Thursday

Mjeuri...hataki nifulia nguo. Nimekosea kumuacha

Dada Dinah habari yako, Mimi naitwa G nina umri wa miaka 25, Tumeachana na mke wangu sasa yapata mwezi mmoja na tuna mtoto mmoja wa kiume ana umri wa mwaka na miezi mitatu.



Kutokana na tabia yake ya ukorofi, ubinafsi na ujeuri na akapata mashoga majirani ambao tabia zao sio nzuri, ilifuka kipindi akabadilika.



Akawa hataki hata kunifulia nguo zangu ila alikua anapenda sana kufanya mapenzi yaani ana nyege sijawahi kuona kila siku tulikua tunafanya mapenzi hata mara nne.



Tabia yake ikanishinda alivyoanza kubadilika na ikabidi nimwache akaenda kwa dada yake Morogoro sasa naskia anafanya kazi bar huko Morogoro.

Nampenda ila moyo wangu umekua mgumu kwake yaani hata sijui nifanyaje na maisha ya kule magumu na kwenda kwao hataki.

Naomba ushauri dada yangu.Mimi naishi Dar es salaam.

************

Dinah anasema: Habari ni njema mkibaba. Shukurani kwa ushirikiano.


Unaacha mke kwa sababu zinazorekebishika(za kizembe)......halafu utamuachaje mke kimtaani hivyo. Au ulimfukuza bila Talaka?



Kama ulivyokwenda kwao na kumposa na ukakubaliwa na hatimae kumuoa.....ndivyo ulivyotakiwa kufanya ila tofauti this time ungekuwa unamrudisha KWAO.



Binti wa watu akipatwa na la kupatwa huko kwa dada yake ambako sio kwao utashitakiwa na Wazazi wake kwa kosa la kumterekeza mtoto wao na kusababisha usumbufu na maisha ya taabu au hata kifo ikitokea bahati mbaya.



Mtu hawezi tu kukurupuka na kuanza kuwa mkorofi au mjeuri......lazima kuna kitu kinasababisha mkeo kuwa na tabia hizo kama kisasi kwavile hawezi kukupiga na hajui kuwakilisha issues zinazomkera kwao.



Baadhi ya wanawake huamua kuwa kama mkeo ili kufikisha ujumbe kwasababu sio kila mwanamke anajua namna ya kuwakilisha kero kwa mumewe.



So atakuwa mjeuri au mkorofi akitarajia wewe mumewe kumuweja chini na kwa panoja mzungumze na pengine wewe kujirekebisha ili yeye asiwe na tabia hizo.


Ikiwa wewe unaumri huo ni wazi mkeo ni mdogo zaidi.....yupo kwenye stage ya kujitambua na kutengeneza marafiki ni sehemu ya kujifunza na kujitambua.


Ikiwa majirani wanatabia mbaya ambazo wewe huzipendi hilo litakuwa tatizo lako. Huenda mkeo alirafikiana nao kwa sababu za kufahamiana na kuongea kama majirani na sio kuiga tabia zao.

Suala la yeye kugoma kukugulia nguo sio sababu kuu ya yeye kuwa mkeo. Yeye alikubali kuwa mkeo kwasababu anakupenda na alitaka penzi lenu linawiri mkiwa pamoja kila siku.


Kwenye ndoa kuna mengi muhimu na kufuliwa nguo sio muhimu. Akiona kuwa ni muhimh kukufulia anapofua zake au za mtoto sawa.....vinginevyo fua mwenyewe.


Kulea mtoto 24hr sio kazi rahisi na juu ya hilo bado kuna shughuli nyingine zinahitaji nguvu na focus ya mkeo.....bila kupewa ushirikiano mkeo atahisi kutokujaaliwa, kutengwa, kutokupendwa au kulemewa na kazi zote za nyumbani plus mtoto.



Mwanamke anapoanza kuhisi hivyo huwa mkali au mjeuri kwa sababu akilini mwake anahisi kuwa humpendi na humjali kwasababu tu kazaa.....pia huoni au kuthamini chochote anachokifanya incl kukugulia.....huonyeshi shukurani.


