Friday

Mume Cheated, sasa anadai tupeane nafasi-Ushauri

"Hi, wadau mwenzenu nina shida, mnajua toka mume wangu acheat wakati nina mimba, sijamsamehe. Tunaongea vizuri na tunalea familia vizuri, ila tatizo nikikumbuka maudhi ya mume wangu basi naacha huduma zote na chumba nahama.

Nakaa hata wiki then tunaongea narudi, najaribu kumsamehe na kusahau nashindwa, nakuwa jeuri sana siwajibiki chochote kuhusu mume. Na hii jeuri inakuwepo muda mwingi zaidi kuliko amani.

Sasa eti kaja na solution, eti we need space from each other so mimi nirudi kwetu kwa atleast 3 weeks or 1 month.. Nikamwambia "mie siendi popote coz siwezi kuacha watoto wangu na I dont need any space. Kama he needs hata yeye ana kwao aende tu. Mi mi kama nitaondoka ni 4 good na naondoka na TALAKA yangu mkononi". Akasema hatuachani ila tunarekebishana. Hapo wadau nisaidieni kuna cha kurekebishana au ana yake?"

Dinah anasema:Pole sana Mdada kwa unayokabiliana nayo, watu hawaelewi ni namna gani kuwa cheated on inauma na ni ngumu kiasi gani kusahau. Unaweza kusamehe vema kabisa , well ukadhani umesamehe (huwezi kusamehe kama huwezi kusahau) na ukawa unazungumza na mumeo lakini uhusiano wenu ninyi wawili hautakuwa the same again unless huyo aliyekosa (kwa case yako Mumeo) afanye kazi ya ziada ili wewe uweze kumuamini tena na hatimae kusahau aliyokutenda......hebu bofya hapa kwa maelezo ambayo yanaweza kukusaidia kiasi fulani.

Sio kwamba unakiburi bali unahasira kutokana na kitendo chake kichafu na hujafanikiwa kusamehe kama ulivyodai mwenyewe kitu ambacho kinaongeza ugumu zaidi kwenye kusahau na kuganga ya mbele. Ingekuwa yeye ndio katendwa yaani kama wewe ndio ungekuwa ume-cheat on him sidhani kama angekuwa na wewe by this time.....angekutwanga TALAKA siku hiyo hiyo.

Nimekutana na watu wachache wenye tatizo kama lako na niliwasaidia na wakafanikiwa na sasa wako pamoja wakiendelea na ndoa zao, na huko ndiko nilikopatia uzoefu na hivyo kujiamini ktk kulielezea hili suala la cheating.

Kwa mtu ambae hajawahi kukutwa na tatizo hili ningumu sana kwake kujua ugumu na maumivu yake na hivyo kudhani kuwa wewe unakiburi tu na unachezea shilingi chooni, lakini ukweli unabaki pale pale kuwa, unampenda mumeo, unataka sana kuendelea kuwa kwenye ndoa lakini hujui how to 4get and move on, kwasababu 1)-huji kwanini alifanya hivyo(cheat), 2)-Je umenusurika dhini ya maambukizo? 3)- Kwanini yeye hana habari na anachukulia kawaida (kwa vile hajaomba msamaha) na maswali mengine lundo.

Wewe kuwa mjamzito ni moja ya sababu kati ya zile nyingi ambazo wanaume huzitumia kama sababu kwa nini hutereza nje a.k.a cheat,.

Tatizo lililopo hivi sasa si yeye ku-cheat japokuwa ndio sababu, ninachokiona hapo ni mume wako kuwa na Majivuno (proud of himself) kwa vile tu yeye ni mwanaume na wewe kuwa needy na muoga kudai haki yako. Kingine ni ukosefu wa maswalisiliano baina yenu.

Mwanaume yeyote ambae hana majivuno na anathamini ndoa yake hawezi kukaa ziku zote hizo bila kuomba msamaha kuhusiana na tabia yake chafu, unless huna uhakika na unahisi tu kitu ambacho kitakufanya ushindwe kuwakilisha hoja.

Kama mgewasiliana kuhusu tukio lililotokea wakati wewe mjamzito na unauhakika kweli alikusaliti ni wazi kuwa angeomba msamaha na kuahidi kuacha hiyo tabia na kubadilika kuwa a loving hubby kwako na a great father kwa watoto wenu.

Cheating sio kitu kizuri na ni sawasawa kabisa na yule muuaji(inategemea na reaction ya mhusika), lakini haina maana kuwa ndio mwisho wa ndoa yenu au mwisho wa uhusiano wenu. Inawezekana kabisa kutokana na tukio hilo mkawa the best couple (am not asking u to cheat on ur lover ili kuwa best...hapana), ila kwa bahati mbaya ikitokea na uko kwenye ndoa kuna hatua za kufuata na kuna njia ya kukabiliana na hilo.

