hivyo ni vema ukaanza kupunguza kiwango unachovuta kwa siku.

Mfano badala ya kuvuta kumi kwa siku kama ilivyo sasa, jitahidi na uvute mbili, jinsi ambavo siku zinakwenda unazidi kupunguza siku za uvutaji...Mf; umeweza kuvuta kila siku sigara mbili sasa anza kuvuta sigara moja kila baada ya siku mbili, endelea kubadilisha the habit, na sasa punguza na vuta moja kila baada ya siku nne.

Utajikuta unavuta moja kila baada ya wiki na baadae itakuwa moja kila baada ya wiki 2, alafu utajikuta unavuta moja kila baada ya mwezi na hatimae utasahau kama umevuta au laa!...haina maana ukaitafute bali jipongeze kwa kufanikiwa.

Hii haitochukua siku mbili au mwezi mmoja bali ni miezi kadhaa hivyo kuwa mvumilivu na kuwa commited kwenye mkakati utakaojiwekea, kumbuka ni wewe pekee mwenye uwezo wa kujizuia kuvuta sigara.

Wakati unaendelea na mkakati wako wa kuacha kuvuta sigara, jaribu kubuni kitu mbadala utakachokuwa unakitumia kujiliwaza au kuondoa mawazo kila unapojisikia mpweke, mwenye huzuni, unapoikumbuka familia yako.....unaweza ukatumia senti unayonunulia sigara kumi kununua kadi ya simu/muda wa kutosha ili kuzungumza na watu ambao ni muhimu kwako au kwenye shughuli zako au zile unazotaka kwenda kuzifanya Nyumbani.

Kwa vile uko mwenyewe huko Ulaya ni wazi kuna wakati unapata upweke sio wa kimapenzi tu bali hata ule wa marafiki, ndugu na jamaa, maisha ya Ughaibuni ni tofauti sana na hapa nyumbani kutokana na Tamaduni zetu kutofautiana.

Unaweza ukajikuta unaishi ili kufanya kazi badala ya kufanya kazi ili uishi, yaani yanakuwa ya upweke sana kwa vile hakuna ile " kujichanganya" kama hapa bongo, kwamba ukitoka kazini kila mtu anakwenda kwake na maisha yake kivyake.

Ni matumaini yangu utachukua ushauri wa waungwana wengine na sehemu ya maelezo yangu na kufanyia kazi kamaulivyo ahidi.

Kila lililojema.

Pages