Mkeo alihitaji ushirikiano na wewe kumuelewa lakini badala yale umemtimua......unadhani nani mbinafsi?


Kungonoana ni afya.....yeye kuhitaji ngono zaidi hakuna uhusiano na urafiki wake na majirani wenye tabia mbaya. Ni muda tu umefika baada ya kuvuka mwaka tangu ajifungue.


Umesema unampenda....hilo ndio muhimu. Angekuwa katoka nje ya ndoa yenu na kumuacha chap chap ningekuunga mkono.


Sasa fanya mpango wa kuwasiliana nae na kutafuta uwezekano wa kuzungumzia issue yenu na kutafuta muafaka.


Kilichotokea kati yenu sio kikuu cha kukufanya umuache mkeo haraka hivyo bila hata kujaribu mazungumzo kwa kujali mahitaji ya mtoto kihisia.

Kila la kheri.

Monday

Nilitaka pasipo....

Hello Dinah,

Shaka message hii itakufikia ukiwa salama wa salimini. Napenda nitangulize samahani kwa kuchukua muda wako, lakini pia naomba unipe nafasi ya kusikiliza tatizo langu ambalo nina imani utanisaidia ki ushauri!.


Ni tatizo ambalo lilinitokea miaka 28 iliyopita ingawa kwa wakati huo kulikuwa na sababu ya msingi kiasilia na likapita kwa kuwa liliendana na wakati wake!.



Mimi ni kijana wa miaka 39, nimeoa na nina watoto 3. Mimi na mke wangu tuna miaka 15 ya ndoa sasa. Wakati wa ujana wangu kabla sijaoa nilikuwa na vigezo fulani vya nje na ndani kwa mwanamke ninapenda kuoa.




Lakini pia nikajiwekea nadhiri kuwa kama nitampatia mimba mwanamke wa ujana wangu sina budi kumuoa kwa kuwa kama nimeridhika kushiriki naye tendo la ndoa nimempenda!.




Nikija kwenye tatizo nililogusia hapo juu. Wakati nabalehe nilipatwa na ugonjwa wa kupenda kama sio kutamani iliyonipelekea kujihisi naumwa homa, kukosa hamu ya kula huku nikihisi njaa sana.Tatizo hili nilipoendelea kukua lilitoweka.



Sasa ni hivi karibuni nilipokutana na mwanamke mmoja(mke wa mtu)ambaye kwa macho yangu ana vigezo vyote vya nje nilivyokuwa nimejiwekea ujanani!. Nilihisi mapigo kwenda kasi lakini nikaamua kuuchuna.




Tulipokuwa kwenye mazungumzo ya kawaida tulibadilishana namba za simu, kumbe naye alikuwa amepatwa na yale yaliyo nipata wakati tunaonana kwa mara ya kwanza.



Baada ya muda fulani tulianzisha uhusiano wa kimapenzi wa siri, mapezi yetu haya tumekuwa tukiyafurahia ajabu tunapokuta.


Sasa mimi nimekuwa nikijiuliza kwa nini napatwa na hii hali ya kama vile ndio nina balehe!? Yaani kukosa hamu ya kula nisipo muona kwa siku kadhaa, kujisikia kuumwa, kumfikiria sana nk.



Hali hii inaniathiri hata kushindwa kuchangamka na watoto wangu kama kawaida. Hii hali nitaishinda vipi wakati nipo katikati ya bahari siwezi kwenda mbele wala kurudi nyuma? Nisaidie dada Dinah tafadhari.

Nategemea kusikia machache kutoka kwako ni mimi. KPM


***********

Dinah anasema: Hello.....bila ya samahani. Ahsante kwa ushirikiano.

Hehehehe nahisi unaogopa Uzee. Miaka 40 sio uzee mwenyewe naisujiria kwa hamu hapa.(still nina hasira na wewe kwa kuumiza watoto).


