Tuesday

Naomba Ufumbuzi wa Haraka nisimpoteze Mpenzi!

"Habari da Dinah? I hope wee mzima na unaendelea na shughuli nzito ya uelimishaji wa jamii. Am greatful topics zako nyingi zimenisaidia. Mimi ni mdada mwenye umri wa miaka 24, nina ujauzito wa miezi sita na nusu sasa.
Niliposhika mimba nilipata taabu ya kutapika na kushindwa kula kwa miezi kama 4 hivi. Mpenzi wangu alivumilia sana kwani nilimfanyia visa sana ingawa haikuwa makusudi.
Sasa shida ya kwanza ni kwamba anataka tufanye mapenzi lakini mimi nashindwa kwani uchafu umezidi kutoka na ni mwingi mno mpaka inakera, imefikia hatua navaa pantyliners kila siku.
Hii hali inanifanya nihisi kama vile mpenzi wangu hatosikia raha na mimi sipendi kuwa weti hivyo kwani nasikia kichefuchefu lakini wakati huohuo sitaki mpenzi wangu anaitelekeze.
Pili Sehemu zangu za siri zimebadilika rangi na kuwa nyeusi wakati rangi yangu ya ngozi ni lighter kiasi, pia nikinyoa natokwa na vipele vidogo vidogo, sasa sitaki mpenzi wangu anione nikiwa hivyo, je nitaondoaje vipele na kurudisha rangi yangu ya awali?
Nilikwenda kwa Gyno wangu kuangaliwa na sikuwa na maambukizo yeyote
Je kuna dawa asilia ambayo naweza kuitumia? maana hizi dawa za kizungu nyingi hazifai kutumiwa wakati wa ujauzito.
Tatu Matiti yangu yanauma na kuwasha sana, basi huwa najikuna mpaka najikwaruza ili kupoza napaka mild steroid lakini wapi!! Sasa how will we have sex when matiti yako hivyo?
Nne Mpenzi wangu hupenda mwili wangu ukiwa bonge kiasi, sasa kpindi cha miezi 4 nilipokuwa naumwa na kushindwa kula nimepungua sana, yaani na tumbo langu kubwa bado sijafikia mwili wangu kabla ya ujauzito kwani nilikuwa a bit kibonge.
Mpenzi kaniletea Dada zake waje kunisaidia kupika ili nile na kuwa na afya lakini wapi! alafu mbaya zaidi ni kuwa nikikonda naonekana so terrible na I really feel unattractive na i think nikikubali kumvulia nguo hatoniona navutia tena. Sitaki kumpoteza mpenzi wangu.
Kila siku natoa sababu za kuumwa, tafadhali naomba ufumbuzi wa haraka kwani mpenzi ameanza kuwa bitter and unhappy ninapomkwepa kwani anasema anataka kuwa karibu na mimi."

Sunday

Romance kuisha

Dada dinna hongera kwa ushauri wako mzuri,mimi naomba kuuliza mnaposema romance hufa kutokana na mwanamke kupoteza mvuto baada ya kujifungua au kuwa na watoto mbona unakuta mwanaume anatoka nje ya ndoa na anakuwa na uhusiano na mke wa mtu ambaye tayari naye ameshazaa na ana watoto je hiyo imekaaje?
Kwenye topic "Kwanini Romance hufa baada ya kipindi fulani kwenye ndoa"
Umesema b

Nimevumilia tofauti zake kwa Ex, ila hili lanishinda...

"Habari da Dinah!
Jamani nimeshawishika kukuchagua wewe kama msaada kwangu, umri wangu ni miaka 29ti mwenye jitihada sana katka maisha. Kinachonikatisha tamaa ni mpenzi wangu ambae simuelewi kama ana ugonjwa au la, maana ni miezi tisa sasa hanifikishi kila tukianza kufanya mapenzi.

Hali hii aliyonayo mpenzi wangu hakuwepo awali, imejitokeza mwaka huu na sasa ni mwezi wa tisa anawahi kukojoa sekunde chache tu tangu tuanze tendo. Imefikia hatua ya kujichua mwenyewe na hata kufikiria kutoka nje ya uhusiano wetu ili niridhike kingono...so horrible!

Licha ya tatizo hilo nimekuwa nikivumilia tofauti alizonazo compared to my ex relations, ukweli ni kuwa he is not smart as my either he is romantic, nimejaribu kum-pimp atleast aweze kunivutia  lakini habadiliki, yaani ni kama anapuuzia vile.


Tatizo ni uoga wa kumuacha kwani ataniona kama namkimbia kwa mapungufu aliyonayo kimwili na kikazi. Nisaidieni mwenzenu kwani nahisi nina mwanaume jina. Asanteni"

Nifuate ndoa nchi nyingine, niache ajira?-Ushauri

"Dada Dinah na wachangiaji wote, tafadhali naomba ushauri au mawazo kwani nipo kwenye kipindi cha kufanya maamuzi magumu.

Nina mchumba wangu ambae tunataka kufunga ndoa, lakini nitakapofunga ndoa nitalazimika kuhama kutoka Nchi moja kwenda nyingine na kuacha ajira yangu.

Kinachonichanganya hasa ni suala la kuacha kazi, yaani mawazo juu ya hilo hunipa maumivu ya tumbo na huonga huniingia.

Naomba ushauri kutoka kwa yeyote aliyepitia hii hali katika maisha yake, asanteni"

Nahisi Bf hajali, je nifanye nini?

"Da Dinah pole na majukumu, mimi nina tatizo kidogo na boyfriend wangu wa miaka 34. Tumefahamiaka kwa muda wa miaka 3 na tumekuwa wapenzi kwa miezi 8.
Kipindi chote hicho sijawahai kufika kwake wala kukutana na ndugu yake mmoja, mawasiliano ni ya tabu hata nikianza kumshirikisha jambo langu huonyesha kama vile hana interest. Kwa kifupi I dont feel secured with him.
Je! nifanye nini kuimarisha uhusiano wetu kama kuna hiyo nafasi? Maana nikimwambia kuhusu tabia yake hiyo huwa anasisitiza kwa kusema kuwa ananipenda no matter what na atajirekebisha.
Kweli huwa anabadilika lakini mabadiliko hayo hayadumu muda mrefu, je napaswa kufanya nini?"
Dinah anasema: Asante kwa mail, Kutokana na maelezo yako inaonyesha kuwa mpenzi wako anaendesha maisha mengine ambayo hayuko tayari kukushirikisha kwa sasa na pengine kutokukushirikisha kabisa ikiwa utomwambia au kuonyesha nia ya kutaka kujua anapoishi (sio lazima ufike/uende).
Mabadiliko hayo ya muda mfupi ni ya kukusikiliza, kuonyesha interest kwenye issues zako na mawasiliano sio? Kama anaweza kubadilika kwa muda fulani basi ni wazi kuwa anajua kosa lake na anajitahidi kujirekebisha. Lakini hiyo isikufaye u-relax kwani huyo ni mpenzi wako wa miezi 8 na una haki ya kujua anapoishi japokuwa sio lazima uende nyumbani kwake mapaka mwenyewe awe tayari.
Huwezi juwa huenda anaishi na wazazi wake na hivyo sio heshima kukupeleka wewe nyumbani kwako, vilevile isije kuwa mpenzi wako anafamilia (miaka 34 kibongo-bongo wengi huwa tayari wanawake na watoto), ni vema kama utafanya uchunguzi kimya-kimya ili kujua ukweli kuliko kuendelea kupoteza muda na mtu ambae anaku-treat kama Kimada na sio mpenzi wake.
Ukipata ukweli kuwa jamaa hana familia (mke na watoto au mpenzi mwingine), basi hakikisha unamuweka chini na kuzungumza nae kuhusu uhusiano wenu na kuweka wazi kero zako, umuhimu wake kwenye maisha yako na mengine yote yalioujaza moyo wako na wote kwa pamoja kutatua tatizo kama wapenzi(ikiwa tu hana mtu mwingine).
Lakini kama ukigundua kuwa jamaa anamaisha mengine basi ni vema kuachana nae na wewe kupata nafasi ya kupenda na kupendwa na mkaka mwingine asie na "mzigo", Mkaka atakae weka akili yako na moyo wake wote kwako, Mkaka atakae jali hisia zako na kukusikiliza, mkaka ambae anajua umuhimu wa wewe kujua wapi anaishi....kwa kifupi ni makaka atakae kupenda kwa dhati na mwenye kuthamini uhusiano wa kimapenzi.
Kila la kheri!

