Tuesday

Simjui mwenye Mimba!

Dada Pole na Majukumu, 

Sorry kwa yaliyo nikuta kwani unaweza kuona kama sina heshima kama mtoto wa kike.

Ni hivi nilikua na mpenzi wangu kwa mwaka mzima ila akawa hana mpango wa kunioa nikaanza kufanya mpango nipate mtu ambaye anaweza kujenga familia na yeye.

Kilichofuata sikumwacha mpenzi wangu wa zamani nikawa nadate na wote, sasa nimepata UJAUZITO na sijajua ni wa nani kabisa nachanganyikiwa sana.

Kwani nilipata Hedhi tarehe 10.12.2013, ndiyo ilikua mwisho wa kwenda hedhi. Ila tarehe 21,12,2013 nililala na kitu kipya hadi Asubuhi.

Nikarejea 22 kwetu. Tarehere 24 mkesha wa Xmas nikakesha na wa zamani hadi Asubuhi, najua ni tabia mbaya ila ilibidi kwa sababu mpenzi wangu wa zamani aling'anga'nia nikesha nae.


Sasa January sikuona siku zangu nilipo pima ni mjamzito. Je hapo nani anaweza kuwa ndiye mwenye mtoto.

Nimewaza sana nimekosa jibu sasa nina ujauzito wa miezi miwili.

Naomba ushauri.

**********************

Dinah anasema: ahsante, ila ungekuwa karibu ningekuchapa viboko za miguuni akyanani vile. Khaa! Kuna wanawake wa Bongo mnaujasili wa ajabu na wa kijinga....unaMix wanaume na kwa USHENZI hutumii Kinga!!


Kama ni miezi miwili na ushehe yaani Wiki 9 na siku fulani ni ya huyo Mpya na kama ni miezi Miwili kamili au na siku kadhaa ni ya huyo wa zamani.

Hayo ni mahesabu ya haraka haraka ili kujua mahesabu halisi ni vema kama ungenipatia Mzunguuko wako wa Hedhi je ni wa kawaida, Mrefu, Mfupi au unabadilika kila mwezi.

Hii itasaidia kujua ni tarehe gani kati ya 21-22 au kabla na 24-25 ni lini ulikuwa umepevusha yai....

Mbegu za Mwanaume hukaa ndani kwa muda wa Masaa 72 mpaka Wiki moja, inategemea na ubora/afya za Manii husika.

Sasa kwa vile uliwachanganya itakuwa. Ngumu sana kujua unae share nae Mimba ni nani kwani hatujui "speed" na ubora wa Mbengu za wa kwanza au wa pili kufanya nae ngono.

Mbaya zaidi umewachanganya ndani ya siku chache kati yao.....kwanini usitumie CONDOM jamaniii (*hitting my table*).


Anyway, pole...piga mahesabu tena ili ujue ukaribu wa tarehe za kupevuka na tarehe za kushika Mimba halafu ukifikisha miezi 3 umjulishe unaedhani ndio Mwenyewe, hilo moja.


Pili waambie wote, atakae kubali ndio huyo kwa kipindi hiki cha ujauzito na atakaekataa ndio hivyo tena.


Mtoto akizaliwa fanya utaratibu wa DNA test najua Bongo kwenye Hospitali kubwa Binafsi wanatoa huduma hii.

Vipimo hivyo vitasaidia kujua ukweli halisi na kumpa haki Baba wa mtoto na mtoto husika ikiwa unaamua kuendelea na Ujauzito huo.


Tuone wengine watakushauri nini?

Mapendo tele kwako...

No comments:

Pages