Nini cha kufanya:Kwanza kabisa unatakiwa kujua umesimama wapi na unataka nini out of ndoa yako?
1)- Je unampenda mumeo na ungependa ku-work things aout na mumeo ili ndoa iendelee kuwepo na iwe yenye amani na upendo?(Kuna mengi ya kufanyia kazi ili kufanikisha hilo)

2)-Je Penzi limepauka/chujuka ila unamheshimukwa vile ni baba wa watoto wenu na unahofia watoto wenu wasilelewe na mzazi mmoja ikiwa utatoka ndoani?(Mkiweka mipangilio mizuri watoto watalelewa na ninyi wote, lakini kujilazimisha kukaa kwenye ndoa wakati huna furaha sio afya kwako)

3)-Unahitaji muda zaidi kuponyeka kabla hujafanya uamuzi wa busara? (hapa utahitaji kutengana nae kwa muda ili ku-sort our ur feelings and ur head).

Sasa kutokana na kitendo chake cha kukusaliti unadhani kuwa ukiondoka na kwenda nyumbani yeye atahamishia makazi kwa huyo mwanamke mwingine si ndio? Vipi ikiwa yeye ataondoka nakukuacha hapo nyumbani? Unauhakikahuko aendako ni nyumbani kweli na je itakuwaje kama atabeba na huyo msaliti mwenzie kwenda huko wote? Mana'ke kuna nyumba za wageni na wanaweza kutumia.........

Sulihusho hapa ni kupeana nafasi (kama alivyodai mwenyewe) ili kuona kama kweli bado mnapendana na mnataka ndoa yenu iendelee kuwepo lakini kutokana na hali halisi ya uhusiano wenu itakuwa ngumu kwa vile wewe humuamini tena mumeo.

Mimi nashauri wote wawili msafiri na kwenda mahali ambako hakuna ndugu wala jamaa, mkakae hotelini na huko muende kujaribu kurekebisha mambo baina yenu, kitendo cha kukaa ninyi wawili pakeenu na kuwatumia muda wote pamoja kufanya mambo tofauti ya kufurahi (msihusihe ngono) itasaidia kujua hisia zenu na namna gani mnahitajiana ktk maisha yenu.

Pia itasaidia ninyi wawili kutaka kuzungumza kuhusu maisha yenu, kumbuka siku zote naamini kuwa mwanamke ndio mtu pekee anaweza kubomboa au kujenga ndoa yake......hivyo basi jukumu hili liko mikononi mwako kwahiyo ni wewe pekee ndio uko upande wa kulianzisha na kulizungumzia tatizo lililopo kwenye ndoa yenu hivi sasa.

Lakini je utamuanzaje ili akubali?-Ili kumpata kwanza kabisa muombe msamaha kwa kumtamkia Talaka na kubishia wazo lake la kutengana kwa muda. Mwambie kwa uwazi na kwa upole kuwa hudhani kama ni idea nzuri kutengana na unadhani kuwa mnahitaji kutumia muda mwingi peke yanu bila ndugu, watoto na marafiki ili kusort things out.

Sema kuwa, ikiwa yeye au wewe utasafiri na kuwa mbali mbali itaongeza matatizo badala ya kuyamaliza. Mueleze kuwa mnahitaji muda wa kutosha ili kuzungumza na kurudisha the romance kwenye ndoa yenu kwani unahisi imetoweka ghafla na unadhani inawezekana kabisa ni kutokana na vitendo vyako ambavyo unavifanya kutokana na sababu ambayo utamueleza muda ukifika (hii itampa hamu ya kutaka kujua), na kama kweli alikusaliti atang'amua then na kama hakukusaliti basi atasubiri au anaweza ku-demand umwambie....

Wewe usimwambie mpaka mtakapo safiri nje ya mji au mkoa mwingine.....Kama mnaishi Tz basi Morogoro pale pametulia, Arusha pia kuzuri, Bagamoyo, Kigamboni kule kuna Hotel moja bomba kabisa kwa ajili ya kupumzikia mwisho wa wiki....lakini kuzuri kabisa nadhani ni kwenye Mbuga za wanyama kutokana na asilia ya nchi itawasaidia muwe na mood nzuri zaidi....


Weka wazi hisia zako zilizoumizwa ili mumeo aelewe kuwa bado linakuuma na huwezi kabisaa kusahau (ikiwa unauhakika na usaliti wake). Unajitahidi kusamehe lakini msamaha haukamiliki ikiwa yeye mumeo hajakubali kuwa alikosa na kukuomba msamaha.....kama mwanamke natambua unafanya vyote hivyo kwa kudhani kuwa yeye mumeo atang'amua unataka nini kutoka kwake.

Kwa bahati mbaya hawezi kusoma via vitendo vyako wala hawezi kujua yaliyokichwani mwako isipokuwa pale utakapoamua kuliweka wazi ktk mtindo wa kuwasiliana. Ukiendelea hivyo ataamua kwenda kutafuta amani sehemu nyingine na wewe utabaki unaumia even more.

