Thursday

Ni usawa au Kiburi?

"After thousands of years of male dominance, we now stand at the beginning of the feminine era, when women will rise to their appropriate prominence, and the entire world will recognize the harmony between man and woman". The Rebbe.

Unakumbuka ule Mkutano wa wanawake kule Beijing au unatambua kwanini wanawake wanaitwa "wabeijing"?

Swala la usawa baina yetu wanawake na wanaume lilizua au linaendela kuzua utata kutokanana baadhi ya wanawake ku-abuse maana halisi au nia na madhumuni ya Usawa huo......na matokeo yake wanawake wamekuwa kama wanaume, wamejawa na viburi mbele za wapenzi/waume wao n.k. hii ni kutokanana kutoelewa kwanini hasa wamama wale walikusanyanakule "Beijingi" kudai Usawa.

Ukweli ni kwamba hakuna mwanaume anataka kuwa au kuoa "mwanaume mwenzie" kwa maana kwamba unatakiwa kubaki mwanamke no matter how much you earn, no matter how educated you are, no matter how tall you are.....having said that sina maana kuwa ndio uwe kila kitu "sawa/ndio bwana/mume wangu" type.


Usawa tunaotakiwa kuutolea mcho ni ule wa kujitahidi ktk elimu, ufanyaji wa kazi kwa bidii (kupata cheo kutokanana uwezo wako sio kwa jinsia yako), kuchangia maendeleo ya familia zetu namaisha yetu kwa ujumla, kuongoza aukushika nyazifa mbali-mbali ambazo awali zilidhaniwa kuwa ni za kiume tu n.k.


Sio kuwa mlevi kwa vile wanaume wanalewa, kuwa na wapenzi wengi wengi kwa vile baadhi ya wanaume wanafanya hivyo, kutongoza kama wanavyotongoza wanaume kwa vile tu "tuko sawa", kula kiasi kikubwa cha chakula kwa vile tu wanaume wanakula kuliko sisi (hushangai kwanini wanaume wanakula sana lakini hawana pot bellies eti?) na mambo mengine mengi ambayo wanaume wanayafanya kwa sababu zao binafsi kwa vile ni wanaume au kulinda ego zao.

Ukikutana na mwanaume ambae anapenda au vutiwa na "kiburi chako" ukidhani ndio usawa ujue huyo ni Player.

Ndio "fact" ya leo......unamchango? swali je?

Mwisho mzuri wa wiki.

No comments:

Pages