Monday

Nashindwa kumuacha mume wa mtu-Nifanyeje?


"Natumaini wewe ni mzima na waafya. Mimi ni mwanamke wa miaka 24, naomba ushauri wako kama mdogo wako. Mimi nimetokea kumpenda mume wa mtu na nina amini ananipenda pia. Tumekuwa na mausiano kwa mwaka mmoja bila hata mke wake kujua na nina tamani sana kumjua mke wake.

Tatizo langu ni kuwa sijiamini kama huyu Mume wa mtu atakuja kuwa nami kama mpenzi wake wa kudumu, mimi binafsi nashindwa kumuacha kwasababu Jamaa mwenyewe ni innocent and very caring.
Naomba ushauri nifanye nini?."
Dinah anasema: Mie mzima wa afya namshukuru Mungu, Nashukuru sana kwa Mail yako na hongera kwa kuwa wazi pia kuwa na nia ya kuachana na huyo mume wa mtu lakini hujui uanzie wapi?
Ninaamini nia yako ni kuachana nae na labda ulipogundua kuwa ni mume wa mtu ulitaka kufanya hivyo lakini kutokana na hali ya kujali na upole anaokuonyesha unadhani kuwa ni mtu mwema na hivyo kuzidi kumdondokea kimapenzi. Ikiwa kama nia yako sio kuachana nae hakika usingekuja hapa kuomba ushauri na badala yake ungeendelea kivyako.
Uhusino wenu umekuwa kwa mwaka mmoja kwa vile mkewe hajui na wala hajahisi kuwa mumewe ana-cheat labda kwa vile anajali na amevaa ngozi ya kondoo hivyo mkewe anamuamini kupita kiasi na hivyo kutohisi kitu chochote kibaya.
Kama mkewe angejua au angehisi kuwa mumewe anagawa umasikini nje ya ndoa yao hakika angempa wakati mgumu sana na kupelekea Jamaa kuachana na wewe.
Sasa hebu tuambie kitu gani kinakufanya utamani sana kumuona mkewe? Ili umwambie kuwa mumewe ana-cheat (ni jambo jema japo ni ngumu kwa yeye kukuamini hasa kama mumewe atakataa na kudai kuwa wewe unamtaka) AU unataka kufanya ushindani ili kuzua ugomvi juu ya mumewe (sio vema kuumiza hisia za mwanamke mwenzio kiasi hicho).
Hisia za Mapenzi:
Kutokana na uzoefu hakika natambua kuwa ni ngumu sana kukabiliana na hii kitu kwani hupangi au kuchagua nani wa kumpenda, hisia za kimapenzi hujitokeza tu kwa mtu yeyote na wakati wowote, lakini kabla hisia hizo hazijaota mizizi (hazijakukaa sana) ni vema kuwa mdadisi kuhusu mtu uliempenda ili kujua ukweli kuhusiana na maisha yake ya sasa kimapenzi. Na mara tu baada ya kugundua kuwa amefunga ndoa ni vema kumkwepa.
Kutojiamini:
Ofcoz huwezi kuwa na hali ya kujiamini au kuwa na uhakika wa wewe kuwa mpenzi wake wa kudumu kwani huyo mwanaume sio wako na sio single ni mume wa mtu, siku yeyote ikiwa mkewe atagundua kuwa kajisahau na kuanza kurudisha yale yote ambayo labda mumewe anakosa na sasa kuja kupata kwako.
Vinginevyo, kama walivyogusia baadhi ya wachangiaji ni kuwa, ikiwa Imani zenu za Dini zinaruhusu na mkewe wa kwanza akaridhia then utakuwa mke wa pili.
Matokeo yake:
Wee bado ni binti mdogo wala huitaji kujiweka kwenye matatizo makubwa kama kuharibu ndoa ya mtu na vilevile kuishi na hatia ya kuharibu maisha ya watoto ambao ni matunda ya ndoa hiyo. Kumbuka watoto waliozaliwa kama matunda ya ndoa hiyo wataumia kama atakavyoumia mama yao.
Utakuwa umewanyang'anya baba yao, utakuwa umewaharibia maisha yao kwani hakuna mtoto anataka kumuona mama yake anaumia (unajua watoto tulivyo karibu na mama zetu). Huenda hujui yote haya kwa vile hukulelewa katika mazingira ya ndoa (kama mmoja wa wachangiaji alivyogusia), mazingira tuliokulia husaidia sana kwenye maamuzi yetu.
Nini cha kufanya:
Achana na huyu mume wa mtu kwania anakupotezea muda wako na kukuzibia bahati ya kukutana na wanaume, kwani kuna vijana wengi tu wenye umri mkubwa zaidi yako lakini hawajaoa na pia wapo vijana wenye umri wako (24-29) ambao wako huru.
Kila la kheri.

No comments:

Pages