Inasemekana kuwa watu wakikaribia kufika miaka 40 huanza kujisikia kama walivyokuwa na miaka 20.....mwili unataka kizunguuko mingi ambayo pengine mke hawezi kuitoa kwasababu ama yupo busy na watoto au anajihisi kuwa kungonoka sio muhimu tena bali future ya watoto in your case mnao 3.



Bila kuwa wazi kwa mkeo kuhusu hisia zako ni wazi utaishia kutafuta mbadala ili kutimiza haja zako. Sasa suburi mkeo afikie hapo ulipo ndio utakapojua tamu ya chungu.



Sio kila mtu anajua suala hili la miaka 40.....baadhi huamini kuwa wanapepo lakini ni mabadiliko tu ya kibaiolojia.



Kufanya ngono na kusababisha Mimba which ndio sababu kuu ya kungokoka sio mapenzi na haimaajishi kupenda. Ulijidanganya na matokeo yake umeleta watoto 3 Duniani ili wateseke......wakose mapenzi ya Baba kwa sababu nafasi yao imechukuliwa na hawara ambae ni mke wa mty.


.....ulitakiwa kujua kosa lako kabla ya kupoteza muda wa mkeo kwa miaka 15 na kukongoroa mwili wake kwa kukuzalia watoto 3. Vilevile kama kweli ulijua mama wa watoto wako 3 sio "type" yako hukupaswa kuendelea kuzaa past mtoto mmoja.



Cheating haina excuses....na excuse yako hapa hainifanyi nikuonee huruma wala kukuelewa. Huyo mwanamke unaetoka nae ni mke wa mtu ni wazi kuwa ni Malaya na hana heshima kwenye ndoa yake kama wewe.

Since unaonyesha kutokutaka kuendelea na huyo mwanamke ni wazi umegundua value ya familia yako.


Kumbuka kuwa wewe upo kwenye control. Ulienda mwenyewe kwa huyo mwanamke.....hakukushika shati na kukuvuta so jirudishie control hiyo na acha Uzinzi.


Ukiendelea kufanya siri ni wazi kuwa utaendelea na cheating. So ni vema kumueleza mkeo ulichokifanya ili aache kukuamini hali itakayokusaidia kwani atakuwa akikufuatilia......kabla hujamwambia soma hapo chini. Ukishamsogeza karibu ndio umwambie ili kuepuka uwezekano wa kukutaliki.



Unakaribia umri wa miaka 40.....wanao 3 wanakuhitaji zaidi kuliko huyo mkimama. Jiulize ni legacy gani utawaachia wanao?



Update uhusiajo wenu kila mwaka ili moto uendelee.....weka effort kwenye ndoa yako na uanze kustarehe na mkeo.


Kama sio kawaida yako mkeo atashtuka....mueleze unavyojisikia na pamoja msaidiane. Hali hiyo itakyishia by the time umegonga 40 au 42. So imagine kupoteza familia yako ya miaka 15 kwa ajili ya hisia za miaka 2.


Kapime HIV.....ilinde familia yako....ipende....itukuze.

Thursday

Acha wivu kwani nilipokuoa ulikuwa na Bikira


Dada D, nachukua nafasi hii kukupongeza kwa kuwa umekuwa una jibu maswali mbali mbali kwa ufasaha sana. Kuna mambo mawili napenda kukuuliza


i)nafasi ya bikira kwenye kuoa. Je Mwanamme akioa binti asiyekuwa na bikira anakuwa ameoa mke wa mwenzie?



Baba mmoja alikuwa anaugomvi na mkewe tatizo ilikuwa wivu, mwanamke alikuwa anataka kujua ameongea na nani? mbona anafuta msg kwenye simu yake ndo jamaa akamwamwambia mkewe kuwa kwani wakati nakuoa ulikuwa na Bikira? Mbona una kuwa na wivu wa kijinga?



Je kuoa binti asiyekuwa na Bikira inaathari gani ndani ya ndoa.