Monday

Mjamzito, Kazini Moto nyumbani hakuna mapenzi, Nifanyeje?

"Habari dada Dinah,
Hongera kwa kazi kubwa unayoifanya ya kutuelimisha, ubarikiwe sana. Mimi nina umri wa miaka 28, ni mama wa mtoto mmoja na kwa sasa ni mjamzito.

Dada Dinah ninapitia kwenye kipindi kigumu kwani baba mtoto hanijali kabisa yaani hajishughulishi kunisaidia kitu chochote na anapachukia nyumbani. Hana mapenzi na mimi na nimeacha kazi baada ya manyanyaso kazini.

Maisha yangu yamekuwa na huzuni kubwa, najiona nina bahati mbaya nasijui nifanyeje? Mume wangu hana muda wa kuongea na mimi, nashindwa hata kula chakula vizuri. Naombeani msaada wa mawazo na namna ya kumfanya mume wangu anijali na kunionyesha mapenzi kipindi hiki cha ujauzito."

Dinah anasema: Pole sana, kwakweli ni kipindi kigumu kwani sasa najua mtu unavyojisikia unapokuwa mjamzito. Ni ngumu kuamini mume anaweza kumfanyia mkewe vitendo hivyo.

Nashindwa kujizuia kuuliza maswali hili:-
Kabla hujashika Ujauzito huu wa pili mliwahi kujadili suala la kuzaa mtoto wa pili au mimba imetokea tu bila kupanga?

Mimi nakushauri uzungumze na Mama mkwe wako kuhusu tabia/vitendo vya mume wako na yeye anaweza kuzungumza na mwanae (lazima atamsikiliza mama yake) na wakati huohuo zungumza na mama yako mzazi wa ndugu yeyote wa karibu kutoka upande wako na wote kwa pamoja wanaweza kuitisha mkutano/kikao.

Ikiwa mumeo ataendelea na tabia yake baada ya kikao cha familia zote mbili, usilazimishe sana na badala yake wewe tafuta namna ya kurudi nyumbani kwenu/kwa wakwe (inategemea na taratibu za huko uliko olewa) kwajili ya mapumziko mpaka utakapojifungua.

Ujitahidi kula vizuri na kujitahidi kuondoa mawazo ili usiharibu afya yako na ya mtoto tumboni. Baada ya kujifungua utakuwa na nguvu ya kukabliana na mumeo uso kwa uso na kujaribu kurekebisha tofauti zenu.

Sasa hivi jitahidi ku-focus kwenye afya yako na afya ya mtoto alafu hayo mengine yafuate baadae. Mungu akutie nguvu, akupe amani na ujasili ili uweze kujifungua salama.

Kila la kheri!

Thursday

Nini cha kuzingatia siku ya kwanza?

"Habari za asubuhi dada Dinah, pole na kazi. Nilikuwa naomba mnisaidie mawazo yenu. Mimi ni mwanamke ambae nasoma Chuo kwa sasa na nina maswali yafuatayo:-




1-Sijawahi kufanya tendo hata sikumoja na nina hamu kweli ila tatizo naogopa, naomba masaada.




2- Je! nitakapoamua kufanya ni mambo gani ya kuzingatia kwenye ile siku ya kwanza maana sijui kitu.




3-mambo ya kitandani sijui kabisa, naomba mnipe mastaili ya ukweli mpaka mwenyewe achanganyikiwe.




4-la mwisho da Dinah kama unaweza kunisaidia picha za watu wanafanya majambozi hapo utakuwa umenisaidia.




Kazi njema"

Tuesday

Nikisema sina hela ananuna, busu, kumbatio ni tatizo, nimbadilishe vipi?

"Hi da Dinah

Pole na hongera kwa kutoa elimu kwa vijana wa kitanzania. Mimi ni kijana wa miaka 23 na ni muajiliwa wa kampuni moja hapa Tanzania, tatizo langu ni kutopata mpenzi anayejali na kuthamini hisia zangu .



Natamani kuwa na mpenzi anayeendana na mitazayamo yangu ya kimaisha, kwa sasa ninae mpenzi lakini ni mtu anayependa pesa zaidi, siku ukimwambia huna basi atanuna na wakati mwingine anasema kuwa anahisi humpendi.



Na mbaya zaidi huwa hapendi kutoka na mimi ila marafiki zake its okay na hata hugs and kisses huwa kwake ni tatizo.Niini nifanye niweze kumbadilisha au niachane nae na kupata yule anayeendana na hisia nizitakazo? kwamba tupendane na tuendane kwenye masuala ya kimaisha?



Kwasababu wakati mwingine nahisi kuwa labda nina mkosi na sitokuja pata chaguo la moyo wangu nitakae mpenda na yeye anipende na sio kupenda pesa zangu."



Asaliti ndoa yetu usiku asubuhi anaenda kuhubiri neno la Mungu-Nimfanye nini?

"Mimi ni mwanamke ambae niko kwenye ndoa miaka minne sasa. Ila ninatatizo naomba mnipe maoni na ushauri. Mume wangu ambae nilimpenda kupitiliza nimegundua amekuwa akitoka nje ya ndoa yetu pale nilipoanza kumufatilia sana ingawa alikuwa mjanja sana.



Kinachoniuma saaana huyo mwanamke aliekuwa akitoknae nilianza kumuhisia kipindi hatujafungandoa, kila siku nilikuwa nikiona msg zake akimtukana mtu fulani ila nikijaribu kumuuliza mume wangu anasema kuwa ni mambo tu ya kazini. Lakini kila nilipokuwa nikiona msg nahisi kusutwa!



Hivi sasa tuna watoto wawili na nilikuwa muamini zaidi mume wangu nakila ninapo shitukia ishu kuwa labda anatoka kusaliti ndoa yetu na kumhoji kama ni kweli, mume wangu anakasirika na kuniomba nipige magoti nisali na kuomba Msamaha.



Nilikuwa nikifanya hivyo na hata yeye kuomba pamoja nami huku maombezi yake yakiwa Mungu atupe tuweze kuaminiana. Hajawahi kupunguza mapenzi kwangu wala kuonyesha ila siku moja nimekamata msg nyingine nikajifanya mimi ni mume wangu na hapo ndipo nilipogundua mwanamke huyo anavyo enjoy na mume wangu.



Kinachoniumiza sana alikuwa akitumia rafiki yake huku mara nyingi nyingi kujifanya kuwa ni mgonjwa anahitaji kwenda hospitoli anadai asindikizwe na mume wangu kumbe ilikuwa njia yakumtoa tu. Akitoka asubuhi kusaliti ndoa yetu anahubiri Kanisani kama kawaida na huku akisukuma Injili.



Yaani nikifikiria hapo nahisi kumchukia, hata mida mingine sijisikii kumpikia kutokana na ahadi nyingi tele tele na huku akionya watu wengi kuhusu ndoa. Naombeni jamani mniambie nifanye nini kumsamehe sijamsamehe ila aliishaomba msamaha nakunieleza kuwa kila nililoligundua ni ukweli! ninaumia sana.



Nilimwambia asubiri nitampa jibu. Sasa mawazoni mwangu najiandaa na nikipata kazi nitamuacha kwani nikifanya uamzi mapema naweza kuumia sijuwi niko sahihi au nakosea?



