Thursday

Haonyeshi kuumia baada ya kumuacha...

Habari dada dinah, pole na kazi pia hongera kwa kuelimisha
jamii.


Nimekua nikifatilia sana blog hii na kujifunza mengi, ila leo na
mie yamenikuta
(kabla ya yote kwanza naomba ulihifadhi jina langu).

Mimi ni Kijana wa Kiume mwenye miaka 22 nilivyoanza
chuo mwaka jana nilikutana na Msichana ambaye sijawahi ona!! inshort
nikampenda na nilichukua muda kumchunguza kama anatabia nzuri na
nikagundua kua anatabia nzuri na anafaa.


Tukaanza mahusiano ya kimapenzi na huu ni mwezi wa Sita ila
hatujawahi kufanya Ngono kwa sababu huwa anaogopa sana kwasababu hajawahi kuguswa.

Nimevumilia yote lakini sasa akaanza kuonyesha kutokunijali kama
mwanzo na hanitreat kama mpenzi ila kama rafiki nimemwambia
abadilike mara nyingi lakini hanielewi.


Mara ya mwisho wiki iliyopta
nikamuuliza mbona unanipa mapenzi nusu nusu akanambia kwasababu
haniamini! Nilishangaa coz najua anauhakika asilimia mia kua yupo peke
yake akaongea na mengine mengi yakuniudhi.

Some time anaenda kwa marafiki
zangu anakaa mpaka masaa mawili huko...pia fb na whatsapp
anachat muda mwingi na hufanya hivyo wakati nikiwa nae.

Kiukweli heshima yangu hanipi kama
mwanzo tena, sasa nimeamua kumuacha ili nipunguze hizi stress na maumivu coz nampenda mpaka nimepitiliza.

Tangu nimemuacha haonyeshi dalili za
kuumia wala kujali wakati mimi nazidi kuumia. Hii ni mara ya pili kumbuka niliamua kumwacha baada ya kuchoshwa na stress zake ila nampenda na natamani
hata arudi tena tuendelee na mapenzi. Nifanyaje???


Dinah anasema: Salama kabisan ahsante na shukurani kwa ushirikiano.

Dogo una asili ya u control freak eti! Kabla hujaanza uhusiano ukamchunguza kwanza, uliporidhika ndio ukaanzisha uhusiano nae.....ndani ya Miezi sita una demand msichana afanye mambo ka' Mkeo na umemuacha mara Mbili in 6months kwasababu hafanyi utakayo.

Unataka akuheshimu vipi? Ikiwa hakutukani mbele za watu au kukukebehi mbele ya ndugu, jamaa na marafiki as Gf atakuwa anakuheshimu....au unataka asikae na rafiki zako au asi-chat na rafiki zake kwenye Mitandao?


Ikiwa wewe unamiaka 22 ni wazi yeye ataluwa hivyo au mdogo zaidi, katika hali halisi Wasichana wadogo ndivyo walivyo....bado anajitambua, anajifunza mambo kama Binti anaeelekea kuwa Mwanamke, anapenda kuzungumza na marafiki na kujenga uzoefu na watu mbali mbali.


Nadhani ama umeaninishwa mambo kuhusu mahusiano ya kimapenzi ambayo ni tofauti na hali halisi ya Maisha au umejiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi bila kujua uhusiano wa kimapenzi ni nini hasa!


Huwezi kumtawala Binti wa watu kwa jinsi ulivyoelezea na yeye kuendelea kutaka kuwa na wewe kama Mpenzi wake.....inawezekana hapendezwi na tabia yako ndio maana ameamua akufanye uwe rafiki tu.

Nadhani timing ya wewe kumuacha ilikuwa mbaya, umemuacha wakati yeye tayari alikuwa kakuweka kwenye "friends zone" hivyo hakupata au hapati maumivu ya kuachwa kama mpenzi(hana habari).


Kama kweli unampenda na unapenda akurudie basi ni vema kubadilika kwanza halafu ndio ujaribu kumshawishi tena kwa kuomba msamaha na kumhakikishia kuwa hutokuwa ukimtawala.

Akikubali kurudiana na wewe unatakiwa ku-relax na kumuacha awe huru kuzungumza na wenzake iwe mitandaoni au vinginevyo ailimradi tu havuki mipaka.

Akikataa basi nadhani ni vema umuache aendelee kuwa yeye na kujifunza who she is kama msichana na wewe zingatia Masomo na huko Mbele utakutana na mwingine na kuanzisha uhusiano mwingine.

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

No comments:

Pages