***************

Dinah anasema: duh! Huyo mume mtu lazma atakuwa anatereza nje ya ndoa yake na kumkashifu mkewe ni sehemu ya kuzuia mkewe asiendelee kumfuatilia kwa kuogopa kukashifiwa tena.


Hapo Kisaikolojia mke ata back off akijiona mwenye "makosa" kwa kuolewa bila Bikira.


Nafasi ya mwanamke kwenye ndoa ni ileile iwe aliolewa akiwa bikira au hakuwa nayo.


Hapana! Ikiwa hujagunga ndoa na bikira haina maana umeoa mke au mume wa mwenzio. Ili mtu awe mke au mume wa mtu ni lazima taratibu fulani zifuatwe na ubikira sio moja wapo (unless bado unaishi 1900). Kisheria ukilaa na mkibaba au mkimama kwa miaka miwili inahesabiwa kama ndoa.


Kungonoka ni muhimu, ni tendo la kuunganisha viungo vya uzazi....by doing so sio kugunga ndoa.
****************


ii)Kuna haja gani kwenda honey moon wakati mmeshazaa mtoto na wengine watoto wawili. Au ni kwenda kuteketeza pesa, tafadhali nitoe ushamba ka sio uluga luga.

kazi njema.

***************

Dinah anasema: Unless bado tunaishi miaka ya 1900 ambapo Fungate ilimaanisha siku 7 za kuzoeshana endiketa.....kutoana Bikira na pengine kushika mimba.



Siku hizi Fungate ni uamuzi wa mtu baada ya kufunga ndoa. Wengi wanachukilia kama mapumziko maana watu wamefanya maandalizi ya sherehe za ndoa kuwa complicated na kujaa mastress .....kwamba badala ya kurudi Kazini siku moja baada ya kufunga ndoa unataka ukapumzike.....thank God vikao vimeiaha badala ya halleluja nina mke/mume.




Wengine mpaka leo tumezaa watoto wawili bado hatujaenda Fungate......sasa kwani muda ulikuwepo? Tulikuwa busy na kazi na maisha matokeo yake tukaamua kuzaa na maisha yamekuwa busier kuliko so honeymoon is out of the window.



Kama pesa ni zao wanandoa wacha waziteketeze kwani wamezifanyoa kazi lakini kama ni za michango aka za kuomba nadhani hata mimi sitopendezwa.

Natumaini nimekujibu kama ulivyotarajia.

Asante kwa ushirikiano.

Tuesday

Copy and Paste hii


Imekuwa kawaida kwa baadhi ya  Blogger KUIBA kazi zangu na kufanya zao kwa kuongeza picha au kubadili kichwa cha habari.




Kwa miaka Saba blog yangu inamashabiki na wapenzi hivyo wanapoona kazi yangu imetumiwa kwingine huja kunitonya.




Nimekuwa nikidharau kwa muda wote huo na wakati mwingine kufurahi kuwa kazi yangu inapendwa mpaka wengine kuikopi na kuipesti au kuanzisha Blog ili kublog post zangu za miaka ya nyuma kama zao.




Mwaka huu sitaki ujinga tena. Nitafanya kila liwezekanalo kuhakilisha post zinazoibwa Mwaka huu zinaondolewa kwenye blog husika na Google.





Hii tabia ilinifanya nipungize kutoa Masomo mara kwa mara kwasababu mijitu haitoi Credit kwangu au hata kuweka link ya Blog yangu kama kielelezo cha wapi wametoa maelezo husika......ni lwasababu wanataka ionekane wao ndio wajuzi.





Niandikayo yanatokana na uzoefu wangu binafsi kama mwanamke wa Kabila fulani......hivyo sio kila mtu atakuwa na uzoefu uleule hata kama anayoka kabila moja na mimi.




Najaribu kufanya Mawasiliano na Google as well third parties ili wanisaidie kutatua  issue hii.
Ahsante kwa uvumilivu na endelea kuniyonya kila unapoona maelezo ya Dinahicious kwenye blog.....forum....social media n.k.



Shukurani kwa ushirikiano na uvumilivu.

