Wednesday

Siko Comfortable kuwa karibu na Ma'mkwe-Ushauri

"Hongera sana dada Dinah kwa jinsi unavyotusaidia kwenye mambo mbalimbali, nimeshapost maswali yangu mawili lakini umeyatia kapuni dada yangu kulikoni?? chonde chonde usilitie na hili kapuni.

Dinah anasema: Mama M, sijapokea swali lolote kutoka kwako, hili ni la kwanza. Kwa kawaida kila swali linanolifikia ni muhimu na huwa nali-publish kwa kufuata lini nimepokea.

****************************************************************************

Mimi ni mwanamke niliyeolewa na nina watoto wawili, mume wangu alishawahi kunicheat hapo awali na nikagundua lakini bado aliendelea. Mpaka sasa bado sijatulia kutokana na kutendwa na mume wangu.


Mimi na mama mke hatupatani kutokana na yeye mama kumtetea mume wangu alivyonicheat. Mama huyu alinifokea sana na kuniambia nimuache mume wangu, Yaani alinijia juu mpaka wake wa mashemeji zangu wakawa wanamsema kwa kumwambia anavyofanya sio vizuri.


Nimejifungua hivi karibuni na mtoto sasa anamiezi saba, sijawahi kuwasiliana na mama mkwe wangu tangu mwezi wa kumi na mbili mwaka jana alipokuja kwangu hapa Dar ambapo aliondoka vibaya na hata kusema kuwa kamwe hata kanyaga kwangu.


Mama mkwe yeye anaishi Mkoani, na kiukweli mimi nilikuwa nikimuonyesha heshima zote wala sijawahi kumchukia wala kujibishana nae sembuse kubadilishana maneno makali. Nakumbuka kuna wakati nilimpelekea nguo za Christmass, lakini aliziponda sana akasema atazitupa "nguo gani mbaya hivyo"? japokuwa ilikuwa ni suti nzuri tu jamani! mpaka wifi yangu (mtoto wake) akajisikia vibaya akaja kuniambia mbele ya mama yake ambaye aliona aibu na kuanza kukana.


Tatizo kubwa naona kama huyu mama mkwe anachuki binafsi na mimi japokuwa ndio mchezo
wake kwani keshawakorofisha sana hata hao wake wengine wa mashemeji zangu ila naona kwangu kazidi.

Sasa hivi niko kwenye uhusiano mzuri kiasi na mume wangu japo bado machungu hayajaisha ila anajitahidi, aliniita akaniomba nimsamehe mama yake akidai kuwa "nyie wanawake mnajuana wenyewe sijui kwa nini anakuchukia hivyo" akaniomba nimsamehe na niwe nampigia simu na niwe karibu nae. Siku mjibu kitu mume wangu na wala sikumpigia huyo mama mkwe kwani mimi nimejifungua hata yeye angeweza kuja au kunipigia simu naa kuulizia mtoto lakini anaongea na mwanae tu.

Swali: Mume wangu anataka tukambatize mtoto wetu mkoani (kwa mama mkwe) Xmass hii na mimi sijisikii huru kwani sitamani hata kumuona yule mama kwa alivyonipa stress kwenye maisha yangu, yani hapa sijaandika yote, hata watu baki na ndugu zangu wanajua matatizo niliyoyapata kutokana na chuki ya mama mkwe.

Naomba ushauri kwanza, nikubali nikambatizie mtoto huko kwa mama mkwe au la, na kama nikikubali kwenda huko je nimnunulie huyu mama zawadi kama nguo?? kwani mume wangu huwa hana utaratibu wa kununua nguo za mama yake kabisa!! tafadhali nisaidieni nideal vip na huyu mama??
Wenu mama M"

Dinah anasema: Pole sana kwa kukabiliana na chuki ya mama mkwe wako, hili ni tatizo kubwa linalowakabili wanawake wengi sana hapa Duniani. Hata mimi sijui ni kwanini hasa mtu umchukie mkweo kiasi hicho. Tena mbaya zaidi ni pale Mumeo akiwa ndio mtoto wa Kiume kwa kwanza/mwisho/mtoto wa kiume pekee kwenye familia yao.....hapa mama wakwe/wifiz huwa hawataki mchezo!