Ikiwa hunauhakika na usaliti wake pia mueleze kuwa ulipokuwa mjamzito ulikuwa unahisi au kama uliambiwa bsi sema wazi kuwa kuna watu walikuambia kuwa mumeo anatoka na mtu fulani na tangu siku hiyo imani nae mumeo imekutoka na hunashindwa kumuamini tena.

Kama akikana kutokana na tuhuma hizo (ikiwa huna uhakika) then inabidi kuwekeana rules kama inawezekana ili kukuongezea au kukurudishia wewe ile hali ya uaminifu juu yake mume(kwamba uanze kumuamini tena).

Ndoa ni ngumu sana kama hakuna mawasiliano ya kutosha au hujui namna ya kuwasiliana na mwenza wako, ndoa ni ngumu kama hakuna uaminifu baina yenu, ndoa ni ngumu kama hakuna maelewano wala masikilizano, ndoa inaweza kuwa ndoano kama hakuna amani ndani ya nyumba yenu.

Ndoa ni our third job kwa wale wote wenye kazi, watoto na waume/wake pia ni our second job kwa wale wote ambao bado hamjazaa lakini mna wake/waume na kazi. Hivyo tukitaka ndoa zetu ziwe Imara, bora, nzuri, zenye furaha na amani hatuna budi kuwajibika na kuzifanyia kazi kila siku iendayo kwa Mungu kama vile unavyokwenda kazini kila siku ili kulipwa mshahara lakini tofauti ya ndoa ni kuwa haina mwisho wa wiki wala likizo ila malipo yake ni zaidi ya Mshahara ikiwa utawajibika vema.

Nakutakia kila la kheri ktk kurudisha ndoa yake kwenye track kama kweli unataka kuendelea kuwa ndani yake.

Ubarikiwe!

Thursday

Nilipinduliwa nikaolewa tena ila mume2 simuelewi-Ushauri

"Dear Dinah
Mimi ni mdada wa miaka 28 niliolewa na mume wa kwanza na nilijaliwa kupata nae watoto
wawili.Mume alikua hodari sana kwa kila kitu katika mambo ya ndoa na tulipendana
sana hadi nilipopinduliwa na mwanamke mwenzangu bahati yake sasa ndio anakula raha
zote.

Nilivumilia saana baada ya kupinduliwa kwa vile mwanamme tulipendana saana
na hasa nilizingatia kuhusu watoto kwani alionyesha mapenzi saana pia kwa watoto wetu wa
kinyume na sasa nilivyoachika.

Kama unavyojua ndoa za waislam ni mwaname ndio
anapoama kumuacha mwanamke huwa na haki japo wewe bado unampenda akiamua
kukuacha huwa halazimishwi kuwa na wewe ila mwanamke ni hadi uwe na sababu
ya kimsingi kama vile ametaka tigo au analewa na hakutimizii mahitaji, lakini mambo mengine
huwa huwezi kuachika!

Dinah anasema: Hii wala sio haki, mwanamke unakandamizwa kwa kenda mbele kha! Eti mpaka uwe na sababu. Pole kwa kuachwa ukiwa bado unampenda mumeo wa kwanza.

Anyway hayo yamepita! Nilikaa nimeumia kwa muda wa miaka sita sikutamani tena
mwaname yoyote kwani pale nilipoishi sikupata mwaname aliemfikia ex wangu hata robo
yake kwa hiyo nikaendesha tu maisha yangu mwenyewe na watoto wangu.

Kama unavyojua jinsia hasa mwanamke ukishaolewa na kuonja utamu wa ngono,
nilifanikiwa kumpata mwaname mwingine nchi nyingine lakini alikua na asili ya nchi
yangu lakini tu alizaliwa kule. Sasa tulikubaliana kuowana na tukajaliwa kuishi
nchi ambayo niliishi mimi. Na huyu pia tulipendana sana ila kwa bahati mbaya
hakuweza kupata kazi kwani nchi hiyo ilikua na ubaguzi sana wa wageni!


Nilibahatika kushika mimba na nilitabiriwa kuwa nitazaa mtoto wa kiume
kitu ambacho kilinifanya niende ughaibuni mwa Ulaya kwani ningezaa mtoto
wa kiume nchini mwangu baada ya muda mtoto huyo angelazimika arudi
kwao kwani watoto hawafati mama! Tulikubaliana vizuri na mume wangu
na tulikua tunawasiliana kama kawaida na mapenzi yalikua mazuri tu.

Kitu cha kushangaza niliposettle huko ulaya ughaibuni mwenzangu
kanibadilikia kabisa! Namfahamisha njia za wenzie wanavyofanya
ili tuweze kuishi pamoja lakini haonyeshi interest kabisa kuja kuishi
na mimi na kisingizio eti wenzake wamemwambia maneno mengi kuhusu
mimi eti namsema na kusema namsimanga!

Na kibaya kabisa hata mtoto wake ambae toka azaliwe hajamuona, hamjali kabisa
na sasa ndio hana hata mawasiliano na nikimpigia simu anaongea
kama kalazimishwa! Nikimuandikia email hajibu!

