Friday

Nataka kuchumbua ila majibu yake mmh-Ushauri.

"Naitwa Michael miaka 25 ni mara yangu ya kwanza kwenye libeneke kuomba ushauri. Kuna binti anaitwa Joy ana miaka 23 ambaye ningependa awemchumba wangu, lakini nakuwa katika wakati mgumu kutokana na majibu anayonipa nikiwasiliana naye kupitia simu. Wakati huu hatukuwa karibu.

Majibu anayonipa hasa kwenye story za kawaida tunazopiga yanaonyesha uelekeo wa yeye kunikubali lakini nikimuuliza kuhusu mimi na yeye kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi ananiambia muda wake wa kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi bado, na nikimuuliza lini atakuwa tayari kasema "ni katika kipindi cha miaka 3 ijayo".

Nilimuahidi kumsubiri lakini akakataa kwa kisingizio kuwa asingependa kuniumiza wala mimi kumuumiza yeye.Tumekuwa karibu sana katika kipindi cha miezi 3 ya mawasiliano kupitia simu kiasi cha yeye kuniambia mambo mengi kuhusu familia yake na mengine yangehitaji mtu wa karibu sana kuyajua.

Mambo kuhusu boyfriend wake wa kwanza na jinsi walivyoachana, sifa za mume ambaye anamhitaji na zote ziliniangukia.Nilipomuuliza kama ananipenda na kunihtaji alisema ananipenda lakini kunihitaji hakuwa na jibu kamili.

Sasa wakati mgumu nilionao ni je niendelee kumbembeleza au nimuache? nikitaka kufanya hivyo roho yangu inasita kwani kwa jinsi anavyokuwa mgumu ndio nazidi kumpenda. Nifanyeje? Michael"

Dinah anasema:Mike hebu kuwa mkweli, unauhakika ktk umri wa miaka 25 uko tayari kumuoa huyo binti au ni gia tu ya kumpata kimapenzi? Kama kweli unauhakika na unania ya kumchumbia na kuja kufunga nae ndoa nasikitika kusema kuwa yeye kwa sasa hayuko tayari kwa ajili hiyo na amekuwa wazi kwako, kuwa anakupenda lakini hayuko tayari labda baada ya miaka 3...hapo uamuzi ni wako ku-take risk na kumsubiri au kuendelea na maisha yako.

Uamuzi wa kumsubiri unaweza kukupa matokeo mawili tofauti moja ni chanya au hasi, kwamba akawa nawe kama mpenzi/mchumba au akawa na mtu mwingine....ndio maana nikasema take risk.

Kitendo cha huyu binti kukuambia vitu vingi ambavyo wewe unadhani anapaswa kuambiwa mtu wa karibu zaidi kama vile mpenzi, ni kwa sababu anakuamini kama rafiki yake. Inawezekana kabisa hata upendo alionao ni wa kirafiki na sio wa kimapenzi na ndio maana anakosa jibu unapomuuliza suala la yeye kukuhitaji wewe kama mpenzi.

Katika hali halisi ni Binti mdogo ambae tayari amewahi kuwa kwenye uhusiano, kama mpenzi aliyekuwa nae alikuwa ndio mpenzi wake wa mwanzo ni wazi kuwa itamchukua muda mrefu kidogo kama hajaingia kwenye uhusiano mpya na mwanaume yeyote sio wewe tu.

Kutokana na maelezo yako nahisi kuwa huyu binti bado anahisia na yule ex, hisia zinazomfanya ashindwe kufanya uamuzi kwa vile hana uhakika kama bado anampenda yule au la! Inawezekana pia kajiwekea hiyo miaka mitatu kuweza kujua hisia zake ziko wapi.

Kitu ambacho kimepelekea yeye kukuambia kuwa asingependa kukuumiza au wewe kumuumiza, pale ulipoahidi kumsubiri ndani ya miaka mitatu ambayo kwa mujibu wake ndio atakuwa tayari kuingia kwenye uhusiano.

Nimependezwa na uwazi wa huyu Binti, kajaribu kuwa mkweli ili kukusaidia wewe kufanya uamuzi na kuendelea na maisha yako lakini wakati huohuo uendelee kuwa rafiki na mtu wake wa karibu.

Mimi nakushauri umuache (kwani kubembeleza kukizidi huwa kunaudhi sana) lakini endelea kuwa pale kama rafiki, msikilize, mshauri, msaidie na yote muhimu kwa marafiki. Ukionyesha kuwa umeheshimu "msimamo" wake lakini bado unaendeleza urafiki ni wazi atakuwa comfortable na wewe na pengine baada ya hiyo miaka mitatu wewe ukawa the one.