Tatizo letu wanadamu huwa tunategemea kupendwa mara tu baada ya kuungana na familia nyingine (kufunga ndoa), Jamani! Mtu mmoja kukupenda haina maana Ukoo mzima ukupende. Kama ikitokea kwa bahati nzuri mkapendana poa, ikitokea hawakupendi safii tu au kama wewe huwapendi ni kawaida vilevile (kwani mlizaliwa pamoja bwanaaa!).....kitu muhimu ni kuheshimiana na kila mmoja wenu kujua mipaka yake kati ya yule aliye waunganisha in ur case mumeo.


Unachotakiwa kuzingatia ni Kumpa heshima lakini kamwe usijipendekeze kwa mama mkwe huyo, usijilazimishe kumpenda (huwezi kulazimisha hisia kama hazipo kubali kuwa hazipo), kutokumchukia (mchukulie kama alivyo na dharau uchokozi na chuki zake kwako), hata siku moja usimzungumzie vibaya kwa watu wengine (kwa kufanya hivyo itakufanya ujenge chuki dhidi yake) kumbuka kuwa huyo ni bibi wa watoto wako hivyo kubali kuwa hakupendi na muache kama alivyo aili mradi tu hamkai nyumba moja.

Ni kama kuwa Kazini/Shuleni, kutakuwa na watu wanakupenda na wengine hawakupendi(ni nature ya mwanadamu)....... lakini huwezi kuacha kazi au masomo kwa vile tu watu fulani wanakuchukia. Unawadharau na kufanya kazi/masomo yako kwa bidii.

Ukiangalia kwa undani asilimia kubwa ya wanawake huwa na tabia ya kuchukiana kweli kweli bila sababu, inawezekana kabisa mtu humjui lakini unajenga chuki. Sasa mimi nadhani hii asili ya baadhi ya wanawake kuwa na chuki za ovyo-ovyo ndio husababisha baadhi ya wakwe zetu kuwa hiyo kwani uanamke hauwatoki hata kama ni watu wazima sana.


Wataalam wa Saikolojia wanadai kuwa mama na mtoto wa kiume huwa na bond maalum, ukaribu huo kati ya mama na kijana wake kuendelea kwa muda mrefu sana. Mama huyu huendelea kudhani kuwa Kijana anahitaji kumsikiliza na kufanya maamuzi ambayo yeye mama anakubaliana nayo kama akipinga basi Kijana hapaswi kuendelea na maamuzi hayo na kiendelea basi atakumbwa na mabaya (si umewhai kusikia kuwa Radhi ya mama ni Kali kwa mtoto wa kiume kuliko wa kike? Jiulize kwanini iwe kwa mtoto wa kiume tu?).


Sasa Kijana anapokuwa na kuanza kujitegemea mama hupata hisia za kupoteza sehemu kubwa maisha yake na hivyo ataendelea kujiweka karibu na kutaka kujua kila kitu ambacho Kijana wake anakifanya. Ikitokea Kijana kaamua kuchumbia Binti ampendae mama huyu anaweza kukubali au kupinga (huwezi kuambiwa hili ni suala la familia yao).


Mama akikubali basi ataanza kujiweka sana kwenye uhusiano wenu na kuhoji vitu kama vile mtafunga ndoa lini? nani asimamie, aina ya nguo zitakazo valiwa, sherehe iwe wapi na iwe vipi? n.k. Baada ya kufanikiwa kufunga ndoa mama huyu ataanza "nataka mjukuu" wakati tayari wapo wengine waliozaliwa na dada/kaka wa mumeo....

Hii yote ni katika kutafuta ushindi na kukuonyesha wewe Mkwe (anakuona kama mwanamke mwingine unaechukua nafasi yake kwa mwanae) kuwa yeye ndio mwenye sauti na mamlaka kwani huyo Mumeo ni mtoto wake hivyo anatakiwa kufanya akisemacho yeye na sio wewe.