Nimejitahidi kufuata mafunzo yangu niliyofundishwa, kwani na mie pia kabla ya hii blong
yako nilialikwa na hadi nilikua nyakanga nimejitahidi kumfanyiakila aina ya mapenzi ili kuboresha ndoa yetu, ikiweno kumsemesha maneno mazuri vitendo na hata kumvumilia na wakati mwingine hata kujifanya mtumwa kwake pia huchangia mafunzo yote
ninayoyapata kumtumia na yeye pia kama general kwani nahofia yeye ni negative thinking na hapendi kuambiwa.

Eti unamfundisha lakini mwaname habadilika kabisa! Najua ananipenda lakini anapenda kunitesa kwani nimeshadai talaka hadi nimechoka haniachi na huniignore tu pindi nikiomba talaka!

Kibaya zaidi pindi nikimwambia mapenzi au kufanya mambo mazuri huwa
haonyeshi kufurahia kabisa lakini nastahimili na kushindwa, nikilalamika
hapo ndio hujibu Bomu yaani utajuta kuzaliwa na pia mara nyingi hupenda
kujibu urgument than mapenzi.

Imefikia hata hapo nchini kwangu hataki niende na hunipa sababu zake ambazo haziniingii akilini na nikilazimisha kwenda basi atanikimbia akae mbali eti kikazi hadi siku zangu ziishe nisafiri
na nikimpigia simu au kumtext hapokei au harudishi text au kupiga simu.


Alitokea kwenda kwao hata bila ya kuniambia na mimi kwa mapenzi yangu
nilifurahi na kutaka kumfuata lakini alivyojua nataka kwenda kwanza alinambia hakai
sana amekwenda tu kibisahara kidogo, nilivyosema nitakwenda na tutarudi nchi yangu
pamoja alinikatia hata simu akawa hapokei na matokeao nikaambiwa eti
simu niliyokua nampigia imeibiwa nikaona sasa huko ndio kukataliwa.


Nikawa najaribu hadi nikafanikiwa kumpata nchini mwangu nikawa naongea
nae lakini hana mood na hata nikimwambia naumwa au mtoto anaumwa
haonyeshi kutujali kabisa!

Email anasoma lakini hajibu kwani nikimpigia
huzungumzia salam alizozipata lakini hajibu na kila mara mie tu ndio
nimpigie na mara nyingi nikimpigia anakua hana mood ya kuongea na mimi!


Nampenda saana lakini naumia nimejitahidi sasa mwaka wa tatu lakini mwaname
haonyeshi hata dalili ya kubadilika!na anadharau sijapata kuona au kusikia!
naomba ushauri ndugu yenu nifanyaje kwani sipendi kuachika
na hata nikiachika sitamani tena mwanamme kwani wanaume
unakaa nao vizuri baada ya muda wanabadilika kitu kinakufanya
unachukia maisha yako na maisha ya ndoa na mapenzi kwa ujumla!.


Nimekaa kusoma tu za wenzangu huona mengine yanazidiana na yangu
lakini mimi sina raha ya maisha na hata mtoto wangu, na kila kitu kwangu
naona hakina faida ila nasoma dini yangu lakini mara nyingi huwa katika majonzi
na kuona kama mimi sina bahati duniani na leo nimeona na mimi nipate
ushauri kutoka kwako Dinah na wengine.
Ni mimi Salha"

Dinah anasema:Salha mpendwa asante kwa kunivumilia (nimekuwa busy kimtindo).
Ni mwanamke mvumilivu sana na sina budi kukupa hongera kwa hilo. Inasikitisha huyu mume wako wa sasa anasikiliza zaidi marafiki badala ya kujali maisha yake yeye kama yeye na familia yake ambayo ni wewe na mtoto aliyezaliwa.

Kama ulivyosema ndoa ya mwanzo ilikuwa ya kiislamu, sina shaka hata hii ya sasa ni ya kiislamu. Kwa mujibu wa Imani hii ya Dini inasemekana* (usininukuhu) kuwa mwanamke ni mtu wa kukaa ndani tu na mwanaume ndio mtu wa kujishughulisha na kuhakikisha anamtimizia mkewe mahitaji yake yote.

Apart from Imani hiyo ya Dini, utafutaji, uwindaji na kumuangalia mwanamke na kumpa mahitaji yake yote au kujitahidi angalau kidogo sio lazima yawe yote, wanaume wanaamini kuwa ni jukumu lao na hii ni kutokana na EGO zao as men.

Kutokana na maelezo yako inaonyesha kuwa hajisikii vema au niseme hatuko comfortable wewe kumfanyia kila kitu na yeye anakaa tu akisubiri kupewa au kuambiwa nini cha kufanya (ulipokuwa unampa mbinu za kujiunga nawe huko Ulaya) na "mwanamke" si unajua wanaume wengine na dharau zao, wanadhani wanawake zetu ni ku gossip tu na hatuna uwezo wa kujituma na kufanya mambo makubwa kimaisha na kijamii.