Thursday

Chanzo cha Nyumba ndogo.

Dada habari za Kazi? kwa muda nimekuwa na maswali mengi, juu ya chanzo cha michepuko katika jamii.
Mimi ni kijana wa umri wa miaka 35, ni baba mwenye mke mmoja na watoto wawili wa kiume.





Nimebahatika kujenga nyumba kwa ajili ya kupangisha, Lakini nimegundua sehemu kubwa ya wanaopangishiwa ni wadada ambao ni nyumba ndogo.





Inakuwa kama sehemu ya kuja kuwaficha, wengine hata kazi hawana wanawategemea wanaume wao. Nimegundua wakati wa kwenda kudai kodi yangu, nikaambiwa na majirani mwenyewe haishi hapo anakuja mchana na kuondoka.






Kwenye appartment sita, wapangaji 4 nimekuta wanaishi style ya kihivyo. Kwa kweli nimejiuliza nini chanzo cha nyumba ndogo hasa. naomba usitoe jina langu.
*************







Dinah anasema: Njema tu mkibaba. Ahsante kwa ushirikiano.
Nakumbuka niliwahi kulizungumzia hili miaka 7 iliyopita wakati naanza kublog.







Kuna sababu nyingi za watu kuwa na nyumba ndogo na moja kuu ni kutokuwa na mapenzi ya dhati na ukosefu wa nidhamu kwa mke au mume wako na kutojali hisia za watoto.





Sababu nyingine ni ndoa za kulazimishwa/ lazimika kwamba unaoa au kuolewa kwasababu Imani yako ya Dini inakulazimu kufanya hivyo au unahisi umri umekwenda na hutaki kuzeeka bila mtoto au mke/mume.







Ndoa za kutaka Makaratasi(Uraia kwa wanaoishi nchi za watu), kutaka mali so mtu anafunga ndoa bila mapenzi bali circumstances.
Huwezi ishi maisha yako yote kwenye ndoa bila mapenzi.





Ipo siku utamdondokea mtu kimapenzi lakini hutotaka kutoka kwenye ndoa kwasababu ukitoka unaharibu mambo mengine yaliyosababisha ufunge ndoa in first place.






Hivyo mtu anakaa kwenye ndoa kama status lakini mapenzi yanakuwa kwingine.
Baadhi ni kuingia kwenye ndoa wakiwa bado hawajamaliza "ujana"  yaani hawapo tayari ku-commite kwa mtu mmoja au ni umalaya wa mtu tu.





Wengine ni kutoridhika/tamaa, ego kwa baadhi ya wanaume, ulimbukeni na kujaribu ku fit in.





Kukata tamaa kwa baadhi ya wanawake na kukubali ku-share mwanaume na mwanamke anaemjua hivyo kudhani mwanaume alioko kwenye ndoa ndio mtulivu kuliko vijana, kwamba akiwa na mume wa mtu anajua akitoka kwake anakwenda kwa mkewe na sio kwingine.....which is sad.






Sababu nyingine ni walioko kwenye ndoa kung'ang'ania ndoa mbaya au za mateso wakiamini kuwa ndoa zao zimepangwa na Mungu na hivyo ipo siku Mungu atambadilisha mwenza wake na atarudi kwake.






Mara zote nasisitiza kuwa usikimbilie kufunga ndoa kwa sababu nyingine bali mapenzi.
Na kwa mkimama angalau olewa na mtu mwingine sio yule aliyekutoa Bikira kwasababu ukiingia kwenye ndoa ukiamini bikira yako kwake ndio italinda ndoa unajidanganganya.






Mapenzi ya kweli hayaishi wala hayachushi wala kuchosha bali hukua kama siku zinavyokwenda so long mnafanyia kazi uuusiano wenu kwani mapenzi pekee hayaaimamishi ndoa au uhusiano bali kile unachokipokea na kukitoa kwenye ndoa hiyo.







Ndoa ni zaidi ya Bikira, Ngono, kupikiwa futari na kuzaa. Ndoa inahitaji mambo mengi mno na baadhi nimekwisha yagusia kwenye blog hii.



