Wednesday

Mpenzi hanijali, hanithamini tena,nifanyeje?

"Dada Dinah pole na kazi za kutueimisha sisi tulio katika ulimwengu huu wenye raha na karaha zake. Mimi ninaishi na mwanaume ambaye hatujafunga ndoa ila tumezaa mtoto mmoja na ilibidi tuanze kuishi pamoja kabla ya ndoa kwa sababu ya kusaidiana malezi ya mtoto.

Kikubwa kinachonikera kwake ni kwamba hanijali tena, hanithamini wala haoni na mimi ni sehemu ya maisha yake,nasema hivyo kwa sababu kila ninapohitaji msaada wowote toka kwake hanisaidii kabisa.

Ukija katika suala la kugonoka jamani mimi mwenzenu naweza kaa hata mwezi mzima hajanigusa wala nini na tunalala kitanda kimoja kila siku na hata tuki sex yeye anafanya mradi yafike basi na si kutombana ili kila mmoja wetu aridhike nakumfurahia mwenzie.

Kingine, anachelewa kurudi nyumbani yeye ni mfabiashara k/koo na duka anafunga saa kumi na moja kamili ila mpaka afike nyumbani ni saa 3-4 au hata saa 5 usiku nimeshaongea naye lakini wala hanielewi kabisa.

Jamani naomba ushauri wako dada na wachangiaji wengine kwani nahisi kutokumpenda tena, mwenzenu nifanyeje ili tuwe na mapenzi kama walivyo wengine? Poleni kwa msg ndefu".

No comments:

Pages