Sasa tatizo la huyu mume wako wala sio kubwa sana japokuwa litachukua muda mrefu kidogo kwa yeye kubadilika, tatizo lake ni kutojiamini kama mwanaume na kujishitukia kuwa anapoteza uanamme wake kwa vile wewe ni mwanamke unaejituma na kumuangalia yeye na watoto wako.

Kuna uwezekano mkubwa akawa anadhani kuwa, mumeo wa zamani ambae ni baba wa watoto wawili wa mwanzo ndio anaerekebisha mambo hapo nyumbani na yeye kama mumeo wa sasa anahisi kuwa ni useless na njia pekee ya kuonyesha uanaume wake kwako ni kwa kuwa na kiburi, m-bishi au mkorofi ndani ya uhusiano wenu.

Mwenyewe umekili kuwa anakupenda na wewe unampenda hivyo basi sio mbaya kama mtajitahidi na kuifanya ndoa hiyo kuendelea na pia kuwa bora kwakurekebisha maeneo machache ambayo mimi nadhani ndio chanzo cha yeye ku-withdraw kama mpenzi.


Kitu muhimu hapa ni ninyi wawili kushirikiana na kuwa kitu kimoja kama mke na mume na wakati huohuo wapenzi, na ili kufanikisha hili mumeo anapaswa kuacha tabia ya kusikiliza zaidi watu wengine na kujitahidi kuwaridhisha ili asionekane "anatawaliwa na mkewe".

Wanaume wengine ni wajinga wajinga, wakiona mwanaume mwenzao kapata mwanamke muhangaikaji na anajituma huwa wanapatwa na wivu na kuanza kum-feed mamneno ya uongo ili tu asifanikiwe kimaisha. Nasema hivyo kwa vile umegusia suala ya rafiki zake kusema wewe unamnyanyasa yeye. Hawa marafiki lengo lao ni kuharibu ndoa yenu na kwa vile mumeoo ana-give in upuuzi wao wewe unataeseka ndani ya ndoa yako.

Nini cha kufanya: Kwa vile umefanya yote ( kwa mujibu wa maelezo yako) nakujitahidi kumuonyesha mapenzi nakuongea nae vizuri kwa mapenzi lakini yeye haonyeshi kubadilika. Kuna uwezekano namna unavyowakilisha hoja zako sivyo ambavyo inatakiwa kwa mwanaume wa namna hiyo (asie jiamini,mwenye kiburi na dharau).

Mwanaume kama huyu ukimuibukia na issue inayokutatiza ktk mtindo wa mawasiliano na kumuonyesha mapenzi mara zote anakuona kuwa unajipendekeza kwake na kuwa uko-needy (kumbuka ni ndoa yako ya pili hivyo anadhani kuwa hutokwenda popote na utaendelea kuwa nae milele na kuvumilia upuuzi wake).

Sasa kama inawezekana wee mfuate huko kwenye nchi yake (huko anako ishi), kisha fanya nae mazungumzo kuhusu issues zote zinazokutatiza na zimekuwa zikikunyima raha kwa muda wa miaka mitatu sasa. Wakati unawakilisha hoja zako hakikisha hubembelezi na wakati huohuo humfokei (usiwe na hasira) na badala yake kuwa firm.

PSSST**Kwa vile hamjaonana kwa muda mrefu anaweza kutanga Ngono, hakikisha ukimpa usimfanyie mautundu yako yote au hata kama unavipya na badala yake kuwa mvivu-mvivu hivi, sio sana ila hakikisha unajifikiria wewe zaidi na sio yeye linapokuja suala la kupata utamu/kilele.**

Sasa kuna sheria za kuwakilisha hoja au issues zinazokutatiza kwenye ndoa au uhusiano wa kimapenzi kwa mujibu wa aliyenifunza nayo ni (1)-Vizia siku ambayo mumeo hayuko moody na tengeneza mazingira mazuri (badilisha mpangilio wa vitundani, ongeza/punguza mapembo.

(2)-Anza kwa kuelezea hisia zako juu yake, umuhimu wenu kwa watoto na namna gani basi watoto wote wanavyo muhitaji kama baba (hii itamfanya asihisi kuwa anatengwa na watoto wa ex mumeo)

(3)-Kumbushia maisha yenu ya kimapenzi mlivyokuwa mkianzana na jinsi gani ulikuwa unafurahia na kiasii gani basi unakosa hayo yote. Mueleze namna gani unajisikia kila unapozungumza nae na hisia hizo zinavyozidi kila mnapokuwa pamoja.

Mwambie kuhusu hisia zako dhidi ya marafiki zake, sio kwamba unawachukia lakini unahisi kuwa wanachukua nafasi yako...kwamba mumeo anafanya maamuzi kwa kufuata marafiki zake na sio wewe mkewe.

