Sunday

Je anaweza kumsamehe Ba'Mkuu?-Ushauri.

"Dada Dinah mie nakuja tofauti kidogo. Nimekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Kijana mmoja kwa mwaka na nusu sasa. Nampenda na pia nadhani yeye ananipenda kwani huwa ananifanyia yote ambayo mimi nahisi ni kwaajili ya mapenzi yake kwangu.


Kipindi cha mwaka tumeishi pamoja baada ya yeye kuja na idea ya kusave ili tufunge ndoa mwakani, maana yake huku tunakosihi maisha ni ghali sana. Kwa vile ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuishi na mwanaume nyumba moja nikamuomba mpenzi ahamie kwangu badala ya mimi kuhamia kwake na akakubali.


Nilifanya hivyo kwa vile nilikuwa naogopa kunyanyaswa kama uhusiano wetu hautofika mbali. Namshukuru Mungu tangu tumeanza kukaa pamoja maisha yamekuwa mazuri ukiachilia migongano ya hapa na pale na kupishana kwenye baadhi ya mambo. Tumefanikiwa kusave kiasi cha kutosha kwa ajili ya kufunga ndoa kuanza maisha kama mke na mume.

Kitu cha kushangaza Mpenzi wangu hajawahi kuzungumzia wanafamilia yake, mwanzoni nilidharau tu kwa vile sikutaka kumkorofisha japokuwa kuna donge linanikaa rohoni nikitaka kujua kwanini hazungumzii familia yake wala kunitambulisha kwao kwa simu!

Huwa nafikiria vitu vingi sana juu ya mpenzi wangu huyu lakini kwa vile nampenda huwa najipa moyo maisha yetu ya ndoa ni kati yangu mimi na yeye na sio watu wengine. Siku moja nikaamua kukaa nae chini na kuuliza kama utani tu.

Mpenzi wangu alicheka alafu akaniambia, alikuwa anasubiri mpaka baada ya kufunga ndoa ndio aniambie ukweli kuhusu maisha yake lakini kwa vile nimeuliza basi atasema na lolote nitakaloamua basi ataliheshimu. Akaendelea kuwa yeye hana ndugu wala wazazi na alilelewa na baba yake mkubwa ambae alimtesa sana.

Nilimuonea huruma sana na nikatamani kumkatisha lakini pia nilitaka kujua mwisho wa story yake. Mpenzi wangu ilimbidi atoroke pale nyumbani na kudandia treni kwenda kijijini ambako kulikuwa na bibi na babu yake, alipelekwa shule na kufanikiwa kufaulu na kuendelea na Sekondari lakini baada ya tu ya kumaliza kidato cha nne Babu akafariki Dunia.

Maisha yalikuwa magumu kwani bibi hakuwa akifanya kazi na wala hakupokea msaada kutoka kwa baba mkubwa. Akaamua kuacha shule na kuanza kufanya kazi ya kulimia watu mashamba ili aweze kupata hela ya kula yeye na bibi.

Baada ya miaka michache kupita bibi nae akafariki na yeye akabaki mkiwa, hivyo akaamua kurudi Dar ili kutafuta kazi na kwa bahati nzuri alipata kazi kwenye Ubarozi fulani kama mlinzi. Akajiandikisha Chuo cha ufundi lakini masomo ya jioni na kujilipia mwenyewe. Alifanikiwa kumaliza na kufaulu, akiwa na kiu ya kwenda Chuo Kikuu aliomba Udhamini kutoka kazini kwake kwani gharama za masomo zilikuwa juu sana.

Boss wake baada ya kusikia historia ya maisha yake na kugundua kuwa hana ndugu akamdhamini akasome nje ambako ndio tumekutana. Baada ya kuniambia yote hayo nilijisikia vibaya na kujuta kwanini niliuliza, nilimuonea huruma mwanaume mzima kutoa machozi.

Nilipomuuliza kwanini hakuwa wazi tangu mwanzo? akasema hakutaka niwe nae kwa kumuonea huruma kutokana na maisha yake ya zamani bali niishi nae kwa vile nampenda.