Nadhani kwa leo niishie hapa.

Tuesday

Mume mlevi na anakisukari....

Da Dinah pole sana na majukumu ya kusaidia shida za watu mbalimbali. Mimi ni mpenzi sana wa blog yako.



Ni mama wa mtoto mmoja nilifunga ndoa miaka sita iliyopita na Elimu ya chuo ila bado sijaajiriwa nafanya ujasiliamali.



Miaka minne iliyopita tuliishi maisha ya furaha sana na mume wangu, tulikuwa watu wenye hofu ya Mungu.


Ikatokea mume wangu akaamishwa kazi kutoka tulipokuwa tunaishi so tukakaa mbali mbali kwa mda wa miaka miwili. Ndani ya mda huo mume wangu akaanza kuwa mlevi na mvutaji wa sigara kupita kiasi.



Hata akija nyumbani kusalimia hurudi saa tisa usiku akiwa chakari na kuanza kunitukana.


Alianza kujiskia vibaya kiafya na baada ya kwenda kupima akakutwa na sukari na akazuiliwa kunywa na kuvuta.


Kwa sasa nimemfuata tuko pamoja ila tabia yake inaniumiza sana ya kuchelewa kurudi nyumbani na akiwa amelewa na kuvuta sana sigara.



Nimekuwa sio mtu wa furaha tena kila siku ni stress na pia anawivu sana kiasi kwamba ananihisi vibaya wakati yeye ndio alikuwa mwanaume wangu wa kwanza na sijawahi kumsaliti hata siku moja.



Mara nyingine nawaza sijui niondoke maana sioni tena raha ya mapenzi da Dinah please nahitaji msaada nifanyeje maana anaahidi kuacha ila kila siku kasi inaongezeka.

*************

Dinah anasema: Ahsante mrembo na shukurani sana kwa ushirikiano.

Unajua binadamu hupenda ku-adopt mazingira mageni ili kuweza ku-fit in.....hii tuwatokea watu wengi tu hata mimi ni mmoja wao ila tofauti ni kwamba ninajijua so huwa natulia na kujikumbusha mimi ni nani na sihitaji ku fit in bali kuwa mimi as an individual.



Wengine huanza ulevi kama mumeo, baadhi huibua tambia za ajabu ajabu au za kitoto, wengi huamua kuacha familia zao na kuanza maisha upya (wakipandishwa vyeo) na wachache hutumia pesa kiholela.


Nahisi kuwa mumeo alikuwa akipata shida kuwa mbali na familia yake akakutana na wafanyakazi wenzake wenye tabia aliyoi-adopt na akaizoea na mazoea yakajenga tabia.


Kumbuka mumeo hakuwa na mahali pa kwenda baada ya kazi kama alivyozoea kabla ya kuhamishwa.....kwani alikuwa anarudi kwako mkewe na mtoto, huko mbali ilimuia vigumu....nadhani.


Sitetei ulevi wake ila najaribu kukufanya uelewe kuwa huenda uhamisho na upweke umepelekea awe na tabia aliuonayo.



Baada ya kugundulika kuwa anakisukari na hataki kufuata ushauri aa Daktari wa kuacha pombe na sigara ni wazi kuwa anataka kufa kabla ya wakati wake(anajiua).


Kabla hajafa kuna matatizo mengine ambayo yatabadilisha maisha yenu kutokana na ugonjwa wake huo na bila kuwa na mke supportive hakika maisha yatakuwa magumu.



Tafuta muda uzungumze kwa hisia na mumeo (akiwa hajalewa)na kuweka wazi hofu yako juu ya Ugonjwa wake na tabia yake ya kurudi usiku wa manane akiwa chakari.



Kisha mpige mkwara......mwambie wazi kuwa kama mkewe unalojukumu la kuhakikisha anakula vizuri na anafuata masharti ya Daktari ili kuweza kuepuka madhara makuu ya Kisukari.


