Thursday

Mume ni mwema lakini hataki kazi wala hatoi Unyumba-Ushauri!

"Habari mpenzi,
nimevutiwa sana na blog yako, kwa kweli ina story za kusikitisha na ukweli kuhusu maisha. Mimi ni mwanamke niliyeolewa naona nina matatizo ambayo nimekaa nayo kimya kwa muda mrefu bila kujua nimwombe nani msaada.

Nimejaribu kuongea na Mama yangu mzazi lakini nimepewa ushauri wa kuvumilia, nimejaribu kuongea na Mama mkwe wangu ushauri ni huo huo sasa sijui labda nipate ushauri toka kwa watu wengine sasa.

Story inaanza hivi; tumependana na mume wangu bila kuwa na kasoro, baada ya mwaka wa uchumba tukafunga ndoa Kanisani. Baadaya ya kuoana tu mungu akanijalia ujauzito nikazaa mtoto wa kike mwaka uliofuata, basi ilikuwa ni furaha tu.

Baada ya miaka miwili nikajaliwa mtoto wa pili wa kiume sasa, basi nayo ilikuwa heri. Sikuwahi kugombana na mume wangu wala kukosana kwa aina yoyote, maisha yalikuwa ni matamu haswa kwani ni msikivu kweli kweli. Chochote ukimwambia anafanya hata kupika hata kufua nguo zangu za ndani.....duuuh hadi wengine walikuwa wananiambia nimempa limbwata.


Basi baada ya kuzaa mtoto wa pili nikashangaa mwenzangu hana time na mimi si kwamba halali nyumbani laah anakula na tunalala wote, watoto anaangalia na matumizi yote anatoa lakini penzi kitandani hakuna, basi ikapita miezi kadhaa bahati mbaya kazi yake aliyokuwa anafanya ikaharibika.

Akawa hana kazi lakini hatukukata tamaa ya maisha tulianza kutafuta tukisaidiana maisha na tulikuwa na miradi yetu midogomidogo ilikuwa inatusaidia. Lakini bado pamoja na yeye kushinda nyumbani tu labda akihangaika kuomba kazi huku na huku mimi nikirudi kutoka kazi hana time ya kufanya mapenzi ila kuongea tunaongea vizuri na hatugombani hata siku moja.

Nikapata woga wa kumuuliza mwenzangu kama ana tatizo maana naona jogoo huwa anasimama kama kawa hasa wakati wa asubuhi lakini hajawahi kunitamkia ananitamani au kunitaka kuwa anataka tufanye mapenzi, mhhhh nikaja nikaona hii kweli kali.


Miezi sita ikapita hatujagusana ila tunakaa vizuri sana kula wote, kulala wote na kushare vitu vingine tu kama kutoka out n.k. Sasa limekuja suala la kazi, kila ninapomuombea kazi kwa watu na kuitwa kwa ajili ya mahojiano hapati. Juzijuzi nilimuombea kazi mahali nifanyapo kazi na akaitwa lakini akakataa kwenda akadai yeye hawezi kwenda kufanya kazi mahali ambapo mimi nafanya kazi.

Hapo mhh sikumuelewa nikajaribu kumueleza vizuri kuwa hatutakuwa ofisi moja ila jengo moja hakukubaliana na mimi . Sasa dada dinah, mtu kama huyo unamfanyaje?

Mwaka mzima umekaa ukishikilia familia na ukisali Mungu ampe kazi, ukimvumilia na kumpenda ingawa hakupi unyumba bila sababu maalum, sasa na kazi hataki kufanya anachagua badala ya kufanya yoyote for the sake of the kids, je nifanyeje? tafadhali naomba msaada hapo kama ni wewe ungefanyaje?-Magy"

Dinah anasema: Mpendwa Magy asante sana kwa ushirikiano na uvumilivu as nimechelewa kujibu, lakini natumaini maoni na ushauri wa wasomaji umesaidia wakati unasubiri kutoka kwangu.

Nitakupa maelezo na ushauri katika sehemu mbili, moja kuhusu kutokufanya Mapenzi na pili suala la yeye kugoma kufanya kazi sehemu moja na wewe.