(4)-Muulize ni kitu gani hasa kinamuudhi kuhusu wewe? na ni kitu gani hakipendi kuhusu uhusiano wenu pia angependa kubadilisha nini ikiwa atapewa nafansi ya kubadili kitu kuhusu uhusiano wenu na ndoa kwa ujumla......mara nyingi hii itamfaya na yeye akuulize maswali hayo hayo kitu ambacho ndio unakihitaji.

(5)-Kumbuka kumpa nafasi ya kujieleza ikiwa anataka kufanya hivyo, usilazimishe aseme kitu kama haonyeshio kufanya hivyo (hapa inamaa unayosema yanamuingia taratibu).

(6)-Fikiri huku unaasikiliza maelezo yake na wakati huo huo kuelewa. Kwamwe usiongee wakati yeye anajieleza na ikiwa yeye ataingilia wakati unajieleza kaa kimya na umsikilize lakini kumbuka kufikiri huku unaongea/sikiliza hii itasaidia kuepusha mabishao.

(7)-Kamwe usionyeshe Kiburi wala usimuonyeshe kuwa unamuhitaji sana hata kama ni kweli unamuhitaji, mdhihilishie kuwa wewe ni mwanamke unaejiamini na unaweza kuendesha maisha bila mwanaume lakini huwezi kuzuia moyo wako kupenda, na mtu pekee unampenda ni yeye mumeo. Hivyo humuhitaji (as in need) bali unataka awepo kwenye maisha yako na watoto wako.

(8)-Sasa mueleze yote yalioujaza moyo wako, kumbuka kutokulalamika, kubembeleza, kulaumu, wala ku-demand na kubwa kabisa hakuna kuonyesha mapenzi.....mpe straight face na tazama macho yake....this is your moment inaweza kubadilisha mwenendo mzika wa ndoa yako.

(9)-Mara tu baada ya maongezi kuisha usionyeshe ile "straight face" na badala yake kuwa more loving na ikitokea anataka mambo fulani huu ndio wakati wa kumuonyesha zile vitu adimu, ambavyo hawezi kuvipata ovyo-ovyo.

(10)-Badilisha mtindo wa maisha yako, you are only 28 hivyo bado mdogo na unaweza kuwa bonge la sista duu kwa maana ya mavazi na kujipenda (sio lazima uvae nguo za ajabu ajabu unawez akuvaa kufuatana na Imani yako ya Dini lakini ukavutia nakupendeza). Hakikisha unavutia kuliko ilivyo sasa.

Ibua interest mpya, mfano kufanya mazoezi ili kuweka mwili wako vema zaidi na utavutia zaidi ukiwa mtupu, valia nguzo za ndani zenye mvuto, ongeza ubunifu kwenye mapishi yako n.k

Endelea namtindo huu mpya wa kimaisha na baada ya wiki chache utaona mabadiliko......lakini kama haitatokea ndani ya wiki chache (nazungumiza kati ya wiki 2-miezi 3) basi itakuwa ni wakati muafaka kupata msaada kutoka kwa wale waliowafungisha ndoa.

Kila la kheri!

Friday

Ushuhuda kutoka kwa Asif King!

Habari za saa hizi dada Dinah na wachangiaji wote. Mimi ni Asif King sijui unanikumbuka? nilikuja hapa kuomba msaada wa mawazo na ushauri kuhusu mke wangu ambae anaishi Ughaibuni na watoto wetu wawili. Napenda kusema Mungu awabariki sana kwa kuweza kuokoa ndoa yangu. Kama isingekuwa Blog hii na wachangiaji wake hasa kiongozi wao Dinah basi ndoa yangu ingekuwa historia.

Ni karibu miezi miwili tangu nilipopata ushauri wenu na kuufanyia kazi na ninamshukuru Mungu mke wangu alinisikiliza na kuonyesha kunielewa na kuahidi kurudi nyumbani mara moja ili tuongee vizuri. Kama kawaida nilimtumia tiketi na akaja na sasa ninavyoongea yuko hapa Tanzania na watoto watafuata baada ya kufunga shule kwa ajili ya mapumziko ya summer, hivi sasa wanaangaliwa na Ndugu huko huko Ughaibuni.

Leo hii nimeamua kuja hapa kusema yaliyotokea kwani sasa nina uhakika na maamuzi ya mke wangu kuwa kweli atabaki hapa nyumbani kama mlivyonishauri nimshawishi.

Kwakweli sina jinsi ya kuwashukuru Ndugu zangu kwa wema wenu na muda wenu mliotumia kunishauri kupitia Blog hii, nilikuwa nimekata tamaa kabisa na nikawa tayari kupoteza ndoa yangu lakini Dinah akaniambia kwanini nikimbilie kuoa mwanamke mwingine wakati sijajaribu kuiokoa ndoa yangu? Dada kwa kweli kama ni kipaji basi ni cha pekee, hakuna mtu alinishauri yote niyoyapata hapa kwa Dinah, naahidi kuja tena hapa kama tutatetereka tena kwenye ndoa yetu.

