Thursday

Ushuhuda kutoka kwa Wakawe!

"Ni mimi wa KAWE, niliyekuwa nazinguliwa na demu!!!!!!!!!.Nimekubali wadau hapa panafundisha. Ktk maoni yenu nimejaribu kufanyia kazibaadhi ili nianglie matokeo.

Nilianza na kummchunia kama sipo naye hata kimawazo, nikawa naondoka simuagi tukikutana nampa hi halafu nakuwa sina time naye kwa story wala kwa ishu yoyote. Hapo hapo nikamwambia kwakuwa amenikataa natafuta demu mwingine.

Akaniambia tafuta! Sikumchelesha kesho yake nikaigiza demu chumbani na yeye akamuona lakini hakufanya lolote kwa muda huo. Siku hiyo usiku nilimuona anakuja na vazi la usiku hana hata chupi, akaniuliza aliyekuwa humu chumbani mchana ni nani?

Nikamjibu mpenzi wangu, akaangua kilio na kunirukia nilipokuwa hakuongea lolote ila nikutomasa na kuniambia TANGIA LEO NAOMBA TUWE WAPENZI. Hapo hapo kanipa mpaka sasa nimapenzi motomoto.

Ananiambia alikuwa ananipenda ndio maana aliHitaji nimsumbukie kumpata ili nikikumbuka nilivyosumbuka kumpata nitashindwa na nikweli siwezi kumuacha wala kuhangaika kwingine !Kama mungu atajalia nitarudi jamvini kuwajuza habari za ndoa.

SHUKRANI WADAU NYOTE.
NI MIMI WA KAWE.

Dinah anasema: Hiongera sana kwa kufanikiwa kupata mpenzi uliyekuwa ukimtaka baada ya kufanyia kazi ushauri wa wachangiaji. Mimi nasema asante sana kwa kurudi tena hapa na kutuambia unavyoendelea na kuahidi kuja tena mara baada ya kurekebisha masuala ya ndoa.

Mungu awabariki wote kwenye maisha yenu kama wapenzi na kila la kher kwenye maandalizi ya kutangaza ndoa.

No comments:

Pages