Monday

Nifanye nini Mke wangu awe Msafi!

Dada Dinah vipi mambo. Mimi nikijana mwenye umri wa miaka 25, nimeoa na nina mtoto Mmoja.

Mke wangu ananiboa yaani ni mchafu aoshi uke akikojoa, akioga asubuhi mpaka asubuhi. Nikimwambia hanielewi yaani mpaka nafikiria kumuacha hebu naomba ushauri wako dada.

*******

Dinah anasema: Poa!


Swali lako ka' la kutunga vile. Si umshukuru Mungu angalau anaoga mara moja kwa siku? Watu wanaoga mara Moja kwa wiki siku nyingine wafanya ku-wash/refresh/jifuta kutokana na shida ya Maji.


Hiyo tabia mkeo ameianza hivi karibuni au alikuwa hivyo kabla hamjafunga ndoa? Maana kwenye kila ndoa inayofungwa Binti hupewa "darasa" na usafi ni moja ya somo linalosisitizwa au ilikuwa ndoa ya Mkeka?!!


Wataka kumuacha mkeo na kuumiza hisia za mtoto wako kwa sababu/tabia ambayo inarekebishika.


Kuna tofauti ya kuongea na mtu(upendo na heshima) na kumwambia (dharau na command).....watu wengi huchanganya au hawajui tofauti yake.


Kutokana na maelezo yako na jinsi ulivyoandika inaonyesha wazi huna mapenzi ya dhati kwake, huna heshima kwake na unamchukulia kama "chombo" au kitu.


Nikionacho hapa ni kuwa Ndoa yenu inakosa Nguzo muhimu 4 za uhusiano wa Kimapenzi/Ndoa.

1-Mawasiliano: Zungumza nae kwa mapenzi, muelekeze na kumfundisha (labda hajui) faida ya usafi, muonyeshe "topic ya jinsi ya kujiswafi" ipo kwenye topics za 2007.


2-Ushirikiano: Kila unapoenda kuonga nenda nae na muogeshane so kama unaoga x3 kwa siku nae atakuwa anaoga mara tatu kwasababu unaoga nae.


3-Usaidizi:Msaidie shughuli za kulea na nyingine za ndani au mtafutie msaidizi, sometimes mtoto anaweza mfanya mama ajisahau(akose muda/kuchoka).


Kwasababu yupo nyumbani na wewe unakwenda kazini, haina maana yeye wa nyumbani hafanyi kazi au hachoki. Wote mnafanya kazi katika Mazingira tofauti na kazi zote zinachosha....pengine ya kulea mtoto inachosha zaidi.

4-Heshima: Mheshimu kama yeye na ukubali kuwa yupo tofauti, kalelewa tofauti na mazingira aliokulia na tamaduni pia ni tofauti hivyo m-treat ipasavyo bila dharau au kum-bully kwa vile tu ni mwanamke(Mfumo Dume).


Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

No comments:

Pages