Kila la kheri.

Saturday

Mume ataja jina la binti yetu wakati wa Tendo!-Ni kawaida?

"Dada dinah habari ya mwaka mpya natumaini mwaka umeuanza vizuri. Mimi ndio mara yangu ya kwanza kutuma swali langu lakini ni mpenzi wa blog yako.


Mimi nimeolewa na ndoa yetu imejaaliwa mtoto moja wa kike mwenye umri wa miaka mitatu, mimi na mme wangu tumekuwa pamoja kwa miaka mitano sasa. Jana (1/01/10 ndio ilikwa mwaka mpya hatukutoka tulikuwa tu home kwavile nchi tuliyopo ni baridi sana na snow kwa kwingi sana.


Hivyo tuliamua kukaa home na fungua mwaka mpya home, ilipofika saa sita kufunga mwaka na kufungua mwaka tulifungua champagne na kunywa kwa furaha tukakaa mpaka saa saba usiku ndio tukaanza kufanya mapenzi, yaani mwanzo ilikuwa poa sana mara katikati ya mapenzi ndio mme wangu akataja jina la mwanangu badala ya jina langu katikati ya mapenzi.


Tulivyo maliza mavitunzi ndio nikamuliza kuhusu kuita jina la mwanangu katikati ya mavituzi, akasema amezoea kuita hilo jina all the time ndio maana amejisahu na kuita hilo jina. Dada dinah naomba uniambie kama hii ni kawaina na kama imewahi kutokea kwa watu wengine hapa.
Naombeni michango yenu.
Ni mimi Samatha"

Dinah anasema: Samatha asante kwa email yako, lakini naomba kuuliza kidogo kabla sijakupa maelezo na pengine itasaidia watu wengine kukupa michango ya uhakika zaidi. Je hilo jina la mtoto ni nani alichagua? Mumeo na wewe ukakubali au wewe na yeye akalikubali? Je jina la mtoto na lako linafanana kwa mbali Mfano Dinah na Daniela, Maria na Marian/Mariam n.k....inawezekana ni jina la Ex n.k.

Huenda alitaka kukuita mama____(jina la mtoto) na akaishia jina la mtoto akasahau "mama".

Asante Samatha kwa nyongeza ya maelezo (nenda kwenye comments), naungana na mchangiaji aliyehoji Uraia/Makuzi ya mumeo, hakika sio ubaguzi lakini sio watu wa mataifa mengine tu wanawarudi watoto wao. Hapa Tanzania wapo wengi tu lakini kutokana na kulinda "heshima ya familia" watu hukaa kimya nakutunza siri.


Natambua inaumiza kumfikiria mumeo jinsi ambavyo watu wengine wanamdhania, lakini mimi nakuomba ufanye ushunguzi bila kumuuliza binti wala baba yake. Kuwa karibu zaidi na binti yako ili kuondoa wasi wasi. Samahani kama maelezo hayo yatakuwa yamekukwaza. Inawezekana hajawahi kumuingizia wala hana mpango huo ila huwa anamchezea-chezea.


Ujue watoto wa kike huwa tunakuwa karibu sana na baba zetu, lakini kutokana na mazingira yetu hapa Bongo inakuwa ngumu sana kuwa that karibu na baba, yaani baba hapewi nafasi ya kubadili nepi ya mtoto wa kike achilia mbali kumuogesha.

Lakini kwa watoto wa nje ya Tanzania huwa karibu zaidi kutokana na mazingira baba hulazimika ku-baby sit wakati mama anaenda kazini n.k. hivyoinawezekana kabisa mtu akaibua a sick tabia ya kumchezea mwanae wa kike ktk harakati za kutafuta namna ya kumbembeleza n.k.

Kuna babaz wanawazoesha kuwachezea watoto wao wa kike na kuwapandikiza imani kuwa "baba anakupenda ndio maana anafanya hivi". Wengine wanaimani za kishirikina, ili kufanikiw abasi mudi mwanao, baadhi hulazimika kuwarudi watoto wao kama sehemu ya Mila....wenyewe wanaita Suna!

***************************MUNGU APISHE MBALI!

Tendo la ndoa ni tamu, ni takatifu linawafanya wote wawili kuwakaribu zaidi in a way mtu mwingine yeyote hawezi kujua achilia mbali kuhusika. The moment na utamu wake, mihemo na sauti za mahaba, harufu za majimaji ya miili yenu na namna mnashikana n.k hakika HUWEZI kabisa kulopoka jina la mwanao au la mtu mwingine yeyote unless otherwise umewahi ku-share the momet like that with au u r willing to do so!


