Wednesday

Nini kiswahili kwa "affectionate"


Kwa wanawake wengi wa Kibongo hawajui au hawajali umuhimu wa kuwa “affectionate” as long as anapatiwa pesa za chakula na manunuzi mengine binafsi kila siku, sina hakika kuwa hawatilii maanani hii kitu kwa vile wanaume wetu wa kibongo wengi sio “affectionate” kwa sababu zao binafsi au kudhani kuwa ni sio kitu muhimu sana au “sio utamaduni wetu”(hata denda sio utamaduni wetu lakini mbona tunakulana tu eti?)


Katika hali halisi ni muhimu sana japo mpenzi wako hajui jinsi ya kuomba au akijaribu kukupa “affection” anakatishwa tamaa au kushushuliwa (told off) kuwa anadeka mno au “hukui tu” au hajiheshimu n.k. labda kwa vile wamekuwa pamoja muda mrefu au tayari kawa mama.


Nimeshuhudia baadhi ya wanaume wakilalama kuwa wapenzi wao hawaonyeshi shukurani kwa yale mwengi ambayo wanawafanyia wake/wapenzi wao lakini wanashindwa kuelewa kuwa mtu hawezi kushukuru kwa vitu au mambo unayomfanyia wakati hayaitaji au kwake sio muhimu sana kama yale ambayo anayahitaji ambayo wewe mwanaume huyafanyi.


Au ni kweli unayafanya lakini jinsi unavyo yawakilisha hayo uyafanyayo kama “affection” kwa mpenzi wako ni tofauti na vile mpenzi wako anataka au angependa na kwa bahati mbaya hasemi au hakuambii vile anataka na matokeo yake nyote wawili mnakuwa hamna raha au amani mioyoni mwenu japo kuwa mnapendana kwa dhati.


Ni wazi kuwa kila mmoja wetu anamahitaji yake ktk swala zima la uhusiano wa kimapenzi ambayo ni tofauti kabisa “no matter how compatible you might be”, hivyo ni jambo la muhimu sana kuyaweka wazi mahitaji yako(sio chakula, maladhi na matibabu bali mambo ya kushikana, busu, outings, ukaribu, mazungumzo, ngono, kuwa pale kwa ajili yake n.k.) kwa mwenza wako ili aweze kuyatimiza.


Kumbuka kuwa hakuna mtu anazaliwa anajua kila kitu bali sote tunajifunza kila siku, na nafasi nzuri ya kujifunza ni kumzoea (bila kumshushia heshima) mpenzi wako kama rafiki,mpenzi na mwenza….ondoa au acha kabisa heshima ya uongo (Uoga) na badala yake be youself ili akupende 4 who u are sio who u pretend 2 be.


Huwezi kuamini kuwa baba mtu mzima hawi-affectionate kwa mkewe aliyeoa miaka ya 80s lakini anakuwa “very affectionate” kwa binti mke mdogo anaetoka nae a.k.a kimada……I don’t real get it?


Jamani mapenzi hayana ukubwa wala udogo, mapenzi hayazeeki, mapenzi huendelea kuwepo bila kujali mmekuwa pamoja kwa muda mrefu kiasi gani…..mapenzi ni hisia zilizo ndani yako na hazina uhusiano na kuzaliwa kwa watoto au kuzeeka hivyo sote hatuna budi kuyaonyesha kwa uwazi kwa wenza wetu


Muonyeshe mwenzio jinsi unavyompenda kwa vitendo sio kwa kungonoana kwani huko sio kupenda kwa vitendo bali ni hitaji lingine linalojitegemea ambalo nalo ni muhimu pia kwenye uhusiano (sio zamu yake leo).

*Sasa hebu leo mwambie mpenzi wako ni nini hasa hupendi akufanyie na nini hasa unapenda afanye kuonyesha “affection” kwako.


Natambua kutokana na utamaduni wetu kuna mambo mengine huwa tunashindwa kuyafanya kwa kuhofia jamii itatudhaniaje…..who cares….hawakulishi…..hawakuvishi na kila mtu anaishi kimtindo wake na kufurahia maisha kivyake hivyo wewe ukihisi unataka kuonyesha penzi kivitendo mkiwa marikiti au kituo cha daladala just do it! sio mpaka mfike uchochoroni!


Kuwa "affecionate" ni muhimu sana pia ikiwa wewe na mpenzi wako hamlingani kiuwezo ktk kubilingishana.......kuna watu kungonoka sio muhimu sana kwao kutokana na sababu zao mbali-mbali lakini hiyo haina maana hawahitaji kupendwa au kupetiwa-petiwa.

Siku njema.

No comments:

Pages