Mungu awabariki sana tena sana wote mliochangia, wote mlionipa ushauri mzuri na kunitaka nisioe, wote mlionipa moyo na matumaini ya kuwa mvumilivu. Nimeamini ukichangia tatizo unapata suluhisho haraka kuliko kukaa nalo moyoni. Ule ukurasa na maoni yake yote nime print na nimeyatuza kwenye faili langu kwa kumbu kumbu.

Nisiwachoshe sana jamani, mke ananisubiri. Kwaherini na endeleeni kuokoa ndoa za wengine kama mlivyo okoa yangu.

Dinah anasema: Habari ni njema tu.
Shukrani kwa kurudi tena mahali hapa, nimesoma wakala wako nikahisi machozi yananilengalenga kwa furaha, D'hicious imeokoa Ndoa nyingine tena!

Hongera sana Asif kwa kufanikiwa kuokoa ndoa yako na hatimae kuvinjari na mkeo. Kusoma Mkasa wa huyu bwana unaweza kubonyeza hapa

Tuesday

Nahisia zaidi ya za Kirafiki, nimwambie?-Ushauri

"Hi Dinah,
Nilikuwa natembela blogs nikaona ya kwako, imenivutia na nikaona hapa naweza pata ushauri.

Mimi ni mdada wa miaka 34, nina binti wa miaka 8. kwa hivi sasa mie nipo single sina mume. Ninachoomba ushauri ni hiki.

Nilikutana na mkaka mmoja baada ya yeye kupewa contacts zangu na rafiki yangu ambae alikuwa amenitumia zawadi kutoka nyumbani. Baada ya hapo tulipanga kukutana na tukakutana, ikatokea kwamba tumelewana na tukawa marafiki sana.

Kila siku lazima tuongee katika simu na pia sms, muda ulivyoenda ikawa kama vile lazima tuwasiliane kila siku isipokuwa hivyo huwa najihisi kuna jambo limepungua. Nae baadae akakiri kwamba inakuwa hivo kwake.

Ikafika likizo ya Christimas akanialika kwa wazazi wake mimi pamoja na mwanagu, tukaenda tukafurahi na kurudi. SASA tangu kipindi hicho nimekuwa napata hisia tofauti kimapenzi na za kirafiki kwake.

Yeye ananiambia ananimiss anatamani kuniona lakini hasemi kama hisia zake zimekuwa zaidi ya Urafiki. Nitakutanae week mbili zijazo anakuja kwangu je nimwambie how I feel? lakini pia sitaki kupoteza rafiki....

Nifanyeje? nisaidie jamani i dont want to loose a friend and I also want to know what we feel for each other.

Thanks
Jenifer"

Dinah anasema:Shukrani kwa kustop mahali hapa na kuniandika maelezo haya. Huyo mwanaume anajua kabisa kuwa unampenda au unamtaka zaidi ya urafiki lakini hana uhakika kama utamkubali awe kama "mpenzi" kutokana na urafiki wenu.


Wengi huamini kuwa hakuna urafiki wa watu wa jinsia mbili tofauti ukaishia urafiki tu unless wewe na yeye muwekeane mipaka na kuidumisha vinginevyo ile kitu inaitwa "chemistry" inaweza ikabadili urafiki na mkawa wapenzi.


Naelewa hofu yako ya kupoteza urafiki na huyo Kijana iwapo utaweka wazi hisia zako lakini ukweli ni kuwa wanaume huwa hawana hizo hisia za "akinikataa nitamuangalia vipi usoni kama rafiki", hivyo mwanaume ambae ni rafiki yako akikutaka huwa anafocus kwenye hisia na anajua kabisa ukimtosa ataendeleza urafiki japokuwa wewe kama mwanamke utashindwa kutokana na aibu au kujisikia vibaya kwavile umemtolea nje ,pengine unaweza kudhani kuwa amekushushia heshima hasa kama huna hisia nae.


Lakini kwa case yako, wewe mwanamke ndio mwenye hisia kali za kimapenzi juu yake hivyo basi hakuna ubaya kama utaziweka wazi hisia zako hizo na yeye akajua wazi kuwa umemzimia, sio lazima sana umwmabie kwa maneno unaweza kutumia uanamke wako na ukafanya kwa
vitendo zaidi, wanaume ni waelevu sana na hunyaka chapchap ile "lugha ya machoni".

Nafurahi kusema kuwa hakuna mapenzi matamu kama yale yalioanza na kuegemea kwenye urafiki, mara nyingi mapenzi ya namna hii huwa hayana kukinahi wala kupauka kwa vile wote wawili mnafahamiana vema kama marafiki hivyo mnakuwa tayari mmeweka msingi mzuri kabisa wa maisha yenu ya baadae kama wapenzi.

Ni matumaini yangu utayafanyia kazi yale yote yaliyoelezwa na wachangiaji, mimi kama Dinah nasema dada, go for it....muonyeshe tu kuwa safari zako zooote hapo umefika na mabegi umeshusha....