Hii yote ni kwasababu hakuna njia nyingine ya kumuamini hasa pale anaponiambia yote "tumkabizi Mungu" nahisi hata hilo jina asiwe analitaja. Nikiwa mbali na yeye ninajihisi kufurahi nikimuona nahisi kujinyonga sasa jamani mnasemaje hapo naombeni ushauri wenu. Asante"



Monday

Naogopa mkewe asije kujua uhusiano wetu, nifanyaje?

"Thanxs dada dinah kwa ushauri unaotupa wanawake wenzio. Ila dada naomba ushauri wako pamoja na wachangiaji wengine. Mimi nina mahusiano na mume wa mtu na nampenda sana naye ananipenda sana na pia ndio mwanaume wa kwanza kwangu.

Ila dada naogopa mke wake asije kujua, huwa namwambiai huyu mwanume lakini yeye ananipa moyo kuwa hilo halitotokea. Huyu mwanaume ananitunza vizuri tu na pia kaninunulia nyumba na full furniture. Nyumba hii iko mbali na anapoishi na familia yake.

Tatizo wakati ninapomuhitaji huwa simpati kwani unakuta muda mwingine yupo bisy na kazi au familia yake. Dada nifanye nini wakati nampenda sana?"

Dinah anasema:Natambua kuwa hii Post itawakera wengi, Mimi binafsi sikubaliani na tabia hii kwani kitendo cha kutoka na mume wa mtu ni Kosa kubwa. Lakini tukumbuke matusi na maeno makali hayatosaidia huyu dada kufanya uamuzi wa maana. Tafadhali mshauri kwa busara bila kum-attack huyu Binti.
Asante!

Sunday

Kitu kidogo tu anitishia kuachana, nimuache kweli au?-Ushauri

"Habari yako dada Dinah???
I hope upo pouwa sana and well, thanks for everything you have been taught us and may God Bless u always...

My name is (dinah kahifadhi jina) am Tanzanian but currently am in Malaysia studying, I am having a problem with my GirlLover and I completely dont understand her! My girllover lives in Tanzania and am here (in Malaysia). Every end of the year I go to Tanzania to see her, I have no other reasons for me to go there apart from seeing her.

Anapenda sana kunitishia kuniacha yaani kitu kidogo tu atanuna na kunitumia msg'z kama "maisha mema na usinipige simu wala kuni text" tena kwa kosa dogo sana ambalo liko juu ya uwezo wangu, kosa lenyewe ni kutopokea sms zake kwavile network ilikuwa inamatatizo.

Pia nikifanya kosa bahati mbaya basi atanuna wiki moja au mbili, yaani nisimsemeshe. Lakini yeye akifanya kosa kama nililofanya mimi na akiomba msamaha ni hapo hapo umsamehe na usimpomsamehe hapo on the spot ataanza kunitishia kuwa "basi kama huwezi kusamehe on the spot tuachane" na kosa hilo hilo nilikifanya mimi naweza kuomba msamaha kwa wiki mbili mfululizo lakini hanisamehei and it's annoying.

Nampenda sana na nimeshamtambulisha home na yeye ameshanitambulisha kwao na familia zetu ni friends lakini hii tabia yake inaniboa sana, pia hivi vitisho vyake vya "tuachane" vinanifanya nisisome kwa raha yaani performance inashuka.

Nampenda sana na I can't afford to loose her... sasa nifanye nini ili aache kunitishia hivo vitisho au njia ni kuachana nae na nikiongea nae sometimes anakubali kuendelea na mimi but kitu kidogo anarejea hiyo tabia.

Naomba ushauri jamaa, ni kuachana nae au njia ni ipi hasa?"

Niliolewa nikiwa nampenda wa zamani, nimuepuke vipi?

"Hi Dinah na wachangiaji wengine,
Kwa kweli napata tabu hebu nisaidie kwa hili; Mpenzi niliekuwa nae zamani nilimpenda sana lakini kwa bahati mbaya tukakosana. Sasa nimeolewa as you know ndoa hupangwa na Mungu lakini bado nampenda na huku nina mume what should I do kuepukana nae huyo wa zamani"?

Wednesday

Mpenzi hanijali, hanithamini tena,nifanyeje?

"Dada Dinah pole na kazi za kutueimisha sisi tulio katika ulimwengu huu wenye raha na karaha zake. Mimi ninaishi na mwanaume ambaye hatujafunga ndoa ila tumezaa mtoto mmoja na ilibidi tuanze kuishi pamoja kabla ya ndoa kwa sababu ya kusaidiana malezi ya mtoto.

Kikubwa kinachonikera kwake ni kwamba hanijali tena, hanithamini wala haoni na mimi ni sehemu ya maisha yake,nasema hivyo kwa sababu kila ninapohitaji msaada wowote toka kwake hanisaidii kabisa.

Ukija katika suala la kugonoka jamani mimi mwenzenu naweza kaa hata mwezi mzima hajanigusa wala nini na tunalala kitanda kimoja kila siku na hata tuki sex yeye anafanya mradi yafike basi na si kutombana ili kila mmoja wetu aridhike nakumfurahia mwenzie.

Kingine, anachelewa kurudi nyumbani yeye ni mfabiashara k/koo na duka anafunga saa kumi na moja kamili ila mpaka afike nyumbani ni saa 3-4 au hata saa 5 usiku nimeshaongea naye lakini wala hanielewi kabisa.

Jamani naomba ushauri wako dada na wachangiaji wengine kwani nahisi kutokumpenda tena, mwenzenu nifanyeje ili tuwe na mapenzi kama walivyo wengine? Poleni kwa msg ndefu".

Tuesday

Miaka 10 kwenye uhusiano na mtoto moja bila ndoa, je nimuache?

"Habari dada Dinah,
Pole kwa majukumu na hongera kwa kuelimisha jamii. Mimi ni mdada nina miaka 32 toka Arusha. Nina uhusiano na mwanaume kwa muda wa miaka 10 na nimezaa naye mtoto mmoja.

Kabla ya kuwa na mimi huyu mwanaume alishawahi kuwa na wanawake tofauti na amezaa watoto wawili kila mmoja na mama yake.Katika uhusiano wetu tumefanikiwa kununua nyumba moja yeye alichangia hela nyingi kuliko mimi ila mimi niliifanyia ukarabati mkubwa, hati nilisaini mimi na alinikabidhi.

Nyumba hiyo ninaishi mimi na mtoto wangu, yeye anaishi nyumba nyingine na watoto wake hao wawili na huwa nafika hapo ila hajawahi kunikaribisha ndani wala kunitambulisha kwa watoto wake.

Alishawahi kunitambulisha kwa baadhi ya ndugu na rafiki zake na kwa staff wenzie ofisini. Huyu mwanaume amekuwa msaada sana kwangu na familia yangu, kwetu wanamfahamu kama baba wa mtoto wangu.

Mimi nataka kuachana na huyu mwanaume kwa sababu naona ananipotezea muda pamoja na kwamba ananisaidia. Ila kuna ndugu zangu wananishauri nisimuache. Mimi binafsi naona hayupo serious kwani angekuwa serious na mimi au kuwa na mpango na mimi sidhani kama angekaa nyumba tofauti na mimi.

Pili, muda wa miaka kumi ni mrefu sana kama angekuwa na mpango na mimi nadhani angenioa. Nimejaribu kuongea naye mara nyingi takribani miaka 6 sasa kuhusu suala la ndoa lakini kila siku jibu lake kuwa ana mipango anaikamilisha kwanza lakini haniweki wazi ni mipango gani hiyo.

Tatu, Pamoja na kwamba huwa anakuja kwangu na tunafanya mapenzi lakini si kivile na mara nyingi huwa nakuwa mpweke, kwa kifupi huwa anakuja anavyotaka yeye so nakuwa sipo uhuru na mapenzi.

Nne hakuna relation yeyote kati ya mtoto wangu na watoto wake yaani kwa kifupi mambo yake mengi haniweki wazi hizo ndio sababu ambazo zinanifanya niamue kuachana naye pamoja na kwamba ananihudumia kwa kila kitu.

