Monday

Condoms au Dawa za kuzuia Mimba

"Mke wangu anataka tutumie kondom, hiyo ni kweli? Nimeoa miaka 6 iliyopita, tumejaliwa watoto wawili wa miaka 4.5 na mwingine ni mwaka Mmoja.

Tangu tumepa mtoto wa pili, Mke wangu alianza visingizio kuwa yeye hatatumia njia nyingine za Uzazi tofauti na Condom kwani njia zingine zinamsababishia kuumwa Mgongo, Joto kali na mengine mengi.


Mie kutumia Condom najiona kana kwamba nipo na Changudoa, sipati raha hata tone, nimemueleza haelewi, nishauri nifanyeje?"

***********


Dinah anasema: Hello there! Ahsante kwa Ushirikiano.


Kabla ya yote unapaswa kutambua kuwa Raha/Utamu wa Ngono upo Akili(kichwani) na sio kwenye Uume, Uume ni kitendea kazi.


Suala la kuona kama upo na Changudoa kwasababu ya kutumia Condom ni Dharau kuu kwa Mkeo! Inamaana ukivaa Condom unapoteza mapenzi na hisia zote za Huba kwa Mkeo na hivyo unafanya tu ili kuji-relief?

Ikiwa Mkeo anasumbuliwa na Dawa za kuzia Mimba na kumfanya aumwe kama alivyokuambia hakika hawezi kukuelewa. Wewe kama mumewe ulipaswa kumuelewa na kumpa-support na kwa pamoja ama kukubaliana na matumzi ya Condom au kutafuta/jaribu aina nyingine ya Dawa za kuzuia Mimba.


Ikiwa kila dawa anazojaribu zinamsababishia matati kiafya ni vema kutotumia na badala yake mtumie Condom kama alivyo-suggest, kama hutaki na Nyama to Nyama ni muhimu kuliko Afya ya Mkeo basi kazibwe Mirija ili usiwezi kumtia Mimba.

Unapaswa kutambua Dawa hizo (baadhi) zinahomono na huwafanya wanawake wengi wapate "side effects" mbaya sana.

Wengine huwa wakali, wakatili, wazembe/wachafu, wanapoteza hamu ya kufanya mapenzi, wanapoteza hali ya kukupenda wewe, kujipenda wao au watoto, maumivu ya Kichwa yasiyoisha, kupata Hedhi kwa muda mrefu (miezi 3-9), Unene/Kujaa maji, Mapigo ya Moyo kuwa juu n.k.


Wanaume wengi (hasa Waafrika) mpo nyuma sana kwenye ku-support Wake zao kwenye matumizi ya Condom kwa kuamini kuwa Condom inazuia raha na "nimemuoa hivyo hakuna kutumia Condom"...Condom ni njia nzuri sana ya Kuzuia Mimba ikiwa njia nyingine zinasumbua.

Techology ya Condom imekuwa sana na mengi yamebadilika, kuna Condom nyepesi kama ngozi lakini Imara(hazipasuki)....explore aina za Condom Mwanaume, za bure waachie Wanafunzi na watu wasio na Uwezo.

Condom za leo haziwashi, sio nzito(lakini Imara), hazinukii kama mpira....nunua kulingana na mahitaji yako.

Wekeza kwenye Condom Mwanaume sio unashupalia Nyama to Nyama na kutojali matatizo ya Kiafya ya Mkeo utadhali Uhai wapo depends on Nyama to Nyama!



Mapendo tele kwako...

Friday

Mapenzi na Kazi, unakabiliana vipi?

"Mimi ni msichana wa miaka 24, nimekua na mahusiano na boyfriend wangu miaka mitatu sasa mwaka wa kwanza tulikua na matatizo kutokana na Ex wake aliyekua anamng'ang'ania na kuwashirikisha ndugu wa mwanaume ili wamsaidie arudiane nae.


Bahati nzuri mpenzi wangu ni mtu mwenye msimamo kidogo haku-fall kwa hilo na yote niliyavumilia..kama wapenzi tumekua na ups and down na tumevumiliana nimeshafanya makosa sana lakini bado ameendelea kuwa na mimi.

