Tuesday

Mpenzi atishia kujiua Kisa sms ya Ex akiomba msamaha!-Ushauri

"Kwanza pole na hongera kwa kazi unayofanya ya kutoa ushauri kwa jamii. Mimi ni msichana mwenye miaka 23, nina mpenzi ambaye siku hizi ni kama kafichua makucha vile. Tumekuwa pamoja kwa muda wa mwaka mmoja.

Kilichonifanya niandike leo Dinah, ni huyu mpenzi wangu! mwanzo tulikuwa tunapendana sana na ahadi tele tele, yaani mikwaruzano haikuwepo na muda wote huo hatukuwahi kukosana. Basi siku moja tulikuwa tumekaa sehemu akaniomba nimuhamishie wimbo kutoka kwenye simu yangu kwenda kwenye simu yake.

Kwa utani tu nikamwambia nimeiacha simu nyumbani, jamaa akaja juu kwamba nimemdharau nikamuomba msamaha lakini wapi! akanipokonya simu huku akiuliza "unaficha nini?" Nikamwambia samahani lakini hakukubali na hivyo akachukua simu na akaenda nayo kwake.
Ile simu alikuwa kaninunulia yeye, kwenye simu hiyo kulikuwana sms za x- boyfriend akiniomba msamaha ili turudiane.

Mpenzi wangu akazidi kukasirika na kupandisha sana na akampigia huyo kaka nilieachana nae nakumpandishia aache kunifatilia. Kinachomuuma hasa ni bada ya kugundua kwenye zile sms kuwa Ex wangu anamzidi Elimu kwani kamaliza Chuo Kikuu na pia anamzidi kifedha. Lakini mimi sinampango nae huyo jamaa wala elimu yake wala fedha zake kwani niliisha achana nae na analijua hilo.


Sasa tatizo kubwa hapa ni kuwa mpenzi wangu huyu ananitishia kuwa atajiua na hatanii kweli, ni Mchaga alafu pia nimemzidi kielimu kwani hivi sasa niko Chuo Kikuu mwaka wa pili yeye aliishia Kidato cha 4 na kuanzisha Biashara zake zinazomuingizia hela.

Mimi kuwa Chuo Kikuu ndio limekuwa tusi tukiongea kidogo tyu utasikua "au kwa vile sijasoma najiua ili nikuache huru" Mpenzi wangu anamiaka 25 aliniambia hajawahi kuwa na mwanamke na mimi ni wake wa kwanza.

Dinah najieleza na kuomba kila kukicha na sasa ni miezi 3 imepita lakini msimamo wake ni ule ule wa kujiua, nikamwambia nirudishie simu lakini kila tukipanga kuonana anasema yuko busy. Nikimuomba ninunue simu nyingine hataki, ikabidi nijinunulie mwenyewe simu nyingine kama ile ile ili kuendeleza mawasiliano.

Sasa jamani huyu mwanaume niendelee nae? kama nikiendelea nae na nikajamkosea tena si atajiua!! na nisipoendelea nae na yeye akajiua mimi sinitakuwa matatizoni na Degree yangu ikaishie Segere?
Naomba ushauri kutoka kwa wachangiaji wote".

No comments:

Pages