Kwanini hafanyi mapenzi na wewe lakini anasimamisha!!
Kuna sababu nyingi ambazo zinaweza kumfanya mwanume apoteze hamu ya kufanya mapenzi, kumbuka hamu na nguvu ni vitu viwili tofauti tena kwa wanaume kusimamisha pia kuko kwa aina mbili kusimamisha kwa vile wako tayari kungonoka na kusimamisha kwa vile ni sehemu ya ujinsia wao kwa maana kuwa kuna aina mbili za mwanaume kusimamisha:- (1)-kutokana na mawazo ya kingono (2)-kutokana na kuwa stimulated kwa kushikwa au kuguswa na kitu kama vile shuka, chupi, mkono n.k


Mfano ni mwanaume kusimamisha asubuhi, ile haina maana kuwa anataka ngono japokuwa inaweza kufanyika ngono kama akikuona ukopembeni na ukamvutia then akapata mawazo ya kingono on top of msimao ambao ulisababishwa na mzunguuko wa damu wakati kalala......


Hivyo basi yeye kutokufanya ngono na wewe haina maana anamatatizo ya nguvu za kiume. Nadhani tatizo kubwa linaweza kuwa moja kati ya haya :-

Mosi, Hofu ya kuachishwa kazi (katika hali halisi unapewa taarifa mapema kuwa utapunguzwa/fukuzwa kazi), sasa ile hofu ilisababisha msongamano wa mawazo (stress) na hivyo kupoteza hamu ya kungonoka.

Pili, mabadiliko ya mwili wako baada ya kujifungua mtoto wa pili (Chunguza hapa), na jitahidi kurekebisha.....jipende na hakikisha unavutia zaidi, fanya mazoezi ya misuli kuanzia ya ulimi mpaka ya Uke.

Tatu, hapati attention ya kutosha kutoka kwako kama mpenzi labda kwa vile wewe huna muda as una-deal na watoto bila ushirikiano wake kutokana na stress.......(peleka watoto kwa bibi yako au kwa ndugu yeyote mnae muamini) mara moja kila baada ya wiki 2.

Nne, Yeye kuwa muanzilishi wa kutaka/kufanya ngono kitu ambacho huwa kina udhi/kera na kuchosha na hivyo mtu anaamua kutokufanya kabisa......(Kuanzia sasa usisubiri yeye aanze, anzisha wewe). Hii itamfanya ajiamini na kuhisi kuwa anavutia pia anafurahi kuona kuwa mkewe sio Gogo, pia mara moja kwa wiki mfanyie mumeo jambo litakalo mfurahisha, pagawisha na kumridhisha kingono).

Nini chakufanya kwa ujumla: Mumeo anahitaji ushirikiano mkubwa kutoka kwako, ushirikiano huo sio wa kumtafutia kazi au kumsukuma atafute kazi (kitu ambacho anakijua wazi yeye kama mwanaume) kwani kwa kufanya hivyo unamfanya apoteze ile hali ya kujiamini kama mwanaume na pia unasumbua Ego yake kwani yeye kama mwanaume kamili najaua kuwa ni wajibu wake kuwa provider kwa familia yake, sasa unapo-take over nakujaribu kumtafutia kazi inaweza kuchangia kumfanya azidi kuhisi kuwa yeye ni useless.

Natambua unafanya hivyo katika harakati za kumpa ushirikiano, kuonyesha uko pale kwa ajili yake na tayari kumsaidia mumeo kwa faida ya watoto wenu, yote haya wewe kama mwanamke ungefurahi kuyapokea kutoka kwa mumeo kama ungepoteza kazi......lakini sio mwanaume. Mwanaume anapewa ushirikiano kivingine.

Huyu mumeo anamengi sana akilini mwake hivyo hakuna nafasi kabisa ya kuweka mawazo ya kingono (kama unawajua wanaume vema utanielewa ninachokisema hapa). Sasa ili kumsaidia arudie hali yake ya kawaida unatakiwa kufanya kazi ya ziada......