Ongeza.... Lakini unanikatisha tamaa na nisingependa kuanza kuuguza au kuwa mjane ningali kijana kwa sababu za kujitakia.




Endelea, imefikia mahali nahisi pombe au unaokunywa nao ni muhimu kwako kuliko mimi na mwanetu.....unatumia muda mwingi na wao ukiwa huna pombe.....ukirudi nyumbani unapombe kichwani!



Sikutambui tena kwani mume wangu hakuwa hivi.....mume wangu hakuwa mlevi na mume wangu hakuwa akirudi nyumbani kesho yake......nimemkumbuka mume wangu namtaka mume wangu!(toa na machozi hapa....lia haswa).



Usipo acha pombe na kubadilisha tabia na kurudi kuwa mume wangu niliyekupenda bila pombe basi nitabeba mwanangu na nitaondoka nikuache ujifie peke yako. Nakupa wiki ubadilike.



Mumeo anahitaji support kutokana na Kisukari chake....sio big deal ila watu tunapokea magonjwa ya kudumu tofauti hivyo basi wakati umempa Mkwara na muda anza kuonyesha support ya Kisukari chake kwenye lishe unayomtayarishia.


Mkumbushe kila kwa wakati, hakikishs kila mlo iuna matunda na mboga za majani nyingi kuliko wanga na nyama.


Anywe maji zaidi na asitumie sukari kabisa au atafute mbadala n.k.

Asipobadilika baada ya mwezi tangu umpige mkwara basi hamishia kesi kwa aliewafungisha ndoa na wazazi wenu.

Natumai maelezo haya yatakusaidia kwenye kufanya maamuzi yenye busara.

Kila la kheri.

Thursday

He cheated X4 with same kimama


hello dada Dinah.
Mimi ni msichana wa miaka 26, nina mpenzi wangu nampenda sana ila ame cheat na sio mara moja.

Nimekaa nae muda wa mwaka na nusu. Mara ya kwanza tulipendana sana na sikuhisi kitu nampenda mno nae ananipenda sana huyu kijana na ni wa umri wangu.

Siku moja nikawa niko kwake na laptop yake naangalia movie yeye hayupo....mara nikaingia kwa file la camera nikakuta videos kama 4. Kufungua video moja ni yeye yupo anafanya mapenzi na mwanamke pale ndani kwake kitandani anajirekodi kwa kutumia laptop.



Nilipanic sana nka save zile videos. Mwanamke simjui ila anaonekana Malaya tu jinsi ananyoonekana. Alivyorudi nikamuonyesha..akalia na kukiri ni shetani.....nkaondoka kama baada ya muda na kuomba msamaha nikasamehe.




Ila dada Dinah ishapita miezi kama minne ila kila mara nakumbuka ile video na nakosa raha, nakosa hamu ya kufanya nae mapenzi, nakosa raha kabisaa.



Najaribu ila nimeshindwa kusahau namuangalia na kuumia sana kwanini anifanyie hivo
baaadae kabisa nkaja kujua huyo dada wa video ni bar maid.


Nkampigia Simu basi akasema ye keshatembea na huyu mwanaume wangu mara nne na anampa pesa, yeye anafanya tu biashara maisha magumu.


Inauma zaidi kua sio mara moja tu kalala nae ila mara nne anasema kaka alimuambia mimi siishi pale ndani ni wa kuja nakuondoka tu coz aliona nguo zangu na viatu na vitu wakati ukweli ni kwamba naishi nae pale ila nlikua nasafiri kikazi siku mbili au tatu ndio akamleta usiku.



Dada dinah hata kwenye video anafanya nae mapenzi hata hajavaa kondomu, nliogopa sana juu ya afya yangu lakini
nampenda sana nae anadai ananipenda japo ana mapungufu.



Tatizo ni kwamba nlikuta bado anampigia huyo barmaid tena usiku, nkamuuliza we mbona unawasiliana nae na nikakuuliza unawasiliana? akanidanganya eti rafiki ake ndio alikua anataka kuongea na huyo barmaid.


