Wednesday

Mpenzi karudi Ulaya na kukata mawasiliano je nimeachwa?

"Dada Dinah pole na hongera sana kwa kazi nzuri.
Mimi ni msichana wa miaka 28, Naomba ushauri kama ifuatavyo. Nina mpenzi wangu wa muda mrefu nampenda sana, alikuwa Ulaya kwa miaka 3 na tulikuwa tunawasiliana vizuri sana.

Akarudi hapa bongo kurenew Visa yake na tulikaa pamoja vizuri kipindi chote hicho, siku moja nikamuuliza je vipi kuhusu maendeleo ya uhusiano wetu? akasema kwa sababu kazini kapewa wiki tatu tu za kuwa hapa Bongo hatutaweza kufanya lolote.


Akaniahidi kuwa ikiwa atanyimwa kibali cha kurudi huko Ulaya basi tutaendelea na mambo yetu na akifanikiwa kuongezewa muda basi ataenda Ulaya halafu atanitumia mwaliko, akaniambia nimsaidie kusali apate kwa sababu akikosa itamchukua muda mpaka atafute kazi hapa Tz.


Mimi nikasali, na kweli Mungu akatusikiliza alivyoenda Ubalozini akapata Visa na akarudi zake Ulaya, November mwishoni 2009, tukawasiliana siku tatu tu, mara mawasiliano yakakata nikamtumia sms nikimuuliza vipi mbona siku hizi kimya sana? hakujiibu, na mara akawa hapokei simu na wala hajibu email wala sms kwa mwezi sasa.

Hapa nimebaki nashangaa nini kinaendelea tena?wakati tulikuwa ok kabisa. Kinachoniuma ni kwa nini hataki kuongea na mimi? kwa nini hapokei simu?na ni kwa nini hakuongea nami kuhusu mipango yake alipokuwa hapa?
Nifanye nini?naombeni ushauri.
Pne"

Dinah anasema:Asante sana kwa mail yako na pole kwa maumivu ya moyo na hofu kuu uliyonayo juu yampenzi wako, isije kuwa mpenzi wako kapatwa na masahibu makubwa huko aliko. Hebu kwa kuanzia tu ili kupata amani moyoni, check na ndugu au jamaa zake wa karibu kujua kama Mpenzi ni mzima huko aliko alafu tunaendelea na mengine nikirudi......

Mungu apishe Mbali!

No comments:

Pages