Tatizo linapokuja hapa, mpenzi wangu ameajiriwa na mimi bado nipo Chuo ila Ofisi yao ilitangaza nafasi za kazi za muda mfupi akani recomend nikapata kazi ila akasema tuseme sisi ni marafiki maanake Ofisi itaona amemtafutia kazi mpenzi wake kitu ambacho sio kizuri.


Nikakubali manake kazi yenyewe ilikua ya muda, kuanza kazi pale nikakutana ma mdada ambaye anampenda boyfriend wangu though my boyfriend anamchukulia kama rafiki. Yupo nae close and all that.


Siku moja tukatoka Out kama Ofisi, kwa vile tumeamua kufanya mahusiano yetu yawe siri hata siku hiyo tukashindwa kuwa pamoja matokeo yake akawa karibu na wadada wengne wa Ofisini mmoja wapo akiwa huyo anayempenda my bf.

Kwa hasira nikaishia kunywa pombe hadi nikapoteza kumbukumbu kabisa nikarudishwa nyumbani na my bf na he took care of me. Nikajisikia vibaya mno kwa nilichokifanya.


Kesho yake akanambia nililewa nikafanya ujinga kitu ambacho sikumbuki, akasema nimemuumiza sana na kwa mara ya kwanza akalia. Najua nilifanya makosa na hiyo ikawa mwisho wa kunywa pombe!


Siku hiyo tukaamua kuachana ila tukawa tunaendelea na mawasiliano, ikapita kama Mwenzi tukaanza tena kulala pamoja but kipindi hiko haikua serious sana.

Nikawaza vile mimi ndio nilikua responsible kwa uhusiano wetu kuvunjika basi ntavumilia tu ikapita kama three months tukawa sawa and tokea hiyo incident ni mwaka sasa.


Tatizo ni lile lile hataki watu wa ofisini wajue uhusiano wetu japo ndugu zake wote na marafiki zake wote wanajua uhusiano wetu. Kipindi hiki nimerudi tena kufanya hapo kazi anadai wanawake wa pale Ofisini anawajua vizuri wakijua sisi ni wapenzi sitafanya kazi kwa amani, kwamba kutakua na maneno sana ila siku itafika watajua tu ukweli.

Nampenda mno namuamini pia ila kwenye hilo suala linakua chanzo cha ugomvi kati yetu wakati mwingine. Nakua njia panda

Nishauri dada yangu. And sorry kwa maelezo marefu."


*******

Hello there, usijali maelezo marefu yaliyokamilika nayapenda na ndio huyafanyia kazi. Shukurani sana kwa ushirikiano.

Hapo kuna mawili-matatu! Moja inawezekana Mpenzi wako alikuwa na Uhusiano na mtu ambae bado yupo hapo Ofisini au Mkubwa wake wa Kazi hapendi wafanya kazi wawe na wapenzi wao mahali pa kazi(kuepusha uzembe na kupendeleana) na mpenzi wako hataki upoteze kazi.....(Fanya uchunguzi hapa, usikurupuke ukakosa vyote).

Pili, Mpenzi wako hataki ijulikane kuwa wewe ni mpenzi wake na hivyo kasaidia au alisaidia wewe kupata kazi pale ofisini kwake....kasema ni marafiki na labda baadae ukipata ajira ya moja kwa moja atajifanya amekudondokea na hapo kuanzisha uhusiano(wakati ukweli mnaujua wenyewe).

Ni vema mpenzi wako atambue kuwa kufanya uhusiano Siri wakati yeye anakuwa karibu na Wanawake wengine huku wewe ukishuhudia ni ngumu na inaumiza sana (anakunyanyasa Kiakili na Kihisia).


Kufanya kazi hapo ni muhimu kwako kwa ajili ya uzoefu na pengine ajira ya kudumu hapo baadae hivyo usilazimishe sana kujulikana na watu wengine hapo Ofisini (hawana umuhimu sana kama Ndugu zake) na hakika unaweza kupewa Ukweli(umbea) wa nini mpenzi wako alikuwa akifanya na mtu fulani hapo ofisini(tuseme ni Ex) na hapo kukawa na ugomvi au makundi na kufanya maisha ya kikazi Jehanam.