Dada Dinah sina uaminifu tena, nasahau week moja afu nakumbuka tena kila kitu naumia. Nataka huyu ndio awe mume wangu na tuko steji za kupanga ndoa sasa nifanyaje?

Confused, nampenda sana ila hilo ndio tatizo naomba unisaidie nifanyaje.

Nashindwa kuamua natamani hata ningeondoka hiyo mwaka jana nlivoona hiyo video ila muda huu nimesamehe ila ipo kichwani yaani nahisi kama kila muda ana cheat tu.

***************

Dinah anasema: Hiya mrembo pole kwa maumivu ya moyo na maaumbuko ya akili.....mapenzi matamu ukimpata akupendae zaidi ya umpendavyo vinginevyo ni shida bin taabu.


Mie huwa nashindwa kuelewa kinachowafanya watu kusamehe mtu alietereza nje......hilo kosa halisameheki na hakuna excuses ku justfy Umalaya wake na akome kumsingizia Shetani kwa maamuzi yake machafu.


Mtu akiku cheat kamwe huwezi kusahau so ukisema umemsamehe ni wazi kuwa unajidanganya.


Cheaters hukimbii kulia na kuomba msamaha kama sehemu ya ku jitter na ku baki kwenye control.....kwamaana kwamba ukimsamehe hutoweza kuzungumzia uchafu wake tena.....umemsamehe so yameisha. ..sijui unanipata?


Na ukisha samehe cheater kwa mara ya kwanza.....utaendelea kusamehe tu na yeye anaendelea ku cheat kwa vile anajua "mapungufu" yako yalipo ambayo ni kumpenda kupindukia wakati yeye hana mapenzi kwako.



Huyo mwanaume hana mapenzi, utu, heshima na hajui thamani yako kwahiyo hakufai so achana na " nataka awe mume wangu"....hawezi kuwa mumeo unless unataka kuishi unavyoishi maisha yako yote yaliyobaki bila kujua furaha na raha ya kuishi na mwanaume.


Mwanaume anafanya mapenzi na mtu kitandani kwetu na kutunza kumbukumbu ya video kitu kinachoashiria hataki kusahau halafu bado unataka awe mumeo? Really?


Akitoka nenda kachukue kilicho chako hapo kwetu au mwachie (ikiwa havina thamani) kisha sepa bila kumwambia.....Hata akikutafuta usimwambie kwanini umeachana nae na poteza mawasiliano yake.


Sio mara zote tuna achana na wapenzi tukiwa hatuwapendi....tunatoka kwenye uhusiano tukiwa tunawapenda na ndio mana huwa inauma sana.....Lakini kutokana na issues zisizovumilika inabidi kuanza upya bila yeye.


Ukijipa nafasi ya kulia (kuomboleza) na kukubali mwisho basi unasonga mbele kama ifuatavyo.

Kuna topic ya jinsi ya ku songa mbele nadhani niliandika 2014...ipi tie.


Ni binti mdogo na mrembo, kuwa Imara na songs mbele bila yeye kwani ana kupoteza muda wa kukutana na mwanaume mwema na mwenye mapenzi ya dhati.

Kila la kheri.

Wednesday

Naomba radhi.......

Habari za leo?

Ni kwamba kikompyuta changu kimegoma ku-start kwa muda sasa. Nimejaribu kutumia ufundi wangu imeshindikana so nimeipeleka kwa fundi.



Sasa inanibidi nitumie simu ambayo inanisumbua sana kwenye ku type na inabidi nifanye editing kutokana na kuchapia in which sina muda na hii inafanya nishindwe ku publish kama nipendavyo.




Kama ulivyoshuhudia  mechapia  vya kutosha kwenye post mbili zilizopita is just too much....naomba  radhi na tafadhali endelea kuwa mvumilivu.



Nitajitahidi kujibu swali moja wiki hii halafu nitatoa somo ambalo mtalifurahia kama wapenzi.


Usikose....na ahsante kwa kuachana blog hii.

Pages