Mf: kuongea nae vizuri, kumshauri/kumpa matumaini, kumshirikisha kwenye maamuzi (japokuwa hawezi kuchangia kwa sasa), kuonyesha unampenda na kuvutiwa nae zaidi sasa hana kazi kuliko alivyokuwa na kazi(anzisha ngono, cheza na mwili wake na kuwa mtendaji mkuu), kuonyesha kuwa unaweza kusimama wewe kama mama bila kuonyesha stress au kuzidia (anajua kuwa unazidiwa lakini sio lazima umuonyeshe au kulalamika kwani itamuangamiza kiakili), usionyeshe kukerwa na yeye kutokuwa na kazi, kumpa matumaini kuwa kazi ni kazi tu as long as senti zinaingia n.k.


Kwa kufanya hayo niliyogusia na mengine ambayo baadhi ya wachangiaji wameshauri hakika mumeo atakuwa comfortable na mawazo yanaweza kupungua na hivyo kuanza kupata nafasi ya kufikiria ngono akilini mwake na hata kuanza kuona kuwa unamvutia tena.


Kufanya nae kazi Jongo moja: Ukiachilia mbali matatizo mengine yanayoweza kujitokeza kwa kufanya kazi sehemu moja (unless otherwise Taaluma zenu zinafanana na mnawekeana mipaka vinginevyo sio nzuri/afya kwa uhusiano wenu wa kimapenzi.


Kama nilivyogusia hapo juu, kwa baadhi ya wanaume kusaidiwa na wake zao ktk mtindo wa ku-take over kama ulivyofanya wewe huwapotezea hali ya kujiamini na kuhisi kuwa "wameolewa" achilia mbali mwnaume huyo aende kufanya kazi Jengo moja na mkewe ambae ndio actually kamtafutia hiyo kazi na usikute kazi yenyewe ni ya kiwango kidogo kuliko mkewe........hapo haji mtu!

Uless kuna matatizo mengine kwenye ndoa yenu ambayo hukutaka kuyaweka hapa, lakini tatizo lako sio kubwa kiasi cha kutishia uhai wa ndoa yenu. Hakikisha unafanyia kazi ushuri uliopewa na nina kuhakikishia kila kitu kitakuwa safii na Unyumba utaupata lakini kwa sasa jitahidi ku-initiate ngono kila unapojisikiwa kutaka kufanya hivyo, usisubiri yeye akufuate au akuombe!....ni mumeo huyo hivyo unamfanya atake kufanya kwa kutumia uanamke wako au yeye anakufanya wewe utake kufanya kwa kutumia uanaume wake.

Kama ingekuwa mimi ningefanyaje: Mimi kama Dinah, kwanza kabisa ningekubali mabadiliko na kujaribu kubadili mtindo wa maisha yetu kama familia ili ku-save. Ningeonyesha mapenzi kwa mume wangu kuliko mwanzo, ningehakikisha namuondolea stress kwa kutumia mbinu mbali mabali za kumkanda na kuongea nae bila kulalamika wala kuonyesha kuwa nimezidiwa na majukumu.


Kila wakati ningemfanya aone kuwa niko nae sambamba ktk hardship na sio yake peke yake bali yetu sote. Ningempa support na kumshauri kuhusiana na kazi/biashara (sio lazima kuajiriwa) kwa kumpa mawasiliano au kumuonyesha sites/magazeti lakini sio kwa ku-take over na kuingilia Ego yake.


Ningemshawishi kwa maneno na vitendo kuwa kufanya mapenzi kunasaidia kuondoa au kupunguza stress, nikifanikiwa basi nitahakikisha namfanyia mambo hadimu ambayo najua yanaondoa stress hata kwa masaa mawili (which itamfanya anitake kingono mara kwa mara).

Kwa vile naelewa kuwa kipindi hiki cha hardship kinamfanya mume wangu kushindwa kutumia akili yake kufikiria/taka ngono na kusimamisha, basi ningetumia njia ya kumsisimua kwa kufanyia kazi mwili wake na kuhakikisha akili yake ime-relax kabla sijaanza zoezi zila la kumsisimua kingono.

Nakutakia kila lililojema!

No comments:

Pages