Muhimu ni kuzungumza na mpenzio na kumueleza unavyojisikia bila hasira, kisha wote kwa pamoja muelewane kuwa yeye apunguze au aache kabisa ukaribu na wanawake wote hasa yule ambae unadhani kuwa anampenda mpenzi wako.

Kama yupo serious na uhusiano wenu na mnapendana (mwambie) basi ni vema tukaweka Mipaka dhidi ya watu wa jinsia tofauti wanaotukaribia ili kusiwe na maumivu Kihisia na Kiakili.

Inawezekana kabisa kuwa na uhusiano Kazini kama Wafanyakazi na Wapenzi mkiwa nje ya Kazi ikiwa mtafuata hayo hapo juu.

Hili likishindikana basi ni vema mmoja wenu aombe uhamisho au abadilishe kazi.


Kila lililo Jema.

Mapendo tele kwako...

Thursday

Mzee aniharibia Nyumba!

"Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28, mpenzi wangu ana Ishirini na Tisa na tumeishi nyumba moja yapata mwaka.











Kwa sasa tunatofauti kidogo. Mpenzi wangu alianzisha uhusiano na Mzee ambaye ni mkubwa kwetu. Baada ya muda niligundua kuwa kabla ya uhusiano wao huyo Mzee alikua karibu na familia yake.











Hivyo tuligombana na ugomvi ulikuwa wa muda mnamo /11/2014 niliamua kumpigia simu huyo mzee na alikua mstaarabu na kuahidi kuachana na huyu Msichana.











Alipojua nimefanya hivyo tuligombana kwa maneno mpaka ikafikia hatua ya kupigana, nilimuumiza na yeye akaamua kwenda kwao.









Kwa sasa ninajaribu kurudisha penzi letu lakini napata shida sana nifanye nini ikiwa bado namuhitaji?"





*************





Dinah anasema: Habari gani? Ahsante kwa ushirikiano.







Ikiwa Mpenzi wako amekusaliti kwa kutoka na mzee huyo na ukajaribu kukomesha uhusiano wao kwa kuzungumza na Mzee husika ili akuachie Mpenzio. Lakini Mpenzi wako akakasirika na kugombana kutokana na kitendo cha wewe kupigania penzi lenu unadhani Mwanamke kama huyo anakupenda au kukuthamini?











Mtu anapofikia mahali anatetea Kosa lake au kutafuta sababu ku-justify anachokifanya au mtu anaetenda nae kosa ni wazi kuwa huna umuhimu kwake.









Kitendo cha wewe kumpiga na kumuumiza sio kizuri(ni Kosa Kisheria), pamoja na kumpenda kwako sidhani kama ni sahihi kuendelea kupigania Penzi ambalo ni la upande mmoja tu (wako), angekuwa anakupenda kwa dhati msingefikia mlipofikia.









Jitahidi kusahau na utafute namna ya kusonga mbele na maisha yako bila yeye.





Nakutakia kila lililo jema.

Mapendo tele kwako...

Tuesday

Mbinu za Kupendwa Ukweni!

"Dinah habari, nilikuwa nataka kujua jinsi ya kuelewana na kupendana na ndugu wa Mume wangu katika kutafuta google ndio nikakutana na Blog hii.

Mie na Mume wangu tumefunga Ndoa miaka kadhaa na tumejaaliwa watoto Watatu. Mwanzoni hatukuwa na matatizo yeyote kati ya Shemeji na Wifi zangu.

Matatizo yameanza hivi karibuni na chanzo sikijui. Nimejitahidi sana kuwapenda ndugu wa Mume wangu lakini hawapendeki. Kila wakija kwangu ni maneno, imefikia hatua wanasema nimembadilisha Kaka yao.


Nikiongea na Mume wangu kuhusu habari hizi, yeye anaishia kusema niwadharau.

Je, nifanye nini ili kuwe na Amani miongoni mwetu? Naomba ushauri au kama kuna hatua, mbinu zozote za kuwafanya ndugu wa mume wangu wanipende, wanikubali. Ahsante".


**************


Dinah nasema: Nakumbuka nilikwisha zungumzia kuhusu hili ila kwa namna nyingine kati ya mwaka 2007 na 2008 (angalia kwenye Topic zilizopita hapo Kulia).

