Sunday

Ndoa ni Mwaka huu! Mwenzangu anatereza na mdada nimjuae!

"Habari yako,
Naitwa M*(Dinah amehifadhi jina) na ninaishi Sinza,
Kwa upande wangu sina swali ila ninapenda kupata ushauri kutoka kwako.
Nina umri wa Miaka 30 na nipo katika uhusiano kwa takribani miaka miwili na ninatarajia kufunga ndoa mwezi huu wa tano.

Tatizo linakuja kwa huyu mwenzangu anajihusisha kimahusinao na dada mmoja ambae namfahamu na kila nikimuuliza anakataa lakini Ofisini kwa huyu mwenzangu wanafahamu uhusiano wao, yeye na huyo mdada mwingine.

Sasa nashindwa nifanye nini na nikangalia ndoa ipo karibu,
naomba ushauri wako/wenu.

Hivi sasa amebadirika sana kitabia."

No comments:

Pages