Binafsi bado nampenda sana, tena kwa dhati ila kwa kweli nimechemsha kwa hilo. Nilishawahi kumwambia kuwa nimechoka na ninataka tuachane, aliumwa presha mpaka akalazwa. Toka nimekuwa na uhusiano naye sijawahi kuwa na mwanaume mwingine nje ya uhusiano wetu na nilishawakataa wengi kwa ajili yake lakini kwa sasa nimechoka.

Hofu yangu ni kuwa baada ya kuachana itabidi tuuze hiyo nyumba na nitahangaika na makazi mimi na mwanangu. Pia nahofia usalama wake maana bado atabaki kuwa baba wa mtoto wangu.

Ninaomba wana-blog wenzangu mnishauri katika hili ili niweze kuchukua maamuzi sahihi. Samahanini sana kwa maelezo yangu marefu, Madada wa Arusha".

Monday

Wazazi na jamaa wanasema nitafute msomi kama mimi, does it matter?

"Pole na kazi dada Dinah, kwanza nitangulize shukrani zangu kwa watu wote wanao toa ushauri na kutuelimisha mambo mbali mbali katika hii blog. Mimi ni mwanamke mwenye umri miaka 25, nimekuwa na boyfriend wangu kwa muda wa miaka 6, nilianza mahusiano nae nikiwa namalizia kidato cha nne, ila kwa sasa nipo chuo nachukua masters degree.

Mimi na boyfriend wangu huyu tunapendana sana, na pia namsaidia mambo mengi sana ya kifedha na hata yakimaisha (nikimaanisha ushauri), kwani kwa bahati mbaya hakufanikiwa kwenda shule kutokana na matatizo ya kifamilia, elimu yake ni ya kidato cha nne.

Hiyo yote ni kutokana na Wazazi wake kutojishughulisha nae tokea zamani, hawakujali suala la elimu, kutokana na hili alipitia maisha magumu saana kiasi cha kumfanya aanze kufanya dili mbalimbali ili apate hela za kuendesha maisha, na pia aliweza hata kupanga chumba akawa anaishi mwenyewe na kununua assets mbalimbali za nyumba.

Kwa ujumla ni mtu ambae anajipenda na anapenda maisha mazuri tatizo ni uwezo tu na kazi ya maana ambayo itakidhi mahitaji yake yote. Pamoja na hili anasaidia hata ndugu zake pia. Hivi karibuni mambo hayamuendei vizuri kabisa japo hajakata tamaa.

Anajitahidi hivyo hivyo, kwa sababu hii mara nyingi ananiomba mimi nimsaidie kifedha kwa sababu nampenda inabidi nimsaidie nimpe hela za matumizi na muda mwingine hata za kulipia nyumba. Na fanya hivyo kwasababu nampenda, na yeye ananipenda, yupo tayari hata kesho kuishi na mimi.

Swali langu lina kuja hivi, mimi nimesoma nategemea kupata master degree yangu miezi kadhaa ijayo, kwa ujumla namshukuru Mwenyezi Mungu ninamahitaji yangu yote, ila tatizo huyu boyfriend wangu, hajasoma ila ni mtu ambaye anajitahidi hivyo hivyo sio mvivu anapenda maisha mazuri, ila watu wanasema hatutadumu kwa muda mrefu kutokana na tofauti zetu, je mnasemaje kwa hili?

Swali la pili ni hili, tumejuana kabla hata sijaanza chuo, kwa kipindi chote hicho tulikuwa pamoja mpaka sasa nategemea kumaliza masters tupo pamoja, na pia ndio boyfriend wangu wa kwanza sijawahi kuwa na mwingine, je mnanishauri vipi hapa?

Kwani baadhi ya watu wananiambia nitafute mtu aliesoma kama mimi kwani tutaelewana zaidi kimaisha. Kuhusu suala la wazazi, wazazi wake wananipenda saana, ila tatizo lina kuja upande wa wazazi wangu wanataka nitafute msomi mwenzangu, ila kwa mimi siko tayari kwani nampenda huyu nilionae.

Kwasasa haijalishi kwani nipo tayari kumsaidia kwa lolote ili tu awe na maisha mazuri. Je hii ni sahihi? Naombeni ushauri wenu, je kuna future hapa kweli au tunaforce mambo tu kwa muda kwani yatakuja nizidia huko baadae kama asipo pata kazi au biashara ya maana.

Naombeni ushauri wenu na mtazamo wenu.

Dada K".

Dinah anasema:Asante mdogo wangu, natumaini kuwa umefanyia au unaendelea kufanyiakazi maelezo mazuri kutoka kwa wachangiaji, yasome yote kisha uyachanganue alafu uchanganye ndio ufanye uamuzi.

Amemdis mdada aliekuwa nae kwa miaka 4, je atafanya the same kwangu?

"Pole na kazi dada,

Naomba unishauri kitu, mimi nina boyfriend wangu ambaye ametoka kwenye mahusiano na msichana waliedumu naye miaka 4.Hofu yangu je atanidis na mimi kama alivyomuacha huyo mwingine baada ya muda mrefu?


Sasa hivi simuelewi-elewi kwani anapenda sana kushika simu yangu na kusoma sms zangu tena wakati mwingine sms inaingia hata mimi sijaisoma tayari yeye anasoma.


Juzi nilienda kulala kwake lakini hakuonyesha kunijali, je ni dalili kuwa atakuwa na mwingine? je niachane nae? au niendelee nae lakini nisiwe naenda kwake?


Nilijaribu kumuuliza kama anamalengo yeyote na mimi,akasema ndioa anamalengo mazuri. Hiyo juzi nilipokwenda kwake nilimfulia nguo na kwa bahati mbaya zikaibiwa.


Nimemtumia sms lakini hajanibu hadi this time, je na mimi nikae kimya au nimtafute? Nitashukuru nikipata ushauri wako dada na nitaufanyia kazi ushauri wako.Please usiniweke kibarazani.
Kazi njema, be blessed"

Dinah anasema:Asante sana kwa mail yako, namshukuru Mungu ananipa nguvu kila siku.

Wengi wetu tunapoingia kwenye mahusiano mapya ni wazi tumeacha au tumeachwa. Kuachwa kwa mtu hakukuhusu wewe,japokuwa ni muhumu kujua nini kilitokea au kusababisha mpaka wakaachana ili ikusaidie wewe kuepuka au kujua namna ya kukabiliana na same tatizo kama litajitokeza.


Kwa kawaida humchukua mtu yeyote muda mrefu kuwa tayari kupenda tena na kujenga uhusiano mpya baada yakutoka kwenye uhusiano wa zamani.


Sina hakika mpenzi wako amekuwa na wewe baada ya muda gani tangu aachane na huyo mpenzi wake wa awali, lakini kutokana na ulichokisema hapa(vitendo vyake) inaonyesha jamaa bado hajapona maumivu ya mapenzi aliyopata kabla yako.


Kutokana na maelezo yako ni wazi kuwa unaharaka ya kufunga ndoa na wakati huohuo unaogopa kuachwa ukiamini kuwa "kama aliacha yule, hatamimi ataniacha". Sio lazima iwe hivyo.


Unapoingia kwenye uhusiano unatakiwa kuzingatia nini utawekeza kwenye uhusiano ili uhusiano na mpenzi wako kuwa Imara na uliotawaliwa na mapenzi. Huitaji kuishi kwenye hofu ya kuachwa au kufikiria maisha yake kabla yako!


Kosa dogo ulilofanya ni kuanza kwenda nyumbani kwake na kumfanyia shughuli kama vile wewe ni mchumba/mkewe, mwanaume hafuliwi wala kupikiwa mara kwa mara ikiwa uhusiano bado ni mchanga, unaweza kumsaidia vijishughuli kwa mapenzi lakini isiwe kila weekend, utakuwa unamugopesha na atakudhania kuwa unataka kufanya nyumbani kwake ni kwako.....hii can scare him off.


