Sunday

He's too busy kuwa na mimi, nampenda-anipenda-Ushauri

"Hi dinah,

Mimi ni msichana wa miaka 27, nina mpenzi ambaye tulianza mahusiano yetu tangu 2007. Tulipoanza mapenzi yetu yalikuwa motomoto, tulionana mara kwa mara na tulielewana vizuri tu. Ilifikia mahali na kunitamkia kwamba ifikapo October 2009 tutafunga ndoa.

Kwa kweli nilifurahi sana, kwasababu ni mtu ambaye ananijali sana. Chakushangaza kadri siku zinapozidi kwenda amekuwa bize sana na promises zimekuwa nyingi. Tunapopanga kuonana au kutoka out mara nyingi hatokei, nikimtumia sms anaweza asijibu kabisa, then baadaye anatoa sababu zisizokuwa za msingi na kusisitiza kwamba bado ananipenda sana.

Isitoshe sijamuuliza kuhusu ahadi aliyoitoa ya ndoa maana naona kama nitamforce. Kwa kweli naumia sana moyoni kwa sababu hana muda na mimi yuko bize kupita kiasi, lakini anadai ananipenda.

Sitaki kumjibu vibaya wala kumtamkia its over kwasababu nampenda nataka aje kuwa baba watoto wangu lakini ananiumiza kwa sababu ya the way he treats me. Naomba ushauri wako kwasababu kuna kitu kimenikaa moyoni nashindwa hata la kufanya.

Nimejitahidi kukaa kimya lakini wapi bado ananipigia simu na kunitumia sms bado kuwa bado
ananipenda. Sasa najiuliza mapenzi gani haya wakati mtu mwenyewe hana muda na mimi, muda wote ni wakazi ambayo anafanya hapahapa Dar.

Ni mimi mdau,
mery."

Dinah anasema: Hello Mery, asante kwa mail na ufafanuzi kuhusu umri wa mpenzi wako ambao hakika ni umri ambao vijana wehu huanza kutulia kiakili (anakaribia miaka 31). Nakubaliana na wewe kwenye swali la "mapenzi gani haya wakati yeye hana muda na mimi?".

Kutokana na tabia yake (kwa mujibu wa maelezo yako) kuna mawili-matatu yanawezekana:-
(1)-Inawezekana ni kweli anashughuli nyingi za kikazi zinazomzuia kukutana na wewe.

(2)-Vilevile kuna uwezekano mkubwa tu kuwa anaendesha maisha kivingine na anakuweka wewe kama spare tire incase huko aliko hakutokwenda atakavyo.

(3)-Hana mpango wa kuwa na wewe tena ila hajui namna gani ya kumaliza uhusiano hivyo anafanya hivyo ili wewe ukate tamaa na uchoke kumsubiri na hivyo u call it a day.

Kwanini basi nimedhania hivyo? Kwa sababu huyu bwana alikutamkia kuwa atakuoa au mtafunga ndoa mwezi wa Kumi mwaka huu lakini hakuchukua hatua zozote zinazoendana na matamshi yake Mf-Kujitambulisha kwenu na kupewa utaratiubu wa kufunga ndoa na wewe na hatimae kuanza maandalizi...mwezi Octoba sio mbali na nijuavyo mie maandalizi ya kufunga ndoa hasa kwa kufuata taratibu za kijamii Tanzania huchukua muda mrefu.

Kwenye uhusiano wenu kuna ukosefu wa mawasiliano, kwa maana kwamba hamzungumzii maisha yenu kama wapenzi kwa uwazi, wewe unadhani kuzungumzia ahadi yake ni kama kumlazimisha na yeye huenda anahisi kutokuzungumzia kwako suala la ndoa ni dalili kuwa huna mpango wa kuolewa nae au hauko tayari.

Unajua, kuna tofauti ya kati ya kukumbushia jambo ktk mtindo wa kuzungumza na kukumbushia jambo hilohilo ktk mtindo wa kudai/lazimisha (demand).....napata picha hapa kuwa hukujua tofauti hizo na wewe ukadhania kuwa kukumbushia ni ku demand yeye afunge ndoa nawe.

Nini cha kufanya: Kwa unampenda mpenzi wako na unaamini kuwa na yeye anakupenda lakini kwa bahati mbaya hatujui ni nini hasa kinasababisha yeye kuwa hivyo alivyo, fuata haya nitakayokueleza ili kupata ukweli utakao kusaidia kufanya uamuzi wa busara....

Naja midaz....

No comments:

Pages