Kila lililo jema.

Sunday

Nifanye nini kupata mtoto wa Kiume-Msaada

"Mimi na mume wangu tumejaaliwa mtoto wa kike miaka miwili na miezi saba sasa. Tunaomba mungu sana hapo baadae tupate mtoto wa kiume hebu nipe darasa najua unaelewa haya mambo kuwa pamoja na kusali upate wa kiume je Kitaalam unataimu vipi ili iwe kweli wa kiume dear?Pia kama nataka twins pia nafanyaje?

Nitashukuru sana ukinipa data kwani ndio nataka kujiandaa kumtafutia Bridgitte mdogo wake baada ya miaka miwili. Naomba nisikuchoshe nikutakie siku njema na baraka msalimie baby wako Conso a.k.a mama Bridgitte"

Dinah anasema: Dada Conso na Shamimu asanteni kwa ushirikiano wenu, hakika suala hili ni common sana miongozi mwa wazazi wengi wanaopenda kuwa na pea za watoto weye jinsia tofauti.

Natambua kuwa mtoto yeyote akizaliwa upendo, hali ya kujali na furaha ni ileile bila kujali jinsia yake, lakini kama ingewezekana basi wengi tungependa kuwa na mchanganyiko wa jinsia...namna gani basi utafanikisha hilo ndio mbinde!

Kupata mtoto wa kiume inategemea zaidi familia zenu ninyi wawili, kwa maana kuwa kwenu kuna wanaume na wanawake kiasi gani hali kadhalika upande wa familia ya mume wako, ikiwa wanawake ni wengi zaidi kwenu na kwa mumeo pia wadada wengi basi utazaa watoto wakike tu au wengi (inategemea unataka kuzaa wangapi).

Lakini kama kwao mumeo wanawake wengi na kwenu wanaume wengi basi mtoto wa kiume kupatikana ni rahisi zaidi, ila ikiwa kwa mumeo kuna wanaume wengi na kwenu wanawake wengi bado uwezekano wa wewe kuzaa wa kike tu au wengi ni mkubwa.

Hivyo basi, ili kupata mtoto wa kiume inategemea zaidi na upande wako wewe mwanamke, nikiwa na maana kwenu kuna wanaume wangapi kwa maana ya wajomba, kaka zako, baba wakubwa na wadogo n.k. (ila binamu hawahesabiki).

Nini cha kufanya kupata mtoto wa kiume.
Kuna njia kuu mbili nizijuazo mimi ambazo zinaweza kusababisha wanandoa kupata mtoto wa kiume na njia hizo ni zile za Kisasa/Kitaalamu na asilia....nitafafanua kidogo asilia ambayo ndio naijua zaidi na ile ya kitaalamu ni straight foward.....lakini kabla napenda ufahamu yafuatayo;-

(1)-Mbegu zinazosababisha mtoto wa kiume hutoka haraka na kwa speed kubwa sana ili kuungana na Yai vilevile hufa haraka (hufa ndani ya masaa 3 ya mwanzo).

(2)-Mbegu zisababishazo mtoto wa kike hujivuuuta sana (maringo ya wanawake yanaanza b4 hata hatujawa viumbe kha! hihihihi) na hubaki hai kwa zaidi ya masaa 72 (zaidi ya siku tatu).

(3)-Bao zito na lenye afya ndio muhimu kusababisha mtoto wa kiume (mlishe mumeo lishe bora).

Hivyo basi ili kufanikisha hili unapaswa kutegea siku ambazo wewe unajua yai lako limepevuka na linasubiri kurutubishwa na mbegu ya kiume. Ukingonoka kwenye siku hatari kuliko zote ni wazi kuwa zile mbegu za jinsia ya kiume zitakuwa za kwanza kurutubisha yai na kufanya mimba ambayo itakuwa ya mtoto wa kiume. Hii ni njia asilia.

Njia ya kisasa ni ile ya kitaalam kuchukua yai lako na kuchagua mbegu za kiume tu kutoka kwa mumeo nakurutubia manualy (nje ya mwili wako) kisha wanakupandikiza, yaani wanakuwekea mimba (yai na mbegu walizounganisha) kwenye Womb (mji wa mimba) na hapo kunakuwa na uhakika wa kuzaa sio tu mtoto wa kiume bali wanaweza kuwa mapacha 2-3 wa kiume.....inaghalimu mamilioni ya shilingi though.

Kidokezo; imni ya kujaribu mpaka upate mtoto wa kike au kiume bila kuzingatia kwenu mkoje intrms of jinsia sio njema kwani mtajikuta mnazaa watoto ambao hamtaeza kuwamudu.

Natumaini maelezo yangu na ya wachangiaji wengine yatakuwa yamekusaidia kwa namna moja au nyingine, kwa niamba yao basi twawatakia kila lililo jema na Mungu afanikishe matakwa yenu kwa mapenzi yake.

Midaz!

Pages