Wednesday

D'hicious leo ni Mwaka wa Saba!

Hongera na Ahasnte kwa kuichagua Blog hii siku ya leo ambapo inatimiza Miaka Saba.









Napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru wewe Msomaji, Mtembeleaji, Mchangiaji na zaidi ni wewe unaenitumia Mwaswali kwa kuamini kuwa nitakupatia Ushauri ambao kwa namna moja au nyingine utasaidia kupanua mawazo yako na hivyo kufanya uamuzi sahihi.











Kwa dhati kutoka Moyoni nasema ahsante sana kwa kunipa nguvu ya kukaa chini na kufikiria nikupe ushauri gani na Changamoto ya nikushauri vipi?











Kuna Baadhi ya Watu hunipa Changamoto kweli kweli, wakati mwingine nashindwa ku-switch off "kichwani" swali/maelezo husika na hivyo kabla usingizi haujanipitia naanza kufikiria namna ya kujibu/shauri.











Kumbuka tu kuwa Ushauri unaotolewa kwenye D'hicious sio sheria, hivyo ni hiari yako kufuata yote, kuacha yote au kuchukua unayodhani yatakusaida kwenye kutatua issues zako.











Mwisho kabisa napenda kusema ahsante kwa my little ones kwa kulala mapema so that I can write this Post.









Mungu aendelee kutupa afya njema, atupe akili na upeo wa kuweza kuona na kukabiliana na issues kwenye Ndoa/Mahusiano yetu ili tuishi kwa Amani na furaha.





Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

No comments:

Pages