Vilevile hukupaswa kumuuliza malengo yake kwako na badala yake ungetumia mbinu nyingine ili kujua msimamo wake juu ya uhusiano wenu kama wapenzi, kumbuka uhusiano unajengwa na watu wawili.


Hawezi kuwa na malengo kwako kwani wewe sio mwanae bali ni mpenzi wake, lakini anaweza kuwa na malengo fulani juu ya uhusiano wenu na wewe unapaswa kuwa na malengo fulani kwenye uhusiano huo ila nina uhakika yeye hajawahi kukuuliza unamalengo gani kwake....has he?


Huyu mwanaume inaonyesha kuwa aliachwa(wanaume wengi hawapendi kusema waliacha kwa vile ni aibu kwao)kutokana na kitendo chake cha ku-withdraw na kuangalia-angalia simu yako ni dalili tosha kuwa jamaa alitendwa au niseme alikuwa cheated na hivyo inakuwa ngumu kukuamini na ndio maana anafuatilia sana SMS na simu ili asije umizwa tena.


Kitendo cha yeye kutokukujali ulipokuwa kwake inawezekana alikuwa amechoka au anamawazo(kama ulikuwa unataka ngono), na mwanaume anapokuwa ktk hali hiyo huwa ngumu sana kungonoka lakini kwa kumsaidia (kuzungumza nae na kumpa matumaini, kumpoza, kumliwaza n.k.)anaweza kuwa sawa na tendo likafanyika.



Nini cha Kufanya: Mtumie ujumbe au mpigie simu na kumuomba msamaha kwa kusababisha nguo zake kuibiwa. Najua kosa sio lako lakini omba radhi kwa hilo, kwani anaweza kuwa na hasira kuwa usingezifua zisingeibiwa hasa kama uliamua kufua bila yeye kutaka ufanye hivyo....hilo moja.

Pili, mdogo wangu punguza safari za kwenda kwake na badala yake mpigie zungumza nae kwa simu na kupanga mihadi ya kukutana mahali au kwenda kutembea sehemu na ikitokea anakualika kwenda kwake baada ya matembezi au chakula then nenda kwake lakini usilale unless anaomba ufanye hivyo.


Unapokuwa huko kwa Jamaa usijipe shughuli kama vile wewe ni mchumba/mkewe tayari. Unaweza kuandaa labda Chai asubuhi na kutandika kitanda kwa vile mmekitumia, pia unaweza kusafisha vifaa ulivyotumia lakini sio unafanya usafi nyumba nzima na kumfulia juu.

Muonyeshe mapenzi ya dhati ulionayo bila kuhoji malengo yake, hakikisha unampatia ile hali ya kukuamini kuongeza mawasiliano Mf:kwa kumueleza mipango yako ya siku na kuomba yeye akueleze mipangilio yake ya wiki au siku na hivyo kujua lini mtakutana tena kama wapenzi n.k

Mfanyie mambo yakingono na ya kimapenzi (nje ya kitanda) na kitabia ambayo unauhakika hakuna mtu amewahi kumfanyia.....njia rahisi yakujua ni kuwa wazi kwake na kumhoji kimahaba na yeye atakuambia anapenda Binti mwenye tabia gani, nini hawaji kufanya lakini angependa kujaribu/kukifanya kingono n.k.

Acha kuwa na haraka za kuolewa, furahia uhusiano wako kama ulivyo na hakikisha unafanya mambo ya kimapenzi ili atangaze ndoa yeye mwenyewe bila kusukumwa na maswali yako kuhusu malengo yake.

Kumbuka ndoa nzuri ni ile inayotokana na uamuzi wa watu wawili wanaopendana kwa dhati na wenye lengo la kuishi pamoja maisha yao yote yaliyobaki.

Kila la kheri.

Sunday

Ndoa ni Mwaka huu! Mwenzangu anatereza na mdada nimjuae!

"Habari yako,
Naitwa M*(Dinah amehifadhi jina) na ninaishi Sinza,
Kwa upande wangu sina swali ila ninapenda kupata ushauri kutoka kwako.
Nina umri wa Miaka 30 na nipo katika uhusiano kwa takribani miaka miwili na ninatarajia kufunga ndoa mwezi huu wa tano.

Tatizo linakuja kwa huyu mwenzangu anajihusisha kimahusinao na dada mmoja ambae namfahamu na kila nikimuuliza anakataa lakini Ofisini kwa huyu mwenzangu wanafahamu uhusiano wao, yeye na huyo mdada mwingine.

Sasa nashindwa nifanye nini na nikangalia ndoa ipo karibu,
naomba ushauri wako/wenu.

Hivi sasa amebadirika sana kitabia."

Nimeshika Mimba, Je nitamwambiaje mama?

"My dear,
mimi ni msichana wa miaka 25, bado nipo chini ya himaya ya bi mkubwa, nimepata mimba na siku zote nasema sitatoa mimba. Sema bi mkubwa wangu nitamueleza vipi? Naombeni msaada jamani tafadhali dada dinah na wachangiaji wengine kwani nipo njia panda.

Boyfriend yeye yu tayari kuwa baba japo wote bado twamalizia masomo si fikirii sana juu ya yeye kwa sasa, yeye si ngumu kujadiliana naye isipokuwa mama yangu, sijui nianzie wapi kumwambia??? msaada tafadhali tafadhali...".

Monday

Mume wangu anatereza nje na "dada" zake na kuzaa ovyo, nifanye nini?


"Dada Dinah,Salaams.

Naona nianze moja kwa moja matatizo yangu. Mimi ni mwanamke umri miaka 38, nimeolewa miaka mitatu iliyopita, sina mtoto. Ninaishi na mume wangu pamoja na binti wa mume wangu ambaye anasoma boarding.


Tatizo kubwa ni kuwa nimeshindwa kumzalia mtoto mume wangu na hivyo ume wangu kazaa na housegirl wetu. Kabla hajampa ujauzito, aliomba nimfukuze akidai hana adabu. Baadaye nikaambiwa na majirani kuwa housegirl wetu ana mimba. Sikujua ni ya nani hadi hapo baadaye.


Baada ya muda nikagundua kuwa mume wangu anatembea na msichana jirani aliyekuwa akimuita dada kwa vile wanatoka sehemu moja. Dada huyo alikuwa akija kututembelea na wakati mwingine akitusaidia kazi wakati mimi nikisafiri. Kazi yangu ni ya kusafiri na baadaye nikahamishiwa Wilayani kabisa.


Kurudi kwangu nyumbani ni siku za weekend tu.Kumbe yule dada akawa anakuja kulala na mume wangu usiku. Nikaambiwa na majirani. Nilipomuuliza kama kawaida alikataa. Yule mwanamke baada ya kuona nimegundua amehama mkoa na kuhamia Dar.


Hivi karibuni nimetumiwa sms na msichana akiniambia kuwa ana mimba ya mume wangu na kuwa kaipatia nyumbani kwangu kwenye kitanda changu na kuwa eti nisubiri kuletewa watoto. Nilipofuatilia nikagundua kuwa huyo msichana ni mwanafunzi wa Sekondari na wanatokea sehemu moja pia na mume wangu.


Nilipomuuliza mume wangu alikanusha kama kawaida. Lakini baadaye nikapata taarifa kuwa mume wangu kampiga sana yule msichana hadi kulazwa Hospitali kwa kuwa eti kanitumia sms. Nilipomuuliza alikubali, halafu baadaye alikanusha akidai kuwa ingekuwa ni stori ya kweli basi angeshitakiwa police.


Kweli mambo ni mengi, mojawapo likiwa la mume wangu kutopenda kabisa mimi kugusa simu yake. Nilishakuta sms za wanawake wawili kwenye simu yake, mmoja ninayemfahamu. Hata nikiamka kujisaidia usiku, yeye anashituka akihofia simu zake zisiguswe. Mume wangu anao marafiki wengi wa kike yeye akiwaita ni dada zake na wengi wa kabila lake la Wapare, ambao wengine ndio hao anaotembea nao.


