Friday

Ndoa na Kaka wa kambo (step Brother) ni sahihi?

"Mimi ni msichana wa miaka 23, nina kaka yangu baba mmoja na mama tofauti. Yeye ananipenda na mimi nampenda na tumekwisha wahi kufanya mapenzi mara kadhaa. Yeye ameahidi kuwa atanioa. Sisi ni Waislamu, je ni sawa tunachokifanya kama sio sawa tufanyeje?"

Dinah anasema:Inasemekana na kuaminika kuwa Kibaiolojia na Kiuumbaji ( Mungu alivyotuumba ) mtu na ndugu yake hawawezi kutamaniana, ndugu kwa maana ya kuwa mmechangia damu ya mzazi mmoja. Lakini ndugu wengine kama Binamu, wapwa n.k. wanaweza kutamaniana na hata kupendana kwa vile hawachangii damu moja bali wazazi wao ndio wanaochangia damu.

Pia inasemekana watoto waliochangia sehemu moja ya damu (kama wewe na kaka yako wakambo) wakitamaniana ina maana kuwa uwezekano mmoja wenu sio toto halisi (Kibaolojia) wa baba. Yaani huenda wewe baba yako ni mwingine na sio huyo unaeamini kuwa ndio baba yako au kama wewe ni mtoto wa huyo Baba basi kuna uwezekano kuwa huyo kaka yako sio mtoto wa kweli wa Mzee wenu (mama zenu ndio wanajua ukweli halisi ktk hili au mfanye vipimo vya DNA kujua ukweli).

Kwenye jamii yeyote ile Duniani bila kujali Imani zao za kidini mtu na kaka yake waliochangia damu hawaruhusiwi kuwa wapenzi achilia mbali kufunga ndoa na kuzaa, kwa baadhi ya nchi za Ulaya ndugu kupendana ni kosa la jinai.

Kama hisia za mapenzi ni kali sana miongoni mwenu (which sio kawaida kwa ndugu) basi ni wazi kuwa ninyi sio ndugu na hivyo mnapaswa kuanza mikakati ya kutafuta ukweli kuhusu baba yenu na njia pekee ni either kuongea na mama zenu ili kuwapa ukweli halisi au kufanya DNA test.

Namna ya kupata ukweli:
Msikurupukie mama zenu na ku-demand bali mnahitaji kuwa na mipango nakujua namna za kupata ukweli bila wao kujua kama mmekwisha wahi kungonoana, mana'ke wakijua tayari mnamahusiano mtarushiwa shutuma na mtashindwa kujitete na wao kina mama watakuwa saved kutokana na "kutokujua baba yako au baba wa kaka yako".

Wewe na yeye kwa nyakati tofauti na kila mtu kivyake zungumzeni wazazi wenu wa kike......mwambie "mama mimi nahisi kama vile huyu sio baba yangu! Sina mapenzi wala hisia za baba na mtoto, unadhani kuna uwezekano kuwa huyu sio baba yangu?"......atakupa jibu, hakikisha majibu yake sio ya kusita na wala haonyeshi mshituko pia ukali lakini kama atashituka, kuwa mkali na kusita ujue kuna walakini.

Mwambie kwa kusisitiza kuwa " nataka kujua ukweli kwanini napata hisia hizi, hivyo nitaenda kufanya vipimo vya DNA ili nijue kama kweli huyu ni baba yangu"......mpe muda!

Sisemi kuwa huo ndio ukweli kuwa huyo Mzee sio baba yenu halisi bali kuna uwezekano mkubwa sana kuwa ninyi wawili sio ndugu! Nadhani mmoja wenu huyo sio baba yake mzazi bali ni baba mlezi (alisingiziwa au mama alikuwa hana uhakika na aliyem-mimba).

Kumbuka kuna asilimia kubwa ya akina baba ndani na nje ya ndoa nchini Tanzania wanalea au walilea watoto ambao sio wao. Ili kujua ukweli, ni mama pekee anatakiwa kutoka msafi au kufanya vipimo vya DNA.

Vinginevyo Ni mwiko kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu yeyote ambae mmechangia damu. Toka kwenye uhusiano huo mara moja na usirudie tena.

Kila la kheri!

No comments:

Pages