Thursday

Nianzie wapi Kisheria kumtaliki mume wangu?-Ushauri

"Kwanza napenda kukupongeza kwa kazi yako nzuri, pili mie nilitoa malalamiko yangu kuhusiana na mume wangu ambae hataki kunipa Talaka dada dinah, naomba unielekeze wapi naanzia kwenye vyombo vya Sheria maana issue nataka pia atoke kwangu.

Kuna baadhi ya watu wananiambia Mahakamani hawavunji Ndoa na wengine wananiambia inaweza pelekea hata Miaka miwili kila siku unapigwa Tarehe tu, sio siri dada Dinah ni kama naishi na Chui ndani ya nyumba, kwamba muda wowote anaweza akanibadilikia na kunila nyama"

No comments:

Pages