Sasa mimi sielewi hili kabila, nimegundua kuwa ni Malaya sana, hadi najuta. Mimi nafanya kazi na kipato changu ni kikubwa kuzidi cha mume wangu. Namnunulia nguo nzuri anapendeza, nimemsaidia kumjengea nyumba mama yake na sasa tunajenga ya kwetu. Nampenda sana mume wangu na yeye anadai kunipenda.


Kutokana na hali hiyo afya yangu Kisaikolojia imeharibika, naombaeni ushauri wenu. mngekuwa ni nyie mngefanya nini"?

Wednesday

Baada ya kutendwa ndoani, nachukia wanaume wote....nifanyeje?

"Pole na kazi ya kushauri,kuelimisha n.k jamii. Kwanza napenda kukupa kheri ya mwaka mpya dada DINAH. Mimi ni mwanamke wa miaka 29 ingawa mapema sana this year natimiza 30. Nilipokua na umri wa miaka 24 nilibahatika kupata mchumba na hatimaye kuolewa na kupata mtoto wa kiume, Kwa sasa nimeachika. Wakati wa Uchumba na mwanzoni mwa Ndoa Mume wangu alikua mchaMungu wa kweli kiasi kwamba tulikua tunagombana nisipo swali[ni waislam] Hali ya kimaisha niliyomkuta nayo mume wangu haikua nzuri, ikabidi Baba yangu atusaidie mimi na mume wangu. Hivyo mambo yakawa mazuri tena sana kwani tulianzisha Biashara zetu ambazo kiukweli zilitukubali. Baada ya mambo kuwa mazuri, mwenzangu akaanza kubadilika akawa mlevi,wanawake ndio usiseme! Nilipokwenda nyumbani kujifungua, huku nyuma akawa anaingiza wanawake kila siku tena kwa kuwabadilisha. Niliporudi nikapewa habari zile nikamuuliza akakataa. Basi nikaanza kuchunguza na Mungu aliniwezesha nikabaini ukweli niliyokua nikiambiwa. Kwavile nilibaini mwenyewe,nilikua na vielelezo nilipompatia alikua mpole na kukiri ni kweli akaomba msamaha nami nikamkubalia. Ila kumbe hakua ameacha tabia yake. Nikawaeleza wazazi wake wakamuita na kumsema hakusikia. Tukapelekana BAKWATA akaitwa akasemwa na wakamwambia kwavile amekua mchafu wa tabia kwanza tukapime afya lakini yeye akakataa na kusema kama ni hivyo bora anipe Talaka yangu. Mimi tangu nitoke kujifungua sikua nimeshiriki nae tendo la ndoa na hata baada ya kumsamehe pia sikutaka kushiriki nae kwani nilikua nikimwambia tukapime ndio tushiriki. Kinachonifanya niombe ushauri ni kwamba kwa sasa simuamini mwanamme yeyote naona wote ni wadanganyifu. Niliwahi kupata mwanamme ila aniponitamkia kunioa nikamchukia na kuachana nae. JE,NIFANYEJE?" Dinah anasema: Heri ya mwaka mpya kwako pia, asante sana kwa kuniandikia na kwa uvumilivu, vilevile nakupa pole kwa yote uliyokabiliana nayo katika umri mdogo. Hongera sana kwa kuwa na msimamo wa kugoma kushirikiana nae kimwili mpaka mkapime afya zetu....well technically afya yake yeye mwenye tabia chafu. Hakika, ukiumwa na Nyoka mara moja lazima utaogopa sana hata ukiguswa na jani. Unahitaji muda kuweza kumuamini mwanaume na hiyo ni hali ya kawaida kabisa, wala usihisi presha kutoka kwa Jamii inayokuzunguuka kuwa una mkosi au huwezi kuolewa tena(Hakuna kitu kibaya kama kufungandoa ili kuridhisha Ulimwengu, kumbuka walimwengu hawana wema na huwezi kufurahisha kila mtu kwenye jamii yako). Kitendo cha kuanza kutoka na wanaume wengine kinaonyesha umeanza "kupona" maumivu aliyokupa Mumeo wa ndoa, lakini linapokuja suala la kuwa na uhusiano wa kudumu unashindwa kuji-commit kitu ambacho kinaeleweka. Nini ch akufanya: Usiwe na haraka na usijali wasemayo Walimwengu kuhusu ndoa ya awali au lini utaolewa tena, nenda taratibu na tumia muda wako vema huku ukifurahia maisha kama mwanamke anaejitegemea na mwenye uzoefu (ndoa yako iliyopita ichukulie kuwa ni uzoefu unaokufanya ujue utakacho maishani mwako na sio Mkosi). Ikitokea tena umemdondokea mwanaume kimapenzi, hakikisha unakuwa muwazi kabla uhusiano haujaota mizizi. Mueleze mpenzi huyo nia yako(kwamba huna haraka sana kufunga ndoa). Unatakiwa kuwa a bit smart unapoliweka hili suala wazi kwani kamamwanaume ni mjinga-mjinga anaweza kudhani kuwa unataka akuchumbie kumbe wee huna mpango huo. Sasa unatakiwa kujiwekea malengo, mfano:- Napenda kutekeleza hili na lile kabla sijaamua kutulia na kujenga familia n.k. Natumaini maelezo ya wachangiaji na haya yangu yatakuwa yamesaidia kiasi fulani kujua nini chakufanya, ila kubwa zaidi ya yote ni kujipa muda na kufurahia maisha kama Mdada/mwanamke/single.....kumbuka umeolewa ukiwa na miaka 24, huu ndio u mri wa kufurahia "uanamke"....kwamba wewe ulitoka kuwa Binti wa moja kwa moja na kuwa mke wa na Mama wa.....hujawahi kuwa wewe bila kuwa chini ya.... Kila la kheri.

Monday

Haya nimerudi full time, Shukrani za dhati kwa ushirikiano na uvumilivu!

Habari za siku nyingi mpenzi msomaji, mchangiaji, mtembeleaji na wewe ulieendelea kunitumia maswali japokuwa sikuwa na muda wa kuyajibu kutokana na sababu nilizozieleza kwa kifupi (kulia hapo kwa juu).

Kwa kawaida blog hii huwa haihusishi masuala yangu binafsi isipokuwa yanayohusu maisha halisi ya kimapenzi ya mtu yeyote, lakini kutokana na nitakachogusia hapo chini, nimeshindwa kujizuia bali kukushirikisha ili utambue kuwa Blog haikunishinda bali nilikuwa nakabiliana na mabadiliko ya Kimwili, Kisaikolojia na kihisia kutoka Dinah kuwa mama kwa mara ya kwanza.

Baada ya safari ndefu ya Ujauzito na mkanganyiko wa Homono zilizonifanya nichukie mambo yote yanayohusisha Teknolojia (ndio maana sikuweza kufanya kazi yangu hapa) yote kwa yote namshukuru Mungu nimejifungua salama mtoto wa Kiume siku chache zilizopita.

Mungu awabariki na awape moyo huo huo wa ushirikiano katika kujaribu kusaidiana ili kuendesha maisha ya amani, furaha na upendo kwenye mahusiano na ndoa.

Asanteni.

Thursday

Nianzie wapi Kisheria kumtaliki mume wangu?-Ushauri

"Kwanza napenda kukupongeza kwa kazi yako nzuri, pili mie nilitoa malalamiko yangu kuhusiana na mume wangu ambae hataki kunipa Talaka dada dinah, naomba unielekeze wapi naanzia kwenye vyombo vya Sheria maana issue nataka pia atoke kwangu.

Kuna baadhi ya watu wananiambia Mahakamani hawavunji Ndoa na wengine wananiambia inaweza pelekea hata Miaka miwili kila siku unapigwa Tarehe tu, sio siri dada Dinah ni kama naishi na Chui ndani ya nyumba, kwamba muda wowote anaweza akanibadilikia na kunila nyama"

Monday

Uhusiano una Mwaka, Ex wa Mpenzi amejifungua mtoto wake mwaka huu! Nifanyaje?