Je! Ni sawa kama nitamshauri mpenzi wangu amsamehe baba yake mkubwa na kurudisha uhusiano?"

Dinah anasema: Nimepitia ushauri na maelezo ya wachangiaji na wamegusia vitu muhimu ambavyo natumaini umevifanyia kazi. Nakubaliana na imani yake kuwa hakutaka umuoenee huruma kutokana na hadithi ya maisha yake ya zamani ambayo inauzunisha na alitaka umpende.

Kuna watu wanajenga mahusiano na hata kufunga ndoa na kuendelea kubaki kwenye ndoa kwa vile wanawaonea huruma na sio kuwa wanawapenda. Nikirudi kwa past yake nadhani naungana na wote waliosema chunguza ili kujua ukweli na kama kuna ndugu (watoto wa baba Mkubwa'ke) basi unaweza k uanza kuzungumza nao bila kuwajulisha wewe ni nani (unaweza kujifanya ulisoma nae n.k) ili kujua ukweli wa mambo.

Kama asemayo ni kweli basi heshimu uamuzi wake wa kujiweka mbali na Mzee huyo (kama bado yupo hai) lakini jitahidi kutafuta namna ya yeye kurudisha uhusiano na watoto wa mzee huyo aliyemnyanyasa ili kuepusha watoto wao na wenu kuja kutengeneza mahusiano ya kimapenzi n.k si unajua Dunia ni ndogo hii.

Mimi binafsi sina uzoefu sana na matatizo ya kifamilia lakini nashukuru wasomaji wamekushauri vema kabisa.

Kila la kheri!

Saturday

Mume to be anuna kwa vitu vidogox2-Ushauri

"MAMBO VIPI JAMANI?
MIE NI MDADA WA MIAKA 29, NATARAJIA KUFUNGA NDOA HIVI KARIBU MUNGU AKITUJALIA TUNA MUDA WA MIAKA 6 SASA NA TUNAISHI PAMOJA KWASASA YAANI DADA TATIZO NILILO NALO NI HUYU MWANAUME ANAPENDA KUNUNA KWA VITU VIDOGO YAANI UKIKOSEA KITU KIDOGO ANANUNA NA ANAWEZA KUONGEA MANENO YA KASHFA MPAKA NAOGOPA YANI MIMI HATA SIJUI NIFANYAJE JAMANI ANAWIVU SANA YANI NIKIPIGIWA SIMU AU KUTUMIWA MSG KOSA UNAKUTA KANUNA MARA HANIAMINI YAANI MPAKA NAKEREKA YANI NI VILE BASI TU EMBU NISHAURI DADA NIMFANYAJE HUYU MTU JAMANI MAANA ANANIKWAZA MPAKA BASI."

Dinah anasema: Mambo poua tu mdada, hujambo? samahani kwa kuchelewa kujibu. Binaadamu tumeumbwa tofauti hali kadhalika ninyi wawili ni tofauti sana kitabia, kimalezi hata matakwa yenu ni tofauti natumaini hilo unalifahamu.


Huyu mchumba wako inawezekana hajiamini hali inayopelekea yeye kushindwa kukuamini wewe hasa unapopokea sms au hata kupigiwa siku, mara nyingi mtu mwenye au alikuwa na tabia chafu kupitia simu au hata Internet huwa anakereka "Kisaikolojia" (kwa vile anajua ndio zake au zilikuwa zake yaani anauzoefu fulani hivi ) na kuumia balada ya kuuliza kwa upole na upendo "ni nani huyo ulikuwa unaongea nae" au "nani amekutumia ujumbe.


Mmekuwa pamoja miaka 6, mnapendana na mnakwenda kufunga ndoa ili kuishi pamoja maisha yenu yote hivyo basi ni vema kuanza kurekebishana sasa. Natambua kila mmoja wenu anavijikasoro ambavyo havirekebishiki so u live with them na viji-habit vyake ambavyo vinarekebishika ikiwa mhusika atakubali kuwa anavyo na vinamkera mpenzi wake.

