Tuesday

Ma' mtoto wa Pembeni Msumbufu, nifanyeje?

Mambo dada dinah,



Mimi ni kijana wa umri wa miaka 28 nina mke na mtoto mmoja wa kiume mwenye miaka 3 sasa lakini pia nilizaa na mwanamke mwingine ambaye mwanae ni mwenye miaka 3 pia.









Huyu wa pili tuliiba tu na bahati nzuri akapata mimba ya mtoto huyo ila mimi

nimemwambia sipo tayari kuoa wanawake wawili na yeye ilikuwa si ahadi tuoane.









Nikimwambia aolewe anipe mwanangu hataki anataka aolewe na mimi. Mimi siwezi naomba ushauri nifanyaje? Kama matumizi natoa.





*************



Dinah anasema: Mambo poa kabisa, vipi wewe?





Uliibia na mwanamke mwingine nje ya ndoa bila Kinga alafu kashika Mimba unasema bahati nzuri?! Hiyo ni bahati mbaya tena MBAYA sana.









Bora Mkeo angekukuta na mtoto kuliko kumpelekea mtoto mwenye umri sawa na mwanae....! Wanaume Weusi kwa kusambaza umasikini (kuzaa ovyo) tu mnaongoza!!







Ni rahisi kusema nipe mwanangu nawe uende kuolewa, lakini ukiweka hayo katika vitendo ni ngumu sana.









Sio rahisi kwa mama kuacha mtoto wake mdogo aende kulelewa na mama mwingine(subiri afikishe miaka 15 labda) ambapo mtoto ataamua mwenyewe kukaa na Baba yake au Mama yake.









Pia sio wanaume wengi ambao wanapenda kuoa wanawake ambao tayari wana mtoto/watoto. Most wanaume huwa abuse watoto husika kijinsia.







Nenda Ustawi wa Jamii na ukaelezee issue yako nadhani wao wana-refer kesi yako Mahakamni kwa ajili ya Uamuzi kisheria kuwa utamtunza mwanao kwa kiasi cha pesa watakchokupangia kutokana na kipato chako(hakikisha mkeo anajua kama alikuwa hajui na uwe tayari kwa Vita).









Huyo mwanamke hawezi kukulazimisha umuoe ikiwa wewe mwenyewe hutaki kufanya hivyo kwa vile tayari umeoa.









Ikiwa anatumia mtoto kukutishia kuwa usipofunga ndoa nae atatoa siri au atakuharibia kazi....then itabidi ukamripoti Polisi.









Jifunze kumheshimu na kumthamini Mkeo. Unapotoka nje ya ndoa unaumiza Mkeo, mtoto/watoto wako na mtoto atakaezaliwa nje ya ndoa yenu.





Acha ubinafsi, Uzizi na kusambaza Umasikini.



Kila la kheri!

Mapendo tele kwako...

No comments:

Pages