"Habari dada Dinah pole na majukumu ya kila siku,
mimi ni dada wa miaka 27 nina mchumba ana miaka 35 tumekuwa pamoja kwa muda
wa mwaka na miezi mitatu hivi. Nampenda sana mchumba wangu na yeye naamini ananipenda.

Tatizo limejitokeza hivi karibuni; ni kwamba kabla ya kuwa na mimi alikuwa na mwanamke ambaye alinishanitaarifu kuwa aliachana nae ndio maana mimi nikakubali na tukawa wapenzi. Sasa ananiambia kuwa huyo dada ana mtoto wake tena kamzaa this year, ina maana
hiyo mimba kapata wakati ndio tunaanza uhusiano wetu.

Sijasikia kwa mtu mwingine zaidi yake amesema eti nikisikia kwa watu na yeye
hajaniambia nitamuacha, amesema yeye ananipenda mimi na anataka niwe mke wake. Hapa nilipo nimechanganyikiwa mbaya zaidi badonampenda sana huyu kaka na sijui nifanyaje!

Yaani mpaka sasa sijamuelewa ananidanganya au ananipenda kiukweli, mwenyewe ananiomba msamaha sana kuhusiana na tukio la kuzaa na ex wake.

NAOMBA USHAURI WENU, nifanye nini?

Saturday

Nifanye nini ili mimi na mpenzi tukojoe pamoja?-Ushauri

"Hey Dinah pole sana kwa shughuli za mchana kutwa, pili asante sana kwa kutufundisha wenzangu na mimi ambao tumeanza malavidavi kabla ya kufundishwa Unyagoni. Wengine hatuna Mila za kuingizwa Unyangoni basi tuna taabu.

Mimi ni mwanamke wa miaka 29 nimeanza kungonoka nikiwa na miaka 26 na mwanaume wa kwanza ambaye ndio alinitoa Usichana wangu. Tulikuwa tunakutana kwa mwezi mara 2 hivyo tulikuwa hatuna muda wa kungoana vizuri.

Mwanaume huyu alikuwa anajipendelea yeye hana Commucation na mimi, alikuwa anataka anavyotaka yeye, baada ya muda fulani tukaachana. Sasa hivi niko na mwanaume mwingine ambae kwa bahati nina muda mwingi tu wa kungonoka naye ila tatizo langu kubwa mimi sijawahi hata siku moja kupata raha ya kungonoka.

Nasemea ile raha kama ninavyosikia kwa wenzangu au kwako unavyoandika ushauri kuwa unaweza mkakojoa kwa pamoja sijawahi hata siku moja! Mimi kukojoa kwangu mpaka mpenzi wangu anichezee K tena kwa muda mwingi sana mpaka namuonea huruma.

Basi kwa vile nadhania kuwa namchosha inabidi nimwambie tayari nimefika kumbe bado. Nashukuru sana mwanaume wa watu hapendi niondoke bila mimi kukojoa.Naomba ushauri nifanye nini na mimi niwe napata raha kama wenzangu?

Pili, nifanye nini ili na mimi niweze kumaliza pamoja na mwenzangu?"

Sunday

Nifanye nini ili nami nipate raha na Utamu wa Kungonoka?

"Hey Dinah pole sana ka shughuli na asante kwa kutufundisha wenzangu na mie ambao tumeanza malavidavi kabla ya kufundishwa Unyagoni, maana wengine hatuna Mila za kuingizwa unyagoni basi tuna tabu.

Mimi ni mwanamke wa miaka 29 na nimeanza kujihusisha na masuala ya kimapenzi na ngono na mwanaume wa kwanza nikiwa na miaka 26, tulikuwa tunakutana mara mbili kwa mwezi na hivyo hatukuwa na muda wa kungonoana vizuri. Mwanaume huyu alikuwa anajipendelea yeye kwani hakuwa na communication na mimi alikuwa anataka anavyotaka yeye.

Sasa hivi nimepata mwanaume mwingine na muda wa kuwa nae na kufanya mapenzi ni mwingi zaidi kuliko awali ila tatizo langu kubwa ni kuwa sijawahi hata siku moja kusikia raha ya kufanya tendo kama ninavyosikiwa kutoka kwa wenzangu au kwako Dinah hasa pale mahali ulipoandika kuwa "mnaweza kukojoa pamoja".

Kukojoa kwangu ni mpaka anichezee K kwa muda mrefu wakati mwingine huwa namuonea huruma kwani nahisi kama vile namchisha na hivyo naishia kumwambia "tayari nimefika" kumbe bado. Nashukuru Mkaka huyu najali na huwa hapendi kuacha mpaka ahakikishe nimekojoa ilandio hivyo tena.

Naomba ushauri kutoka kwenu kwenye haya mawili: (1)-Nifanye nini ili na mimi angalau nifurahie ngono kama wenzangu?

(2)-Niifanye nini ili niweze kumaliza na mwenzangu kwa wakati mmoja?

Asanteni.

Natafuta njia ya kushika na kubemba mimba-Nifanyeje?

"Dada Dinah, umri wangu ni miaka 33 miaka miwili tangu nimefunga ndoa nilibeba mimba lakini kwa bahati mbaya iliyoka baada ya miezi mitatu tu, mpaka leo sijashika tena mimba. Nimeenda Hospitali zaidi ya mara moja kwa ajili ya uchunguzi lakini nimeambiwa sina tatizo lolote.

Vilevile nimejaribu kutumia dawa za Kienyeji lakini sijafanikiwa kushika mimba mpaka leo, je kuna njia nyingine yeyote inayoweza kunisaidia kushika mimba tena bila kunywa dawa za Clomid? Naomba mnisaidie....

Nimefurahi sana kupata email yako.

Asante."

Mume Mzinzi lakini hataki kunipa Talaka, nifanyaje?

"Habari dada Dinah pole na majukumu, naomba mnisaidie niko njia panda, mimi niliolewa miaka mitatu ilipota histori fupi ya mimi na huyu mume dada Dinah ni hivi: Tulikuwa wapenzi toka tuko shule, baada ya kumaliza mwenzangu akapata kazi kwenye hotel kubwa tu hapa dar.

Wakati huo mie nikawa niko field Airport tukawa tunaishi pamoja kam amume na mke, visa vikaanzia hapo. Mwanaume akawa anapigiwa siku na wanawaka mara akanza kuwa anarudi nyumbani asubuhi. Ikafikia hatua ya kunifukuza pale na kuanza kubadilisha wanawake dada dinah.

Vitu vilivyoko pale nyumbani vingi tulishirikiana kama wapenzi kwakweli niliumia sana kwasababu nilikuwa nampenda. Basi tulitengana nikarudi kwetu na nikapata ajira baadaya Field. Baada ya miezi kama sita hivi akaja kunibembeleza huku akiniahidi hatarudia tene na amekuja kwa ajili ya kunioa.

Nilikubali dada, tukafunga ndoa na tukabahatika kupata mtoto wa kike, ndungu zangu wakanisaidia kunishughulikia tukapata nyumba ya NHC naye pia alitoa pesa zake ila hati zote ziliandikwa jina langu.

Kama ilivyokuwa kabla ya ndoa akaanza visa tena, sasa akawa ananitukana matusi makubwa mbele ya h/girl mpaka majirani wanasikia mara aniambie "wewe mwanamke gani mie sinimekusaidia tu kukuoa", mara anipige, anarudi Alfajiri akiwa amelewa.

Nimejaribu kumwambia nataka Talaka yangu hataki kunipa, sasa nilichoamua mwezi wa tatu sasa sitaki kabisa kushare nae love. Kinachonikera kwasasa ni kwanini hataki kunipa Talaka yangu aendelee kufanya mambo yake!

Naombeni mnishauri, nitaipataje Talaka yangu kutoka kwa huyu mume ili na mimi niwe huru?
Asanteni.