Nini cha kufanya:
Ni ngumu sana kuwakilisha issue hiyo kwake (Kwa wanaume wengi lawama zote anabeba mwanamke) hivyo unapaswa kutumia UANAMKE wako kuandaa namna/mazingira ya kuwakilisha issue, unaweza kutumia mapenzi ya hisia na mwili, unaweza kumromantisha (kumfanyia kitu romantic), unaweza kubadili mwenendo kwamba kila unapopokea sms unasoma kisha unamuonyesha au unaifugua karibu yake ili aione, na kama ni simu basi hakikisha unamhusisha.....MF-unaulizwa simuni, "unafanya nini" unaweza kusema nipo tu hapa na Mchumba/mwenzangu/mume wangu tunapumzika. N.k

Vilevile kama unajua kuna vitu vidogo vidogo vinamuudhi na vitu hivyo wewe ndio unaevisababisha basi unapaswa "kupumzika" yaania cha kuvifanya. Baada ya muda (wiki nne mpaka miezi 2) unaweza kuwakilisha tatizo lako kwake kwa upole na upendo, hapo hatoweza kukurushia lawama zozote kwa vile tayari ulimhusisha kwenye txts msg na simu unazopokea na ukaacha vile vitu vidogo vidogo vinavyomfanya anune.


Kule kwetu tunapofunzwa huwa tunaambiwa kuwa mwanamke ndio pekee mwenye uwezo wa kubomoa au kujenga nyumba yako (not exactly ila wanatumia hii ili wewe mwanamke ujue nafasi yako na kuwa mwangalifu kwenye uhusiano ili kupunguza matatizo), Pia kumbuka maisha ya kimahusiano na ndoa sio lelemama, yanahitaji kufanyiwa kazi kila siku.


Bibi yangu aliwahi kusema kuwa "kukitokea tatizo ndani ya ndoa jiangalie wewe kwanza na jirekebishe kabla hujaomba mwenzio ajirekebishe"RIP........alitumia kuomba rather than kumtaka mwenzio ajirekebishe.

Usitegemee mabadiliko ndani ya siku au wiki moja bali muda zaidi kwa kuwasiliana, kushirikiana, kukumbushana na kuongozana.

Kila la kheri ktk kuweka sawa hili na kwenye kufunga ndoa.

Thursday

Nahisi naibiwa-Ushauri

"Nafikiri upo salama na unaendelea vizuri na shughuli zako.
Mimi ni mvulana 24, nina girlfriend ambaye tumeanza mahusiano yetu tangu tukiwa form One katika shule moja huko Kibaha mwaka 2002.

Tumeanza mahusiano ya kimwili tukiwa kidato cha tatu mwaka 04 kipindi hicho mwenzangu akiwa na miaka 16, nami nikiwa na miaka 19, nilifurahi sana siku hiyo kwani nilikuwa nakata utepe wa mpenzi wangu .

Tangu hapo ilikuwa kila baada ya mwezi tunakula goodtym mpaka tulivyomaliza kidato cha 4. Matokeo yalipotoka mimi nilichaguliwa kuendelea na kidato cha 5 ktk shule ya Azania mwenzangu hakupata nafasi na pia familiya yake haikuwa na uwezo wa kumsomesha zaidi.

Huku tulipunguza mambo flani kwakuwa elimu ilikuwa ngumu ukilinganisha na ile ya O-level, lakini tulikuwa tunawasiliana kama kawaida na mambo flani ya kizidi tulijiburudisha. Baada ya kumaliza kidato cha sita 6 mwaka 08 nilipata nafasi ya kuendelea na Elimu ya juu katika chuo cha Uhasibu Tanzania Institutes of Accountancy (TIA) tawi la mbeya.

Tangu nijiunge na chuo kila nikikutana kimwili na mwenzangu naona tofauti na nilivyozoea awali kwani sasa ukipiga goli moja tu mambo yanabadilika uke wake unakuwa na maji na mda mwengine naona kama size imeongezeka.