Niligusia kuwa wakati unaandaliwa(Fundwa) ili uende kuishi na mtu mwingine(Mume) na watu wengine (ndugu zake), unaonywa wazi kabisa kuwa uwaheshimu ila usilazimishe wakupende na kamwe usijipendekeze kuwapenda!

Kibinaadamu huwa inatokea una-click na baadhi ya watu na mnakuwa na mahusiano mazuri kama Wifi/Shemeji na wakati mwingine unachukiwa kabla hata hawajakufahamu.


Kosa Kuu ni kuwa tunaaminishwa kuwa ni "lazima" uwapende ndugu wa mwanaume na matokeo yake unasahau kuwa hao "ndugu" ni Binadamu na Binadamu anahisia na hisia hizo sio lazima ziwe za upendo kwako.....sasa ukienda Ukweni full force "nawapenda ndugu zake" hakika itakuumiza.

Pia wakati mwingine wewe mwenyewe inatokea tu unampenda "Wifi" yako na unatamani mngekuwa "marafiki" ukidhani atasaidia kulinda Ndoa yako in case ikabuma.

Ninachojaribu kukuambia hapa ni kuwa, ni muhimu kumchukulia kila mtu kama alivyo na kumheshimu (so long anakuheshimu pia), kama hawakuheshimu basi achana nao (wadharau).

Kumbuka Upendo haulazimishwi. Kama ilivyo Shuleni au Kazini, unakutana na watu ambao huwajui, hujawahi kuwaona maishani mwako lakini inatokea unapatana na baadhi na wengine inakuwa Hola(huwapendi au hawakupendi).

Na pengine unawachukulia kama walivyo tu bila kuwa na hisia ya chuki au upendo kwao hivyo wanakuwa Wanafunzi wenzio au Wafanyakazi wenzio na sio Rafiki zako.

Hakuna mbinu zitakazowafanya ndugu wa Mumeo wawe kama unavyotaka au ulivyotegemea. Wanamaisha yao na familia zao (Wake/Waume na watoto wao).....usipoteze muda na nguvu kulazimisha Upendo ambao haupo, Wekeza Muda na Nguvu zako kwenye zingatia maisha yako, ya wanao na Mumeo.

Likitokea jambo la kuwakutanisha kama Ukoo(tangu umeolewa na Kaka yao) shiriki bila kinyongo, ongea nao kama watu tu (sio Wifi-Shemeji).

Kila lililo jema.

Mapendo tele kwako...

Kumuendekeza mwenza(wa Kiume)!

Unajua tunapoanza mahusiano huwa tunajitahidi kufahamiana na kujuana zaidi kabla hatujaamua kuwa -serious(Ku-ndoa-na).











Baadhi yetu hujitolea "Mhanga" na kwenda kujuana na kufahamiana baada ya kuwa serious(Ndoa-na kwanza mengine yanafuata).











Wachache huamua kuichukulia kila siku kama inavyokuja(hawa bado wanakua au wanaogopa kuji-commite baada ya kutendwa).











Jinsi siku zinavyokwenda ndivyo ambavyo kila mmoja wenu anajifunza jambo au mambo kuhusu mwenzie. Ukigundua kuwa mambo au jambo fulani linaweza kuwa Mzigo huko mbeleni ni vema kuliweka wazi na kulizungumzia kisha kutafuta Mbadala.











Baadhi huamua kuendekeza tabia za mwenza wakitegemea kuwa watabadilika....bila kujua huko mbeleni inaweza kuwa Mzigo. Mfano Uvivu ambao hupelekea mtu kuwa tegemezi, Ulevi au Uchafu n.k.











Baadae mnapokuwa na familia utajikuta unakuwa Single-mother with a husband, kwamba unafanya kila kitu kuanzia kazi za ndani mpaka kutafuta pesa ya Chakula na Matumizi mengine kwa Familia......ukidhani kuwa huko ndio kuwa "independent".











Nimelenga wanaume kwasababu ndio ambao huwa wagumu "kubadilika" kutokana na ile imani kuwa "mwanamke hawezi kunibadilisha" au "usikubali kubadilishwa na mwanamke".









Hakikisha unakuwa Msaada kwa mwenza wako ili awe kwenye mstari na msaidiane, kama hakueleweki....Mpige Mkwara.







Feels great to be Back!

Mapendo tele kwako...

Pages