Saturday

Je kuna namna ya kuamua jinsia ya mtoto?-Msaada

"Hi Dada D,
Naomba ushauri kutoka kwa mtu yeyote mwenye utaalam wa kujua jinsi ya kuamua kupata mtoto wa kiume au wa kike. Cha muhimu ni kujua wakati gani nikikutana na mke wangu atakuwa na mimba ya mtoto wa kiume au wa kike?

Asanteni.

Friday

Nipo na Mpenzi alie-cheat on her X with Me, je anaweza kuni-cheat na mimi?

"Hallo dada Dinah, Nakupongeza kwa kazi nzuri ya kuelimisha jamii kwa maswala mbalimbali ya mahusiano na mapenzi. Hongera sana.

Mimi ni kijana mwenye miaka 33, nina mpenzi niliyekutana naye mwaka mmoja uliyopita na tumeanza kuishi pamoja tangia mwezi wa kumi mwaka 2010. Nina maswali mawili. Mpenzi wangu alishawahi ku-cheat na mpenzi wake wa zamani ambao waliokuwa pamoja miaka 7.

Kwa maelezo yake miaka miwili ya mwisho mpenzi wake wa zamani alikuwa anamdangaya mambo mengi na akapoteza trust kwake, mapenzi yakapungua na kwa kipindi hicho cha miaka miwili wakawa wanaishi nchi tofauti ila walikuwa wanakutana mara moja kwa mwaka kwa mwezi mmoja.

Swali la kwanza;Anadai alim-cheat jamaa yake na mimi na ndio ukawa mwisho wa mahusiano yao. Hivi mwanamke kama huyu anaweza kuaminika kwa mahusiano ya kudumu na mimi?

Mimi binafsi niko commited kuwa naye bila ya kuwa na mwanamke mwingine ila nahisi kama alivyofanya kwa wa zamani yanaweza kunitokea na mimi. vipi maoni yako na wachangiaji wengine kuhusu hili?

Swali la pili: Ninamridhisha mpenzi wangu huyu kwa ratio ya 6:10 yaani kwa kufanya mapenzi mara 10 mara 6 anakuja. Swali ili mwanamke kuridhika na mwanamme kabisa anapenda afike mara zote kumi? yaani kila mkifanya mapenzi lazima aridhike(akojoe)? ninakuwa sina furaha hizo siku ambazo hafiki.

Je mwanamke akiji-stimulate Clitoris akiwa on top huku uki-pump na akafika, itatafsiriwa kama amekuja kwa Vaginal orgasm au Clitoris Orgasm? mimi binafsi napendelea aje kwa Vaginal Orgasm zaidi.

Pia,Je mwanamke anaweza kufurahia ngono ukiishi naye zaidi ya miaka 3 sawa na jinsi mlivyokuwa ndani ya mwaka mmoja? je hamu ya mapenzi itapungua? haitasababisha kutamani new adventure?

Asante dada Dinah".

Sunday

Nilitalikiwa Kisa Usomi, sasa nimepata mpya lakini....Ushauri!

"Hi da Dinah!
Mimi ni msomaji na mfuatiliaji wa blong yako, shortly I like it and I you as well. Nina 30years nafanya kzi kama Mhasibu Ofisini kwa mkuu wa nchi hii! Dinah tatizo langu ni kutaka ushauri kuhusiana na mwanaume nilie nae, lakini kabla naomba nikupe hadithi ilivyokuwa.

Nilipokuwa na 25yrs niliolewa na mwanaume wa Kiislam kama mimi na nikaenda Chuo soon after ndoa! Baada ya kuanza chuo ikawa ni tatizo kwa wifi zangu na Baba mkwe that kwanini nisome kabla ya kuzaa alafu pia mume wangu ni Form 4? Kwa nini nimpite kielimu?

Tatizo likandelea na likawa kubwa, Baba mkwe alimwambia mwanae achague moja a Divorce au la yeye sio baba yake. Nilipokuwa mwaka wa pili mume wangu akanishauri niache chuo nami nikakubali lakini after 2 months mama yangu akaja juu kwanini niache chuo kisa shinikizo la baba mkwe?

Nikaenda kwa mshauri wa wanachuo Chuoni for ushauri, yeye ndio akanishangaa na kuiomba nirudi Chuoni ! In a dilema nikarudi chuo na within a week wifi yangu akaniletea Talaka Chuoni ! Nusu nijiue kwa kuchanganyikiwa ila kwa sababu ni Muislam tena safi sikufanya hivyo!

Niliumia kwasaabu yeye ndio alikuwa mwanaume wangu wa kwanza na sikuhitaji mtu mwingine tena maishani mwangu! Maisha yakapita na nikamaliza Chuo salama na kuanza kazi. Siku moja nikakutana na Ex baba mkwe akiwa na shida fulani, kwenye maongezi akaniambia "mwenzio anakuhitaji tena na bado hajaoa".

Mimi nikamsaidia shida yake bila kumjibu lolote, nilimsaidia kama binadamu lakini roho iliniuma sana kwa kusikia habari kuhusu Ex hubby wangu. Kwa bahati mbaya Baba mkwe alifariki Dunia mwaka 2009 na my Ex hubby akaja kutaka turudiane lakini mimi nikakataa.

Akaanzakunifanyia fujo wherever he sees me! One night nilikutana nae wakati narudi kutoka Kitchen party alinitolea Bastola , thanks God alikamatwa na kuswekwa rumande for a long time !Niliapa siitaji tena mwanaume, ila watu na wazazi hawakukubaliana na mimi , then nikaamua kuwa na mtu ingawa nilikuwa naogopa sana!


Sasa tatizo ni kitandani, yaani kuwa zaidi ya mara kumi nilizojaribu kuwa nae kitandani akitaka kugusa tu basii "kashacheka", akijitahidi na kusimamisha tena bado anaceka kabla hajagusa. Kaenda kwa daktari, kajaribu mazoezi , kasoma article zako nk ! imeshindikana !

NIFANYEJE? Je niachane nae na kusubiri mwingine au nivumilie?
jemmy, DSM "

Nampenda Mdada alienizidi miaka 9, je naweza kuoa?-Ushauri

"Dada Dinah pole na mihangaiko ya hapa na pale ya kila siku. Mimi ni mwanaume wa miaka 23 naenda 24 sasa. Nimetokea kumpenda dada wa miaka 32 ambaye ni rafiki yangu kipenzi. Lengo langu ni kutaka kumuoa kwani moyo wangu umeridhika juu yake.

Sijamtamani kingono but I feel that I am in love with her. Hajawahi kuolewa na wala hana mtoto. Bado sijamweleza nia yangu ya kutaka tuhame kutoka kwenye urafiki tulionao kwenda kwenye uhusiano wa kimapenzi. Kwasasa mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuo kikuu hapa Tz, mwenzangu yeye ni mwalimu.

Tumekuwa pamoja kama marafiki kwa mwaka mmoja sasa. Urafiki wetu ni zaidi ya urafiki kwani tushafanya romantic talk/romance kwa njia ya simu. Naogopa kumweleza nia yangu kwani nahofia kuumiza hisia zangu ikiwa atanikatalia.

Moyo wangu unapata faraja na mateso juu yake. USHAURI ninaoomba kwako dada Dinah na wanablog wengine ni, Je kuna athari zozote yinazoweza kujitokeza kutokana age gap iliopo ikiwa tutaoana?

Na je nimweleze nia yangu au nifute wazo hilo? Wanawake mnalichukuliaje swala la kuolewa na mume mdogo kuliko mke kwa gap kubwa? NAOMBENI MAWAZO YENU NA HEKIMA ZENU. Facts are sacred, opinion are welcome and ideas are respected.

I love u All,

NB. Kilichonivutia kwake ni akili yake iliyokomaa, upendo alionao juu yangu na uelewa mkubwa alionao. Sura huwa si kigezo cha muhimu sana kwangu".

Pages