Wednesday

Nimegundua mume wangu kampa mimba mwanamke wa nje-Ushauri

"Habari dada Dinah, mimi ni moja ya wadau wa blog yako. Nieolewa na ni mama wa mtoto mmoja ana miaka 3+ na ninakaribia kupata baby no.2 panapo majaaliwa mwishoni mwa mwaka huu.

Mwenzenu nina matatizo ambayo naomba wadau wanisaidie kunipa ushauri nini cha kufanya maana nimejaribu kufikiria sioni njia ya kutatua matatizo yangu. Mimi na Mume wangu tangu tumejuana tumekuwa tukiishi kwa amani na upendo, lakini cha kushangaza hivi karibuni nilimuona kabadilika sana kiasi kilichonifanya nianze kuchunguza kulikoni?

Mbona mambo hayaendi sawa kama zamani! baada ya kuanza uchunguzi niligundua mume wangu kuna watu anawasiliana nao sana bila kutaka mimi nifahamu wanawasiliana kwa ajili ya issue zipi. Hapo nilijawa na wasiwasi zaidi nikaamua kutega baadhi ya number kwenye simu ili msg zikitumwa asizione kwenye inbox ila ziingie kwenye folder tofauti.

Nilipokuja kufungua lile folder nilikuta msg nyingi za mdada mmoja ambaye ni mpenzi wake na alikuwa akilalamika kuwa hamtumii msg wala kumpigia simu nakuwa amepunguza kumjali na yeye ni mjamzito na ameamua kuitoa hiyo mimba kisa hamjali sababu hampigii simu.

Nilipoona hizo msg nilitamani kufa hapohapo! maana sikutegemea kama mume wangu angekuwa na mwanamke nje ya ndoa yetu ambayo bado changa. Nikaamua kumuuliza mume wangu akasema hana mwanamke nje na hategemei kuwa na mwanamke nje ya ndoa.

Nami kwa kuonyesha kuwa hamna msg niliyoona nilikaa kimya kwa muda wa wiki mbili bila kumuuliza kitu. Baadae nikakuta msg nyingine ya huyo mwanamke akimuuliza mume wangu anaamuaje kuhusu ujauzito alionao?

Nikaamua kuhamishia ile msg kwenye inbox na kumuomba mume wangu aisome ile msg na anieleze kuna kitu gani kinaendelea. Chakushangaza mume wangu akasema haijui hiyo msg, basi nikamwambia tupige hiyo simu tukiwa wote nae akakubali yule dada alipopokea akaanza na maneno yanaonyesha wao ni wapenzi wa siku nyingi.

Mumue wangu akajidai kumfokea yule dada lakini haikuleta maana yeyote, nikaamua kuchukua ile namba na nikaipigia mimi mwenyewe nikimuomba tukutane kwani nina shida nae, yule dada akakubali lakini hakutokea na simu yangu hapokei tena.

Huku mume wangu hajawahi kulala nje ya nyumba yetu hata siku moja na siku zote yeye huwahi kurudi kutoka kazini kabla yangu maana mimi huwa narudi kuanzia saa kumi na moja na kuendelea na yeye hurudi kuanzia saa nane mchana.

Hapo naomba dada Dinah na wachangiaji wengine mnisaidie kimawazo, nifanyeje maana nimepunguza sana upendo kwake kila nikimuona mume wangu namuona kama ni muuaji maana kama ameweza kufanya mapenzi nje ya ndoa tena bila ya kutumia kinga si anataka kuiteketeza familia yetu?!!

Asanteni"

No comments:

Pages