Kutokana na maelezo yako inaonyesha kuwa Mama mkwe wako hakupewa nafasi sana kwenye uhusiano wenu na ndio maana anakuwa bitter kila kukicha, na kilichonifanya nigundue hilo ni kutokana na maelezo yako kuwa alimtetea mwanae alipotoka nje ya ndoa.....alimtetea mwanae ili aweze kum-win back Kijana wake na wewe ubaki mwenyewe na maumivu yako moyoni.....alitaka Ushindi kwani wewe ndio unaemjali kwa kumnunulia zawadi na si mwanae......kwa mama mkwe huyu hili ni pigo kubwa kwani anadhani kuwa wewe as "mwanamke tu" ndio una-control kila kitu kwenye maisha ya mwanae.


Nini cha kufanya: Mimi binafsi sioni sababu yakwenda kumbatiza mtoto huko Mkoani unless otherwise kuna sababu za msingi kama vile Kabila la Wachaga (Xmas kuliwa Nyumbani Moshi kind muhimu), mnamtegemea yeye Mama mkwe kiuchumi, labda ndugu wengi wako huko Mkoani na wanataka kushuhudia Ubatizo na ili ku-save ni bora ninyi muende huko kuliko wao kuja Dar, Mama mkwe huyo mgonjwa na hawezi kusafiri lakini anataka kumuona mtoto n.k.

Ili kuondoa vurugu, wewe kubali kwenda kubatiza mtoto huko aliko mama mkwe lakini hakikisha unaelewana na mumeo kuwa hamkai sana ili kuepuka "chokochoko" za huyo mwanamama. Utakapo kwenda huna haja ya kumnunulia chochote huyo mwanamama asie na shukrani.....ili apate ujumbe kuwa kuponda zawadi =hakuna zawadi.

Baada ya shughuli ya Ubatizo kuisha ni vema wewe na mumeo kuwasiliana kwa mara nyingine tena kuhusiana na unavyojisikia kwa mama mkwe wako. Usipozungumza na mumeo na kuliweka hili wazi na kumfanya akuelewe ili asaidie kumaliza chuki za mama yake kwako.

Mumeo mpenzi ataendelea kudhani (mwanaume akisema "sijui kwanini mnachukiana, ni mambo yenu wanawake...naomba umsamehe mama") yaya tachukulia kuwa yameisha, kuwa umemsamehe mama yake na hivyo kuendelea kufanya mambo ya kumhusisha mama yake na wewe mara kwa mara hali itakayosababisha maumivu makali ya hisia kwa vile utadhani kuw amumeo hakujali pia hautokuwa comfortable na mkweo.


Liweke wazi suala la wewe kujisikia huna thamani kwa mama mkwe huyo kutokana na dharau zake, kutetea usaliti wa ndoa...tena sisitiza hapa kuwa ukimuona mama mkwe huyo unakumbuka uchafu aliokufanyia mumeo (umesema kuwa bado unamachungu/hujasahau japokuwa unajitahidi kusamehe....itachukua muda mpaka kurudia hali yako ya kawaida). Mwambie yote yalioujaza moyo wako bila hasira wala chuki.

Muombe mumeo amwambie na ikiwezekana amsaidie mama yake abadilishe tabia yake mbaya, na mara baada ya kubadilisha tabia yake basi anza kumnunulia/tumia zawadi lakini sio ktk kujipendekeza bali kumjali.

**Nani alisema maisha ya ndoa ni rahisi eei? Ni magumu ila ukijua namna ya kukabiliana na wanawake (mama mkwe/wifi) kila kitu kina kinaenda vema na kila mmoja wenu anafurahia maisha yake kivyake na familia yake.

Natumaini kuwa maelezo ya wachangiaji na haya yangu yatakuwa yamekusaidia kufanya uamuzi wa busara.

Kila la kheri!

No comments:

Pages