Monday

Mke wa Pili, hanijali kwa hela wala penzi.

Habari dada Dinah, pole na kazi na hongera kwa kazi unayoifanya.

Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka kadhaa, nimeolewa ndoa ya mke wa pili na mume wa kiislamu huu ni mwaka wa pili sasa.


Tumezaa mtoto mmoja mwenye umri wa miaka minne sasa. Cha kushangaza dada Dinah sitambuliki kwao mume wangu na wala mtoto wangu hajulikani.


Ndoa yetu ilikuwa ya siri hakukuwa na sherehe yoyote zaidi ya Sheikh tu na mashahidi aliokuwa amewatafuta huyo Sheikh.

Hela ya matumizi ni shida na hata haki ya Ndoa kama mke mimi siipati kwasababu halali kwangu na hata kuja ni kwa kubeep tu.

Sasa naomba ushauri huyu mwanaume ana malengo na mimi kweli au ananipotezea wakati na kunizibia rizki mimi.


***********

Dinah anasema: Nashukuru na ahsante kwa ushrikiano.


Sasa mrembo mbona jina lako la Kikristo ilikuaje ukakubali kufunga Ndoa ya Kiislamu achilia mbali kuwa mke wa pili kwa siri!!....Au ulilazimisha ndoa baada ya kuzaa na huyo Mume wa mtu?


Kutokana na maelezo yako nadhani wewe ni Kimada wa huyo Mume wa mtu, sio mke wa pili kwake kama ulivyojiaminisha.


Kufungishwa Ndoa na Shekhe haiweki uhalali wa Ndoa yako ikiwa taratibu nyingine hazikufuatwa. Pia kutokana na Ugumu wa Maisha wengine wala sio Mashekhe bali "wafanya biashara".


Sizijui sheria za Dini ya Kiislamu lakini nadhani kabla ya kufunga Ndoa Mke mkubwa na watoto wa ndoa ya kwanza hupewa taarifa na kuna sheria lazima zifuatwe.


Pia mume mtarajiwa huenda kwa mwanamke kuposa na kufuata taratibu zote muhimu za Uchumba.

Mara nyingi Wake wenza huishi nyumba moja au mahali pamoja, na ikitokea mahali hapatoshi au mke Mkubwa hataki ukae nae basi mke mdogo hutafutiwa mahali pengine.


Mume "wenu" hujigawa "sawa sawa" bila upendeleo kwa wake zake wote. Mke mdogo hujulikana kwenye familia nzima mpaka wale wa ndani ndani kule (wasio na uzito).


Sasa kama mwenzangu hayo yote hayapo na Ndoa ilifungwa kwa SIRI bado unaamini tu kuwa wewe ni Mke wake na sio Kimada?!!


Kwabahati mbaya sidhani kama kuna Sheria inayokulinda ili kupata "matunzo" kwa ajili ya mwanao. Huwezi kwenda Mahakmani wala Ustawi wa jamii kuomba msaada kisheria kwasababu huwezi kuthibitisha uhalali wa Ndoa yako.


Labda kama una Cheti cha Kuzaliwa chenye jina na sahihi ya Baba'ke mtoto, ila mzunguuko wake lazima ukate tamaa (kutokana na nature ya uhusiano wako na Mume wa mtu).


Usijutie kosa lako ila ujifunze kufunga miguu mbele ya wanaume wenye wake na familia zao in the future, Uislamu sio sababu ya kumkubali Mume wa mtu hata kama wanakuahidi Ndoa, kataa.


Kosa kubwa ulilofanya ni kuzaa na huyo mwanaume, matokeo yake mnamtesa mtoto ambae hakuomba kuzaliwa na mume wa mtu ambae sasa ni baba yake au wewe.

Hakupotezei Muda bali ameisha kupotezea Muda wako, hakuzibii rizki (hakuna mwanadamu anaweza kukuzibia rizki), nadhani kagundua familia yake na mkewe wanaumuhimu zaidi yako ndio maana anabeep au kuna Mke wa tatu wa siri huko kwingine.

Hama hapo ulipo, tafuta kazi au shughuli ya kukuingizia kipato.....mwanzo utakuwa Mgumu sana lakini ukisimama kama mwanamke na ukajitahidi utafanikiwa tu.


Baada ya kukaa sawa na mtoto kakua then unaweza anza kutoka tena, zingatia ulichojifunza kutokana na kosa lako la mwanzo.


Utakapo anza kutoka tena na mwanaume hakikisha hana familia na pia usikimbilie kuzaa, tumia kinga kwa faida yako na mtoto wako.

Mtoto akikua atamtafuta baba yake....(Kama atataka hilo litokee).

Kila la kheri.

Mapendo tele kwako...

No comments:

Pages