Sielewi kabisa dada inakuaje, najiuliza au ameshaanza kugawa mali yangu?. Nikimuuliza anasema kwamba hiyo ni kawaida kwa msichana kuna kipindi huwa inatokea hivyo, nashindwa kuelewa ukizingatia sijawahi kuingiliana na msichana mwingine zaidi yake nami ndiye niliye fungua mlango wake.

Naomba unisaidie dada angu kwani naogopa asije kuniuwa na Magonjwa. Sasa nafikiria kuachana naye lakini nashindwa ukizingatia nimemzoea, nimvumilivu na tumefanya mambo mengi ya hatari ila kwa hili nashindwa kuvumilia na roho inaniuma sana, huwa najiuliza kwanini size iongezeke wakati mi ndo mfunguzi wa uke wake?.

Naomba unisaidie kwa hili dada Dinah ili nijue ukweli wa mambo ili nifanye uamuzi sahihi.Ahsante!!
HO"

Dinah anasema:Mie niko salama kabisa hapa "naholideika" tu kimtido sehemu sehemu. Asante kwa mail yako na kunivumilia pia as nilikuwa "nabizika". Sasa wewe HO rafiki yangu ulianza uhusiano wa kingono yeye akiwa na miaka 16, ni mtoto na mwili wake ulikuwa bado unajengeka.

Wakati mwili wake unaendelea na mabadiliko ya ukuaji mlikuwa mnaendelea kula good tyme kama ulivyosema mwenyewe hiyo inaweza kuwa sababu ya kwanza. Sababu ya pili nadhani hakuwa akifika kileleni alipokuwa mdogo, sasa amekuwa mdada (mwanamke) anapata kusikilizia utamu na hatimae kukojoa......tuanze na sababu ya kwanza, sawa?

Sababu za Ukuaji:-
Hivi sasa huyu binti atakuwa na miaka 21 kama bado nakumbuka hesabu vema, umri ambao mwili wa mwanamke unakoma kukua yaani yale madadiliko kutokana kuvunja ungo yanakuwa yamekamilika na sasa anakuwa mwanamke kamili yaani mwili wake uko settled...umetulia.

Kwavile alikuwa akingonoka mara kwa mara akiwa ktk kipindi cha ukuaji mwili wake ukatend kukubali mabadiliko ya kingono yaliyosababishwa na uume wako na kuendelea kufanyia kazi sehemu hiyo kama ilivyo, sasa baada ya kuwa mwanamke wa miaka 21 ni kawaida kabisa kwako kugundua mabadiliko kama hayo na kwa kifupi wewe ndie uliyesababisha.......wazazi huwa wanasema acha kuharibu watoto wa wenzako that is what they mean.

Sababu ya kutofikia Mshindo (sitokwenda kwa undani kwa sababu ya Mwenzi mtukufu):-
Jinsi mwanamke anavyofurahi tendo ndivyo ambavyo ute unaongezekana na anapofikia mshindo(kilele) basi mwanamke huyu huzalisha ute mwingi zaidi hali inayoweza kusababisha yeye na wewe mtiaji kuhisi kama vile uke umepanuka kimtindo.

Ndio maana huwa nashauri wapenzi wanaokerwa na hili kubadilisha mkao/mdindo au kumpa muda mwanamke huyo apumzike (sio lazima utoke, unaweza kubaki ndani bila kufanya kitu) mpaka mwanamke huyo atakapo kuwa tayari kuendelea na ute utakuwa umepungua au unaweza kumfuta na kujifuta uume wako kisha mkaanza upya.

Mwisho kabisa napenda kukuhakikishia kuwa binti huyo hakuchezi shere na hata kama angekuwa kifanya hivyo wala usingegundua kwa kumtia, sio rahisi hasa kama anaotoka nao wanauume wenye ukubwa kama wakoa u chini ya hapo.

Ondooa hofu na endelea kupiga kazi kwa bidii.

Kila lilojema HO.

Pages