Haijalishi unapata utamu kiasi gani au wewe mwanamke ni mlopokaji kiasi gani, huwezi kabisa-kabisa kumtaja baba yako au mtoto wako wa kiume. Katika hali halisi wanaume ni wagumu sana kulopoka-lopoka wakati wa tendo na wanapofanya hivyo ni wazi kuna uhusiano mkubwa kati ya jina na tendo (amewahi/anafanya ngono na mtu mwenye jina hilo).


Kama jamaa ni mbongo na anakuita mama nanihii time 2 time ni wazi alikusudia kukuita hivyo il akasahau neno "mama", pia inawezekana kabisa kuna mtu alimkaa sana kichwani (alimpenda kupita kiasi) na utamu alioupata siku hiyo ulimkumbusha huyo mtu mwenye jina linalofanana na mtoto wenu.

Kutokana na uzoefu wangu, wanaume wanatabia ya kuita binti zao majina the last Ex b4 mke aliemuoa hasa kama walipendana sana enzi zao ila mmoja hakuwa tayari kuendelea mbele. Kuna Njemba moja iliwahi kuniambia "Dinah hata kama tukiachana, nikioa nakubalikiwa kuzaa mtoto wa kike lazima nimuite Dinah"......which kafanya hivyo!


Pia inawezekana ni character kwenye Porn movies ambayo mumeo anaipenda namlipokuwa mkifanya akili yake ilikuwa ikimfikiria huyo mtu wa kwenye Kideo, lakini ktk kujitetea ikabidi aseme kuwa alimtaja mtoto kwa vile anamuita na kumtaja kila wakati ili kulinda hisia zako.

Sasa Samatha, kama ni jina la Ex au Porn star basi let it go kwa sasa, akirudia tena kutaja jina hilo ni wazi mtahitaji kuzungumza kuhusu hilo Jina kwa undani zaidi.

Amos, amegusia kitu muhimu sana kwa jamii yetuya Kibongo, baba kuchagua jina la mtoto wa kiume na mama kuchagua jina la mtoto wa kike.

Kila la kheri mdada.

Wednesday

Mpenzi karudi Ulaya na kukata mawasiliano je nimeachwa?

"Dada Dinah pole na hongera sana kwa kazi nzuri.
Mimi ni msichana wa miaka 28, Naomba ushauri kama ifuatavyo. Nina mpenzi wangu wa muda mrefu nampenda sana, alikuwa Ulaya kwa miaka 3 na tulikuwa tunawasiliana vizuri sana.

Akarudi hapa bongo kurenew Visa yake na tulikaa pamoja vizuri kipindi chote hicho, siku moja nikamuuliza je vipi kuhusu maendeleo ya uhusiano wetu? akasema kwa sababu kazini kapewa wiki tatu tu za kuwa hapa Bongo hatutaweza kufanya lolote.


Akaniahidi kuwa ikiwa atanyimwa kibali cha kurudi huko Ulaya basi tutaendelea na mambo yetu na akifanikiwa kuongezewa muda basi ataenda Ulaya halafu atanitumia mwaliko, akaniambia nimsaidie kusali apate kwa sababu akikosa itamchukua muda mpaka atafute kazi hapa Tz.


Mimi nikasali, na kweli Mungu akatusikiliza alivyoenda Ubalozini akapata Visa na akarudi zake Ulaya, November mwishoni 2009, tukawasiliana siku tatu tu, mara mawasiliano yakakata nikamtumia sms nikimuuliza vipi mbona siku hizi kimya sana? hakujiibu, na mara akawa hapokei simu na wala hajibu email wala sms kwa mwezi sasa.

Hapa nimebaki nashangaa nini kinaendelea tena?wakati tulikuwa ok kabisa. Kinachoniuma ni kwa nini hataki kuongea na mimi? kwa nini hapokei simu?na ni kwa nini hakuongea nami kuhusu mipango yake alipokuwa hapa?
Nifanye nini?naombeni ushauri.
Pne"

Dinah anasema:Asante sana kwa mail yako na pole kwa maumivu ya moyo na hofu kuu uliyonayo juu yampenzi wako, isije kuwa mpenzi wako kapatwa na masahibu makubwa huko aliko. Hebu kwa kuanzia tu ili kupata amani moyoni, check na ndugu au jamaa zake wa karibu kujua kama Mpenzi ni mzima huko aliko alafu tunaendelea na mengine nikirudi......

Mungu apishe Mbali!

Pages